2 Wafalme 22 – NEN & NRT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Wafalme 22:1-20

Yosia Mfalme Wa Yuda

(2 Nyakati 34; 35:20-27)

122:1 Yer 1:2; Yos 15:39Yosia alikuwa na miaka minane alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka thelathini na mmoja. Mama yake aliitwa Yedida binti Adaya, kutoka Boskathi. 222:2 Kum 5:32Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana na kuenenda katika njia zote za Daudi baba yake. Hakugeuka upande wa kuume wala wa kushoto.

322:3 2Nya 34:20; Yer 39:14Katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wake, Mfalme Yosia akamtuma mwandishi Shafani mwana wa Azalia, mwana wa Meshulamu, kwenda katika Hekalu la Bwana. Akasema: 422:4 Ezr 7:1; 2Fal 12:4-5“Panda uende kwa Hilkia, kuhani mkuu, umwambie ahesabu zile fedha ambazo zimeletwa katika Hekalu la Bwana, ambazo mabawabu wamekusanya kutoka kwa watu. 522:5 2Fal 12:5Waambie waikabidhi kwa watu walioteuliwa kusimamia kazi ya Hekalu. Waamuru watu hawa wawalipe wafanyakazi ambao wanakarabati Hekalu la Bwana: 622:6 2Fal 12:11-12wale maseremala, wajenzi na waashi. Waambie pia wanunue mbao na mawe yaliyochongwa ili kukarabati Hekalu. 722:7 2Fal 12:15Lakini hawahitajiki kutoa hesabu ya fedha walizokabidhiwa, kwa sababu wanafanya kwa uaminifu.”

822:8 Kum 31:24; Gal 3:10Hilkia kuhani mkuu akamwambia Shafani mwandishi, “Nimekipata Kitabu cha Sheria ndani ya Hekalu la Bwana.” Akampa Shafani, ambaye alikisoma. 9Kisha Shafani mwandishi akamwendea mfalme na kumpa taarifa akisema: “Maafisa wako wametoa ile fedha ambayo ilikuwa ndani ya Hekalu la Bwana na imekabidhiwa mikononi mwa wasimamizi wa marekebisho ya Hekalu.” 1022:10 Yer 36:21Ndipo Shafani mwandishi akampasha mfalme habari kwamba: “Hilkia kuhani amenipa kitabu hiki.” Naye Shafani akakisoma kile kitabu mbele ya mfalme.

11Mfalme aliposikia maneno ya kile Kitabu cha Sheria, akararua mavazi yake. 1222:12 2Fal 25:22; Isa 8:14Akatoa maagizo haya kwa Hilkia kuhani, Ahikamu mwana wa Shafani, Akbori mwana wa Mikaya, Shafani mwandishi, na Asaya mtumishi wa mfalme: 1322:13 Kum 29:24-28; Amo 2:4“Nendeni mkamuulize Bwana kwa ajili yangu, na kwa ajili ya watu na Yuda wote kuhusu yale yaliyoandikwa ndani ya kitabu hiki ambacho kimepatikana. Hasira ya Bwana ni kubwa inayowaka dhidi yetu kwa sababu baba zetu hawakuyatii maneno ya kitabu hiki. Hawajatenda kulingana na yale yote yaliyoandikwa humo kutuhusu sisi.”

1422:14 Kut 15:20Hilkia kuhani, Ahikamu, Akbori, Shafani na Asaya wakaenda kuongea na nabii mke Hulda, ambaye alikuwa mke wa Shalumu mwana wa Tikwa, mwana wa Harhasi mtunzaji wa chumba cha mavazi. Hulda aliishi Yerusalemu katika Mtaa wa Pili.

15Akawaambia, “Hivi ndivyo asemavyo Bwana, Mungu wa Israeli: Mwambieni yule mtu aliyewatuma ninyi kwangu, 1622:16 Yos 23:15; Dan 9:11‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana: Nitaleta maafa juu ya mahali hapa na watu wake, kulingana na kila kitu kilichoandikwa katika kitabu hicho mfalme wa Yuda alichosoma. 1722:17 1Fal 9:9Kwa sababu wameniacha mimi na kufukiza uvumba kwa miungu mingine, na kunighadhibisha kwa sanamu zote zilizotengenezwa kwa mikono yao, hasira yangu itawaka dhidi ya mahali hapa, wala haitatulizwa.’ 1822:18 Yer 21:2Mwambieni mfalme wa Yuda, ambaye amewatuma kumuuliza Bwana, ‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana, Mungu wa Israeli, kuhusu maneno uliyoyasikia: 1922:19 Isa 37:15; Yer 26:6; Law 26:31Kwa kuwa moyo wako ulikuwa msikivu na ulijinyenyekeza mbele za Bwana uliposikia kile nilichosema dhidi ya mahali hapa na watu wake, kwamba wangelaaniwa na kuachwa ukiwa, basi kwa sababu uliyararua mavazi yako na kulia mbele zangu, nimekusikia, asema Bwana. 2022:20 Isa 47:11; 1Fal 21:29Kwa hiyo nitakukusanya kwa baba zako, nawe utazikwa kwa amani. Macho yako hayataona maafa yote nitakayoleta juu ya mahali hapa.’ ”

Basi wakapeleka jibu lake kwa mfalme.

New Russian Translation

4 Царств 22:1-20

Иосия – царь Иудеи

(2 Пар. 34:1-2, 8-13)

1Иосии было восемь лет, когда он стал царем, и правил он в Иерусалиме тридцать один год. Его мать звали Иедида, она была дочерью Адаи, родом из Боцката. 2Иосия делал то, что было правильным в глазах Господа, и ходил всеми путями своего предка Давида, не уклоняясь ни вправо, ни влево.

3На восемнадцатом году своего правления царь Иосия послал писаря Шафана, сына Ацалии, внука Мешуллама, в дом Господа, сказав:

4– Ступай к первосвященнику Хелкии, пусть он пересчитает деньги, принесенные в дом Господа, которые привратники собрали у народа. 5Пусть их отдадут людям, которые были назначены наблюдать за работами при доме, а они пусть заплатят рабочим, которые ремонтируют дом Господа, – 6плотникам, строителям и каменщикам. Пусть они также покупают дерево и тесаный камень, чтобы восстанавливать дом. 7Отчета за доверенные им деньги с них требовать не нужно, потому что они действуют честно.

Книга Закона найдена в храме

(2 Пар. 34:14-28)

8Первосвященник Хелкия сказал писарю Шафану:

– Я нашел в доме Господа книгу Закона22:8 Вероятно первосвященник нашел весь Закон, но, возможно, это было лишь Второзаконие, последняя часть Пятикнижия (см. Втор. 31:24-26)..

Он отдал ее Шафану, и тот ее прочитал. 9После этого писарь Шафан пришел к царю и доложил ему:

– Твои слуги взяли деньги, какие нашлись в доме Господа, и передали их наблюдателям за работами и работникам.

10Затем писарь Шафан сказал царю:

– Священник Хелкия дал мне одну книгу.

И Шафан стал читать из нее перед царем.

11Услышав слова из книги Закона, царь разорвал на себе одежду. 12Он приказал священнику Хелкии, Ахикаму, сыну Шафана, Ахбору, сыну Михая, писарю Шафану и царскому слуге Асаи:

13– Идите, вопросите Господа за меня, за народ и за всю Иудею о том, что написано в найденной книге. Велик Господень гнев, который обрушился на нас из-за того, что наши отцы не слушали слов этой книги, они не поступали так, как она предписывает нам.

14И священник Хелкия, Ахикам, Ахбор, Шафан и Асая пошли к пророчице Олдане, жене Шаллума, сына Тиквы, внука Хархаса, хранителя одежд. Она жила в Иерусалиме, во Втором округе. 15Она сказала им:

– Так говорит Господь, Бог Израиля: «Скажите человеку, который послал вас ко Мне: 16„Так говорит Господь: Я наведу на это место и на его обитателей беду, как написано в книге, которую читал царь Иудеи. 17Из-за того, что они оставили Меня, возжигали благовония другим богам и вызывали Мой гнев всем, что сделали их руки, Мой гнев на это место вспыхнет и не угаснет“. 18Скажите царю Иудеи, который послал вас вопросить Господа: „Так говорит Господь, Бог Израиля, о словах, которые ты слышал: 19Так как твое сердце смягчилось и ты смирил себя перед Господом, услышав, как Я сказал против этого места и его обитателей, что им суждены опустошение и проклятие, и так как ты разорвал свои одежды и плакал предо Мной, то и Я услышал тебя, – возвещает Господь. – 20Поэтому Я возьму тебя к твоим отцам, и тебя похоронят в мире. Твои глаза не увидят всей той беды, которую Я наведу на это место“».

И они передали ее ответ царю.