2 Wafalme 22 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Wafalme 22:1-20

Yosia Mfalme Wa Yuda

(2 Nyakati 34; 35:20-27)

122:1 Yer 1:2; Yos 15:39Yosia alikuwa na miaka minane alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka thelathini na mmoja. Mama yake aliitwa Yedida binti Adaya, kutoka Boskathi. 222:2 Kum 5:32Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana na kuenenda katika njia zote za Daudi baba yake. Hakugeuka upande wa kuume wala wa kushoto.

322:3 2Nya 34:20; Yer 39:14Katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wake, Mfalme Yosia akamtuma mwandishi Shafani mwana wa Azalia, mwana wa Meshulamu, kwenda katika Hekalu la Bwana. Akasema: 422:4 Ezr 7:1; 2Fal 12:4-5“Panda uende kwa Hilkia, kuhani mkuu, umwambie ahesabu zile fedha ambazo zimeletwa katika Hekalu la Bwana, ambazo mabawabu wamekusanya kutoka kwa watu. 522:5 2Fal 12:5Waambie waikabidhi kwa watu walioteuliwa kusimamia kazi ya Hekalu. Waamuru watu hawa wawalipe wafanyakazi ambao wanakarabati Hekalu la Bwana: 622:6 2Fal 12:11-12wale maseremala, wajenzi na waashi. Waambie pia wanunue mbao na mawe yaliyochongwa ili kukarabati Hekalu. 722:7 2Fal 12:15Lakini hawahitajiki kutoa hesabu ya fedha walizokabidhiwa, kwa sababu wanafanya kwa uaminifu.”

822:8 Kum 31:24; Gal 3:10Hilkia kuhani mkuu akamwambia Shafani mwandishi, “Nimekipata Kitabu cha Sheria ndani ya Hekalu la Bwana.” Akampa Shafani, ambaye alikisoma. 9Kisha Shafani mwandishi akamwendea mfalme na kumpa taarifa akisema: “Maafisa wako wametoa ile fedha ambayo ilikuwa ndani ya Hekalu la Bwana na imekabidhiwa mikononi mwa wasimamizi wa marekebisho ya Hekalu.” 1022:10 Yer 36:21Ndipo Shafani mwandishi akampasha mfalme habari kwamba: “Hilkia kuhani amenipa kitabu hiki.” Naye Shafani akakisoma kile kitabu mbele ya mfalme.

11Mfalme aliposikia maneno ya kile Kitabu cha Sheria, akararua mavazi yake. 1222:12 2Fal 25:22; Isa 8:14Akatoa maagizo haya kwa Hilkia kuhani, Ahikamu mwana wa Shafani, Akbori mwana wa Mikaya, Shafani mwandishi, na Asaya mtumishi wa mfalme: 1322:13 Kum 29:24-28; Amo 2:4“Nendeni mkamuulize Bwana kwa ajili yangu, na kwa ajili ya watu na Yuda wote kuhusu yale yaliyoandikwa ndani ya kitabu hiki ambacho kimepatikana. Hasira ya Bwana ni kubwa inayowaka dhidi yetu kwa sababu baba zetu hawakuyatii maneno ya kitabu hiki. Hawajatenda kulingana na yale yote yaliyoandikwa humo kutuhusu sisi.”

1422:14 Kut 15:20Hilkia kuhani, Ahikamu, Akbori, Shafani na Asaya wakaenda kuongea na nabii mke Hulda, ambaye alikuwa mke wa Shalumu mwana wa Tikwa, mwana wa Harhasi mtunzaji wa chumba cha mavazi. Hulda aliishi Yerusalemu katika Mtaa wa Pili.

15Akawaambia, “Hivi ndivyo asemavyo Bwana, Mungu wa Israeli: Mwambieni yule mtu aliyewatuma ninyi kwangu, 1622:16 Yos 23:15; Dan 9:11‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana: Nitaleta maafa juu ya mahali hapa na watu wake, kulingana na kila kitu kilichoandikwa katika kitabu hicho mfalme wa Yuda alichosoma. 1722:17 1Fal 9:9Kwa sababu wameniacha mimi na kufukiza uvumba kwa miungu mingine, na kunighadhibisha kwa sanamu zote zilizotengenezwa kwa mikono yao, hasira yangu itawaka dhidi ya mahali hapa, wala haitatulizwa.’ 1822:18 Yer 21:2Mwambieni mfalme wa Yuda, ambaye amewatuma kumuuliza Bwana, ‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana, Mungu wa Israeli, kuhusu maneno uliyoyasikia: 1922:19 Isa 37:15; Yer 26:6; Law 26:31Kwa kuwa moyo wako ulikuwa msikivu na ulijinyenyekeza mbele za Bwana uliposikia kile nilichosema dhidi ya mahali hapa na watu wake, kwamba wangelaaniwa na kuachwa ukiwa, basi kwa sababu uliyararua mavazi yako na kulia mbele zangu, nimekusikia, asema Bwana. 2022:20 Isa 47:11; 1Fal 21:29Kwa hiyo nitakukusanya kwa baba zako, nawe utazikwa kwa amani. Macho yako hayataona maafa yote nitakayoleta juu ya mahali hapa.’ ”

Basi wakapeleka jibu lake kwa mfalme.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

列王紀下 22:1-20

約西亞做猶大王

1約西亞八歲登基,在耶路撒冷執政三十一年。他母親叫耶底大,是波斯加亞大雅的女兒。 2約西亞做耶和華視為正的事,事事效法他祖先大衛,不偏不離。

發現律法書

3約西亞執政第十八年,他派米書蘭的孫子、亞薩利的兒子沙番書記去耶和華的殿,並吩咐他說: 4「你去見大祭司希勒迦,讓他清點奉獻到耶和華殿中的銀子,那些銀子是殿門守衛從民眾收集來的。 5-6然後把銀子交給負責修理耶和華殿的督工,他們就可以購買木料和鑿好的石頭,雇用木匠、建築工人和石匠來修理耶和華的殿。 7你不用查核他們的賬目,因為他們都是忠誠可靠的人。」

8大祭司希勒迦告訴書記沙番說:「我在耶和華的殿裡找到了律法書。」希勒迦把書交給沙番看。 9沙番稟告王說:「你的臣僕已經把殿裡的銀子清點完畢,交給了殿裡的督工和工人。」 10他又告訴王:「希勒迦祭司給了我一卷書。」沙番就在王面前誦讀這書。 11王聽了律法書上的話,就撕裂衣服, 12吩咐希勒迦祭司、沙番的兒子亞希甘米該亞的兒子亞革波、書記沙番和王的臣僕亞撒雅13「你們為我、為民眾和整個猶大去求問耶和華有關這書卷上的話。耶和華的烈怒已經臨到我們身上,因為我們的祖先沒有遵守這書卷上的話,沒有遵行這書卷上的吩咐。」

戶勒妲的預言

14於是,希勒迦祭司、亞希甘亞革波沙番亞撒雅去求問女先知戶勒妲。她是負責管理禮服的沙龍的妻子,沙龍哈珥哈斯的孫子、特瓦的兒子。戶勒妲住在耶路撒冷第二區。他們向她說明來意。 15她對他們說:「以色列的上帝耶和華要你們回去告訴差你們來見我的人, 16耶和華說,『我要照猶大王所讀的那書上的一切話,降災難給這地方及這裡的居民。 17因為他們背棄我,給別的神明燒香,製造偶像惹我發怒,我的怒火要在這地方燃燒,絕不止息。 18你們告訴差你們來求問耶和華的猶大王,至於你所聽見的那些話,以色列的上帝耶和華說, 19因為你聽到我對這地方及其居民的警告,知道這地方要受咒詛、淪為荒場,便悔改,在我面前謙卑,撕裂衣服,向我哭泣。因此,我垂聽了你的禱告。這是我耶和華說的。 20我會讓你平安入土到你祖先那裡。你不會看到我要降給這地方的一切災難。』」他們便回去稟告王。