2 Wafalme 21 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Wafalme 21:1-26

Manase Mfalme Wa Yuda

(2 Nyakati 33:1-20)

121:1 2Fal 21:16Manase alikuwa na umri wa miaka kumi na miwili alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka hamsini na mitano. Mama yake aliitwa Hefsiba. 221:2 Yer 15:4; 2Fal 16:3Akafanya maovu machoni pa Bwana, akafuata desturi za machukizo za mataifa ambayo Bwana aliyafukuza mbele ya Waisraeli. 321:3 Amu 6:28; Kum 17:3Akajenga upya mahali pa juu pa kuabudia miungu ambapo Hezekia baba yake alikuwa amepabomoa. Pia akasimamisha madhabahu za Baali na kutengeneza nguzo ya Ashera, kama Ahabu mfalme wa Israeli alivyofanya. Akalisujudia jeshi lote la angani na kuliabudu. 421:4 Isa 66:4; Kut 20:24Akajenga madhabahu katika Hekalu la Bwana, ambamo Bwana alikuwa amesema, “Katika Yerusalemu nitaliweka Jina langu.” 521:5 1Fal 17:12Katika nyua zote mbili za Hekalu la Bwana, akajenga madhabahu kwa ajili ya jeshi lote la angani. 621:6 Law 18:21; Kum 18:14; 2Fal 23:26Akamtoa kafara mwanawe mwenyewe katika moto, akafanya uchawi na uaguzi, na akataka shauri kwa wapiga ramli na kwa mizimu. Akafanya maovu mengi sana machoni mwa Bwana na kumghadhibisha.

721:7 Kum 16:21; Law 15:31; Kut 20:24Akachukua nguzo ya Ashera aliyoichonga na kuiweka katika Hekalu, ambalo Bwana alikuwa amemwambia Daudi na mwanawe Solomoni, “Katika Hekalu hili na katika Yerusalemu niliouchagua kutoka kabila zote za Israeli, nitaliweka Jina langu milele. 821:8 2Sam 7:10Sitaifanya tena miguu ya Waisraeli itangetange kutoka nchi niliyowapa baba zao, ikiwa watakuwa waangalifu kufanya kila kitu nilichowaamuru, na kuishika Sheria yote ambayo walipewa na Mose mtumishi wangu.” 921:9 1Fal 14:9; Eze 5:7Lakini hawa watu hawakusikiliza. Manase akawapotosha, hivyo kwamba walifanya maovu mengi kuliko mataifa ambayo Bwana aliyaangamiza mbele ya Waisraeli.

10Bwana akasema kupitia watumishi wake manabii: 1121:11 1Fal 14:9; Mwa 15:6“Manase mfalme wa Yuda ametenda dhambi hizi za kuchukiza. Amefanya maovu mengi kuliko Waamori waliokuwepo kabla yake, na ameiongoza Yuda katika dhambi kwa sanamu zake. 1221:12 Yer 15:4; 1Sam 3:11Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: Nitaleta maafa makubwa juu ya Yerusalemu na Yuda, kiasi kwamba masikio ya kila mmoja atakayesikia habari zake yatawasha. 1321:13 Isa 34:11; Amo 7:7-9Nitanyoosha juu ya Yerusalemu kamba ya kupimia iliyotumika dhidi ya Samaria, na timazi iliyotumika dhidi ya nyumba ya Ahabu. Nitaifutilia mbali Yerusalemu kama mtu afutaye sahani, nikiifuta na kuifunikiza. 1421:14 2Fal 19:4; Za 78:60Nitawakataa mabaki wa urithi wangu na kuwatia mikononi mwa adui zao. Watapokonywa mali zao na kutekwa nyara na adui zao wote, 1521:15 Yer 25:7kwa sababu wametenda uovu machoni pangu na kunighadhibisha tangu siku baba zao walipotoka Misri mpaka siku ya leo.”

1621:16 2Fal 24:4; Mao 4:13; Sef 1:12Zaidi ya hayo, Manase pia alimwaga damu nyingi isiyo na hatia, hivi kwamba aliijaza Yerusalemu kutoka mwanzo hadi mwisho, mbali na dhambi ambayo alikuwa amesababisha Yuda kufanya, na hivyo wakatenda maovu machoni pa Bwana.

17Matukio mengine ya utawala wa Manase, na yote aliyoyafanya, pamoja na dhambi alizotenda, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda? 1821:18 Es 1:5; 7:7Manase akalala pamoja na baba zake na akazikwa katika bustani ya jumba lake la kifalme, katika bustani ya Uza. Naye Amoni mwanawe akawa mfalme baada yake.

Amoni Mfalme Wa Yuda

(2 Nyakati 33:21-25)

19Amoni alikuwa na miaka ishirini na miwili alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka miwili. Mamaye aliitwa Meshulemethi binti Haruzi, kutoka Yotba. 2021:20 1Fal 15:26Akatenda maovu machoni mwa Bwana, kama baba yake Manase alivyofanya. 21Akaenenda katika njia zote za baba yake, akaabudu sanamu ambazo baba yake aliziabudu na kuzisujudia. 2221:22 1Fal 11:33; 1Sam 8:8Akamwacha Bwana, Mungu wa baba zake, wala hakuenenda katika njia za Bwana.

23Watumishi wa Amoni wakafanya fitina juu yake, nao wakamuulia kwake nyumbani. 24Kisha watu wa nchi wakawaua wale wote waliokuwa wamefanya hila dhidi ya Mfalme Amoni. Wakamfanya Yosia mwanawe kuwa mfalme mahali pake.

25Matukio mengine ya utawala wa Amoni na yale aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda? 26Akazikwa kwenye kaburi lake katika bustani ya Uza. Naye Yosia mwanawe akawa mfalme baada yake.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

列王紀下 21:1-26

瑪拿西做猶大王

1瑪拿西十二歲登基,在耶路撒冷執政五十五年。他母親叫謝西芭2他做耶和華視為惡的事,效法耶和華在以色列人面前趕走的外族人的可憎行徑。 3他重建他父親希西迦拆毀的邱壇,效法以色列亞哈巴力築造祭壇,製造亞舍拉神像,並且祭拜和供奉天上的萬象。 4耶和華曾指著祂的殿說:「我的名必在耶路撒冷」,而他卻在耶和華的殿內建造異教的祭壇。 5他在耶和華殿的兩個院子裡建造祭拜天上萬象的祭壇; 6他燒死自己的兒子,獻作祭物;他行邪術,占卜,求問靈媒和巫師,做了許多耶和華視為惡的事,惹耶和華發怒。 7他雕刻亞舍拉神像,放在耶和華的殿中。關於這殿,耶和華曾對大衛和他兒子所羅門說:「我從以色列各支派中選擇了耶路撒冷和這殿,我的名要在這裡永遠受尊崇。 8只要以色列人謹遵我對他們的一切吩咐和我僕人摩西交給他們的律法,我就不再把他們從我賜給他們祖先的土地上趕走。」 9可是以色列人不肯聽從。瑪拿西誘使他們作惡,比耶和華在以色列人面前所毀滅的各族更嚴重。 10於是,耶和華藉著祂的僕人——眾先知宣告: 11瑪拿西王做的這些可憎之事,比以前住在這裡的亞摩利人更嚴重,使猶大人祭拜偶像,陷入罪中。 12所以,以色列的上帝耶和華要在耶路撒冷猶大降下大災難,凡聽見這事的人都必耳鳴。 13我要像懲罰撒瑪利亞亞哈家一樣懲罰耶路撒冷。我要潔淨耶路撒冷,就像人擦淨盤子後倒扣過來。 14我要撇棄我殘存的子民,把他們交給敵人,任其擄掠。 15因為從他們祖先離開埃及那天起直到今天,他們一直做我視為惡的事,惹我發怒。」 16瑪拿西不僅使猶大人犯罪,做耶和華視為惡的事,還濫殺無辜,使耶路撒冷血流遍地。 17瑪拿西其他的事及其一切所作所為都記在猶大的列王史上。 18他與祖先同眠後,葬在他王宮的花園。即烏撒花園,他兒子亞們繼位。

亞們做猶大王

19亞們二十二歲登基,在耶路撒冷執政兩年。他母親叫米舒利密,是約提巴哈魯斯的女兒。 20他效法他父親瑪拿西做耶和華視為惡的事, 21步他父親的後塵,祭拜和供奉同樣的偶像。 22他背棄他祖先的上帝耶和華,沒有遵行耶和華的教導。 23他的臣僕謀反,在王宮裡殺了他。 24民眾殺死那些背叛亞們王的人,立他兒子約西亞為王。 25亞們其他的事及其一切所作所為都記在猶大的列王史上。 26他死後,葬在烏撒花園內他的墳墓裡,他兒子約西亞繼位。