2 Wafalme 20 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Wafalme 20:1-21

Ugonjwa Wa Hezekia

(2 Nyakati 32:24-26; Isaya 38:1-8, 21-22)

1Katika siku hizo, Hezekia akaugua, naye akawa karibu kufa. Nabii Isaya mwana wa Amozi akaenda kwake na kumwambia, “Hili ndilo asemalo Bwana: Tengeneza mambo ya nyumba yako, kwa sababu utakufa, hutapona.”

2Hezekia akaelekeza uso wake ukutani, akamwomba Bwana: 320:3 Mwa 8:1; 2Nya 31:20“Ee Bwana, kumbuka jinsi nilivyoenenda mbele zako kwa uaminifu na kujitoa kwa moyo wangu wote, na kufanya yaliyo mema machoni pako.” Naye Hezekia akalia kwa uchungu.

4Kabla Isaya hajaondoka katika ua wa kati, neno la Bwana likamjia, akaambiwa: 520:5 1Fal 9:3; Za 39:12“Rudi ukamwambie Hezekia, kiongozi wa watu wangu, ‘Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa baba yako Daudi: Nimeyasikia maombi yako na nimeona machozi yako; nitakuponya. Siku ya tatu kuanzia sasa utapanda kwenda Hekalu la Bwana. 620:6 2Fal 19:34; 1Nya 17:19Nitakuongezea miaka kumi na mitano katika maisha yako. Nami nitakuokoa wewe pamoja na mji huu mkononi mwa mfalme wa Ashuru. Nitaulinda mji huu kwa ajili yangu, na kwa ajili ya mtumishi wangu Daudi!’ ”

7Kisha Isaya akasema, “Tengenezeni dawa ya kubandika ya tini.” Wakafanya hivyo na kuiweka kwenye jipu, naye akapona.

8Hezekia alikuwa amemuuliza Isaya, “Kutakuwa na ishara gani kwamba Bwana ataniponya mimi, na kwamba nitapanda kwenda Hekalu la Bwana siku ya tatu tangu leo?”

920:9 Kum 13:2; Yer 44:29Isaya akajibu, “Hii ndiyo ishara ya Bwana kwako kwamba Bwana atafanya kile alichoahidi: Je, kivuli kiende hatua kumi mbele, au kivuli kirudi nyuma hatua kumi?”

1020:10 2Fal 3:18Hezekia akasema, “Ni jambo rahisi kwa kivuli kutangulia mbele hatua kumi, kuliko kukifanya kirudi nyuma hatua kumi.”

1120:11 Yos 10:13; 2Nya 32:31Ndipo nabii Isaya akamwita Bwana, naye Bwana akakifanya kivuli kurudi nyuma hatua kumi ambazo kilikuwa kimeshuka kwenye ngazi ya Ahazi.

Wajumbe Kutoka Babeli

(Isaya 39:1-8)

12Wakati huo Merodaki-Baladani, mwana wa Baladani mfalme wa Babeli, akamtumia Hezekia barua na zawadi, kwa sababu alikuwa amesikia habari za kuugua kwa Hezekia. 13Hezekia akawapokea wale wajumbe na kuwaonyesha vitu vyote vile vilivyokuwa katika ghala zake: yaani fedha, dhahabu, vikolezo na mafuta safi, ghala la silaha na kila kitu kilichokuwa katika hazina zake. Hapakuwa na kitu chochote katika jumba lake la kifalme au katika ufalme wake wote ambacho Hezekia hakuwaonyesha.

14Ndipo nabii Isaya akaenda kwa Mfalme Hezekia na kumuuliza, “Watu hao walisema nini, na wametoka wapi?”

Hezekia akamjibu, “Wametoka nchi ya mbali. Walikuja kutoka Babeli.”

15Nabii akauliza, “Waliona nini katika jumba lako la kifalme?”

Hezekia akajibu, “Waliona kila kitu katika jumba langu la kifalme. Hakuna kitu chochote katika hazina yangu ambacho sikuwaonyesha.”

16Ndipo Isaya akamwambia Hezekia, “Sikia neno la Bwana: 1720:17 2Fal 24:13; Yer 52:17-23Hakika wakati unakuja ambapo vitu vyote katika jumba lako la kifalme, na vyote ambavyo baba zako waliweka akiba mpaka siku hii, vitachukuliwa kwenda Babeli. Hakuna chochote kitakachosalia, asema Bwana. 1820:18 2Fal 24:15; Mik 4:10Nao baadhi ya wazao wako, nyama yako na damu yako mwenyewe watakaozaliwa kwako, watachukuliwa mbali, nao watakuwa matowashi katika jumba la mfalme wa Babeli.”

19Hezekia akamjibu Isaya, “Neno la Bwana ulilosema ni jema.” Kwa kuwa alifikiri, “Lakini si patakuwa na amani na usalama wakati wa uhai wangu?”

20Matukio mengine ya utawala wa Hezekia, mafanikio yake yote, na jinsi alivyotengeneza bwawa na mfereji ambao ulileta maji katika mji, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda? 21Hezekia akafa, akazikwa pamoja na baba zake. Naye Manase mwanawe akawa mfalme baada yake.

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

列王纪下 20:1-21

希西迦的病危与康复

1那些天,希西迦病危,亚摩斯的儿子以赛亚先知前来对他说:“耶和华说,‘你要交待后事,因为你要死了,你的病不能康复。’” 2希西迦把脸转向墙,向耶和华祷告,说: 3“耶和华啊,求你顾念我怎样全心、忠诚地事奉你,做你视为善的事。”希西迦痛哭起来。 4当时,以赛亚还没有走出中院,耶和华对他说: 5“回去告诉我子民的首领希西迦,‘你祖先大卫的上帝耶和华说,我已听见你的祷告,看见了你的眼泪。我要医治你,三天后你就可以上耶和华的殿。 6我要使你的寿命增加十五年,我要从亚述王手中拯救你和这城。为我自己和我仆人大卫的缘故,我要保护这城。’”

7以赛亚说:“拿一块无花果饼贴在王的疮上,他就会痊愈。”

8希西迦以赛亚:“有什么兆头证明耶和华要医治我,三天后我可以上耶和华的殿呢?” 9以赛亚说:“耶和华要给你一个兆头,证明祂言出必行。你要日影前进十度还是后退十度呢?” 10希西迦说:“日影前进十度容易,让日影后退十度吧。” 11以赛亚先知向耶和华祈求,耶和华就使亚哈斯日晷上的日影后退了十度。

巴比伦的使者来访

12那时,巴拉但的儿子巴比伦米罗达·巴拉但听说希西迦病了,便派人送去书信和礼物。 13希西迦接见使者,让他们观看国库里的金银、香料、珍贵膏油、所有兵器和一切宝物。希西迦把宫中及国内的一切都给他们看。

14以赛亚先知来见希西迦王,问他:“这些人说了些什么?他们从哪里来?”希西迦答道:“他们来自遥远的巴比伦。” 15以赛亚问:“他们在你宫里看到了什么?”希西迦答道:“他们看到了我宫中的一切。我把国库里的一切都给他们看了。”

16以赛亚希西迦说:“你听着,耶和华说, 17‘终有一天,你宫中的一切和你祖先积攒到现在的一切,必一件不留地被掳到巴比伦。这是耶和华说的。 18你的子孙当中必有人被掳去,在巴比伦王的宫中做太监。’” 19希西迦以赛亚说:“耶和华借你说的话很好。”因为他想:“至少我有生之年将平安稳妥。”

20希西迦其他的事迹和成就,包括怎样建造水池和挖沟引水入城,都记在犹大的列王史上。 21希西迦与祖先同眠后,他儿子玛拿西继位。