2 Wafalme 18 – NEN & BPH

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Wafalme 18:1-37

Hezekia Mfalme Wa Yuda

(2 Nyakati 29:1–31:21)

118:1 Hos 1:1; Mik 1:1Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Hoshea mwana wa Ela mfalme wa Israeli, Hezekia mwana wa Ahazi mfalme wa Yuda alianza kutawala. 218:2 Isa 38:5Alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka ishirini na tisa. Mama yake aliitwa Abiya binti Zekaria. 318:3 1Fal 14:8; Isa 38:5Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana, kama Daudi baba yake alivyofanya. 418:4 2Nya 31:1; Hes 21:9Akapaondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu, akazivunja sanamu, akakatakata nguzo za Ashera. Akavunja vipande vipande ile nyoka ya shaba Mose aliyotengeneza, kwa kuwa hadi siku hizo wana wa Israeli walikuwa wanaifukizia uvumba (ilikuwa ikiitwa Nehushtani18:4 Nehushtani maana yake Kipande cha shaba.).

518:5 2Fal 19:10; Mit 3:26Hezekia aliweka tumaini lake kwa Bwana, Mungu wa Israeli. Hapakuwepo na mfalme mwingine wa kufanana naye miongoni mwa wafalme wa Yuda, kabla yake au baada yake. 618:6 Kum 6:18Alishikamana na Bwana kwa bidii wala hakuacha kumfuata; alishika amri ambazo Bwana alikuwa amempa Mose. 718:7 Mwa 39:3; Ezr 4:19Naye Bwana alikuwa pamoja naye, akafanikiwa katika kila alichokifanya. Aliasi dhidi ya mfalme wa Ashuru, wala hakumtumikia. 818:8 2Fal 17:9Kuanzia mnara wa ulinzi hadi kwenye mji wenye ngome, aliwashinda Wafilisti, hadi kufikia Gaza na himaya yake yote.

918:9 Isa 1:1Mwaka wa nne wa Mfalme Hezekia, ambao ulikuwa mwaka wa saba wa Hoshea mwana wa Ela kutawala Israeli, Shalmanesa mfalme wa Ashuru alikwenda kuishambulia Samaria na kuuzunguka kwa majeshi. 10Baada ya miaka mitatu Waashuru wakautwaa. Kwa hiyo Samaria ulitekwa katika mwaka wa sita wa utawala wa Mfalme Hezekia, ambao ulikuwa mwaka wa tisa wa utawala wa Hoshea mfalme wa Israeli. 1118:11 Isa 37:12; Eze 16:39Mfalme wa Ashuru akawahamishia Waisraeli huko Ashuru na akawaweka Hala, na Gozani karibu na Mto Habori, na katika miji ya Wamedi. 1218:12 Dan 9:6, 10; 1Fal 9:6Hili lilitokea kwa sababu hawakumtii Bwana Mungu wao, lakini walikuwa wamevunja agano lake, yale yote ambayo Mose mtumishi wa Bwana aliwaamuru. Hawakuzisikiliza amri wala kuzitimiza.

13Katika mwaka wa kumi na nne wa utawala wa Mfalme Hezekia, Senakeribu mfalme wa Ashuru akaishambulia miji yote ya Yuda yenye ngome na kuiteka. 1418:14 2Fal 19:8; Isa 24:5Basi Hezekia mfalme wa Yuda akamtumia ujumbe mfalme wa Ashuru huko Lakishi akisema: “Nimefanya makosa. Ondoka katika nchi yangu, nami nitakulipa chochote unachokitaka kwangu.” Mfalme wa Ashuru akamtoza Hezekia mfalme wa Yuda talanta 30018:14 Talanta 300 za fedha ni sawa na tani 10. za fedha, na talanta thelathini18:14 Talanta 30 za dhahabu ni sawa na tani moja. za dhahabu. 1518:15 1Fal 15:18; Isa 39:2Basi Hezekia akampa fedha yote iliyopatikana ndani ya Hekalu la Bwana na katika hazina ya jumba la mfalme.

16Wakati huu Hezekia mfalme wa Yuda akabandua dhahabu yote iliyokuwa imefunika milango na miimo ya Hekalu la Bwana, akampa mfalme wa Ashuru.

Senakeribu Anaitishia Yerusalemu

(2 Nyakati 32:1-19; Isaya 36:1-22)

1718:17 2Fal 20:20; Isa 20:1Mfalme wa Ashuru akamtuma jemadari wake mkuu, na afisa wake mkuu, na jemadari wa jeshi, pamoja na jeshi kubwa kutoka Lakishi hadi kwa Mfalme Hezekia huko Yerusalemu. Wakaja Yerusalemu na kusimama kwenye mfereji wa Bwawa la Juu, lililojengwa katika barabara iendayo kwenye Uwanja wa Dobi. 1818:18 2Fal 19:2; Isa 22:20Wakaagiza mfalme aitwe. Eliakimu mwana wa Hilkia aliyekuwa msimamizi wa jumba la mfalme, Shebna aliyekuwa katibu, na Yoa mwana wa Asafu mwandishi wakawaendea.

1918:19 Ay 4:6Yule jemadari wa jeshi akawaambia, “Mwambieni Hezekia:

“ ‘Hili ndilo asemalo mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru: Ni wapi unapoweka hili tumaini lako? 20Unasema mnayo mikakati na nguvu za kijeshi, lakini unasema maneno matupu tu. Je, wewe unamtegemea nani, hata ukaniasi mimi? 2118:21 Eze 29:6; Isa 30:5, 7Tazama sasa, unaitegemea Misri, fimbo ile ya mwanzi uliopasuka, ambayo huuchoma na kuujeruhi mkono wa mtu akiiegemea! Hivyo ndivyo alivyo Farao mfalme wa Misri, kwa wote wanaomtegemea. 22Nawe kama ukiniambia, “Tunamtumainia Bwana Mungu wetu”: je, siyo yeye ambaye Hezekia aliondoa mahali pake pa juu pa kuabudia miungu na madhabahu zake, akiwaambia Yuda na Yerusalemu, “Ni lazima mwabudu mbele ya madhabahu haya katika Yerusalemu”?

23“ ‘Njooni sasa, fanyeni mapatano na bwana wangu, mfalme wa Ashuru: Nitakupa farasi elfu mbili, kama unaweza kuwapandisha waendesha farasi juu yao! 2418:24 Isa 10:8Utawezaje kumzuia hata afisa mmoja aliye mdogo kati ya maafisa wa bwana wangu, ijapo unategemea Misri kwa magari ya vita na wapanda farasi? 2518:25 2Fal 19:29Zaidi ya hayo, je, nimekuja kushambulia na kuangamiza mahali hapa pasipo neno kutoka kwa Bwana? Bwana mwenyewe ndiye aliniambia niishambulie nchi hii na kuiangamiza.’ ”

2618:26 Ezr 4:7Ndipo Eliakimu mwana wa Hilkia, Shebna na Yoa wakamwambia yule jemadari wa jeshi, “Tafadhali zungumza na watumishi wako kwa lugha ya Kiaramu, kwa kuwa tunaifahamu. Usiseme nasi kwa Kiebrania watu walioko juu ya ukuta wakiwa wanasikia.”

27Lakini yule jemadari wa jeshi akajibu, “Je, bwana wangu amenituma kutoa ujumbe huu kwa bwana wenu na kwenu tu? Je, hakunituma pia kwa watu walioketi ukutani, ambao, kama ninyi, itawabidi kula mavi yao na kunywa mikojo yao wenyewe?”

28Kisha yule jemadari wa jeshi akasimama na kuita kwa lugha ya Kiebrania, akasema: “Sikieni neno la mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru! 2918:29 2Fal 19:10Hili ndilo asemalo mfalme: Msikubali Hezekia awadanganye. Hawezi kuwaokoa mkononi mwangu. 30Msikubali Hezekia awashawishi kumtumaini Bwana kwa kuwaambia, ‘Hakika Bwana atatuokoa. Mji huu hautaangukia mikononi mwa mfalme wa Ashuru.’

3118:31 Hes 13:23; Yer 14:3“Msimsikilize Hezekia. Hili ndilo mfalme wa Ashuru asemalo: Fanyeni amani nami na mje kwangu. Kisha kila mmoja wenu atakula kutoka kwa mzabibu wake na mtini wake mwenyewe, na kunywa maji kutoka kisima chake mwenyewe, 3218:32 Kum 30:19mpaka nije nikawapeleke katika nchi iliyo kama nchi yenu wenyewe, nchi ya nafaka na divai mpya, nchi ya mkate na mashamba ya mizabibu, nchi ya mizeituni na asali. Chagueni uzima, sio mauti!

“Msimsikilize Hezekia, kwa kuwa anawapotosha asemapo, ‘Bwana atatuokoa.’ 3318:33 2Fal 19:12Je, yuko mungu wa taifa lolote aliyewahi kuokoa nchi yake kutoka mkononi mwa mfalme wa Ashuru? 3418:34 2Fal 17:24; Isa 10:9Iko wapi miungu ya Hamathi na ya Arpadi? Iko wapi miungu ya Sefarvaimu, Hena na Iva? Je, imeokoa Samaria kutoka mkononi mwangu? 3518:35 Za 2:1-2Ni yupi miongoni mwa miungu yote ya nchi hizi ameweza kuokoa nchi yake mkononi mwangu? Inawezekanaje basi Bwana aiokoe Yerusalemu mkononi mwangu?”

36Lakini wale watu wakakaa kimya, wala hawakujibu lolote, kwa kuwa mfalme alikuwa amewaamuru, “Msimjibu lolote.”

3718:37 Isa 33:7; 2Fal 6:30Kisha Eliakimu mwana wa Hilkia msimamizi wa jumba la kifalme, Shebna katibu, na Yoa mwana wa Asafu, mwandishi wakamwendea Hezekia, nguo zao zikiwa zimeraruliwa, na kumwambia yale jemadari wa jeshi aliyoyasema.

Bibelen på hverdagsdansk

2. Kongebog 18:1-37

Kong Hizkija af Juda adlyder Herren

1I kong Hosea af Israels tredje regeringsår blev Hizkija, søn af Ahaz, konge i Juda. 2Han var 25 år gammel, da han blev konge, og han regerede i Jerusalem i 29 år. Hans mor hed Abi og var en datter af Zekarja.

3Hizkija gjorde, hvad der var ret i Herrens øjne, akkurat som sin forfar kong David. 4Han nedbrød offerstederne rundt omkring i landet, knuste stenstøtterne og væltede frugtbarhedspælene. Han slog tilmed den kobberslange i småstykker, som Moses i sin tid havde lavet, for Israels folk var begyndt at bringe ofre til den. De gav den navnet Nehushtan som en anden afgud. 5Hizkija havde en usædvanlig stor tillid til Herren, Israels Gud, ja, hverken før eller efter ham har der i Juda været en konge, som i den henseende kan måle sig med ham. 6Hizkija adlød Herren i alle ting, og han overholdt omhyggeligt de bud, som Herren havde givet Moses. 7Derfor var Herren med ham, og alt, hvad han gjorde, lykkedes for ham. Han gjorde oprør imod den assyriske konge ved at nægte at betale skat. 8Han besejrede også filistrene helt til Gaza og indtog mange svært befæstede byer undervejs.

9Det var i Hizkijas fjerde regeringsår, og i kong Hoseas syvende regeringsår i Israel, at kong Shalmanesar af Assyrien angreb Israel og påbegyndte belejringen af Samaria. 10To år senere, i kong Hizkijas sjette regeringsår og kong Hoseas niende regeringsår, faldt Samaria. 11Det var ved den lejlighed, at assyrerkongen deporterede israelitterne til Assyrien og anbragte dem i kolonierne i Halach og langs Haborfloden i Gozan og i de forskellige mediske byer. 12De havde nemlig nægtet at lytte til Herren, deres Gud, og gøre, hvad han havde befalet dem. De havde brudt hans pagt med dem og overtrådt de befalinger, som Herren havde givet dem gennem sin tjener Moses.

Kong Sankerib invaderer Juda

13I kong Hizkijas 14. regeringsår18,13 Ca. 701 f.Kr. i Sankeribs fjerde regeringsår. angreb assyrerkongen Sankerib alle Judas befæstede byer og indtog dem. 14Kong Hizkija sendte da en fredsdelegation fra Jerusalem med følgende budskab til assyrerkongen, der opholdt sig i Lakish: „Jeg indrømmer, at det var forkert af mig at gøre oprør. Jeg indvilliger i at betale den skat, du måtte forlange, hvis du til gengæld lover at trække dig tilbage.” Assyrerkongen forlangte 10 tons sølv og et ton guld, 15og kong Hizkija var tvunget til at tømme paladsets skatkammer og ribbe templet for sølv. 16Han skrællede endog det guld af templets døre og dørkarme, som han selv havde fået lagt på, hvorefter han gav det hele til assyrerkongen.

17Alligevel sendte assyrerkongen en stor hær af sted fra Lakish mod kong Hizkija i Jerusalem. Styrken blev anført af hærchefen, kongens næstkommanderende og chefen for livvagten. Da de nåede frem, tog de opstilling ved vejen til vaskepladsen, hvor vandledningen kommer ned fra Øvredammen. 18De forlangte, at kong Hizkija skulle komme ud og tale med dem, men han foretrak at sende en delegation, der bestod af tre mænd: hofmarskalen Eljakim, statssekretæren Shebna og rigsarkivaren Joa.

19„Assyrerkongen har sendt mig med følgende budskab, som I skal bringe videre til Hizkija,” sagde Sankeribs næstkommanderende. „Det lyder sådan: Hvad har du at bygge din selvtillid på? 20Tror du, man kan føre krig med ord? Hvem, tror du, vil hjælpe dig i oprøret mod mig? 21Er det Egypten, du støtter dig til, så pas på! For Egypten er som et knækket siv, der stikker hul i hånden på den, der støtter sig til det. Det er den hjælp, man kan forvente af Farao. 22Eller vil du sige, at det er Herren, jeres Gud, I stoler på? Er det ikke den Gud, som du hånede ved at nedrive hans templer og altre på offerhøjene og tvinge alle i Juda til kun at bringe ofre ved alteret i Jerusalem? 23Assyrerkongen vil gerne indgå et væddemål med jer: Han vil stille 2000 heste til rådighed, hvis I kan finde ryttere til dem. 24Jeres hær er så lille, at I ikke engang kan modstå et angreb fra en af mine ringeste officerer. Tror I virkelig, at egypterne vil sende deres heste og vogne for at kæmpe for jer? 25For øvrigt er det efter Herrens vilje, at jeg er kommet, for han har selv sagt, at jeg skal angribe jer og ødelægge jeres land!”

26„Vær venlig at tale til os på det aramæiske sprog,18,26 På grund af Arams og senere Assyriens storrige, blev deres aramæiske sprog stærkt udbredt i hele dette område. Det er beslægtet med israelitternes sprog, hebraisk, som her kaldes judæisk, fordi det drejer sig om indbyggerne i Judas land. for det forstår vi godt,” bad Eljakim, Shebna og Joa. „Tal ikke hebraisk, så længe alle vores folk kan høre jer.”

27„Tror I, kong Sankeribs budskab kun gælder jer og jeres konge?” svarede den assyriske næstkommanderende. „Gælder det ikke lige så meget byens indbyggere? Når vi belejrer byen, er det jo dem, der kommer til at æde deres egne ekskrementer og drikke deres egen urin.”

28Så hævede han stemmen og råbte til folkene på murene—på hebraisk: „Hør, hvad den mægtige assyriske konge har at sige til jer: 29Lad jer ikke narre af kong Hizkija! Han kan ikke frelse jer fra assyrerkongen. 30Lad ham ikke overtale jer til at stole på Herren. Hizkija siger, at Herren vil redde jer og ikke lade assyrerkongen indtage Jerusalem. 31Men det skal I ikke tro på! Hør, hvad kongen af Assyrien tilbyder jer: Overgiv jer—så skal I få lov til at bo trygt her i jeres eget land, spise jeres egne vindruer og figner og drikke vand fra jeres egne vandreservoirer, 32indtil jeg kommer og tager jer med til et sted, der ligner jeres land med masser af korn- og vinmarker og rigeligt med brød og vin, oliventræer og honning. I kan vælge mellem den mulighed og døden. Hør ikke på Hizkija, for han tager fejl, når han påstår, at Herren kan frelse jer. 33Tænk på de andre folkeslag, som assyrerkongen har besejret. Har deres guder måske kunnet redde dem? 34Hvor blev Hamats, Arpads, Sefarvajims, Henas og Ivvas guder af? Hvor var Samarias guder, da vi indtog Samaria? 35Nævn bare én gud, som har været i stand til at frelse sit folk fra assyrerkongen. Hvad får jer så til at tro, at jeres gud kan frelse Jerusalem?”

36Da assyreren havde talt færdig, var der dødstille på murene, for kongen havde forbudt dem at tage til genmæle. 37Så flængede Eljakim, Shebna og Joa deres tøj i fortvivlelse og vendte tilbage til kong Hizkija for at fortælle ham, hvad den næstkommanderende havde sagt.