2 Wafalme 18 – NEN & BDS

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Wafalme 18:1-37

Hezekia Mfalme Wa Yuda

(2 Nyakati 29:1–31:21)

118:1 Hos 1:1; Mik 1:1Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Hoshea mwana wa Ela mfalme wa Israeli, Hezekia mwana wa Ahazi mfalme wa Yuda alianza kutawala. 218:2 Isa 38:5Alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka ishirini na tisa. Mama yake aliitwa Abiya binti Zekaria. 318:3 1Fal 14:8; Isa 38:5Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana, kama Daudi baba yake alivyofanya. 418:4 2Nya 31:1; Hes 21:9Akapaondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu, akazivunja sanamu, akakatakata nguzo za Ashera. Akavunja vipande vipande ile nyoka ya shaba Mose aliyotengeneza, kwa kuwa hadi siku hizo wana wa Israeli walikuwa wanaifukizia uvumba (ilikuwa ikiitwa Nehushtani18:4 Nehushtani maana yake Kipande cha shaba.).

518:5 2Fal 19:10; Mit 3:26Hezekia aliweka tumaini lake kwa Bwana, Mungu wa Israeli. Hapakuwepo na mfalme mwingine wa kufanana naye miongoni mwa wafalme wa Yuda, kabla yake au baada yake. 618:6 Kum 6:18Alishikamana na Bwana kwa bidii wala hakuacha kumfuata; alishika amri ambazo Bwana alikuwa amempa Mose. 718:7 Mwa 39:3; Ezr 4:19Naye Bwana alikuwa pamoja naye, akafanikiwa katika kila alichokifanya. Aliasi dhidi ya mfalme wa Ashuru, wala hakumtumikia. 818:8 2Fal 17:9Kuanzia mnara wa ulinzi hadi kwenye mji wenye ngome, aliwashinda Wafilisti, hadi kufikia Gaza na himaya yake yote.

918:9 Isa 1:1Mwaka wa nne wa Mfalme Hezekia, ambao ulikuwa mwaka wa saba wa Hoshea mwana wa Ela kutawala Israeli, Shalmanesa mfalme wa Ashuru alikwenda kuishambulia Samaria na kuuzunguka kwa majeshi. 10Baada ya miaka mitatu Waashuru wakautwaa. Kwa hiyo Samaria ulitekwa katika mwaka wa sita wa utawala wa Mfalme Hezekia, ambao ulikuwa mwaka wa tisa wa utawala wa Hoshea mfalme wa Israeli. 1118:11 Isa 37:12; Eze 16:39Mfalme wa Ashuru akawahamishia Waisraeli huko Ashuru na akawaweka Hala, na Gozani karibu na Mto Habori, na katika miji ya Wamedi. 1218:12 Dan 9:6, 10; 1Fal 9:6Hili lilitokea kwa sababu hawakumtii Bwana Mungu wao, lakini walikuwa wamevunja agano lake, yale yote ambayo Mose mtumishi wa Bwana aliwaamuru. Hawakuzisikiliza amri wala kuzitimiza.

13Katika mwaka wa kumi na nne wa utawala wa Mfalme Hezekia, Senakeribu mfalme wa Ashuru akaishambulia miji yote ya Yuda yenye ngome na kuiteka. 1418:14 2Fal 19:8; Isa 24:5Basi Hezekia mfalme wa Yuda akamtumia ujumbe mfalme wa Ashuru huko Lakishi akisema: “Nimefanya makosa. Ondoka katika nchi yangu, nami nitakulipa chochote unachokitaka kwangu.” Mfalme wa Ashuru akamtoza Hezekia mfalme wa Yuda talanta 30018:14 Talanta 300 za fedha ni sawa na tani 10. za fedha, na talanta thelathini18:14 Talanta 30 za dhahabu ni sawa na tani moja. za dhahabu. 1518:15 1Fal 15:18; Isa 39:2Basi Hezekia akampa fedha yote iliyopatikana ndani ya Hekalu la Bwana na katika hazina ya jumba la mfalme.

16Wakati huu Hezekia mfalme wa Yuda akabandua dhahabu yote iliyokuwa imefunika milango na miimo ya Hekalu la Bwana, akampa mfalme wa Ashuru.

Senakeribu Anaitishia Yerusalemu

(2 Nyakati 32:1-19; Isaya 36:1-22)

1718:17 2Fal 20:20; Isa 20:1Mfalme wa Ashuru akamtuma jemadari wake mkuu, na afisa wake mkuu, na jemadari wa jeshi, pamoja na jeshi kubwa kutoka Lakishi hadi kwa Mfalme Hezekia huko Yerusalemu. Wakaja Yerusalemu na kusimama kwenye mfereji wa Bwawa la Juu, lililojengwa katika barabara iendayo kwenye Uwanja wa Dobi. 1818:18 2Fal 19:2; Isa 22:20Wakaagiza mfalme aitwe. Eliakimu mwana wa Hilkia aliyekuwa msimamizi wa jumba la mfalme, Shebna aliyekuwa katibu, na Yoa mwana wa Asafu mwandishi wakawaendea.

1918:19 Ay 4:6Yule jemadari wa jeshi akawaambia, “Mwambieni Hezekia:

“ ‘Hili ndilo asemalo mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru: Ni wapi unapoweka hili tumaini lako? 20Unasema mnayo mikakati na nguvu za kijeshi, lakini unasema maneno matupu tu. Je, wewe unamtegemea nani, hata ukaniasi mimi? 2118:21 Eze 29:6; Isa 30:5, 7Tazama sasa, unaitegemea Misri, fimbo ile ya mwanzi uliopasuka, ambayo huuchoma na kuujeruhi mkono wa mtu akiiegemea! Hivyo ndivyo alivyo Farao mfalme wa Misri, kwa wote wanaomtegemea. 22Nawe kama ukiniambia, “Tunamtumainia Bwana Mungu wetu”: je, siyo yeye ambaye Hezekia aliondoa mahali pake pa juu pa kuabudia miungu na madhabahu zake, akiwaambia Yuda na Yerusalemu, “Ni lazima mwabudu mbele ya madhabahu haya katika Yerusalemu”?

23“ ‘Njooni sasa, fanyeni mapatano na bwana wangu, mfalme wa Ashuru: Nitakupa farasi elfu mbili, kama unaweza kuwapandisha waendesha farasi juu yao! 2418:24 Isa 10:8Utawezaje kumzuia hata afisa mmoja aliye mdogo kati ya maafisa wa bwana wangu, ijapo unategemea Misri kwa magari ya vita na wapanda farasi? 2518:25 2Fal 19:29Zaidi ya hayo, je, nimekuja kushambulia na kuangamiza mahali hapa pasipo neno kutoka kwa Bwana? Bwana mwenyewe ndiye aliniambia niishambulie nchi hii na kuiangamiza.’ ”

2618:26 Ezr 4:7Ndipo Eliakimu mwana wa Hilkia, Shebna na Yoa wakamwambia yule jemadari wa jeshi, “Tafadhali zungumza na watumishi wako kwa lugha ya Kiaramu, kwa kuwa tunaifahamu. Usiseme nasi kwa Kiebrania watu walioko juu ya ukuta wakiwa wanasikia.”

27Lakini yule jemadari wa jeshi akajibu, “Je, bwana wangu amenituma kutoa ujumbe huu kwa bwana wenu na kwenu tu? Je, hakunituma pia kwa watu walioketi ukutani, ambao, kama ninyi, itawabidi kula mavi yao na kunywa mikojo yao wenyewe?”

28Kisha yule jemadari wa jeshi akasimama na kuita kwa lugha ya Kiebrania, akasema: “Sikieni neno la mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru! 2918:29 2Fal 19:10Hili ndilo asemalo mfalme: Msikubali Hezekia awadanganye. Hawezi kuwaokoa mkononi mwangu. 30Msikubali Hezekia awashawishi kumtumaini Bwana kwa kuwaambia, ‘Hakika Bwana atatuokoa. Mji huu hautaangukia mikononi mwa mfalme wa Ashuru.’

3118:31 Hes 13:23; Yer 14:3“Msimsikilize Hezekia. Hili ndilo mfalme wa Ashuru asemalo: Fanyeni amani nami na mje kwangu. Kisha kila mmoja wenu atakula kutoka kwa mzabibu wake na mtini wake mwenyewe, na kunywa maji kutoka kisima chake mwenyewe, 3218:32 Kum 30:19mpaka nije nikawapeleke katika nchi iliyo kama nchi yenu wenyewe, nchi ya nafaka na divai mpya, nchi ya mkate na mashamba ya mizabibu, nchi ya mizeituni na asali. Chagueni uzima, sio mauti!

“Msimsikilize Hezekia, kwa kuwa anawapotosha asemapo, ‘Bwana atatuokoa.’ 3318:33 2Fal 19:12Je, yuko mungu wa taifa lolote aliyewahi kuokoa nchi yake kutoka mkononi mwa mfalme wa Ashuru? 3418:34 2Fal 17:24; Isa 10:9Iko wapi miungu ya Hamathi na ya Arpadi? Iko wapi miungu ya Sefarvaimu, Hena na Iva? Je, imeokoa Samaria kutoka mkononi mwangu? 3518:35 Za 2:1-2Ni yupi miongoni mwa miungu yote ya nchi hizi ameweza kuokoa nchi yake mkononi mwangu? Inawezekanaje basi Bwana aiokoe Yerusalemu mkononi mwangu?”

36Lakini wale watu wakakaa kimya, wala hawakujibu lolote, kwa kuwa mfalme alikuwa amewaamuru, “Msimjibu lolote.”

3718:37 Isa 33:7; 2Fal 6:30Kisha Eliakimu mwana wa Hilkia msimamizi wa jumba la kifalme, Shebna katibu, na Yoa mwana wa Asafu, mwandishi wakamwendea Hezekia, nguo zao zikiwa zimeraruliwa, na kumwambia yale jemadari wa jeshi aliyoyasema.

La Bible du Semeur

2 Rois 18:1-37

Les derniers rois de Juda

Le règne d’Ezéchias sur Juda

1La troisième année du règne d’Osée, fils d’Ela, roi d’Israël, Ezéchias, fils d’Ahaz, roi de Juda, devint roi18.1 C’est-à-dire vers 728 av. J.-C. A partir de cette date et jusqu’en 715 av. J.-C., Ezéchias fut corégent avec son père Ahaz..

(2 Ch 29.1-2 ; 31.1)

2Il était âgé de vingt-cinq ans à son avènement et il régna vingt-neuf ans à Jérusalem18.2 Selon certains, de 715 à 686 av. J.-C., selon d’autres, en comptant les années de corégence, de 728 ou 727 à 698 av. J.-C.. Sa mère s’appelait Abi, elle était fille de Zacharie. 3Il fit ce que l’Eternel considère comme juste, en tout point comme l’avait fait son ancêtre David. 4Il fit disparaître les hauts lieux, briser les stèles des idoles, couper le pieu sacré de la déesse Ashéra. Il fit aussi mettre en pièces le serpent de bronze que Moïse avait fabriqué18.4 Voir Nb 21.8-9., car jusqu’à cette époque-là, les Israélites faisaient brûler des parfums pour lui et l’appelaient Nehoushtân.

(2 Ch 31.20-21)

5Ezéchias mit sa confiance en l’Eternel, le Dieu d’Israël. Parmi tous les rois de Juda qui lui succédèrent ou qui l’avaient précédé, aucun ne l’égala. 6Il demeura attaché à l’Eternel, sans se détourner de lui ; il obéit à tous les commandements que l’Eternel avait donnés à Moïse. 7Aussi l’Eternel fut-il avec lui. Il réussit dans toutes ses entreprises. Il se révolta contre le roi d’Assyrie et cessa de lui être assujetti.

8Il battit les Philistins et les poursuivit jusqu’à Gaza18.8 L’une des cinq principales villes de la Philistie., ravageant la ville et son territoire, et s’emparant des villes fortifiées aussi bien que des postes d’observation.

La prise de Samarie par les Assyriens

(2 R 17.3-7)

9Ce fut pendant la quatrième année du règne d’Ezéchias18.9 En 725 av. J.-C., la 4e année de sa corégence avec Ahaz., qui correspond à la septième année de celui d’Osée, fils d’Ela, roi d’Israël, que Salmanasar, roi d’Assyrie, vint attaquer Samarie et l’assiégea. 10Il s’en empara au bout de trois ans, la sixième année du règne d’Ezéchias, c’est-à-dire la neuvième année du règne d’Osée, roi d’Israël ; ainsi Samarie fut prise. 11Le roi d’Assyrie déporta les Israélites en Assyrie et les établit à Halah et sur les rives du Habor, dans la région de Gozân ainsi que dans les villes de la Médie. 12Ces malheurs leur arrivèrent parce qu’ils n’avaient pas obéi aux ordres de l’Eternel, leur Dieu, parce qu’ils avaient été infidèles à son alliance en désobéissant à tout ce que Moïse, le serviteur de l’Eternel, leur avait ordonné, au lieu de l’écouter et de l’appliquer.

L’invasion du royaume de Juda par les Assyriens

13La quatorzième année du règne d’Ezéchias, Sennachérib, roi d’Assyrie18.13 En 701, la 14e année du règne personnel d’Ezéchias. Sennachérib, fils de Sargon II, régna de 704 à 681 av. J.-C. A partir de ce verset et jusqu’à 20.19, le récit est parallèle, à quelques variantes près, à Es 36 à 39., vint attaquer toutes les villes fortifiées de Juda et s’en empara. 14Alors Ezéchias, roi de Juda, fit transmettre au roi d’Assyrie à Lakish18.14 Entre Jérusalem et Gaza, à quelque 35 kilomètres au sud-ouest de Jérusalem. le message suivant : J’ai commis une faute, cesse de m’attaquer. J’accepte de payer le tribut que tu m’imposeras.

Le roi d’Assyrie exigea d’Ezéchias dix tonnes d’argent et une tonne d’or. 15Ezéchias lui fit donc porter tout l’argent qui se trouvait dans le temple de l’Eternel et dans le trésor du palais royal. 16Il dut même arracher les plaques d’or dont il avait fait revêtir les portes et les linteaux du temple de l’Eternel pour les donner au roi d’Assyrie.

Le siège de Jérusalem

(2 Ch 32.9-19)

17Le roi d’Assyrie envoya de Lakish à Jérusalem vers le roi Ezéchias son général en chef, son chef d’état-major et son aide de camp, accompagnés d’une puissante armée. Lorsque les trois officiers supérieurs furent arrivés en haut de la côte près de Jérusalem, ils prirent position près de l’aqueduc du réservoir supérieur qui est sur la route du champ du Teinturier18.17 L’aqueduc est sans doute le canal souterrain qu’Ezéchias a fait creuser (20.20) pour amener l’eau de la source de Guihôn (1 R 1.33) au réservoir de Siloé, au sud-est de la ville. Le champ du Teinturier devait se trouver près d’Eyn-Roguel, au sud de Jérusalem (cf. 2 S 17.17 ; 1 R 1.9 ; Es 7.3).. 18Ils crièrent qu’ils voulaient parler au roi. Eliaqim, fils de Hilqiya, qui avait la charge du palais royal, Shebna, le secrétaire du roi et Yoah, fils d’Asaph, l’archiviste, sortirent de la ville à leur rencontre. 19L’aide de camp du roi d’Assyrie leur dit : Veuillez transmettre ce message à Ezéchias : « Voici ce que déclare le grand roi, le roi d’Assyrie : En quoi mets-tu ta confiance ? 20T’imaginerais-tu que de simples paroles peuvent tenir lieu de stratégie et de puissance militaire ? Sur qui comptes-tu donc pour t’être révolté contre moi ? 21Je le vois : tu t’appuies sur l’Egypte, ce roseau cassé qui blesse et qui transperce la main de celui qui s’appuie dessus. Oui, c’est bien là ce qu’est le pharaon, le roi d’Egypte, pour tous ceux qui se confient en lui ! 22Peut-être me direz-vous : C’est en l’Eternel, notre Dieu, que nous nous confions. Mais n’est-ce pas précisément ce Dieu dont Ezéchias a fait disparaître les hauts lieux et les autels, en disant aux habitants de Juda et de Jérusalem de rendre leur culte uniquement devant l’autel qui se trouve à Jérusalem ? 23Je te lance aujourd’hui un défi au nom de mon souverain, le roi d’Assyrie : Je te donnerai deux mille chevaux, si toi tu es capable de fournir autant d’hommes pour les monter. 24Comment t’y prendrais-tu pour repousser un seul de nos capitaines, même si c’était le moindre des serviteurs de mon maître ? Comptes-tu sur l’Egypte pour te fournir des chars avec leur équipage ? 25D’ailleurs crois-tu que c’est sans l’assentiment de l’Eternel que je suis venu attaquer ce lieu-ci pour le détruire ? C’est l’Eternel qui m’a dit : Va attaquer ce pays et détruis-le ! »

Les Assyriens demandent à la population de se rendre

26Alors Eliaqim, fils de Hilqiya, Shebna et Yoah dirent à l’aide de camp assyrien : Voudrais-tu, s’il te plaît, parler à tes serviteurs en langue araméenne18.26 Langue diplomatique parlée par les hauts fonctionnaires de l’époque. Elle deviendra la langue commune des Juifs à partir du ve siècle av. J.-C., car nous la comprenons. Ne nous parle pas en hébreu alors que les gens sont là, sur les remparts, à écouter !

27Mais l’aide de camp leur répliqua : Crois-tu que c’est à ton souverain et à toi seulement que mon souverain m’a chargé d’adresser ce message ? Crois-tu que ce n’est pas aussi à ces gens assis sur les remparts, qui seront bientôt réduits avec vous à manger leurs excréments et à boire leur urine ?

28Puis l’aide de camp se campa là et se mit à crier d’une voix forte, en hébreu : Ecoutez ce que dit le grand roi, le roi d’Assyrie ! 29Ainsi parle le roi : « Ne vous laissez pas tromper par Ezéchias ! Car il ne peut pas vous délivrer ! 30Ne vous laissez pas persuader par Ezéchias de vous confier en l’Eternel, s’il vous dit : Sûrement l’Eternel nous délivrera, cette ville ne tombera pas aux mains du roi d’Assyrie. 31N’écoutez pas Ezéchias ; car voici ce que vous propose le roi d’Assyrie : Faites la paix avec moi, rendez-vous à moi ! Alors chacun de vous mangera les fruits de sa vigne et de son figuier18.31 Expression commune caractérisant la vie paisible et prospère (1 R 5.5 ; Os 2.14 ; Mi 4.4 ; Za 3.10)., et chacun boira de l’eau de son puits, 32en attendant que je vienne vous emmener dans un pays pareil au vôtre, un pays où il y a du blé et du vin, du pain et des vignes, des oliviers, de l’huile et du miel. Ainsi vous vivrez et vous ne mourrez pas. N’écoutez donc pas Ezéchias ; il vous trompe en vous disant : L’Eternel nous délivrera.

33Les dieux des autres peuples ont-ils délivré leur pays du roi d’Assyrie ? 34Où sont les dieux de Hamath et d’Arpad ? Où sont les dieux de Sepharvaïm, de Héna et d’Ivva18.34 Villes syriennes prises par les Assyriens vers 722 av. J.-C. en même temps que Samarie. ? Ont-ils délivré Samarie ? 35De tous les dieux de ces pays, quels sont ceux qui ont délivré leur pays pour que l’Eternel délivre Jérusalem ? »

36Le peuple garda le silence et ne lui répondit pas un mot, car le roi avait donné cet ordre : Vous ne lui répondrez pas. 37Alors Eliaqim, fils de Hilqiya, qui avait la charge du palais, Shebna, le secrétaire et Yoah, fils d’Asaph, l’archiviste, retournèrent auprès d’Ezéchias, les vêtements déchirés, et lui rapportèrent les paroles de l’aide de camp.