2 Wafalme 17 – NEN & BPH

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Wafalme 17:1-41

Hoshea, Mfalme Wa Mwisho Katika Israeli

117:1 2Fal 15:30Katika mwaka wa kumi na mbili wa utawala wa Ahazi mfalme wa Yuda, Hoshea mwana wa Ela akawa mfalme wa Israeli katika Samaria, akatawala kwa miaka tisa. 217:2 Kum 4:25Akafanya maovu machoni pa Bwana, lakini si kama wafalme wengine wa Israeli waliomtangulia.

317:3 Hos 10:14; Amu 3:15Mfalme Shalmanesa wa Ashuru akainuka dhidi ya Mfalme Hoshea, ambaye hapo mbeleni alikuwa mtumwa wake na kumlipa ushuru. 417:4 Za 146:3; Hos 13:10Lakini mfalme wa Ashuru akagundua kuwa Hoshea alikuwa msaliti, kwa kuwa alikuwa ametuma wajumbe kwa So mfalme wa Misri, naye hakuendelea kulipa ushuru kwa mfalme wa Ashuru tena kama alivyokuwa anafanya kila mwaka. Kwa hiyo Shalmanesa akamkamata na kumtia gerezani. 5Mfalme wa Ashuru akaishambulia nchi yote, akapigana dhidi ya Samaria na kuizunguka kwa majeshi miaka mitatu. 617:6 2Fal 15:29; Isa 10:9Katika mwaka wa tisa wa Hoshea, mfalme wa Ashuru akaiteka Samaria na kuwahamishia Waisraeli huko Ashuru. Akawaweka huko Hala, na Gozani karibu na Mto Habori, na katika miji ya Wamedi.

Israeli Inakwenda Uhamishoni Kwa Sababu Ya Dhambi

717:7 Yos 7:11; Kut 14:15-31Yote haya yalitokea kwa sababu Waisraeli walikuwa wametenda dhambi dhidi ya Bwana Mungu wao, ambaye alikuwa amewapandisha kutoka Misri akiwatoa chini ya utawala wa nguvu wa Farao mfalme wa Misri. Waliabudu miungu mingine 817:8 Law 18:3; Kum 9:4na kufuata desturi za mataifa ambayo Bwana alikuwa ameyafukuza mbele yao, pamoja na desturi ambazo wafalme wa Israeli walizileta. 917:9 2Fal 18:8Waisraeli wakafanya vitu kwa siri dhidi ya Bwana Mungu wao, ambavyo havikuwa sawa. Kuanzia kwenye mnara wa ulinzi hadi kwenye mji wenye maboma walijijengea wenyewe mahali pa juu pa kuabudia miungu katika miji yao yote. 1017:10 Kut 34:13; Mik 5:14Wakaweka mawe ya kuabudiwa na nguzo za Ashera juu ya kila kilima kirefu na chini ya kila mti uliotanda. 11Wakafukiza uvumba kila mahali palipoinuka, kama yalivyofanya yale mataifa ambayo Bwana alikuwa ameyafukuza mbele yao. Wakafanya mambo maovu ambayo yalimghadhibisha Bwana. 1217:12 Kut 20:4Wakaabudu sanamu, ingawa Bwana alikuwa amesema, “Msifanye mambo haya.” 1317:13 1Sam 9:9; Yer 18:11; Zek 1:4Bwana akawaonya Israeli na Yuda kupitia kwa manabii na waonaji wake wote: “Acheni njia zenu mbaya. Shikeni amri na maagizo yangu, kufuatana na sheria yangu yote niliyowaagiza baba zenu kuitii ambayo niliileta kwenu kupitia kwa watumishi wangu manabii.”

1417:14 Kut 32:9; Mdo 7:15Lakini hawakusikiliza, walikuwa na shingo ngumu kama baba zao, ambao hawakumtegemea Bwana Mungu wao. 1517:15 Law 26:11; Kum 32:21Walizikataa amri zake, na agano alilokuwa amelifanya na baba zao, na maonyo aliyokuwa amewapa. Wakafuata sanamu zisizofaa, nao wenyewe wakawa hawafai. Wakayaiga mataifa yaliyowazunguka, ingawa Bwana alikuwa amewaonya akiwaambia, “Msifanye kama wanavyofanya,” nao wakafanya mambo ambayo Bwana alikuwa amewakataza wasifanye.

1617:16 Kut 32:4; Yer 2:5Wakayaacha maagizo yote ya Bwana Mungu wao na kujitengenezea sanamu mbili, walizozisubu katika sura ya ndama na nguzo ya Ashera. Wakasujudia mianga yote ya angani, na wakamtumikia Baali. 1717:17 Kum 18:10-12; Rum 7:14Wakawatoa kafara wana wao na mabinti zao katika moto. Wakafanya uaguzi na uchawi, nao wakajiuza wenyewe katika kutenda uovu machoni pa Bwana, wakamghadhibisha.

18Basi Bwana akawakasirikia sana Israeli na kuwaondoa kwenye uwepo wake. Ni kabila la Yuda tu lililobaki; 19na hata hivyo nao Yuda hawakuzishika amri za Bwana Mungu wao. Wakafuata desturi ambazo Israeli walikuwa wamezianzisha. 2017:20 2Fal 17:6Kwa hiyo Bwana aliwakataa watu wote wa Israeli; akawatesa na kuwaachia katika mikono ya wateka nyara hadi alipowaondoa kutoka kwenye uwepo wake.

2117:21 1Sam 15:27; 1Fal 12:20Alipokwisha kuwatenga Israeli mbali na nyumba ya Daudi, wakamfanya Yeroboamu mwana wa Nebati kuwa mfalme wao. Yeroboamu akawashawishi Israeli waache kumfuata Bwana na akawasababisha kutenda dhambi kuu. 22Nao Israeli wakadumu katika dhambi zote za Yeroboamu mwana wa Nebati, nao hawakuziacha 2317:23 Eze 39:23-24; Amu 6:8hadi Bwana alipowaondoa kutoka kwenye uwepo wake, kama vile alivyokuwa ameonya kupitia watumishi wake wote manabii. Hivyo watu wa Israeli wakaondolewa kutoka nchi yao kwenda uhamishoni Ashuru, nao wako huko mpaka sasa.

Samaria Inakaliwa Tena

2417:24 2Fal 18:34; Amo 6:2Mfalme wa Ashuru akawaleta watu kutoka Babeli, Kutha, Ava, Hamathi na Sefarvaimu na kuwaweka katika miji ya Samaria badala ya Waisraeli. Wakaimiliki Samaria na kuishi katika miji yake. 2517:25 Mwa 37:20; Yer 50:17Wakati walianza kuishi humo, hawakumwabudu Bwana, kwa hiyo akatuma simba miongoni mwao, wakawaua baadhi ya watu. 26Habari ikapelekwa kwa mfalme wa Ashuru, kusema: “Watu uliowahamisha na kuwaweka katika miji ya Samaria hawajui kile Mungu wa nchi hiyo anachokitaka. Ametuma simba miongoni mwao, ambao wanawaua, kwa sababu watu hawajui anachokitaka.”

27Ndipo mfalme wa Ashuru akaamuru hivi: “Mtwae mmoja wa makuhani uliowachukua mateka kutoka Samaria ili arudi kuishi humo na awafundishe watu kile ambacho Mungu wa nchi anataka.” 28Basi mmoja wa makuhani ambaye alikuwa amepelekwa uhamishoni kutoka Samaria akaja kuishi Betheli na kuwafundisha jinsi ya kumwabudu Bwana.

2917:29 Yer 2:28; Mik 4:5Hata hivyo, kila kikundi cha taifa lililoletwa Samaria kilitengeneza miungu yao wenyewe katika miji kadhaa mahali walipoishi, nao wakaiweka mahali pa ibada za miungu ambapo watu wa Samaria walikuwa wametengeneza katika mahali pa juu. 30Watu kutoka Babeli wakamtengeneza Sukoth-Benothi kuwa mungu wao, watu kutoka Kutha wakamtengeneza Nergali, na watu kutoka Hamathi wakamtengeneza Ashima; 3117:31 2Fal 17:24Waavi wakatengeneza Nibhazi na Tartaki, nao Wasefarvi wakachoma watoto wao kama kafara kwa Adrameleki na Anameleki, miungu ya Sefarvaimu. 3217:32 1Fal 12:31Walimwabudu Bwana, lakini pia waliteua aina zote za watu wao ili kuwawakilisha kama makuhani katika mahali pa kuabudia miungu kwenye mahali pa juu pa ibada. 33Walimwabudu Bwana, lakini pia waliitumikia miungu yao kulingana na desturi za mataifa walikotoka.

3417:34 Mwa 17:5; 1Fal 18:31Mpaka leo wanashikilia desturi zao za zamani. Hawamwabudu Bwana wala kuzishika hukumu na maagizo, sheria na amri ambazo Bwana aliwapa uzao wa Yakobo, ambaye alimwita Israeli. 3517:35 Kut 20:3Wakati Bwana alipofanya Agano na Waisraeli, aliwaamuru akisema: “Msiiabudu miungu mingine yoyote wala kuisujudia, wala kuitumikia wala kuitolea dhabihu. 3617:36 Kum 3:20; Za 136:12Bali imewapasa kumwabudu Bwana aliyewapandisha kutoka Misri kwa uwezo wake mkuu na kwa mkono wake ulionyooshwa. Kwake yeye mtasujudu na kwake yeye mtatoa dhabihu. 3717:37 Kum 5:32; Law 19:37Imewapasa daima kuwa waangalifu kutunza hukumu na maagizo, sheria na amri alizowaandikia. Msiabudu miungu mingine. 3817:38 Kum 6:12Msisahau agano nililofanya nanyi, wala msiabudu miungu mingine. 39Bali, mtamwabudu Bwana Mungu wenu, kwani yeye ndiye atakayewakomboa kutoka mikononi mwa adui zenu wote.”

40Hata hivyo hawakusikiliza, lakini waliendelea na desturi zao za awali. 4117:41 1Fal 18:21; Mt 6:24Hata wakati watu hawa walipokuwa wanamwabudu Bwana, walikuwa bado wakitumikia sanamu zao. Mpaka leo watoto wao na watoto wa watoto wao wanaendelea kufanya kama baba zao walivyofanya.

Bibelen på hverdagsdansk

2. Kongebog 17:1-41

Eksilet—Guds dom over Israel

1I kong Ahaz af Judas 12. regeringsår blev Hosea, Elas søn, konge i Israel. Han regerede i Samaria i ni år. 2Han gjorde, hvad der var ondt i Herrens øjne, men ikke så slemt som hans forgængere på Israels trone.

3Kong Shalmanesar af Assyrien angreb og besejrede kong Hosea, så Israel måtte betale skat til den assyriske konge. 4Men Hosea gjorde oprør imod assyrerkongen, idet han henvendte sig til kong So af Egypten og bad ham om hjælp i sit forsøg på at befri Israel fra det assyriske tyranni. Samtidig nægtede Hosea at betale skat til Assyrien. Da skatten udeblev, sendte assyrerkongen bud efter Israels konge og lod ham kaste i fængsel.

5Assyrerkongen drog derefter med sin hær til Israel og belejrede hovedstaden Samaria i tre år. 6I kong Hoseas niende regeringsår måtte byen endelig overgive sig. Israels folk blev deporteret til Assyrien og anbragt i kolonier i byen Halach, i Gozan ved Haborfloden, og i en række mediske byer.

7Nordrigets indbyggere blev sendt i eksil, fordi de dyrkede afguderne og derved syndede imod Herren, deres Gud, som havde ført dem ud af fangenskabet i Egypten. 8Anført af Israels konger begyndte de at følge de samme ugudelige skikke, som blev praktiseret af de folkeslag, som Herren havde jaget ud af landet for at give plads til sit eget folk. 9Israels folk trodsede deres Gud ved at gøre mange ting, som var forkert i Herrens øjne. De indrettede offerhøje rundt omkring i landet i både små og store byer, 10og de opstillede frugtbarhedssymboler og afgudsbilleder på alle offerhøjene og under de store træer. 11De brændte afgudsofre på højene, sådan som folkene, der boede i landet før dem, havde gjort. Alle disse onde handlinger skete i oprør mod Herren, 12for folket tilbad disse afguder på trods af, at Herren klart havde sagt, at det måtte de ikke gøre.

13Gang på gang havde Herren sendt sine profeter for at advare Israel og Juda. Budskabet var altid det samme: „Hold op med jeres afgudsdyrkelse og adlyd i stedet de love og anvisninger, som jeg gav jeres forfædre ved mine profeters medvirken.” 14Men de ville ikke høre efter. De var lige så oprørske som deres forfædre, der ikke havde tillid til, at Herren, deres Gud, ville sørge for dem. 15De forkastede hans love, den pagt han havde oprettet med deres forfædre og stentavlerne med de ti bud, som han havde givet dem. De tilbad indholdsløse afguder og endte selv i tomhed. De efterlignede de folkeslag, som Herren havde sagt, de ikke måtte efterligne. 16De lod hånt om Herrens, deres Guds, bud ved at tilbede to gudebilleder i form af guldkalve. De opstillede søjler for Ashera, og de tilbad Ba’al, foruden solen, månen og stjernerne. 17Ja, de ofrede tilmed deres egne børn som brændofre. De opsøgte okkulte medier og gjorde brug af trolddom. De solgte deres sjæl til at gøre, hvad der var ondt i Herrens øjne. På den måde gjorde de oprør imod Herren, 18og han blev meget vred på Israel og sendte dem langt væk, indtil der kun var en rest tilbage i landet, nemlig Judas stamme.

19Men også Juda nægtede at adlyde Herrens, deres Guds, bud. De fremturede i samme synd og ondskab, som Israel var begyndt på. 20Derfor forkastede Herren alle Jakobs efterkommere. Han straffede dem ved at udlevere dem til deres fjender, indtil alle var ført i landflygtighed.

21Dengang Herren rev Israels rige ud af Davidslægtens hånd, valgte de Jeroboam, Nebats søn, til konge. Det var ham, der lokkede folket til synd og indførte afgudsdyrkelsen. 22Og Israels folk fortsatte derefter ad den vej, Jeroboam havde ledt dem ind på, 23indtil det kom til det punkt, hvor Herren måtte forvise dem fra deres land, helt i overensstemmelse med profeternes advarsler. Det er baggrunden for Israels landflygtighed i Assyrien i dag.

Nybyggerne i Israel

24Assyriens konge sørgede for at forflytte store menneskemængder fra byerne Babylon, Kuta, Avva, Hamat og Sefarvajim til Samarias byer, så de kunne befolke landet i stedet for israelitterne. Således overtog assyrerne Samaria og de andre byer i Israel og bosatte sig der. 25Men fordi nybyggerne ikke fra begyndelsen tilbad Herren, sendte Herren løver iblandt dem, så mange af dem blev dræbt.

26Da skyndte de sig at sende følgende budskab til den assyriske konge: „Vi nybyggere her i Israel kender ikke landets Gud, og nu har han sendt løver iblandt os, som dræber os, fordi vi ikke tilbeder ham.”

27Assyrerkongen gav derefter ordre til, at en af de bortførte præster skulle vende tilbage til Israel og lære nybyggerne at dyrke Israels Gud. 28Da rejste en præst, som oprindelig var kommet fra Samaria, tilbage til Israel og bosatte sig i Betel med det formål at forklare, hvordan man tilbeder Herren.

29Men nybyggerne opgav ikke af den grund deres afgudsdyrkelse. Hver koloni lavede billeder af deres egne guder og opstillede dem på de offersteder, som allerede fandtes i landet. 30Folk fra Babylon dyrkede deres gud Sukkot-Benot, folk fra Kuta dyrkede Nergal, folk fra Hamat dyrkede Ashima, 31guderne Nibhaz og Tartak blev dyrket af avvijitterne, og folk fra Sefarvajim brændte endog deres børn som et udtryk for deres ærefrygt for guderne Adrammelek og Anammelek.

32Samtidig ofrede de til Herren, Israels Gud. De udnævnte deres egne præster, som skulle ofre til Herren ved de offersteder, der var indrettet på bakketoppene. 33Men de holdt fast ved deres nationale og religiøse skikke, som de havde taget med sig hjemmefra. 34Sådan er det den dag i dag. De tilbeder ikke Herren af hjertet eller adlyder de love, han gav til Jakobs efterkommere, den Jakob hvis navn blev ændret til Israel. 35-36For det var med Jakobs efterkommere Herren oprettede sin pagt, da han befalede dem aldrig at tilbede eller ofre til nogen afguder. De måtte kun tilbede Herren, der havde ført dem ud af Egypten med vældig kraft og store mirakler. 37Jakobs efterkommere skulle adlyde alle Guds love og aldrig tilbede fremmede guder. 38Gud havde sagt: „Glem aldrig den pagt, jeg her har oprettet med jer, så I dyrker andre guder. 39Tilbed Herren alene. Han alene kan frelse jer fra jeres fjender.”

40Men Israel ville ikke høre efter. De blev ved med at ofre til afguderne. 41Nybyggerne fra Babylon ofrede til Israels Gud samtidig med, at de ofrede til deres egne guder. Og sådan er det fortsat helt frem til i dag.