2 Wafalme 16 – NEN & NRT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Wafalme 16:1-20

Ahazi Mfalme Wa Yuda

(2 Nyakati 28)

116:1 Isa 1:1; Hos 1:1Katika mwaka wa kumi na saba wa utawala wa Peka mwana wa Remalia, Ahazi mwana wa Yothamu mfalme wa Yuda alianza kutawala. 2Ahazi alikuwa na miaka ishirini alipoanza kutawala, akatawala huko Yerusalemu kwa miaka kumi na sita. Tofauti na Daudi baba yake, hakufanya yaliyo mema machoni pa Bwana, Mungu wake. 316:3 Law 18:21; Kum 9:4Akaenenda katika njia za wafalme wa Israeli, na hata akamtoa mwanawe kafara katika moto, akifuata njia za machukizo za mataifa ambayo Bwana alikuwa ameyafukuza mbele ya Waisraeli. 416:4 Kum 12:2; Eze 6:13Akatoa kafara na kufukiza uvumba katika mahali pa juu pa kuabudia miungu, juu ya vilima, na chini ya kila mti uliotanda.

516:5 2Fal 15:37Kisha Resini mfalme wa Aramu na Peka mwana wa Remalia mfalme wa Israeli wakaondoka kwenda kupigana dhidi ya Yerusalemu na kumzunguka Ahazi kwa jeshi, lakini hawakuweza kumshinda. 616:6 Isa 9:12; 1Fal 9:26Wakati ule, Resini mfalme wa Aramu akaurudisha Elathi kwa Aramu kwa kuwafukuza watu wa Yuda. Kisha Waedomu wakahamia Elathi, nao wanaishi huko mpaka leo.

716:7 2Fal 15:29; Hos 10:6Ahazi akatuma wajumbe kumwambia Tiglath-Pileseri mfalme wa Ashuru kwamba, “Mimi ni mtumishi na mtumwa wako. Njoo na uniokoe kutoka mkononi mwa mfalme wa Aramu na wa mfalme wa Israeli, ambao wananishambulia.” 816:8 2Fal 12:18; 12:18Naye Ahazi akachukua fedha na dhahabu zilizopatikana ndani ya Hekalu la Bwana na katika hazina ya jumba la mfalme, na kuzituma kama zawadi kwa mfalme wa Ashuru. 916:9 Mwa 14:15; Amo 1:5Mfalme wa Ashuru akamwitikia kwa kushambulia Dameski na kuiteka. Akawahamishia wenyeji wake huko Kiri, na kumuua Resini.

1016:10 Isa 6:2Kisha Mfalme Ahazi akaenda Dameski kukutana na Tiglath-Pileseri wa Ashuru. Akaona madhabahu huko Dameski, naye akamtumia Uria kuhani mchoro wa hayo madhabahu, pamoja na maelezo ya mpango kamili wa ujenzi wake. 11Kwa hiyo Uria kuhani akajenga madhabahu kulingana na mipango yote ambayo Mfalme Ahazi alikuwa ameituma kutoka Dameski, na akamaliza ujenzi kabla ya Mfalme Ahazi kurudi. 1216:12 2Nya 26:16Mfalme aliporudi kutoka Dameski na kuona hayo madhabahu, akayasogelea na kutoa sadaka juu yake. 13Akatoa sadaka yake ya kuteketezwa na sadaka ya nafaka, akamimina sadaka ya kinywaji na kunyunyizia damu ya sadaka zake za amani juu ya hayo madhabahu. 1416:14 Kut 40:6; 1Fal 8:64Mfalme Ahazi akayaondoa madhabahu ya zamani ya shaba kutoka hapo mbele ya Hekalu la Bwana, yaliyokuwa yamesimama kati ya ingilio la Hekalu na hayo madhabahu mapya, naye akayaweka upande wa kaskazini mwa hayo madhabahu mapya.

1516:15 Kut 29:38-41Ndipo Mfalme Ahazi akatoa amri zifuatazo kwa Uria kuhani: “Juu ya hayo madhabahu kubwa mapya, toa sadaka ya asubuhi ya kuteketezwa na sadaka ya jioni ya nafaka, sadaka ya mfalme ya kuteketezwa pamoja na sadaka yake ya nafaka, sadaka ya kuteketezwa ya watu wote wa nchi, pamoja na sadaka yao ya nafaka na sadaka yao ya kinywaji. Unyunyize juu ya hayo madhabahu damu yote ya sadaka za kuteketezwa na dhabihu. Lakini mimi nitatumia hayo madhabahu ya zamani ya shaba kwa ajili ya kutafuta uongozi.” 16Naye Uria kuhani akafanya kama Mfalme Ahazi alivyoagiza.

1716:17 1Fal 7:27Mfalme Ahazi akaondoa mbao za pembeni na kuondoa masinia kwenye vile vishikilio vilivyohamishika. Akaondoa ile Bahari kutoka kwenye mafahali wa shaba walioishikilia, na kuiweka kwenye kitako cha jiwe. 1816:18 Eze 16:28Kwa heshima ya mfalme wa Ashuru, akaliondoa pia pazia la Sabato lililokuwa limewekwa ndani ya Hekalu, na akaondoa ile njia ya kifalme ya kuingia kwenye Hekalu la Bwana.

19Matukio mengine ya utawala wa Ahazi na yale aliyoyafanya, je hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda? 2016:20 Isa 14:28Ahazi akalala na baba zake, naye akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi. Naye Hezekia mwanawe akawa mfalme baada yake.

New Russian Translation

4 Царств 16:1-20

Ахаз – царь Иудеи

(2 Пар. 28:1-4)

1На семнадцатом году правления Пекаха, сына Ремалии, в Иудее начал царствовать Ахаз, сын Иотама. 2Ахазу было двадцать лет, когда он стал царем, и правил он в Иерусалиме шестнадцать лет. В отличие от своего предка Давида, он не делал того, что было правильным в глазах Господа, его Бога. 3Он ходил путями царей Израиля и даже принес сына в огненную жертву по омерзительному примеру народов, которых Господь прогнал перед израильтянами. 4Он приносил жертвы и возжигал благовония в святилищах на возвышенностях, на вершинах холмов и под каждым тенистым деревом.

Ахаз просит защиты у ассирийцев

(2 Пар. 28:5-8, 16-21)

5Тогда Рецин, царь Арама, и Пеках, сын Ремалии, царь Израиля, пошли войной на Иерусалим и держали Ахаза в осаде, но не смогли его одолеть. 6В то время Рецин, царь Арама, вернул Араму Элат, прогнав оттуда иудеев. В Элате поселились арамеи, которые и живут там до сегодняшнего дня.

7Ахаз отправил послов сказать Тиглатпаласару, царю Ассирии:

– Я твой слуга и вассал16:7 Букв.: «сын».. Приди и защити меня от царя Арама и от царя Израиля, которые напали на меня.

8Ахаз взял золото и серебро, сколько нашлось в доме Господа и в сокровищницах царского дворца, и послал их в дар царю Ассирии. 9Царь Ассирии исполнил его просьбу, напав на Дамаск и взяв его. Он увел его жителей в плен в Кир, а Рецина предал смерти.

Ахаз перестраивает храм

(2 Пар. 28:23-25)

10Тогда царь Ахаз отправился в Дамаск, чтобы встретиться с Тиглатпаласаром, царем Ассирии. Он увидел в Дамаске жертвенник и послал священнику Урии изображение жертвенника и подробные указания, как его соорудить. 11Священник Урия построил жертвенник по всем указаниям, что прислал из Дамаска царь Ахаз, и завершил его прежде, чем царь Ахаз вернулся. 12Вернувшись из Дамаска и осмотрев жертвенник, царь приблизился к нему и совершил на нем приношения16:12 Или: «и поднялся на него».. 13Он сжег всесожжения и хлебные приношения, совершил жертвенные возлияния и окропил жертвенник кровью жертв примирения. 14Бронзовый жертвенник, который стоял перед Господом, он передвинул с места перед домом – между новым жертвенником и домом Господа – и поставил его с северной стороны нового жертвенника. 15Затем царь Ахаз приказал священнику Урии:

– На большом новом жертвеннике приноси утренние всесожжения и вечерние хлебные приношения, царские всесожжения и его хлебные приношения, всесожжения всего народа страны и их хлебные приношения с жертвенными возлияниями. Кропи жертвенник всей кровью всесожжений и жертв. Но бронзовым жертвенником я буду пользоваться для того, чтобы узнать Божью16:15 Для того, чтобы узнать Божью волю – или: «для гадания». волю.

16И священник Урия сделал все точно так, как приказал царь Ахаз. 17Царь Ахаз отломил ободки у передвижных подставок и снял с них умывальницы. Он снял море16:17 Море – это большой бронзовый бассейн, находившийся во дворе храма и предназначавшийся для ритуальных омовений священников (см. 3 Цар. 7:23-26; 2 Пар. 4:6). с бронзовых волов, которые его поддерживали, и поставил его на каменное основание. 18Крытый субботний проход, который был построен во дворце, и внешний царский вход он убрал от дома Господа ради царя Ассирии.

Смерть Ахаза

(2 Пар. 28:26-27)

19Что же до прочих событий правления Ахаза и того, что он сделал, то разве они не записаны в «Книге летописей царей Иудеи»? 20Ахаз упокоился со своими предками и был похоронен с ними в Городе Давида. А Езекия, его сын, стал царем вместо него.