2 Wafalme 13 – NEN & CARS

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Wafalme 13:1-25

Yehoahazi Mfalme Wa Israeli

1Katika mwaka wa ishirini na tatu wa utawala wa Yoashi mwana wa Ahazia mfalme wa Yuda, Yehoahazi mwana wa Yehu alianza kutawala Israeli katika Samaria, naye akatawala miaka kumi na saba. 213:2 1Fal 12:26-33Akafanya maovu machoni pa Bwana kwa kufuata dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda, na wala hakuziacha. 3Kwa hiyo hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya Israeli na kwa muda mrefu akawaweka chini ya utawala wa Hazaeli mfalme wa Aramu, na Ben-Hadadi mwanawe.

413:4 Kum 4:29; Hes 10:9Ndipo Yehoahazi akamsihi Bwana rehema, naye Bwana akamsikiliza, kwa maana aliona jinsi mfalme wa Aramu alivyokuwa akiwatesa Israeli vikali. 513:5 Mwa 45:7; Amu 2:18Bwana akamtoa mwokozi kwa ajili ya Israeli, nao wakaokoka kutoka kwenye mamlaka ya Aramu. Hivyo Waisraeli wakaishi katika nyumba zao wenyewe kama ilivyokuwa hapo awali. 613:6 1Fal 16:33Lakini hawakuziacha dhambi za nyumba ya Yeroboamu, ambazo alisababisha Israeli kuzitenda, bali wakaendelea kuzitenda. Nguzo ya Ashera pia iliendelea kusimama katika Samaria.

713:7 2Sam 22:43Hapakubaki kitu chochote katika jeshi la Yehoahazi isipokuwa wapanda farasi hamsini, magari kumi ya vita na askari wa miguu elfu kumi, kwa kuwa mfalme wa Aramu alikuwa amewaangamiza hao wengine na kuwafanya kama mavumbi wakati wa kupura nafaka.

8Matukio mengine ya utawala wa Yehoahazi yote aliyoyafanya na mafanikio yake, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli? 9Yehoahazi akalala pamoja na baba zake, akazikwa huko Samaria. Naye Yehoashi13:9 Yehoashi ni namna nyingine ya kutaja jina la Yoashi. mwanawe akawa mfalme baada yake.

Yehoashi Mfalme Wa Israeli

10Katika mwaka wa thelathini na saba wa utawala wa Yoashi mfalme wa Yuda, Yehoashi mwana wa Yehoahazi alianza kutawala Israeli huko Samaria, naye akatawala miaka kumi na sita. 11Alifanya maovu machoni pa Bwana, na hakuacha dhambi yoyote kati ya zile za Yeroboamu mwana wa Nebati ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda, bali aliendelea kuzitenda.

1213:12 2Fal 14:15Na kwa matukio mengine ya utawala wa Yehoashi, yote aliyoyafanya na mafanikio yake, pamoja na vita yake dhidi ya Amazia mfalme wa Yuda, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli? 1313:13 2Fal 14:23; Hos 1:1Yehoashi akalala pamoja na baba zake, akazikwa Samaria pamoja na wafalme wa Israeli. Yeroboamu akawa mfalme baada yake.

1413:14 2Fal 2:12Wakati huu, Elisha alikuwa anaumwa na ugonjwa ambao baadaye ulimuua. Yehoashi mfalme wa Israeli akashuka kwenda kumwona na kumlilia. Akalia, “Baba yangu! Baba yangu! Magari ya vita ya Israeli na wapanda farasi wake!”

15Elisha akasema, “Leta upinde na baadhi ya mishale,” naye mfalme akafanya hivyo. 16Elisha akamwambia mfalme wa Israeli, “Shika upinde mikononi mwako.” Alipokwisha kuichukua, Elisha akaweka mikono yake juu ya mikono ya mfalme.

1713:17 Yos 8:18; 1Fal 20:26Elisha akasema, “Fungua dirisha la mashariki,” naye akalifungua. Elisha akasema, “Piga mshale!” Naye akapiga mshale. Elisha akasema, “Mshale wa ushindi wa Bwana, mshale wa ushindi juu ya Aramu! Utawaangamiza Waaramu kabisa huko Afeki.” 18Kisha akasema, “Chukua mishale,” naye mfalme akaichukua. Elisha akamwambia, “Piga ardhi kwa hiyo mishale.” Akaipiga mara tatu, halafu akaacha.

1913:19 2Fal 13:25Mtu wa Mungu akamkasirikia na akasema, “Ungepiga chini mara tano au sita, ndipo ungeishinda Aramu na kuiangamiza kabisa. Lakini sasa utaishinda mara tatu tu.”

2013:20 2Fal 5:2Elisha akafa, nao wakamzika.

Vikosi vya Wamoabu vilikuwa vinashambulia nchi kwa vita kila mwaka wakati wa vuli. 2113:21 Mt 27:52Ikawa Waisraeli fulani walipokuwa wanamzika mtu, ghafula wakaona kikosi cha washambuliaji, basi wakaitupa ile maiti ya yule mtu ndani ya kaburi la Elisha. Wakati ile maiti ilipogusa mifupa ya Elisha, yule mtu akafufuka na kusimama kwa miguu yake.

2213:22 1Fal 19:17Hazaeli mfalme wa Aramu aliwatesa Israeli wakati wote wa utawala wa Yehoahazi. 2313:23 Kut 2:24; Kum 29:20Lakini Bwana akawarehemu na akawahurumia, akaonyesha kujishughulisha nao kwa sababu ya Agano lake na Abrahamu, Isaki na Yakobo. Hadi leo, hajawaangamiza wala kuwafukuza mbele zake.

2413:24 2Fal 13:3Hazaeli mfalme wa Shamu akafa, naye Ben-Hadadi mwanawe akawa mfalme baada yake. 2513:25 2Fal 10:32Kisha Yehoashi mwana wa Yehoahazi akateka tena kutoka kwa Ben-Hadadi mwana wa Hazaeli ile miji aliyokuwa ameitwaa kwa vita kutoka kwa baba yake Yehoahazi. Yehoashi alimshinda mara tatu, hivyo akaweza kuiteka tena ile miji ya Waisraeli.

Священное Писание

4 Царств 13:1-25

Иоахаз – царь Исраила

1На двадцать третьем году правления иудейского царя Иоаша, сына Охозии, царём Исраила стал Иоахаз, сын Иеву, и правил в Самарии семнадцать лет. 2Он делал зло в глазах Вечного, следуя грехам Иеровоама, сына Невата, к которым тот склонил Исраил, и не отворачивался от них. 3Гнев Вечного вспыхнул на Исраил, и долгое время Он держал их во власти Хазаила, царя Сирии, и его сына Бен-Адада13:3 Это Бен-Адад III, правивший Сирией в начале VIII в. до н. э..

4Но Иоахаз взмолился Вечному, и Вечный услышал его, ведь Он видел, как жестоко царь Сирии притесняет Исраил. 5Вечный дал Исраилу избавителя, и Исраил вышел из-под власти Сирии. Исраильтяне стали жить в мире, как и прежде. 6И всё же они не отвернулись от грехов дома Иеровоама, к которым тот склонил Исраил, но оставались в них. Да и столб Ашеры13:6 Столб Ашеры – культовый символ вавилонско-ханаанской богини Ашеры. Ашера считалась матерью богов и людей, владычицей моря и всего сущего. продолжал стоять в Самарии.

7От войска Иоахаза не осталось ничего, кроме пятидесяти всадников, десяти колесниц и десяти тысяч пеших воинов, потому что царь Сирии истребил остальных, уподобив их пыли во время молотьбы.

8Прочие события царствования Иоахаза, всё, что он сделал, и его свершения записаны в «Книге летописей царей Исраила». 9Иоахаз упокоился со своими предками и был похоронен в Самарии. И царём вместо него стал его сын Иоаш.

Иоаш – царь Исраила

10На тридцать седьмом году правления Иоаша, царя Иудеи, царём Исраила стал Иоаш, сын Иоахаза, и правил в Самарии шестнадцать лет. 11Он делал зло в глазах Вечного и не отвернулся ни от одного из грехов Иеровоама, сына Невата, к которым тот склонил Исраил. Он оставался в них.

12Прочие события царствования Иоаша, всё, что он сделал, и его свершения, включая войну против Амасии, царя Иудеи, записаны в «Книге летописей царей Исраила».

13Иоаш упокоился со своими предками, и Иеровоам сменил его на престоле. Иоаш был похоронен в Самарии с царями Исраила.

Смерть Елисея

14Елисей был смертельно болен. Иоаш, царь Исраила, пришёл навестить его и плакал над ним.

– Отец мой! Отец мой! – восклицал он. – Колесница и конница Исраила!

15Елисей сказал:

– Достань лук и стрелы, – и он сделал это.

16– Возьми лук в руки, – сказал он царю Исраила.

Когда тот взял лук, Елисей положил руки на руки царя Исраила.

17– Открой восточное окно, – сказал он, и тот открыл его.

– Стреляй! – сказал Елисей, и тот выстрелил.

– Стрела победы Вечного, стрела победы над Сирией! – сказал Елисей. – Ты будешь бить сирийцев при городе Афеке, пока не разобьёшь их.

18Затем он сказал:

– Возьми стрелы, – и царь взял их.

Елисей сказал ему:

– Бей ими по земле.

Он ударил три раза и остановился.

19Пророк разгневался на него и сказал:

– Ты должен был бы ударить по земле пять или шесть раз, тогда ты побил бы Сирию полностью. А теперь ты разобьёшь её только три раза.

20Елисей умер и был похоронен.

Позже разбойники из Моава повадились вторгаться в страну каждую весну. 21Однажды во время похорон одного человека исраильтяне увидели банду разбойников и бросили покойника в гробницу Елисея. Когда мёртвое тело коснулось костей Елисея, тот человек ожил и встал на ноги.

Исполнение последнего пророчества Елисея

22Хазаил, царь Сирии, притеснял Исраил во все дни царствования Иоахаза. 23Но Вечный был милостив к ним, жалел их и заботился о них ради священного соглашения с Ибрахимом, Исхаком и Якубом. Он и теперь не хотел истребить их или прогнать от Себя.

24Хазаил, царь Сирии, умер, и его сын Бен-Адад стал царём вместо него. 25И Иоаш, сын Иоахаза, отнял у Бен-Адада, сына Хазаила, те города, которые тот отвоевал у его отца Иоахаза. Три раза Иоаш разбивал его и возвращал исраильские города.