2 Wafalme 11 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Wafalme 11:1-21

Athalia Na Yoashi

(2 Nyakati 22:10–23:21)

111:1 2Fal 8:18Wakati Athalia mamaye Ahazia alipoona kuwa mwanawe amekufa, akainuka na kuiangamiza jamaa yote ya mfalme. 211:2 2Fal 12:1Lakini Yehosheba, binti wa Mfalme Yehoramu, aliyekuwa pia dada yake Ahazia, akamtwaa Yoashi mwana wa Ahazia kwa siri kutoka miongoni mwa wana wa mfalme waliokuwa karibu kuuawa. Akamweka Yoashi pamoja na yaya wake ndani ya chumba cha kulala na kumficha humo ili Athalia asimwone; kwa hiyo hakuuawa. 3Alibaki amefichwa pamoja na yaya wake katika Hekalu la Bwana kwa muda wa miaka sita wakati Athalia alikuwa akitawala nchi.

411:4 2Fal 11:19Katika mwaka wa saba, Yehoyada akatumania wakuu wa vikundi vya mamia, na Wakari,11:4 Yaani Wakerethi (ona 1Sam 30:14; Eze 25:16; Sef 2:5, 6). na walinzi, nao wakaletwa kwake katika Hekalu la Bwana. Alifanya agano nao na kuwaapisha katika Hekalu la Bwana. Ndipo akawaonyesha mwana wa mfalme. 511:5 1Nya 9:25Akawaamuru akisema, “Hivi ndivyo iwapasavyo kufanya: Ninyi ambao mko makundi matatu mnaoingia zamu siku ya Sabato, theluthi yenu inayolinda jumba la kifalme, 6theluthi nyingine Lango la Suri, na theluthi nyingine lango lililo nyuma ya walinzi, ambao hupeana zamu kulinda Hekalu, 7nanyi ambao mko katika makundi mengine mawili ambao kwa kawaida hupumzika Sabato, wote mtalinda Hekalu kwa ajili ya mfalme. 8Jipangeni kumzunguka mfalme, kila mtu akiwa na silaha yake mkononi. Yeyote anayesogelea safu zenu lazima auawe. Kaeni karibu na mfalme popote aendapo.”

9Wakuu wa vikosi vya mamia wakafanya kama vile kuhani Yehoyada aliagiza. Kila mmoja akawachukua watu wake, wale waliokuwa wakiingia zamu siku ya Sabato na wale waliokuwa wakienda mapumziko, nao wakaja kwa kuhani Yehoyada. 1011:10 2Sam 8:7Ndipo akawapa wale wakuu mikuki na ngao zilizokuwa za Mfalme Daudi, zilizokuwa ndani ya Hekalu la Bwana. 11Wale walinzi, kila mmoja akiwa na silaha yake mkononi mwake, wakajipanga kumzunguka mfalme, karibu na madhabahu na Hekalu, kuanzia upande wa kusini hadi upande wa kaskazini mwa Hekalu.

1211:12 Kut 25:16; 1Sam 10:24; Isa 55:12Yehoyada akamtoa mwana wa mfalme na kumvika taji, akampa nakala ya agano, na kumtangaza kuwa mfalme. Wakamtia mafuta, nao watu wakapiga makofi na kupaza sauti, wakisema, “Mfalme aishi maisha marefu!”

13Athalia aliposikia kelele iliyofanywa na walinzi pamoja na watu, akawaendea watu pale penye Hekalu la Bwana. 1411:14 1Fal 1:39; Mwa 37:29; 2Fal 9:23Akaangalia, na tazama alikuwako mfalme, akiwa amesimama karibu na nguzo, kama ilivyokuwa desturi. Maafisa na wapiga tarumbeta walikuwa pembeni mwa mfalme, nao watu wote wa nchi walikuwa wakifurahi na kupiga tarumbeta. Ndipo Athalia akararua mavazi yake na kulia, “Uhaini! Uhaini!”

15Kuhani Yehoyada akawaagiza majemadari wa vikosi vya mamia, waliokuwa viongozi wa jeshi, “Mleteni nje kati ya safu, na mkamuue kwa upanga yeyote anayemfuata.” Kwa kuwa kuhani alikuwa amesema, “Hatauawa ndani ya Hekalu la Bwana.” 16Basi wakamkamata Athalia, na alipofika mahali ambapo farasi huingilia katika viwanja vya jumba la mfalme, wakamuulia hapo.

1711:17 Kut 24:8; Yer 34:8Kisha Yehoyada akafanya agano kati ya Bwana na mfalme na watu kwamba watakuwa watu wa Bwana. Akafanya pia agano kati ya mfalme na watu. 1811:18 Kum 12:3; 1Fal 18:40; 2Fal 10:25Watu wote wa nchi wakaenda kwenye hekalu la Baali na kulibomoa. Wakavunjavunja madhabahu na sanamu, na kumuua Matani kuhani wa Baali mbele ya hayo madhabahu.

Kisha Yehoyada kuhani akawaweka walinzi kwenye Hekalu la Bwana. 1911:19 2Fal 11:4Pamoja naye akawachukua majemadari wa mamia, Wakari, walinzi na watu wote wa nchi, nao kwa pamoja wakamteremsha mfalme kutoka Hekalu la Bwana na kwenda kwenye jumba la mfalme, wakiingilia njia ya lango la walinzi. Ndipo mfalme akachukua nafasi yake kwenye kiti cha enzi, 2011:20 Mit 11:10nao watu wote wa nchi wakafurahi. Mji ukatulia, kwa sababu Athalia alikuwa ameuawa kwa upanga nyumbani kwa mfalme.

21Yoashi alikuwa na umri wa miaka saba alipoanza kutawala.

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

列王纪下 11:1-21

耶何耶大立约阿施为王

1亚哈谢的母亲亚她利雅见儿子死了,便决定除掉王室后裔。 2约兰王的女儿、亚哈谢的妹妹约示芭把亚哈谢的儿子约阿施从被杀的王子中偷出来,将他和乳母藏在一间卧室里,才躲过亚她利雅,使约阿施没有被杀。 3约阿施和他的乳母在耶和华的殿里藏了六年,那时亚她利雅篡位当政。

4第七年,耶何耶大派人召迦利11:4 迦利人”指雇来保护王的外族卫兵。和卫兵的百夫长们到耶和华的殿里,与他们立约,让他们在耶和华的殿里起誓,然后把约阿施王子带到他们面前。 5耶何耶大吩咐他们说:“你们在安息日值班的,三分之一要守卫王宫, 6三分之一要守卫苏珥门,三分之一要守住卫兵院后门。你们要轮流守卫。 7安息日没有值班的两队要在耶和华的殿里保护王, 8各人要手持兵器护卫在王周围。凡擅自闯入者,都要处死。无论王去哪里,你们都要紧随左右。” 9众百夫长依令而行,各自率领安息日值班和休班的随从来见耶何耶大10耶何耶大把耶和华殿中大卫王的矛枪和盾牌交给百夫长。 11从殿右到殿左,在祭坛和殿周围,卫兵都手持兵器护卫王。 12耶何耶大祭司领王子出来,给他戴上王冠,把律法书交给他,膏立他为王。众人都鼓掌高呼:“愿王万岁!”

13亚她利雅听见卫兵和众人的欢呼声,便走进耶和华的殿,众人都聚集在那里。 14她看见王照例站在柱旁,百夫长和吹号的人侍立在王左右,众人都欢呼吹号,便撕裂衣服喊叫:“反了!反了!” 15耶何耶大祭司认为不可在耶和华的殿里处死亚她利雅,便命令领兵的百夫长:“把她带出去。凡跟随她的,都要杀掉。” 16他们抓住她,把她带到马匹进出王宫的入口,在那里杀了她。

17耶何耶大让王及民众与耶和华立约,做耶和华的子民,也让王与民众立约。 18于是,民众出去拆毁了巴力庙,砸碎祭坛和偶像,在坛前杀了巴力的祭司玛坦耶何耶大派守卫保护耶和华的殿, 19然后率领百夫长、迦利人、卫兵和民众,护送王从耶和华的殿下来,经过卫兵院的门进入王宫。这样,约阿施坐上了王位。 20民众都欢喜快乐,城里安定,因为亚她利雅已在王宫那里被处死。 21约阿施七岁登基。