2 Wafalme 11 – NEN & CARSA

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Wafalme 11:1-21

Athalia Na Yoashi

(2 Nyakati 22:10–23:21)

111:1 2Fal 8:18Wakati Athalia mamaye Ahazia alipoona kuwa mwanawe amekufa, akainuka na kuiangamiza jamaa yote ya mfalme. 211:2 2Fal 12:1Lakini Yehosheba, binti wa Mfalme Yehoramu, aliyekuwa pia dada yake Ahazia, akamtwaa Yoashi mwana wa Ahazia kwa siri kutoka miongoni mwa wana wa mfalme waliokuwa karibu kuuawa. Akamweka Yoashi pamoja na yaya wake ndani ya chumba cha kulala na kumficha humo ili Athalia asimwone; kwa hiyo hakuuawa. 3Alibaki amefichwa pamoja na yaya wake katika Hekalu la Bwana kwa muda wa miaka sita wakati Athalia alikuwa akitawala nchi.

411:4 2Fal 11:19Katika mwaka wa saba, Yehoyada akatumania wakuu wa vikundi vya mamia, na Wakari,11:4 Yaani Wakerethi (ona 1Sam 30:14; Eze 25:16; Sef 2:5, 6). na walinzi, nao wakaletwa kwake katika Hekalu la Bwana. Alifanya agano nao na kuwaapisha katika Hekalu la Bwana. Ndipo akawaonyesha mwana wa mfalme. 511:5 1Nya 9:25Akawaamuru akisema, “Hivi ndivyo iwapasavyo kufanya: Ninyi ambao mko makundi matatu mnaoingia zamu siku ya Sabato, theluthi yenu inayolinda jumba la kifalme, 6theluthi nyingine Lango la Suri, na theluthi nyingine lango lililo nyuma ya walinzi, ambao hupeana zamu kulinda Hekalu, 7nanyi ambao mko katika makundi mengine mawili ambao kwa kawaida hupumzika Sabato, wote mtalinda Hekalu kwa ajili ya mfalme. 8Jipangeni kumzunguka mfalme, kila mtu akiwa na silaha yake mkononi. Yeyote anayesogelea safu zenu lazima auawe. Kaeni karibu na mfalme popote aendapo.”

9Wakuu wa vikosi vya mamia wakafanya kama vile kuhani Yehoyada aliagiza. Kila mmoja akawachukua watu wake, wale waliokuwa wakiingia zamu siku ya Sabato na wale waliokuwa wakienda mapumziko, nao wakaja kwa kuhani Yehoyada. 1011:10 2Sam 8:7Ndipo akawapa wale wakuu mikuki na ngao zilizokuwa za Mfalme Daudi, zilizokuwa ndani ya Hekalu la Bwana. 11Wale walinzi, kila mmoja akiwa na silaha yake mkononi mwake, wakajipanga kumzunguka mfalme, karibu na madhabahu na Hekalu, kuanzia upande wa kusini hadi upande wa kaskazini mwa Hekalu.

1211:12 Kut 25:16; 1Sam 10:24; Isa 55:12Yehoyada akamtoa mwana wa mfalme na kumvika taji, akampa nakala ya agano, na kumtangaza kuwa mfalme. Wakamtia mafuta, nao watu wakapiga makofi na kupaza sauti, wakisema, “Mfalme aishi maisha marefu!”

13Athalia aliposikia kelele iliyofanywa na walinzi pamoja na watu, akawaendea watu pale penye Hekalu la Bwana. 1411:14 1Fal 1:39; Mwa 37:29; 2Fal 9:23Akaangalia, na tazama alikuwako mfalme, akiwa amesimama karibu na nguzo, kama ilivyokuwa desturi. Maafisa na wapiga tarumbeta walikuwa pembeni mwa mfalme, nao watu wote wa nchi walikuwa wakifurahi na kupiga tarumbeta. Ndipo Athalia akararua mavazi yake na kulia, “Uhaini! Uhaini!”

15Kuhani Yehoyada akawaagiza majemadari wa vikosi vya mamia, waliokuwa viongozi wa jeshi, “Mleteni nje kati ya safu, na mkamuue kwa upanga yeyote anayemfuata.” Kwa kuwa kuhani alikuwa amesema, “Hatauawa ndani ya Hekalu la Bwana.” 16Basi wakamkamata Athalia, na alipofika mahali ambapo farasi huingilia katika viwanja vya jumba la mfalme, wakamuulia hapo.

1711:17 Kut 24:8; Yer 34:8Kisha Yehoyada akafanya agano kati ya Bwana na mfalme na watu kwamba watakuwa watu wa Bwana. Akafanya pia agano kati ya mfalme na watu. 1811:18 Kum 12:3; 1Fal 18:40; 2Fal 10:25Watu wote wa nchi wakaenda kwenye hekalu la Baali na kulibomoa. Wakavunjavunja madhabahu na sanamu, na kumuua Matani kuhani wa Baali mbele ya hayo madhabahu.

Kisha Yehoyada kuhani akawaweka walinzi kwenye Hekalu la Bwana. 1911:19 2Fal 11:4Pamoja naye akawachukua majemadari wa mamia, Wakari, walinzi na watu wote wa nchi, nao kwa pamoja wakamteremsha mfalme kutoka Hekalu la Bwana na kwenda kwenye jumba la mfalme, wakiingilia njia ya lango la walinzi. Ndipo mfalme akachukua nafasi yake kwenye kiti cha enzi, 2011:20 Mit 11:10nao watu wote wa nchi wakafurahi. Mji ukatulia, kwa sababu Athalia alikuwa ameuawa kwa upanga nyumbani kwa mfalme.

21Yoashi alikuwa na umri wa miaka saba alipoanza kutawala.

Священное Писание (Восточный перевод), версия с «Аллахом»

4 Царств 11:1-21

Попытка Аталии истребить дом Давуда

(2 Лет. 22:10-12)

1Когда Аталия, мать Охозии, увидела, что её сын мёртв, она встала и убила всю царскую семью. 2Но Иехошева, дочь царя Иорама и сестра Охозии, взяла Иоаша, сына Охозии, выкрала его из среды царских сыновей, которых должны были убить, и спрятала его вместе с кормилицей в спальне. Так она укрыла ребёнка от Аталии, и он не был убит. 3Он прятался с кормилицей в храме Вечного шесть лет, пока Аталия правила страной.

Восстание против Аталии

(2 Лет. 23:1-21)

4На седьмом году правления Аталии священнослужитель Иодай послал за сотниками из царской охраны и дворцовой стражи, чтобы их привели к нему в храм Вечного. Он заключил с ними союз, взял с них клятву в храме Вечного и показал им царского сына. 5Он приказал им:

– Вот что вы должны сделать: треть из вас, кто заступает на службу в субботу, будет стеречь царский дворец, 6вторая треть – ворота Сур и последняя треть – ворота, что за дворцовыми стражниками. Вы никого не должны подпускать к храму. 7А два ваших подразделения, что обычно уходят со службы в субботу, должны остаться при храме Вечного охранять царя. 8Встаньте вокруг царя, каждый с оружием в руках, и убивайте всякого, кто подойдёт к вашим рядам. Будьте при царе, куда бы он ни пошёл.

9Сотники сделали всё так, как приказал священнослужитель Иодай. Каждый взял своих людей – и тех, кто заступал на службу в ту субботу, и тех, кто в ту субботу уходил со службы, – и пришёл к священнослужителю Иодаю. 10Он раздал сотникам копья и щиты, которые некогда принадлежали царю Давуду и находились в храме Вечного. 11Стражи с оружием в руках встали вокруг царя – от южной стороны храма до северной, вокруг жертвенника и храма.

12Иодай вывел сына царя, возложил на него корону, дал ему копию Закона и провозгласил его царём. Его помазали, и народ рукоплескал и кричал:

– Да здравствует царь!

13Услышав шум стражи и народа, Аталия отправилась к ним в храм Вечного. 14Она посмотрела и увидела: у колонны, как велит обычай, стоял царь! Возле него были начальники отрядов и трубачи, и весь народ страны ликовал и трубил в трубы. Аталия разорвала на себе одежду и закричала:

– Заговор! Заговор!

15Священнослужитель Иодай приказал сотникам, которые распоряжались войском:

– Выведите её за пределы храма и убейте мечом всякого, кто за ней пойдёт.

(Потому что священнослужитель сказал: «Её нельзя предавать смерти в храме Вечного».)

16Её схватили и повели к царскому дворцу через вход, которым водят коней, и там она была предана смерти.

17А Иодай заключил соглашение между Вечным, царём и народом, что они будут народом Вечного. Ещё он заключил союз между царём и народом. 18Весь народ страны пошёл к храму Баала и разрушил его. Они разбили на куски жертвенники и идолов и убили перед жертвенниками Маттана, жреца Баала.

Затем священнослужитель Иодай установил присмотр за храмом Вечного. 19Он взял с собой сотников, царскую охрану, дворцовую стражу и весь народ страны, и они вместе вывели царя из храма Вечного и вошли в царский дворец через ворота Стражи. Царь сел на своё место на царском престоле, 20и весь народ страны ликовал. А город, после того как Аталия была убита мечом в царском дворце, успокоился.

Иоаш – царь Иудеи

(2 Лет. 24:1-3)

21Иоашу было семь лет, когда он начал царствовать.