2 Samweli 9 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Samweli 9:1-13

Daudi Na Mefiboshethi

19:1 1Sam 20:14-17, 42; 23:18; 18:3; Mit 27:10Daudi akauliza, “Je, hakuna mtu hata mmoja wa nyumba ya Sauli aliyebaki ambaye naweza kumtendea wema kwa ajili ya Yonathani?”

29:2 2Sam 16:1-4; 19:17, 26-29Basi palikuwepo mtumishi wa nyumba ya Sauli aliyeitwa Siba. Wakamwita aje mbele ya Daudi, naye mfalme akamwambia, “Wewe ndiwe Siba?”

Akamjibu, “Naam, mimi ndiye mtumishi wako.”

39:3 1Nya 8:34; Law 21:18; 1Sam 20:14; 2Sam 4:4; Kum 19:15; Mt 5:44; Lk 6:36; Tit 3:3-4Mfalme akauliza, “Je, hakuna yeyote ambaye amebaki wa nyumba ya Sauli ninayeweza kumwonyesha wema wa Mungu?”

Siba akamjibu mfalme, “Bado yupo mwana wa Yonathani, yeye ni kiwete miguu yote.”

49:4 2Sam 17:27-29Mfalme akauliza, “Yuko wapi?”

Siba akajibu, “Yuko nyumbani kwa Makiri mwana wa Amieli huko Lo-Debari.”

5Basi Mfalme Daudi akamtaka aletwe kutoka Lo-Debari, kutoka nyumbani kwa Makiri mwana wa Amieli.

69:6 Mwa 37:7; 2Sam 16:4Mefiboshethi mwana wa Yonathani, mwana wa Sauli, alipofika kwa Daudi, akainama kumpa mfalme heshima.

Daudi akamwita, “Mefiboshethi!”

Mefiboshethi akajibu, “Ndimi mtumishi wako.”

79:7 1Sam 20:14-15; 2Sam 19:28; 21:7; 1Fal 2:7; 2Fal 25:29; Yer 52:33; Mwa 43:18; 50:21; 1Sam 12:19-24; Yer 52:33Daudi akamwambia, “Usiogope, kwa maana hakika nitakutendea wema kwa ajili ya baba yako Yonathani. Nitakurudishia ardhi yote iliyokuwa mali ya Sauli baba yako, nawe daima utakula chakula mezani pangu.”

89:8 2Sam 4:4; 3:8; 1Sam 24:14; 2Sam 16:9Mefiboshethi akasujudu akasema, “Mimi mtumishi wako ni nini hata uangalie mbwa mfu kama mimi?”

99:9 Isa 32:8Ndipo mfalme akamwita Siba mtumishi wa Sauli na kumwambia, “Nimempa mwana wa bwana wako kila kitu kilichokuwa mali ya Sauli na jamaa yake. 109:10 2Sam 16:3; 19:28Wewe, wanao na watumishi wako mtamlimia mashamba Mefiboshethi na kumletea mavuno, ili kwamba mwana wa bwana wako apate mahitaji yake. Naye Mefiboshethi mwana wa bwana wako atakula chakula mezani pangu daima.” (Siba alikuwa na wana kumi na watano, na watumishi ishirini.)

119:11 Ay 36:7; Za 113:8; 1Sam 16:1-4; Mit 12:17Ndipo Siba akamwambia mfalme, “Mtumishi wako atafanya chochote bwana wangu mfalme atakachoagiza mtumishi wake kufanya.” Basi Mefiboshethi akala chakula mezani pa Daudi kama mmoja wa wana wa mfalme.

129:12 2Sam 4:4; 1Nya 8:34Mefiboshethi alikuwa na mwanawe mdogo aliyeitwa Mika, nao watu wote wa nyumba ya Siba walikuwa watumishi wa Mefiboshethi. 139:13 2Sam 19:33-36; 2Fal 25:29; Yer 52:33-34Naye Mefiboshethi akaishi huko Yerusalemu, kwa sababu daima alikula mezani pa mfalme, naye alikuwa kiwete miguu yote.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

撒母耳記下 9:1-13

大衛恩待米非波設

1大衛問:「掃羅一家還有什麼人嗎?我要因為和約拿單的情義而恩待他。」 2有人就去叫掃羅家一個名叫洗巴的僕人來見大衛,王問他:「你就是洗巴嗎?」他說:「僕人正是洗巴。」 3王說:「掃羅家中還有什麼人?我要以上帝的慈愛來待他。」洗巴答道:「約拿單還有一個兒子,是雙腳殘廢的。」 4王說:「他在哪裡?」洗巴答道:「他住在羅·底巴,在亞米利的兒子瑪吉家裡。」 5於是,大衛王派人去羅·底巴把他從亞米利的兒子瑪吉家裡接來。 6掃羅的孫子、約拿單的兒子米非波設來到大衛面前,向他俯伏叩拜。大衛說:「米非波設!」米非波設答道:「僕人在這裡。」 7大衛說:「你不用害怕,我要因為和你父親約拿單的情義而恩待你。我要把你祖父掃羅所有的田地歸還給你,你要常與我同席吃飯。」 8米非波設再次叩拜,說:「僕人算什麼?不過像一條死狗罷了,你竟這樣眷顧我!」

9王又把掃羅的僕人洗巴召來,對他說:「我已把掃羅全家的產業都賜給了你主人的孫子米非波設10你和你的兒子及僕人要為米非波設種田,把出產拿來供養他。他還要常常與我同席吃飯。」洗巴有十五個兒子,二十個僕人。 11洗巴對王說:「僕人必遵行我主我王的一切吩咐。」於是,米非波設像王子一樣常與大衛同席吃飯。 12米非波設有一個小兒子名叫米迦洗巴家中的人都做了米非波設的僕人。 13從此,雙腳殘廢的米非波設就住在耶路撒冷,常常與王同席吃飯。