2 Samweli 8 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Samweli 8:1-18

Ushindi Wa Daudi

(1 Nyakati 18:1-17)

18:1 2Sam 7:9; 21:15-22; 1Nya 18:1Baada ya muda, Daudi akawashinda Wafilisti na kuwatiisha, naye akautwaa Metheg-Amma kutoka mikononi mwa Wafilisti.

28:2 Mwa 19:37; Hes 21:29; Amu 3:15; Isa 45:14; Hes 24:17; 1Sam 14:47; Za 50:8; 72:10Pia Daudi akawashinda Wamoabu. Akawafanya walale chini kwa mstari akawapima kwa urefu wa kamba. Kila alipopima urefu wa hiyo kamba mara mbili hilo kundi waliuawa na alipopima mara ya tatu aliwaacha hai. Kwa hiyo Wamoabu wakawa chini ya Daudi nao wakamletea kodi.

38:3 2Sam 10:16; 1Fal 11:23; 1Sam 14:47; Mwa 2:14; 15:18Zaidi ya hayo, Daudi akapigana na Hadadezeri mwana wa Rehobu, mfalme wa Soba, alipokwenda kurudisha tena utawala wake kwenye eneo la Mto Frati. 48:4 Mwa 49:6; Yos 11:9Daudi akateka magari yake ya vita 1,000, askari wapanda farasi 7,000 na askari 20,000 watembeao kwa miguu. Daudi akawakata wale farasi wote wakokotao magari mishipa ya miguu, isipokuwa farasi 100 hakuwakata.

58:5 Mwa 14:15; 2Sam 10:6; 1Fal 11:24; 2Fal 8:7; 14:28Waaramu wa Dameski walipokuja kumsaidia Hadadezeri mfalme wa Soba, Daudi akawashambulia na kuwaua 22,000 miongoni mwao. 68:6 1Fal 20:34; 2Fal 10:19; 2Sam 3:18Daudi akaweka askari walinzi katika ufalme wa Waaramu huko Dameski, nao Waaramu wakawa watumwa wake na kumlipa ushuru. Bwana akampa Daudi ushindi kote alipokwenda.

78:7 1Fal 10:16; 14:26; 2Fal 11:10Daudi akazitwaa ngao za dhahabu zilizokuwa za maafisa wa Hadadezeri na kuzileta Yerusalemu. 88:8 Eze 47:16Kutoka miji ya Beta8:8 Beta ulikuwa mji wa Aramu-Soba ambao uliitwa Teba kwa Kiaramu; pia uliitwa Tibhathi (1Nya 18:8). na Berothai, iliyokuwa miji ya Hadadezeri, Mfalme Daudi akatwaa shaba nyingi sana.

98:9 1Fal 8:65; 2Fal 14:28; 2Nya 8:4; Lk 14:31-32Tou, mfalme wa Hamathi, aliposikia kwamba Daudi amelishinda jeshi lote la Hadadezeri, 10akamtuma mwanawe Yoramu kwa Mfalme Daudi kumsalimu na kumpongeza kwa ushindi wake katika vita dhidi ya Hadadezeri, kwa kuwa Hadadezeri alikuwa amepigana vita na Tou. Yoramu akamletea Daudi vyombo vya fedha, dhahabu na shaba.

118:11 1Fal 7:51; 15:15; 1Nya 26:26; 2Nya 5:1; 1Nya 18:11; 22:14-16; Mik 4:13; Ufu 21:24Mfalme Daudi akaviweka vifaa hivi wakfu kwa Bwana, kama vile alivyokuwa amefanya kwa fedha na dhahabu kutoka kwa mataifa yote aliyokuwa ameyashinda: 128:12 2Sam 10:14; 5:25; Hes 24:20; 1Sam 27:8yaani Edomu, Moabu, Waamoni, Wafilisti na Waamaleki. Pia akaweka wakfu nyara alizoteka kutoka kwa Hadadezeri mwana wa Rehobu, mfalme wa Soba.

138:13 2Sam 7:9; 2Fal 14:7; 1Nya 18:12; Za 60Naye Daudi akapata sifa baada ya kurudi kutoka kuwaua Waedomu 18,000 katika Bonde la Chumvi.

148:14 Hes 24:17-18; Za 108:9; Isa 34:5; 63:1; Yer 49:7; Eze 25:12; Mwa 27:29, 37-40; Za 144:10; 2Sam 22:44; Za 18:43Akaweka kambi za askari walinzi katika Edomu yote, nao Waedomu wakawa chini ya Daudi. Bwana alimpatia Daudi ushindi kila alipokwenda.

Maafisa Wa Daudi

158:15 Mwa 18:19; 1Fal 11:18; 14:8; 15:11; 22:43; 2Fal 12:2; Ay 29:14; Za 5:12; 119:121; Ebr 11:33Daudi akatawala Israeli yote, akitenda lililo haki na sawa kwa watu wake wote. 168:16 2Sam 2:13; 20:24; 1Fal 4:3; Isa 36:3, 22; 2Sam 19:13Yoabu mwana wa Seruya alikuwa jemadari wa jeshi; Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mweka kumbukumbu; 178:17 1Sam 2:35; 15:24, 29; 2Sam 20:25; 1Fal 1:8; 4:4; 1Nya 6:8, 53; 16:39; 24:3; 27:17; 2Nya 13:10; Eze 40:46; 43:19; 44:15; 48:11; Mk 2:26; 1Fal 4:3; 2Fal 12:10; 19:2; 22:3; Isa 36:3; Yer 36:12Sadoki mwana wa Ahitubu na Ahimeleki mwana wa Abiathari walikuwa makuhani; Seraya alikuwa mwandishi; 188:18 2Sam 20:23; 23:20; 1Fal 1:8; 2:25, 35, 46; 4:4; 1Sam 30:14; 1Nya 18:17Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa msimamizi wa Wakerethi na Wapelethi; nao wana wa Daudi walikuwa washauri wa mfalme.

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

撒母耳记下 8:1-18

大卫战胜敌人

1后来大卫打败并征服了非利士人,夺取了他们的都城。 2他又打败了摩押人,让他们并排躺在地上,然后用绳子去量,每两绳之内的人都要被杀掉,第三绳的人留下性命。从此,摩押人臣服于大卫,向他进贡。

3利合的儿子琐巴哈大底谢出来要恢复他在幼发拉底河一带的势力,大卫打败了他, 4俘获一千七百名骑兵和两万名步兵,砍断拉战车的马匹的蹄筋,只留下够拉一百辆战车的马匹。 5大马士革亚兰人前来支援琐巴哈大底谢大卫杀了他们两万二千人, 6还派军驻守亚兰国的大马士革亚兰人臣服大卫,向他进贡。耶和华使大卫无往而不胜。 7大卫夺走哈大底谢侍从的金盾牌,带回耶路撒冷8又从哈大底谢统治的比他比罗他两座城中夺走大量的铜。 9哈马陀以听说大卫打败哈大底谢全军, 10就派儿子约兰带着许多金银铜器去朝见大卫王,向他请安,祝贺他打败了哈大底谢。因为陀以常常和哈大底谢交战。 11-12大卫王把这些器皿和他征服亚兰人、摩押人、亚扪人、非利士人、亚玛力人和利合的儿子琐巴哈大底谢时所得的金银都分别出来,奉献给耶和华。 13大卫在盐谷杀了一万八千亚兰人,声威大振。 14他又在以东全境设驻军,以东人都臣服于他。耶和华使他无往而不胜。

15大卫统治全以色列,他秉公行义治理百姓。 16那时,洗鲁雅的儿子约押做元帅,亚希律的儿子约沙法做史官, 17亚希突的儿子撒督亚比亚他的儿子亚希米勒做祭司长,西莱雅做书记, 18耶何耶大的儿子比拿雅统管基利提人和比利提人。大卫的众子都做首领。