2 Samweli 22 – NEN & NVI

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Samweli 22:1-51

Wimbo Wa Daudi Wa Sifa

(Zaburi 18)

122:1 Kut 15:1; Amu 5:1; Za 18:2-50Daudi alimwimbia Bwana maneno ya wimbo huu wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli. 222:2 1Sam 2:2; Za 31:3; 91:2; 71:3; 144:2; Kum 32:4; Za 18:2; Mit 18:10; Mt 18:10Akasema:

Bwana ni mwamba wangu,

ngome yangu na mwokozi wangu,

322:3 Mit 10:29; Yoe 3:16; Kum 23:15; 32:37; Za 14:6; 31:2; 59:16; 71:7; 91:2; 94:22; Isa 25:4; Yer 16:19; Mwa 15:1; Kum 33:17; Lk 1:69; Za 9:9; 52:7Mungu wangu ni mwamba wangu,

ambaye kwake ninakimbilia,

ngao yangu na pembe ya wokovu wangu.

Yeye ni ngome yangu, kimbilio langu

na mwokozi wangu,

huniokoa kutoka kwa watu wenye jeuri.

422:4 Za 48:1; 96:4; 145:3Ninamwita Bwana, anayestahili kusifiwa,

nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.

522:5 Za 69:14-15; Yon 2:3“Mawimbi ya mauti yalinizunguka,

mafuriko ya maangamizi yalinilemea.

622:6 Za 116:3; Mdo 2:24Kamba za kuzimu22:6 Kuzimu kwa Kiebrania ni Sheol, maana yake ni Shimo lisilo na mwisho. zilinizunguka,

mitego ya mauti ilinikabili.

722:7 Mwa 35:3; Amu 2:15; 2Nya 15:4; Za 4:1; 77:2; 120:1; Isa 26:16; Za 34:15; 116:4; 116:4; Kut 3:7Katika shida yangu nalimwita Bwana,

nilimlilia Mungu wangu.

Kutoka Hekaluni mwake alisikia sauti yangu,

kilio changu kikafika masikioni mwake.

822:8 Amu 5:4; Za 97:4; Kut 19:18; Za 68:8; 77:18; Yer 10:10; Ay 9:6; 26:11; Za 75:3“Dunia ilitetemeka na kutikisika,

misingi ya mbingu ikatikisika,

vilitetemeka kwa sababu

alikuwa amekasirika.

922:9 Za 50:3; 97:3; Ebr 12:29; Ufu 11:5; Isa 6:6; Eze 1:13; 10:2; Hab 3:5Moshi ukapanda kutoka puani mwake,

moto uteketezao ukatoka kinywani mwake,

makaa ya moto yawakayo

yakatoka ndani mwake.

1022:10 Kut 19:9; Law 16:2; Kum 33:26; 1Fal 8:12; Ay 26:9; Za 104:3; Isa 19:1; Yer 4:13; Nah 1:3; Isa 64:1Akazipasua mbingu akashuka chini,

mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.

1122:11 Mwa 3:24; Kut 25:22; Za 104:3Alipanda juu ya kerubi akaruka,

akapaa juu kwa mbawa za upepo.

1222:12 Kut 19:9Alifanya giza hema lake la kujifunika:

mawingu meusi ya mvua ya angani.

1322:13 Ay 37:3; Za 77:18Kutokana na mwanga wa uwepo wake

mawingu yalisogea,

ikanyesha mvua ya mawe

na umeme wa radi.

1422:14 1Sam 2:10; Isa 30:30Bwana alinguruma kutoka mbinguni,

sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.

1522:15 Kum 32:23; Za 7:13; 77:7; Hab 3:11Aliipiga mishale na kutawanya adui,

umeme wa radi na kuwafukuza.

1622:16 Za 6:1; 50:8, 21; 106:9; Nah 1:4; Isa 30:33; 40:24; Kut 14:21Mabonde ya bahari yalifunuliwa,

na misingi ya dunia ikawa wazi

kwa kukaripia kwake Bwana,

kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwake.

1722:17 Za 144:7; Kut 2; 10“Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika;

alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.

1822:18 Lk 1:71Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi,

kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.

1922:19 Za 23:4Walinikabili siku ya msiba wangu,

lakini Bwana alikuwa msaada wangu.

2022:20 Ay 36:16; Za 31:8; 118:5; 22:8; Isa 42:1; Mt 12:18; 2Sam 15:26Alinileta nje mahali penye nafasi tele,

akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.

2122:21 1Sam 26:23; Za 26:6; Ay 17:9; 22:30; 42:7-8; Za 24:4Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu;

sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.

2222:22 Mwa 18:19; Za 128:1; Mit 8:32Kwa maana nimezishika njia za Bwana;

sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.

2322:23 Kum 6:4-9; Za 119:30-32, 102; Kum 7:12Sheria zake zote zi mbele yangu,

wala sijayaacha maagizo yake.

2422:24 Mwa 6:9; Efe 1:4; Yn 1:47Nimekuwa sina hatia mbele zake,

nami nimejilinda nisitende dhambi.

2522:25 1Sam 26:23Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu,

sawasawa na usafi wangu machoni pake.

2622:26 Mt 5:7“Kwa yeye aliye mwaminifu unajionyesha kuwa mwaminifu,

kwa asiye na hatia unajionyesha kutokuwa na hatia,

2722:27 Mt 5:8; Law 26:23-2422:27 1Nya 27:9-10kwa aliye mtakatifu unajionyesha kuwa mtakatifu,

lakini kwa aliyepotoka unajionyesha kuwa mkaidi.

2822:28 Kut 3:8; 1Sam 2:8-9; Za 72:12-13; Mit 30:13; Dan 4:31; Sef 3:11; Isa 2:12-17; 5:15; Za 12:5; Mt 5:3Wewe huwaokoa wanyenyekevu,

lakini macho yako ni juu ya wenye kiburi

ili uwashushe.

2922:29 Za 27:1; Isa 2:5; Mik 7:8; Ufu 21:23; 22:5Wewe ni taa yangu, Ee Bwana.

Bwana hulifanya giza langu

kuwa mwanga.

30Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi,

nikiwa pamoja na Mungu wangu

nitaweza kuruka ukuta.

3122:31 Kum 32:4; Mt 5:48; Za 12:6; 119:140; Mit 30:5-6; Mwa 15:1; Dan 4:37; Ufu 15:3“Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu;

neno la Bwana halina dosari.

Yeye ni ngao kwa wote

wanaokimbilia kwake.

3222:32 Kut 32:31; 1Sam 2:2; Isa 45:5-6Kwa maana ni nani aliye Mungu

zaidi ya Bwana?

Ni nani aliye Mwamba

isipokuwa Mungu wetu?

3322:33 1Sam 2:2; 2Sam 7:22; Za 27:1; Kum 18:13Mungu ndiye anivikaye nguvu

na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.

3422:34 Isa 35:6; Hab 3:19; Kum 32:13Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu,

huniwezesha kusimama mahali palipo juu.

3522:35 Za 144:1; 7:12; 11:2; Zek 9:13Huifundisha mikono yangu kupigana vita;

mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.

3622:36 Efe 6:16Hunipa ngao yako ya ushindi,

unajishusha chini ili kuniinua.

3722:37 Mit 4:11Huyapanua mapito yangu,

ili miguu yangu isiteleze.

38“Niliwafuatia adui zangu na nikawaseta,

sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.

3922:39 Za 44:5; 110:6; Mal 4:3Niliwaseta kabisa, nao hawakuweza kuinuka tena;

walianguka chini ya miguu yangu.

4022:40 Yos 10:24; 1Fal 5:3; Za 44:5Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita;

uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.

4122:41 Kut 23:27Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia,

nami nikawaangamiza adui zangu.

4222:42 Isa 1:15; Za 50:22; 1Sam 14:37; 28:6; Ay 27:6; Mit 1:28Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa;

walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.

4322:43 1Fal 20:10; 2Fal 13:7; Isa 41:2; Amo 1:3; Za 7:5; Isa 41:25; Mik 7:10; Zek 10:5; Isa 5:25; 10:6; 22:5Niliwaponda kama mavumbi ya nchi;

niliwaponda na kuwakanyaga kama tope barabarani.

4422:44 Kut 11:3; 2Sam 3:1; 8:1-14; Isa 55:3-5; Kum 28:13“Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu wangu;

umenihifadhi mimi kama kiongozi wa mataifa.

Watu ambao sikuwajua wananitumikia,

4522:45 Za 66:3; 81:15; Kum 33:29nao wageni huja wakininyenyekea,

mara wanisikiapo, hunitii.

4622:46 Mik 7:17Wote wanalegea,

wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.

4722:47 Kut 15:2; Kum 32:15; Za 18:31; 89:26; 95:1Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu!

Atukuzwe Mungu,

Mwamba, Mwokozi wangu!

4822:48 Hes 31:3; Za 144:2; 1Sam 25:39; Za 94:1Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi,

ayawekaye mataifa chini yangu,

4922:49 Za 140:1; 27:6aniwekaye huru toka kwa adui zangu.

Uliniinua juu ya adui zangu;

uliniokoa toka kwa watu wajeuri.

5022:50 Za 9:11; 47:6; 68:4; Rum 15:9Kwa hiyo nitakusifu, Ee Bwana,

katikati ya mataifa;

nitaliimbia sifa jina lako.

5122:51 Za 21:1; 144:9-10; 1Sam 16; 13; Za 89:20; Mdo 13:23; 2Sam 7:13; Za 89:24, 29Humpa mfalme wake ushindi mkuu;

huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake,

kwa Daudi na wazao wake milele.”

Nueva Versión Internacional

2 Samuel 22:1-51

Salmo de David

22:1-51Sal 18

1David dedicó al Señor la letra de esta canción cuando el Señor lo libró de las manos de todos sus enemigos y de las manos de Saúl. 2Dijo así:

«El Señor es mi roca, mi amparo, mi libertador;

3es mi Dios, la roca en que me refugio.

Es mi escudo, el poder que me salva,22:3 el poder que me salva. Lit. el cuerno de mi salvación.

¡mi más alto escondite!

Él es mi protector y mi salvación.

¡Tú me salvaste de la violencia!

4»Invoco al Señor, que es digno de alabanza,

y quedo a salvo de mis enemigos.

5Las olas de la muerte me envolvieron;

los torrentes destructores me abrumaron.

6Los lazos del sepulcro22:6 sepulcro. Lit. Seol. me enredaron;

las redes de la muerte me atraparon.

7»En mi angustia invoqué al Señor;

llamé a mi Dios

y él me escuchó desde su Templo;

¡mi clamor llegó a sus oídos!

8La tierra tembló, se estremeció;

se sacudieron los cimientos de los cielos;

temblaron a causa de su enojo.

9Por la nariz echaba humo,

por la boca, fuego consumidor;

¡lanzaba carbones encendidos!

10Rasgando el cielo, descendió,

pisando sobre oscuros nubarrones.

11Montando sobre un querubín, surcó los cielos

y se remontó22:11 se remontó (mss. hebreos; véanse Siríaca, Targum, Vulgata, Sal 18:10); apareció (TM). sobre las alas del viento.

12De las tinieblas y los oscuros nubarrones

hizo tiendas que lo rodeaban.

13De su radiante presencia

brotaron carbones encendidos.

14Desde el cielo se oyó el trueno del Señor;

resonó la voz del Altísimo.

15Lanzó flechas y dispersó a los enemigos;

con relámpagos los desconcertó.

16A causa de la reprensión del Señor

y por el resoplido de su enojo,22:16 por … su enojo. Lit. por el soplo del aliento de su nariz.

las cuencas del mar quedaron a la vista;

al descubierto quedaron los cimientos de la tierra.

17»Extendiendo su mano desde lo alto,

tomó la mía y me sacó del mar profundo.

18Me libró de mi enemigo poderoso,

de aquellos que me odiaban y eran más fuertes que yo.

19En el día de mi desgracia me salieron al encuentro,

pero mi apoyo fue el Señor.

20Me sacó a un amplio espacio;

me libró porque se agradó de mí.

21»El Señor me ha pagado conforme a mi justicia;

me ha premiado conforme a la limpieza de mis manos.

22He guardado los caminos del Señor

y no he cometido el error de alejarme de mi Dios.

23Presentes tengo todas sus leyes;

no me he alejado de sus estatutos.

24He sido íntegro ante él

y me he abstenido de pecar.

25El Señor me ha recompensado conforme a mi justicia,

conforme a mi limpieza ante sus ojos.

26»Tú eres fiel con quien es fiel

e íntegro con quien es íntegro;

27sincero eres con quien es sincero,

pero sagaz con el que es tramposo.

28Das la victoria a los humildes,

pero tu mirada humilla a los altaneros.

29Tú, Señor, eres mi lámpara;

tú, Señor, iluminas mis tinieblas.

30Con tu apoyo me lanzaré contra un ejército;

contigo, Dios mío, podré asaltar murallas.

31»El camino de Dios es perfecto;

la palabra del Señor es intachable.

Escudo es Dios a los que se refugian en él.

32Pues ¿quién es Dios sino el Señor?

¿Quién es la Roca sino nuestro Dios?

33Es él quien me arma de valor

y hace perfecto mi camino;

34da a mis pies la ligereza del venado

y me mantiene firme en las alturas;

35adiestra mis manos para la batalla

y mis brazos para tensar un arco de bronce.

36Tú me cubres con el escudo de tu salvación;

tu ayuda me ha hecho prosperar.

37Has despejado el paso de mi camino,

para que mis tobillos no se tuerzan.

38»Perseguí a mis enemigos y los destruí;

no retrocedí hasta verlos aniquilados.

39Los aplasté por completo. Ya no se levantan.

¡Cayeron debajo de mis pies!

40Tú me armaste de valor para el combate;

doblegaste ante mí a los rebeldes.

41Hiciste retroceder a mis enemigos,

y así exterminé a los que me odiaban.

42Pedían ayuda y no hubo quien los salvara.

Al Señor clamaron, pero no respondió.

43Los desmenucé. Parecían el polvo de la tierra.

Los pisoteé como al lodo de las calles.

44»Me has librado de los conflictos con mi pueblo;

me has puesto por líder de las naciones;

me sirve gente que yo no conocía.

45Son extranjeros, y me rinden homenaje;

apenas me oyen, me obedecen.

46Esos extraños se descorazonan

y temblando salen de sus refugios.

47»¡El Señor vive! ¡Alabada sea mi Roca!

¡Exaltado sea Dios, la Roca de mi salvación!

48Él es el Dios que me vindica,

el que pone los pueblos a mis pies.

49Tú me libras de mis enemigos,

me exaltas por encima de mis adversarios,

me salvas de los hombres violentos.

50Por eso, Señor, te alabo entre las naciones

y canto salmos a tu nombre.

51»“Él da grandes victorias a su rey;

a su ungido David y a sus descendientes

les muestra por siempre su gran amor”».