2 Samweli 21 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Samweli 21:1-22

Wagibeoni Walipiza Kisasi

121:1 Mwa 12:10; Kum 32:24; Kut 32:11; Hes 27:21; 1Sam 22:10-15; Law 18:25; Hes 35:33; Isa 26:21Wakati wa utawala wa Daudi kulikuwa na njaa kwa miaka mitatu mfululizo, kwa hiyo Daudi akautafuta uso wa Bwana. Bwana akasema, “Ni kwa sababu ya Sauli na nyumba yake iliyotiwa madoa ya damu, kwa sababu aliwaua Wagibeoni.”

221:2 Yos 9:15; 9:3Mfalme akawaita Wagibeoni na kuzumgumza nao. (Wagibeoni hawakuwa wa wana wa Israeli, ila walikuwa mabaki ya Waamori. Waisraeli walikuwa wameapa kuwaacha hai, lakini Sauli katika wivu wake kwa ajili ya Israeli na Yuda, alikuwa amejaribu kuwaangamiza.) 321:3 1Sam 26:19; 2Sam 20:19Daudi akawauliza Wagibeoni, “Niwatendee nini? Nitawaridhishaje ili mbariki urithi wa Bwana?”

421:4 Hes 35:33-34Wagibeoni wakamjibu, “Hatuna haki ya kudai fedha wala dhahabu kutoka kwa Sauli au jamaa yake, wala hatuna haki ya kumuua mtu yeyote katika Israeli.”

Daudi akawauliza, “Mnataka niwafanyie nini?”

5Wakamjibu mfalme, “Kwa habari ya mtu aliyetuangamiza na kufanya hila mbaya dhidi yetu ili kwamba tuangamizwe na tusiwe na yeyote katika Israeli, 621:6 Hes 25:4; 1Sam 10:24; Amu 20:4tupatieni wazao wake saba wa kiume tuwaue hadharani mbele za Bwana huko Gibea ya Sauli, aliyekuwa amechaguliwa na Bwana.”

Basi mfalme akasema, “Nitawakabidhi kwenu.”

721:7 2Sam 4:4; 1Sam 18:3; 2Sam 9:7; 1Sam 20:8, 15Mfalme akamhifadhi Mefiboshethi mwana wa Yonathani, mwana wa Sauli, kwa sababu ya kile kiapo mbele za Bwana kati ya Daudi na Yonathani. 821:8 2Sam 3:7; 1Sam 18:19Lakini mfalme akamchukua Armoni na Mefiboshethi, wana wawili wa Rispa binti Aiya, ambao alikuwa amemzalia Sauli, pamoja na wana watano wa Merabu binti Sauli, aliokuwa amemzalia Adrieli mwana wa Barzilai, Mmeholathi. 921:9 2Sam 16:8; Rut 1:22; 2Sam 6:17Akawakabidhi kwa Wagibeoni, ambao waliwaua na kuwaweka wazi juu ya kilima mbele za Bwana. Wote saba walianguka kwa pamoja; waliuawa katika siku za kwanza za mavuno, mara tu uvunaji wa shayiri ulipokuwa unaanza.

1021:10 Mwa 40:19; 1Sam 17:44; Kum 21:23; 2Sam 3:7Rispa binti Aiya akachukua nguo ya gunia, akajitandikia juu ya mwamba. Kuanzia mwanzo wa mavuno mpaka mvua ziliponyesha juu ya miili ya hao waliouawa, Rispa hakuruhusu ndege wa angani kuwagusa wakati wa mchana, wala wanyama wa mwitu wakati wa usiku. 11Daudi alipoambiwa kile Rispa binti Aiya, suria wa Sauli, alichokuwa amekifanya, 1221:12 1Sam 31:11-13; Amu 21:8; 1Sam 11:1; Yos 17:11; 17:11; 1Sam 31:10; 28:4alikwenda akachukua mifupa ya Sauli na mwanawe Yonathani kutoka kwa watu wa Yabeshi-Gileadi. (Walikuwa wameichukua kwa siri kutoka uwanja wa watu wote huko Beth-Shani, mahali ambapo Wafilisti walikuwa wamewatundika baada ya kumuua Sauli huko Gilboa.) 13Daudi akaileta mifupa ya Sauli na ya mwanawe Yonathani kutoka huko, pia mifupa ya wale waliokuwa wameuawa na kutupwa ilikusanywa.

1421:14 Yos 18:28; 7:26; 2Sam 24:25; 1Nya 8:34Wakazika mifupa ya Sauli na ya mwanawe Yonathani katika kaburi la Kishi, babaye Sauli, huko Sela katika nchi ya Benyamini, nao wakafanya kila kitu mfalme alichoagiza. Baada ya hayo, Mungu akajibu maombi kwa ajili ya nchi.

Vita Dhidi Ya Wafilisti

(1 Nyakati 20:4-8)

15Kwa mara nyingine tena kulikuwa na vita kati ya Wafilisti na Israeli. Daudi akashuka pamoja na watu wake ili kupigana dhidi ya Wafilisti, naye akawa amechoka sana. 16Naye Ishbi-Benobu, mmoja wa wazao wa Warefai,21:16 Yaani majitu. ambaye mkuki wake ulikuwa na uzito wa shekeli 300 za shaba,21:16 Shekeli 300 za shaba ni sawa na kilo 3.5. alikuwa amejifunga upanga mpya, naye alisema angemuua Daudi. 1721:17 2Sam 20:6; 1Fal 11:36; 15:4; 2Fal 8:19; 2Nya 21:7; Za 132:17; 2Sam 18:3Lakini Abishai mwana wa Seruya akaja kumwokoa Daudi; akampiga huyo Mfilisti, akamwangusha chini na kumuua. Ndipo watu wakamwapia Daudi, wakisema, “Kamwe hutakwenda tena nasi vitani, ili kwamba taa ya Israeli isije ikazimwa.”

1821:18 1Nya 11:29; 27:11Baada ya muda, kukawa na vita nyingine na Wafilisti, huko Gobu. Wakati huo Sibekai, Mhushathi, akamuua Safu, mmoja wa wazao wa Warefai.

1921:19 1Sam 17:4-7Katika vita vingine na Wafilisti huko Gobu, Elhanani mwana wa Yaare-Oregimu, Mbethlehemu, alimuua nduguye Goliathi, Mgiti, ambaye mkuki wake ulikuwa na mpini kama mti wa mfumaji.

2021:20 1Nya 20:6Katika vita vingine tena, vilivyopiganwa huko Gathi, kulikuwako na mtu mmoja mkubwa mwenye vidole sita katika kila mkono na vidole sita kila mguu, jumla vidole ishirini na vinne. Yeye alikuwa pia mzao wa Mrefai. 2121:21 1Sam 17:10; 16:9Alipowadhihaki Israeli, Yonathani mwana wa Shimea, nduguye Daudi, akamuua.

22Hawa wanne walikuwa wazao wa Warefai huko Gathi, nao walianguka kwa mikono ya Daudi na watu wake.

New International Version

2 Samuel 21:1-22

The Gibeonites Avenged

1During the reign of David, there was a famine for three successive years; so David sought the face of the Lord. The Lord said, “It is on account of Saul and his blood-stained house; it is because he put the Gibeonites to death.”

2The king summoned the Gibeonites and spoke to them. (Now the Gibeonites were not a part of Israel but were survivors of the Amorites; the Israelites had sworn to spare them, but Saul in his zeal for Israel and Judah had tried to annihilate them.) 3David asked the Gibeonites, “What shall I do for you? How shall I make atonement so that you will bless the Lord’s inheritance?”

4The Gibeonites answered him, “We have no right to demand silver or gold from Saul or his family, nor do we have the right to put anyone in Israel to death.”

“What do you want me to do for you?” David asked.

5They answered the king, “As for the man who destroyed us and plotted against us so that we have been decimated and have no place anywhere in Israel, 6let seven of his male descendants be given to us to be killed and their bodies exposed before the Lord at Gibeah of Saul—the Lord’s chosen one.”

So the king said, “I will give them to you.”

7The king spared Mephibosheth son of Jonathan, the son of Saul, because of the oath before the Lord between David and Jonathan son of Saul. 8But the king took Armoni and Mephibosheth, the two sons of Aiah’s daughter Rizpah, whom she had borne to Saul, together with the five sons of Saul’s daughter Merab,21:8 Two Hebrew manuscripts, some Septuagint manuscripts and Syriac (see also 1 Samuel 18:19); most Hebrew and Septuagint manuscripts Michal whom she had borne to Adriel son of Barzillai the Meholathite. 9He handed them over to the Gibeonites, who killed them and exposed their bodies on a hill before the Lord. All seven of them fell together; they were put to death during the first days of the harvest, just as the barley harvest was beginning.

10Rizpah daughter of Aiah took sackcloth and spread it out for herself on a rock. From the beginning of the harvest till the rain poured down from the heavens on the bodies, she did not let the birds touch them by day or the wild animals by night. 11When David was told what Aiah’s daughter Rizpah, Saul’s concubine, had done, 12he went and took the bones of Saul and his son Jonathan from the citizens of Jabesh Gilead. (They had stolen their bodies from the public square at Beth Shan, where the Philistines had hung them after they struck Saul down on Gilboa.) 13David brought the bones of Saul and his son Jonathan from there, and the bones of those who had been killed and exposed were gathered up.

14They buried the bones of Saul and his son Jonathan in the tomb of Saul’s father Kish, at Zela in Benjamin, and did everything the king commanded. After that, God answered prayer in behalf of the land.

Wars Against the Philistines

15Once again there was a battle between the Philistines and Israel. David went down with his men to fight against the Philistines, and he became exhausted. 16And Ishbi-Benob, one of the descendants of Rapha, whose bronze spearhead weighed three hundred shekels21:16 That is, about 7 1/2 pounds or about 3.5 kilograms and who was armed with a new sword, said he would kill David. 17But Abishai son of Zeruiah came to David’s rescue; he struck the Philistine down and killed him. Then David’s men swore to him, saying, “Never again will you go out with us to battle, so that the lamp of Israel will not be extinguished.”

18In the course of time, there was another battle with the Philistines, at Gob. At that time Sibbekai the Hushathite killed Saph, one of the descendants of Rapha.

19In another battle with the Philistines at Gob, Elhanan son of Jair21:19 See 1 Chron. 20:5; Hebrew Jaare-Oregim. the Bethlehemite killed the brother of21:19 See 1 Chron. 20:5; Hebrew does not have the brother of. Goliath the Gittite, who had a spear with a shaft like a weaver’s rod.

20In still another battle, which took place at Gath, there was a huge man with six fingers on each hand and six toes on each foot—twenty-four in all. He also was descended from Rapha. 21When he taunted Israel, Jonathan son of Shimeah, David’s brother, killed him.

22These four were descendants of Rapha in Gath, and they fell at the hands of David and his men.