2 Samweli 18 – NEN & CARST

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Samweli 18:1-33

Kifo Cha Absalomu

1Daudi akakusanya watu aliokuwa nao na kuweka majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia. 218:2 Amu 7:16; 1Sam 11:11; 26:6; 2Sam 15:19Daudi akatuma vikosi vya askari: theluthi moja ilikuwa chini ya amri ya Yoabu, theluthi ya pili chini ya Abishai mwana wa Seruya nduguye Yoabu, na theluthi ya tatu chini ya Itai, Mgiti. Mfalme akaviambia vikosi, “Hakika mimi mwenyewe nitakwenda pamoja nanyi.”

318:3 1Sam 18:7; 2Sam 21:17Lakini watu wakasema, “Haikupasi kwenda, ikiwa sisi tutalazimika kukimbia, wao hawatatujali. Hata kama nusu yetu tukifa hawatajali, lakini wewe una thamani ya watu kama sisi kumi elfu. Ingekuwa bora zaidi kwako basi kutupatia msaada kutoka mjini.”

4Mfalme akajibu, “Nitafanya lolote linaloonekana jema zaidi kwenu.”

Kwa hiyo mfalme akasimama kando ya lango wakati watu wote wakitoka nje kwa makundi ya mamia na maelfu. 5Mfalme akawaamuru Yoabu, Abishai na Itai, “Kuweni wapole kwa kijana Absalomu kwa ajili yangu.” Vikosi vyote vikasikia mfalme akitoa amri kwa kila jemadari kumhusu Absalomu.

618:6 Yos 17:15-18Jeshi likatoka kwenda kwenye uwanja wa vita kupigana na Israeli, hivyo vita vikapiganwa katika msitu wa Efraimu. 718:7 Mit 11:21Huko jeshi la Israeli likashindwa na watu wa Daudi, siku hiyo majeruhi walikuwa wengi kiasi cha watu ishirini elfu. 8Vita vikaenea nchi nzima, watu wengi zaidi wakifia msituni siku hiyo kuliko waliouawa kwa upanga.

918:9 2Sam 14:26; 17:23; Ay 18:5-14; Mt 27:5; 1Kor 11:14Basi ikawa Absalomu alikutana na watu wa Daudi. Yeye alikuwa amepanda nyumbu wake, naye nyumbu alipopita chini ya matawi yaliyosongana ya mwaloni mkubwa, kichwa cha Absalomu kilinaswa kwenye mti. Akaachwa akiningʼinia hewani, wakati nyumbu aliyekuwa amempanda aliendelea kwenda.

10Mmojawapo wa wale watu alipoona, akamwambia Yoabu, “Nimemwona Absalomu akiningʼinia kwenye mti wa mwaloni.”

1118:11 2Sam 3:39; 1Sam 18:4Yoabu akamwambia huyo mtu, “Nini! Ulimwona Absalomu? Kwa nini hukumpiga papo hapo mpaka chini? Ndipo ningekupa shekeli kumi18:11 Shekeli kumi za fedha ni sawa na gramu 115. za fedha na mkanda wa askari shujaa.”

12Lakini huyo mtu akamjibu Yoabu, “Hata kama ningepimiwa shekeli 1,00018:12 Shekeli 1,000 za fedha ni sawa na kilo 11.5. mikononi mwangu, nisingeinua mkono wangu dhidi ya mwana wa mfalme. Tukiwa tunasikia, mfalme alikuagiza wewe na Abishai pamoja na Itai, akisema, ‘Mlindeni kijana Absalomu kwa ajili yangu.’ 1318:13 2Sam 14:19-20Nami kama ningekuwa nimemtendea kwa hila, na hakuna lolote linalofichika kwa mfalme, wewe mwenyewe ungejitenga nami.”

1418:14 2Sam 2:18; 14:30Yoabu akasema, “Mimi sitapoteza muda hapa pamoja nawe.” Hivyo akachukua mikuki mitatu mkononi mwake, akamchoma Absalomu nayo moyoni alipokuwa angali hai akiningʼinia katika ule mwaloni. 1518:15 2Sam 15:10Nao wabeba silaha kumi wa Yoabu wakamzunguka Absalomu, wakampiga na kumuua.

1618:16 2Sam 2:28; 20:22Kisha Yoabu akapiga tarumbeta, navyo vikosi vikaacha kuwafuata Israeli, kwa maana Yoabu aliwasimamisha. 1718:17 Yos 7:26; 8:29; Yer 22:18, 19; Mao 3:53Wakamchukua Absalomu, wakamtupa katika shimo kubwa huko msituni na kulundika lundo kubwa la mawe juu yake. Huko nyuma, Waisraeli wote wakakimbilia nyumbani kwao.

1818:18 Mwa 14:17; 50:5; Hes 32:42; 2Sam 14:27; 1Sam 15:12; Ay 13:12; 18:17-19; Za 34:16; 109:13; Mit 2:22Wakati wa uhai wa Absalomu alikuwa amechukua nguzo na kuisimamisha katika Bonde la Mfalme, kwa maana alifikiri, “Sina mwana atakayeendeleza kumbukumbu ya jina langu.” Akaita nguzo hiyo kwa jina lake mwenyewe. Nayo inaitwa Mnara wa Ukumbusho wa Absalomu mpaka leo.

Daudi Aomboleza Kifo Cha Absalomu

1918:19 2Sam 15:36; Amu 11:36; 2Sam 17:17Basi Ahimaasi mwana wa Sadoki akasema, “Niruhusu mimi nikimbie na kumpelekea mfalme habari kwamba Bwana amemwokoa mfalme kutoka mikononi mwa adui zake.”

20Yoabu akamwambia Ahimaasi, “Leo si wewe utakayepeleka habari. Unaweza kupeleka habari wakati mwingine, lakini leo haikupasi kupeleka, kwa sababu mwana wa mfalme amekufa.”

21Ndipo Yoabu akamwambia mtu mmoja Mkushi, “Nenda, ukamwambie mfalme kile ulichoona.” Mkushi akasujudu mbele ya Yoabu akaondoka mbio.

22Ahimaasi mwana wa Sadoki akamwambia tena Yoabu, “Liwalo na liwe, tafadhali niruhusu nikimbie nyuma ya huyo Mkushi.”

Lakini Yoabu akajibu, “Mwanangu, mbona wataka kwenda? Wewe huna habari yoyote itakayokupa tuzo.”

23Ahimaasi akasema, “Liwalo na liwe, nataka kukimbia.”

Kwa hiyo Yoabu akamwambia, “Haya, kimbia!” Ndipo Ahimaasi akakimbia kufuata njia ya kupitia tambarare, akafika kabla ya huyo Mkushi.

2418:24 1Sam 14:16; Yer 51:12; 1Sam 4:13; 2Sam 13:34; 2Fal 9:17; Isa 21:6-9Wakati Daudi alipokuwa ameketi kati ya lango la ndani na la nje, mlinzi akapanda juu ya paa la lango kupitia ukutani. Alipotazama nje, akaona mtu mmoja akikimbia peke yake. 25Mlinzi akampazia mfalme sauti na kumpa taarifa.

Mfalme akasema, “Ikiwa yuko peke yake, lazima atakuwa na habari njema.” Naye yule mtu akazidi kusogea karibu.

2618:26 1Fal 1:42; Isa 52:7; 61:1Kisha mlinzi akaona mtu mwingine anakuja akikimbia, akamwita bawabu, “Tazama, mtu mwingine anakuja akikimbia peke yake!”

Mfalme akasema, “Lazima atakuwa analeta habari njema pia.”

2718:27 2Fal 9:20Mlinzi akasema, “Ninaona kuwa yule wa kwanza anakimbia kama Ahimaasi mwana wa Sadoki.”

Mfalme akasema, “Yeye ni mtu mwema. Analeta habari njema.”

28Ndipo Ahimaasi akamwita mfalme, akasema, “Mambo yote ni mema!” Akasujudu mbele ya mfalme uso wake mpaka ardhini, akasema, “Ahimidiwe Bwana Mungu wako! Yeye aliyewatoa watu wale walioinua mikono yao dhidi ya mfalme bwana wangu.”

29Mfalme akauliza, “Je, huyo kijana Absalomu yuko salama?”

Ahimaasi akajibu, “Kulikuwa na machafuko mengi mara tu Yoabu alipokuwa anataka kumtuma mtumishi wa mfalme pamoja nami mtumishi wako, lakini sijui ilikuwa nini?”

30Mfalme akasema, “Simama kando na usubiri hapa.” Basi akasogea kando na kusimama hapo.

3118:31 Za 27:3; 55:18Ndipo huyo Mkushi akawasili na kusema, “Mfalme bwana wangu, sikia habari njema! Leo Bwana amekuokoa kutoka kwa wale wote walioinuka dhidi yako.”

3218:32 Amu 5:31; 1Sam 25:26Mfalme akamuuliza huyo Mkushi, “Je, kijana Absalomu yuko salama?”

Huyo Mkushi akajibu, “Adui wa mfalme bwana wangu na wote wale walioinuka kukudhuru na wawe kama huyo kijana.”

3318:33 Kut 32:32; Mwa 43:14; 2Sam 19:4; Rum 9:3; Mit 10:1; 19:13Mfalme akatetemeka. Akapanda chumbani juu kupitia langoni akilia. Alipokuwa akienda, akasema, “Ee mwanangu Absalomu! Mwanangu, mwanangu Absalomu! Laiti ningekufa badala yako: Ee Absalomu, mwanangu, mwanangu!”

Священное Писание (Восточный перевод), версия для Таджикистана

2 Царств 18:1-33

Подготовка Довуда к битве

1Довуд осмотрел людей, которые были с ним, и назначил над ними тысячников и сотников. 2Довуд отправил войска – треть под началом Иоава, треть под началом сына Церуи Авишая, брата Иоава, и треть под началом гатянина Иттая.

Царь сказал воинам:

– Я сам непременно выступлю вместе с вами.

3Но люди сказали:

– Не ходи. Если мы будем вынуждены бежать, они не обратят на это внимания. Даже если половина из нас погибнет, они не обратят внимания, но ты стоишь десяти тысяч из нас18:3 Или: «потому что теперь есть десять тысяч таких, как мы».. Поэтому лучше тебе помогать нам из города.

4Царь ответил:

– Я сделаю так, как вам кажется лучше.

И царь стоял у ворот, пока весь народ не выступил отрядами по сотням и тысячам. 5Царь приказал Иоаву, Авишаю и Иттаю:

– Ради меня обращайтесь с юношей Авессаломом мягко.

И все воины слышали, как царь давал приказ об Авессаломе каждому из военачальников.

Гибель Авессалома

6Войско выступило в поле, чтобы сразиться с Исроилом, и битва произошла в лесу на земле Ефраима. 7Исроильское войско было разбито там людьми Довуда, и потери в тот день были очень велики – двадцать тысяч человек. 8Битва распространилась по всем окрестностям, и лес погубил в тот день больше жизней, чем меч.

9Авессалому случилось встретиться с людьми Довуда. Он был на своём муле, и когда мул пробегал под большим дубом, волосы Авессалома запутались в густых ветвях. Сам он остался висеть в воздухе, а мул, на котором он ехал, побежал дальше. 10Когда один из людей увидел это, он доложил Иоаву:

– Я только что видел Авессалома висящим на дубе.

11Иоав сказал человеку, который доложил ему об этом:

– Что! Ты видел его? Почему ты не поверг его там же на землю? Я бы с радостью наградил тебя сто двадцатью граммами18:11 Букв.: «десятью шекелями». серебра и воинским поясом.

12Но человек ответил:

– Даже если бы мне в руки отвесили двенадцать килограммов18:12 Букв.: «тысячу шекелей». серебра, я бы не поднял руки на царского сына. Мы сами слышали, как царь приказал тебе, Авишаю и Иттаю: «Ради меня защитите юношу Авессалома». 13С другой стороны, если бы я рискнул своей жизнью18:13 Или: «если бы я поступил с ним по-предательски». – ведь от царя ничего не скроешь, – ты остался бы в стороне.

14Иоав сказал:

– Нечего мне терять с тобой время.

Он взял в руку три дротика и вонзил их в сердце Авессалому, пока тот, ещё живой, висел на дубе. 15И десять оруженосцев Иоава окружили Авессалома, поразили и умертвили его.

16Затем Иоав затрубил в рог, и воины прекратили преследовать Исроил, потому что Иоав остановил их. 17Они взяли Авессалома, бросили его в большую яму в лесу и воздвигли над ним огромную груду камней. Тем временем все исроильтяне разбежались по своим домам.

18Ещё при жизни Авессалом взял камень и поставил его в долине Царей как памятник себе, потому что думал: «У меня нет сына, чтобы сохранить в памяти моё имя». Он назвал камень своим именем, и называется он «Памятник Авессалома» по сегодняшний день.

Довуду приносят весть о смерти Авессалома

19Ахимаац же, сын Цадока, сказал:

– Позволь мне побежать и принести царю весть о том, что Вечный избавил его от рук его врагов.

20– Сегодня весть понесёшь не ты, – сказал Иоав. – Ты можешь принести вести в другой раз, но сегодня не делай этого, потому что сын царя умер.

21И Иоав сказал одному эфиопу:

– Ступай, расскажи царю о том, что ты видел.

Эфиоп поклонился Иоаву и побежал.

22Сын Цадока Ахимаац снова сказал Иоаву:

– Будь что будет, позволь мне побежать вслед за эфиопом.

Но Иоав ответил:

– Мой сын, зачем ты хочешь идти? За такую весть не получишь награды.

23Он сказал:

– Будь что будет, я хочу бежать.

И Иоав сказал:

– Беги!

Ахимаац побежал по дороге Иорданской долины и обогнал эфиопа. 24В то время как Довуд сидел между внутренними и внешними воротами, дозорный поднялся на стену и стоял на крыше над воротами. Подняв глаза, он увидел человека, который бежал один. 25Дозорный позвал царя и доложил об этом. Царь сказал:

– Если он один, то, должно быть, у него хорошая весть.

А человек всё приближался и приближался. 26Потом дозорный увидел другого бегущего человека и закричал привратнику:

– Вот ещё один человек бежит!

Царь сказал:

– Должно быть, и он несёт хорошую весть.

27Дозорный сказал:

– Судя по бегу, первый – это Ахимаац, сын Цадока.

– Это хороший человек, – сказал царь. – Он идёт с хорошей вестью.

28И Ахимаац, приблизившись, закричал царю:

– Всё хорошо!

Он поклонился царю лицом до земли и сказал:

– Хвала Вечному, твоему Богу! Он отдал тебе людей, которые подняли свои руки на господина моего царя.

29Царь спросил:

– В безопасности ли юноша Авессалом?

Ахимаац ответил:

– Я видел сильное волнение как раз тогда, когда Иоав собирался послать твоего раба, но я не знаю, что это было такое.

30Царь сказал:

– Стань в сторону и подожди здесь.

Он отошёл в сторону и встал там.

31Эфиоп прибыл и сказал:

– Господин мой царь! Слушай добрую весть! Вечный избавил тебя сегодня от всех, кто восстал против тебя.

32Царь спросил эфиопа:

– В безопасности ли юноша Авессалом?

Эфиоп ответил:

– Пусть со всеми врагами господина моего царя и со всеми, кто восстаёт против тебя, случится то же, что и с этим юношей.

33Царь был потрясён. Он пошёл в комнату над воротами и заплакал. Когда он шёл, он говорил:

– О, сын мой Авессалом! Сын мой, сын мой Авессалом! Если бы только мне умереть вместо тебя, о, Авессалом, сын мой, сын мой!