2 Samweli 11 – NEN & CARS

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Samweli 11:1-27

Daudi Na Bathsheba

111:1 1Fal 20:22; 2Sam 2:18; 1Nya 20:1; Kum 3:11Katika mwanzo wa mwaka mpya, wakati wafalme watokapo kwenda vitani, Daudi akamtuma Yoabu pamoja na watu wa mfalme na jeshi lote la Israeli. Wakawaangamiza Waamoni na kuuzunguka kwa jeshi mji wa Raba. Lakini Daudi akabaki Yerusalemu.

211:2 Kum 22:8; Yos 2:8; Mt 5:28; Mwa 34:2; Ay 31:1; Za 119:37Ikawa siku moja wakati wa jioni Daudi aliinuka kitandani mwake na kutembeatembea juu ya paa la jumba lake la kifalme. Kutokea kule kwenye paa, akamwona mwanamke akioga. Mwanamke huyo alikuwa mzuri sana wa sura, 311:3 1Nya 3:5; 2Sam 23:34-39naye Daudi akatuma mtu mmoja kuuliza habari za huyo mwanamke. Huyo mtu akamwambia Daudi, “Je, huyu si Bathsheba binti Eliamu, naye ni mke wa Uria, Mhiti?” 411:4 Law 20:10; Za 51; Yak 1:14-15; Kum 22:22; Law 15:25-30; 18:19; Kut 20:17; Ebr 13:4Ndipo Daudi akatuma wajumbe kumleta. Huyo mwanamke akaja kwa Daudi, Daudi akakutana naye kimwili. (Huyo mwanamke ndipo tu alikuwa amejitakasa kutoka siku zake za hedhi.) Kisha akarudi nyumbani kwake. 511:5 Law 20:10Huyo mwanamke akapata mimba akampelekea Daudi ujumbe, kusema, “Mimi ni mjamzito.”

611:6 1Nya 11:41Ndipo Daudi akapeleka ujumbe kwa Yoabu, “Unipelekee Uria, Mhiti.” Naye Yoabu akamtuma Uria kwa Daudi. 7Uria alipofika, Daudi akamuuliza habari za Yoabu, hali za askari na vita kwamba inaendeleaje. 811:8 Mwa 18:4; 43:24; Lk 7:44; Za 44:21; Mwa 19:2Kisha Daudi akamwambia Uria, “Teremka nyumbani kwako ukanawe miguu yako.” Basi Uria akaondoka kutoka kwenye jumba la kifalme, tena zawadi zikamfuata kutoka kwa mfalme. 911:9 Ay 5:12-14Lakini Uria akalala kwenye ingilio la jumba la kifalme pamoja na watumishi wote wa bwana wake, na hakuteremka kwenda nyumbani kwake.

10Daudi alipoambiwa kwamba, “Uria hakwenda nyumbani,” Daudi akamuuliza, “Je, si ndiyo tu umefika kutoka safari ya mbali? Kwa nini hukwenda nyumbani?”

1111:11 2Sam 7:2; 1Sam 21:5; 4:4; 2Sam 20:6; Mt 10:25; 2Tim 2:3Uria akamwambia Daudi, “Sanduku la Mungu, na Israeli na Yuda wanakaa kwenye mahema, naye bwana wangu Yoabu na watu wa bwana wangu wamepiga kambi mahali pa wazi. Ningewezaje kwenda nyumbani kwangu ili nile, ninywe na kukutana na mke wangu? Hakika kama uishivyo sitafanya jambo la namna hiyo!”

1211:12 Ay 20:12-14; Yer 2:22-23Ndipo Daudi akamwambia, “Kaa hapa siku moja zaidi, nami kesho nitakutuma urudi.” Kwa hiyo Uria akakaa Yerusalemu siku ile na siku iliyofuata. 1311:13 Mwa 9:21-22; 19:33-35; Kut 32:21; 1Fal 20:16-21; Mit 20:1; 23:29-35; Hos 4:11; Gal 5:21Kwa ukaribisho wa Daudi, Uria akala na kunywa pamoja naye, Daudi akamlevya. Lakini jioni Uria alitoka kwenda kulala juu ya mkeka wake miongoni mwa watumishi wa bwana wake, hakwenda nyumbani.

1411:14 1Fal 21:8; Za 19:13; 62:9; Mhu 8:11; Yer 9:1-4; Mik 7:3-5Asubuhi yake Daudi akamwandikia Yoabu barua, akamtuma Uria kuipeleka. 1511:15 2Sam 12:9; 12:12Ndani ya barua aliandika, “Mweke Uria mstari wa mbele mahali ambapo mapigano ni makali sana. Kisha wewe uondoke ili Uria aangushwe chini na kuuawa.”

16Hivyo Yoabu alipokuwa ameuzingira mji kwa jeshi, akamweka Uria mahali ambapo alijua kuwa ulinzi wa adui ulikuwa imara sana. 17Wakati watu wa mjini walipotoka kwenda kupigana dhidi ya Yoabu, baadhi ya watu katika jeshi la Daudi wakauawa, zaidi ya hayo, Uria, Mhiti, akafa.

18Yoabu akampelekea Daudi maelezo yote ya vita. 19Akamwagiza mjumbe hivi, “Utakapokuwa umemaliza kumpa mfalme maelezo ya vita, 20hasira ya mfalme yaweza kuwaka, naye aweza kukuuliza, ‘Kwa nini mlisogea karibu hivyo na mji kupigana? Hamkujua kuwa wangeweza kuwapiga mishale kutoka ukutani? 2111:21 Amu 8:31; 9:50-54; 2Sam 20:21; Ay 31:3Ni nani aliyemuua Abimeleki mwana wa Yerub-Besheth? Je, mwanamke hakutupa juu yake jiwe la juu la kusagia kutoka ukutani, kwa hiyo akafa huko Thebesi? Kwa nini mlisogea hivyo karibu ya ukuta?’ Ikiwa atakuuliza hivi, ndipo umwambie, ‘Pia mtumishi wako Uria, Mhiti, amekufa.’ ”

22Mjumbe akaondoka. Alipowasili akamwambia Daudi kila kitu alichokuwa ametumwa na Yoabu kusema. 23Mjumbe akamwambia Daudi, “Watu walituzidi nguvu wakatoka nje ya mji dhidi yetu kwenye eneo la wazi, lakini tuliwarudisha nyuma mpaka kwenye ingilio la mji. 24Ndipo wapiga upinde walitupa mishale kwa watumishi wako kutoka ukutani, na baadhi ya watu wa mfalme wakafa. Zaidi ya hayo, Uria, Mhiti, mtumishi wako amekufa.”

25Daudi akamwambia mjumbe, “Ukamwambie Yoabu hivi, ‘Jambo hili lisikutie wasiwasi, upanga hula huyu sawa na ulavyo mwingine. Zidisha mashambulizi dhidi ya mji na uangamize.’ Mwambie Yoabu hivi ili kumtia moyo.”

26Mke wa Uria aliposikia kwamba mumewe amekufa, akamwombolezea. 2711:27 Kum 34:8; 2Sam 12:9; Za 51:4-5; Ay 10:14; 11:11; Za 45:7; Mit 15:9; Hab 1:13Baada ya muda wa maombolezo kwisha, Daudi akamtaka aletwe nyumbani kwake, naye akawa mkewe, na akamzalia mwana. Lakini jambo alilokuwa amefanya Daudi lilimchukiza Bwana.

Священное Писание

2 Царств 11:1-27

Давуд и Вирсавия

1Весной, когда цари идут на войну, Давуд послал Иоава со своими приближёнными и всем исраильским войском, и они нанесли поражение аммонитянам и осадили их главный город Раббу. Давуд же оставался в Иерусалиме.

2Однажды вечером, поднявшись с постели, Давуд прогуливался по крыше своего дворца. С крыши он увидел купающуюся женщину. Женщина была очень красива, 3и Давуд послал разузнать о ней.

Посланный сказал:

– Это Вирсавия, дочь Элиама и жена хетта Урии.

4Тогда Давуд послал людей, чтобы привести её. Она пришла к нему, и он лёг с ней. (Она только что очистилась от своей ежемесячной нечистоты.) Затем она вернулась домой11:4 Или: «Затем она очистилась от своей нечистоты и вернулась домой». Нечистота – см. Лев. 15:18-30..

5Эта женщина забеременела и послала сказать Давуду:

– Я беременна.

6Тогда Давуд отправил Иоаву приказ:

– Пришли ко мне хетта Урию.

И Иоав послал его к Давуду. 7Когда Урия пришёл к нему, Давуд расспросил его об Иоаве, о воинах и о ходе войны. 8Затем Давуд сказал Урии:

– Ступай домой и отдохни.

И Урия вышел из царского дворца, а вслед за ним понесли царский подарок. 9Но Урия лёг спать у входа во дворец со всеми слугами своего господина и не пошёл к себе домой. 10Когда Давуду сказали: «Урия не пошёл домой», он спросил его:

– Разве ты не после дороги? Почему ты не пошёл домой?

11Урия ответил:

– Сундук соглашения, Исраил и Иудея находятся в шатрах, и мой господин Иоав, и все люди моего господина находятся в открытом поле. Как же я могу пойти домой, чтобы есть, пить и спать со своей женой? Верно, как и то, что ты жив, – я не сделаю подобного!

12Тогда Давуд сказал ему:

– Оставайся здесь и сегодня, а завтра я отправлю тебя обратно.

И Урия оставался в Иерусалиме в тот день и на следующий день. 13По приглашению Давуда он ел и пил с ним, и Давуд напоил его допьяна. Но вечером Урия вышел, чтобы лечь спать на своей циновке со слугами своего господина. Он не пошёл домой.

14Поутру Давуд написал Иоаву письмо и отправил его с Урией. 15В письме было сказано: «Поставьте Урию там, где будет самое яростное сражение, и отступите от него, чтобы он погиб». 16И когда Иоав осаждал город, он поставил Урию там, где, как он знал, были самые сильные защитники. 17Когда горожане вышли из города и сразились с Иоавом, некоторые воины из войска Давуда пали, и хетт Урия тоже был убит.

18Иоав послал Давуду подробные известия о битве. 19Он научил вестника:

– Когда ты закончишь рассказывать царю эти известия о битве, 20царь может разгневаться и спросить тебя: «Зачем вы так близко подходили к городу сражаться? Разве вы не знали, что они станут стрелять со стены стрелами? 21Кто убил Ави-Малика, сына Гедеона?11:21 Букв.: «Иеруб-Бешета» – вариант имени Иеруб-Баал, второго имени Гедеона (см. Суд. 6:32). Разве не женщина бросила в него со стены обломок жёрнова, и он умер в Тевеце?11:21 См. Суд. 9:50-54. Зачем вы так близко подходили к стене?» Если спросит у тебя это, скажи ему: «А ещё твой раб хетт Урия погиб».

22Вестник пустился в путь и, когда прибыл, передал Давуду всё, с чем послал его Иоав. 23Вестник сказал Давуду:

– Те люди наступали на нас и вышли против нас в открытое поле, но мы отогнали их обратно к городским воротам. 24Лучники стреляли в твоих рабов со стены, и некоторые из царских слуг погибли. Твой раб хетт Урия тоже погиб.

25Давуд сказал вестнику:

– Скажи Иоаву так: «Пусть это тебя не огорчает, меч поражает то одного, то другого. Соберись с силами против города и разрушь его». Скажи так, чтобы ободрить Иоава.

26Когда жена Урии услышала, что её муж погиб, она оплакивала его. 27После того как время траура миновало, Давуд привёл её в свой дом, она стала его женой и родила ему сына. Но то, что сделал Давуд, не было угодно Вечному.