2 Nyakati 9 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Nyakati 9:1-31

Malkia Wa Sheba Amtembelea Solomoni

(1 Wafalme 10:1-13)

19:1 Mwa 10:7; Eze 20:49; Lk 11:31; Mt 12:42; 13:11, 35; Za 49:4; 78:2; Mit 1:5Malkia wa Sheba aliposikia habari za umaarufu wa Solomoni, huyo malkia akaja Yerusalemu kumjaribu kwa maswali magumu. Alifika akiwa na msafara mkubwa sana, pamoja na ngamia waliobeba vikolezi, kiasi kikubwa cha dhahabu na vito vya thamani, alikuja kwa Solomoni na kuzungumza naye kuhusu yote ambayo alikuwa nayo moyoni mwake. 2Solomoni akamjibu maswali yake yote, wala hakukuwa na jambo lolote lililokuwa gumu kwake asiweze kumwelezea. 39:3 1Fal 5:12Malkia wa Sheba alipoona hekima yote ya Solomoni na jumba la kifalme alilokuwa amejenga, 4chakula kilichokuwa mezani pake, jinsi maafisa wake walivyokaa, wahudumu katika majoho yao, wanyweshaji wake na sadaka za kuteketezwa alizotoa katika Hekalu la Bwana alipatwa na mshangao.

5Akamwambia mfalme, “Taarifa niliyosikia kwenye nchi yangu mwenyewe kuhusu mafanikio na hekima yako ni kweli. 69:6 2Nya 6:32Lakini sikuamini yaliyosemwa hadi nilipokuja na kuona kwa macho yangu mwenyewe. Naam, sikuambiwa hata nusu yake; katika hekima na mali umezidi sana kuliko ile taarifa niliyoisikia. 7Heri watu wako! Heri hawa maafisa wako wasimamao mbele yako daima na kusikia hekima yako! 89:8 1Fal 2:12; 1Nya 28:5; Za 72:8-9Ahimidiwe Bwana Mungu wako, ambaye amependezwa sana nawe, na akakuweka juu ya kiti chake cha ufalme utawale kwa niaba ya Bwana Mungu wako. Kwa sababu ya upendo wa Mungu wako kwa Israeli na shauku yake ya kuwadhibitisha milele, amekufanya wewe mfalme juu yao, ili kudumisha haki na uadilifu.”

99:9 2Nya 8:18Naye akampa mfalme talanta 1209:9 Talanta 120 za dhahabu ni sawa na tani 4.5. za dhahabu, kiasi kikubwa cha vikolezi na vito vya thamani. Haikuwahi kamwe kuletwa vikolezi vizuri kama vile Malkia wa Sheba alivyompa Mfalme Solomoni.

109:10 1Fal 5:2-6; 2Nya 8:18; 1Fal 9:27-28; 10:11; Za 72:10(Watumishi wa Hiramu na wa Solomoni wakaleta dhahabu kutoka Ofiri, tena wakaleta shehena kubwa ya miti ya msandali na vito vya thamani. 11Mfalme akatumia hiyo miti ya msandali kuwa ngazi kwa ajili ya Hekalu la Bwana na kwa jumba la kifalme, pia kwa kutengeneza vinubi na zeze kwa ajili ya waimbaji. Kiasi hicho kingi cha msandali hakijawahi kuingizwa Yuda tangu siku ile.)

12Mfalme Solomoni akampa Malkia wa Sheba kila kitu alichotamani na kukiomba, zaidi ya vile alivyokuwa amemletea mfalme. Kisha malkia akaondoka na kurudi katika nchi yake, yeye na watumishi wake.

Fahari Ya Solomoni

(1 Wafalme 10:14-25)

13Uzito wa dhahabu ambayo Solomoni alipokea kwa mwaka ulikuwa talanta 666,9:13 Talanta 666 za dhahabu ni sawa na tani 25. 149:14 Isa 21:13; Eze 27:21; Yer 25:24; Isa 45:14; Za 68:29; 72:10; Isa 60:6mbali na mapato yaliyoletwa na wafanyabiashara na wachuuzi. Wafalme wote wa Arabuni na watawala wa nchi wakamletea Solomoni dhahabu na fedha.

15Mfalme Solomoni akatengeneza ngao kubwa 200 kwa dhahabu iliyofuliwa. Kila ngao ilikuwa na dhahabu yenye uzito wa shekeli 6009:15 Shekeli 600 za dhahabu ni sawa na kilo 3.5. 169:16 2Nya 12:9; 1Fal 7:2Akatengeneza pia ngao ndogo 300 za dhahabu iliyofuliwa, kila ngao ikiwa na uzito wa mane tatu9:16 Mane tatu za dhahabu ni sawa na kilo 1.7. za dhahabu. Mfalme akaziweka katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni.

179:17 1Fal 22:39Kisha mfalme akatengeneza kiti kikubwa cha kifalme kwa kutumia pembe za ndovu na kukifunika kwa dhahabu safi. 18Kiti hicho kilikuwa na ngazi sita na mahali pa kuwekea miguu vyote vya dhahabu. Pande zote za kiti kulikuwa na mahali pa kuegemeza mikono, na simba wawili wakisimama kando ya hiyo mikono. 19Simba kumi na wawili walisimama kwenye ngazi sita, mmoja katika kila upande wa kila ngazi. Hakuna kitu kama hicho kilichokuwa kimefanyika kwenye ufalme mwingine wowote. 20Vikombe vyote vya Mfalme Solomoni vya kunywea vilikuwa vya dhahabu na vyombo vyote vya nyumbani katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni vilikuwa vya dhahabu safi. Hakukuwa na kitu kilichotengenezwa kwa fedha, kwa sababu fedha ilionekana ya thamani ndogo wakati wa Solomoni. 219:21 1Fal 10:22; Isa 2:16; Yer 10:9; Yn 1:3; 1Fal 22:48; Za 48:7; Isa 60:9; Za 72:10Mfalme alikuwa na meli nyingi za biashara9:21 Au: za Tarshishi (ona pia 1Fal 10:22; 22:48; 2Nya 20:36; Isa 2:16; 60:9). baharini zilizoendeshwa na watu wa Hiramu. Kwa mara moja kila miaka mitatu zilirudi, zikiwa zimebeba dhahabu, fedha, pembe za ndovu na nyani wakubwa na wadogo.

229:22 1Fal 3:13; 2Nya 1:12; Kol 2:2-3; Mt 12:42; 1Fal 10:23-24; Za 89:27Mfalme Solomoni alikuwa mkuu zaidi kwa utajiri na hekima kuliko wafalme wote wa dunia. 239:23 1Fal 4:34Wafalme wote wa dunia wakatafuta kukutana na Solomoni ili kusikia hekima ambayo Mungu alikuwa ameiweka katika moyo wake. 249:24 Za 45:12; Isa 18:7; Za 72:10-15Mwaka baada ya mwaka, kila mmoja ambaye alikuja, alileta zawadi, vyombo vya fedha na dhahabu, majoho, silaha na vikolezi, farasi na nyumbu.

259:25 1Sam 8:11; 1Fal 4:26; 10:26; 2Nya 1:14Solomoni alikuwa na mabanda 4,000 kwa ajili ya farasi na magari ya vita, farasi 12,000 ambao aliwaweka katika miji ya magari ya vita na katika Yerusalemu pamoja naye. 269:26 1Fal 2:21; Za 72:8-9; Mwa 15:18-21; 1Fal 4:21Solomoni akatawala juu ya wafalme wote kuanzia Mto Frati mpaka kwenye nchi ya Wafilisti na kuendelea hadi mpaka wa Misri. 279:27 1Fal 10:27Mfalme akafanya fedha kuwa kitu cha kawaida kama mawe huko Yerusalemu, mierezi akaifanya kuwa mingi kama mikuyu vilimani. 289:28 Kum 17:16; 1Fal 10:26; Isa 31:1; 2:7; 2Nya 1:16Farasi wa Solomoni waliletwa kutoka Misri na kutoka nchi nyingine zote.

Kifo Cha Solomoni

(1 Wafalme 11:41-43)

299:29 2Sam 7:2; 1Nya 29:29; 1Fal 11:29; 2Nya 10:2; 12:15; 13:22Kwa habari za matukio mengine ya utawala wa Solomoni, kuanzia mwanzo hadi mwisho, je, hayakuandikwa katika kumbukumbu za nabii Nathani, katika unabii wa Ahiya Mshiloni na katika maono ya Ido mwonaji kuhusu Yeroboamu mwana wa Nebati? 309:30 1Fal 11:42-43Solomoni alitawala Israeli yote miaka arobaini, akiwa Yerusalemu. 319:31 1Fal 2:10Kisha Solomoni akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa katika mji wa Daudi baba yake. Naye Rehoboamu mwanawe akawa mfalme baada yake.

New International Reader’s Version

2 Chronicles 9:1-31

The Queen of Sheba Visits Solomon

1The queen of Sheba heard about how famous Solomon was. So she came to Jerusalem to test him with hard questions. She arrived with a very large group of attendants. Her camels were carrying spices, huge amounts of gold, and valuable jewels. She came to Solomon and asked him about everything she wanted to know. 2He answered all her questions. There wasn’t anything too hard for him to explain to her. 3So the queen of Sheba saw how wise Solomon was. She saw the palace he had built. 4She saw the food on his table. She saw his officials sitting there. She saw the robes of the servants who waited on everyone. She saw the robes the wine tasters were wearing. And she saw the burnt offerings Solomon sacrificed at the Lord’s temple. She could hardly believe everything she had seen.

5She said to the king, “Back in my own country I heard a report about you. I heard about how much you had accomplished. I also heard about how wise you are. Everything I heard is true. 6But I didn’t believe what people were saying. So I came to see for myself. And now I believe it! You are twice as wise as people say you are. The report I heard doesn’t even begin to tell the whole story about you. 7How happy your people must be! How happy your officials must be! They always get to serve you and hear the wise things you say. 8May the Lord your God be praised. He takes great delight in you. He placed you on his throne as king. He put you there to rule for him. Your God loves Israel very much. He longs to take good care of them forever. That’s why he has made you king over them. He knows that you will do what is fair and right.”

9She gave the king four and a half tons of gold. She also gave him huge amounts of spices and valuable jewels. There had never been as many spices as the queen of Sheba gave to King Solomon.

10The servants of Hiram and the servants of Solomon brought gold from Ophir. They also brought algumwood and valuable jewels. 11The king used the algumwood to make steps for the Lord’s temple and the royal palace. He also used it to make harps and lyres for those who played the music. No one had ever seen anything like those instruments in Judah before.

12King Solomon gave the queen of Sheba everything she wanted and asked for. In fact, he gave her more than she had brought to him. Then she left. She returned to her own country with her attendants.

Solomon’s Greatness

13Each year Solomon received 25 tons of gold. 14That didn’t include the money brought in by business and trade. All the kings of Arabia also brought gold and silver to Solomon. So did the governors of the territories.

15King Solomon made 200 large shields out of hammered gold. Each one weighed 15 pounds. 16He also made 300 small shields out of hammered gold. Each one weighed almost eight pounds. The king put all the shields in the Palace of the Forest of Lebanon.

17Then he made a large throne. It was covered with ivory. And that was covered with pure gold. 18The throne had six steps. A gold stool for the king’s feet was connected to it. The throne had armrests on both sides of the seat. A statue of a lion stood on each side of the throne. 19Twelve lions stood on the six steps. There was one at each end of each step. Nothing like that throne had ever been made for any other kingdom. 20All of King Solomon’s cups were made out of gold. All the things used in the Palace of the Forest of Lebanon were made out of pure gold. Nothing was made out of silver. When Solomon was king, silver wasn’t considered to be worth very much. 21He had many ships that carried goods to be traded. The crews of those ships were made up of Hiram’s servants. Once every three years the ships returned. They brought gold, silver, ivory, apes and peacocks.

22King Solomon was richer than all the other kings on earth. He was also wiser than they were. 23All these kings wanted to meet Solomon in person. They wanted to see for themselves how wise God had made him. 24Year after year, everyone who came to him brought a gift. They brought gifts made out of silver and gold. They brought robes, weapons and spices. They also brought horses and mules.

25Solomon had 4,000 spaces where he kept his horses and chariots. He had 12,000 horses. He kept some of his horses and chariots in the chariot cities. He kept the others with him in Jerusalem. 26Solomon ruled over all the kings from the Euphrates River to the land of the Philistines. He ruled all the way to the border of Egypt. 27The king made silver as common in Jerusalem as stones. He made cedar wood as common there as sycamore-fig trees in the western hills. 28Solomon got horses from Egypt. He also got them from many other countries.

Solomon Dies

29The other events of Solomon’s rule from beginning to end are written down. They are written in the records of Nathan the prophet. They are written in the prophecy of Ahijah. He was from Shiloh. They are also written in the records of the visions of Iddo the prophet about Jeroboam. Jeroboam was the son of Nebat. 30Solomon ruled in Jerusalem over the whole nation of Israel for 40 years. 31Then he joined the members of his family who had already died. He was buried in the city of his father David. Solomon’s son Rehoboam became the next king after him.