2 Nyakati 7 – NEN & NUB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Nyakati 7:1-22

Hekalu Lawekwa Wakfu

(1 Wafalme 8:62-66)

17:1 Kut 19:18; Mwa 15:17; Law 9:24; Kut 16:10; Dan 9:20; 1Fal 8:54; Isa 65:24; Mdo 4:31; Amu 6:21; 1Fal 18:38; 1Nya 21:26; 2Nya 5:13; Eze 10:3; Ufu 21:23Baada ya Solomoni kumaliza kuomba, moto ukashuka kutoka mbinguni na kuteketeza sadaka ya kuteketezwa na dhabihu, nao utukufu wa Bwana ukalijaza Hekalu. 27:2 2Nya 5:14; Kut 29:43; 1Fal 8:11Makuhani hawakuweza kuingia ndani ya Hekalu la Bwana kwa sababu utukufu wa Bwana ulilijaza. 37:3 1Nya 16:34; Ezr 3:11; 2Nya 5:13; 20:13; 20:21; Za 103:17Waisraeli wote walipoona moto ukishuka na utukufu wa Bwana ukiwa juu ya Hekalu, wakapiga magoti sakafuni wakasujudu nyuso zao mpaka chini, nao wakamwabudu na kumshukuru Bwana wakisema,

“Yeye ni mwema;

upendo wake unadumu milele.”

47:4 1Fal 8:62Ndipo mfalme na watu wote wakatoa dhabihu mbele za Bwana Mungu. 5Naye Mfalme Solomoni akatoa dhabihu ya ngʼombe 22,000 pamoja na kondoo na mbuzi 120,000. Hivyo ndivyo mfalme na watu wote walivyoweka wakfu Hekalu la Mungu. 67:6 1Nya 15:16-24; 2Nya 5:12Makuhani wakasimama kwenye nafasi zao, vivyo hivyo Walawi wakiwa na vyombo vya uimbaji vya Bwana ambavyo Mfalme Daudi alikuwa ametengeneza kwa ajili ya kumsifu Bwana, navyo vilitumika wakati aliposhukuru, akisema, “Upendo wake wadumu milele.” Mkabala na Walawi, makuhani walipiga tarumbeta zao, nao Waisraeli wote walikuwa wamesimama.

77:7 Hes 16:37; 2Nya 36:14; Ebr 13:10-12; 1Fal 8:64Solomoni akaweka wakfu sehemu ya katikati ya ua uliokuwa mbele ya Hekalu la Bwana na hapo akatoa sadaka za kuteketezwa na mafuta ya sadaka za amani, kwa sababu madhabahu ya shaba aliyokuwa ametengeneza haikutosha kuweka sadaka hizo zote za kuteketezwa, sadaka za nafaka na za mafuta.

87:8 2Nya 30:26; Mwa 15:18; Neh 8:17; Yos 13:3Hivyo Solomoni akaiadhimisha sikukuu wakati ule kwa muda wa siku saba, na Israeli wote pamoja naye. Walikuwa kusanyiko kubwa sana, watu kutoka Lebo-Hamathi hadi Kijito cha Misri. 97:9 Law 23:36Katika siku ya nane walifanya kusanyiko, kwa kuwa walikuwa wanaadhimisha kuwekwa wakfu kwa madhabahu kwa muda wa siku saba na sikukuu kwa muda wa siku nyingine saba zaidi. 10Katika siku ya ishirini na tatu ya mwezi wa saba Solomoni akawaaga watu waende nyumbani mwao, wakishangilia na kufurahi mioyoni mwao, kwa wema mwingi Bwana Mungu aliomtendea Daudi na Solomoni na kwa ajili ya watu wake Israeli.

Bwana Mungu Amtokea Solomoni

(1 Wafalme 9:1-9)

11Solomoni alipomaliza kujenga Hekalu la Bwana na jumba la kifalme, naye akiwa amefanikiwa kutenda yale yote aliyokuwa nayo moyoni mwake kufanya katika Hekalu la Bwana na katika jumba lake mwenyewe la kifalme, 127:12 Kum 12:5; Mwa 12:7; Za 78:68-69Bwana akamtokea Solomoni usiku na kumwambia:

“Nimesikia maombi yako nami nimechagua mahali hapa kwa ajili yangu mwenyewe kuwa Hekalu kwa ajili ya dhabihu.

137:13 2Nya 6:26; Kum 11:17; Amo 4:7“Wakati nitakapofunga mbingu ili isiwepo mvua, au nikiamuru nzige kula mazao ya nchi au nikituma tauni miongoni mwa watu wangu, 147:14 Yak 4:10; Eze 18:32; Kut 10:3; 1Nya 16:11; Kut 15:26; 2Nya 6:27kama watu wangu, wanaoitwa kwa Jina langu, watajinyenyekesha na kuomba na kuutafuta uso wangu na kuacha njia zao mbaya, basi nitasikia toka mbinguni na kuwasamehe dhambi yao na nitaiponya nchi yao. 157:15 1Fal 8:29; 2Nya 6:40; Neh 1:6Sasa macho yangu yatafumbuka na masikio yangu yatasikiliza kwa makini maombi yaombwayo mahali hapa. 167:16 Kum 12:5; 2Nya 6:6Kwa maana sasa nimechagua na kutakasa Hekalu hili ili kwamba Jina langu lipate kuwa huko milele. Macho yangu na moyo wangu utakuwepo huko daima.

177:17 1Fal 9:4“Kwa habari yako wewe, kama ukienenda mbele zangu kama Daudi baba yako alivyoenenda na kufanya yote nikuamuruyo, nawe ukizishika amri zangu na sheria zangu, 187:18 Mik 5:2; 2Sam 17:13; 1Nya 17:12; 2Nya 6:16Nitakiimarisha kiti chako cha enzi kama nilivyoagana na Daudi baba yako niliposema, ‘Hutakosa kamwe mtu wa kutawala juu ya Israeli.’

197:19 Kum 28:15; Law 26:14, 33“Lakini kama ukigeuka na kuyaacha maagizo na amri nilizowapa na kwenda kuitumikia miungu mingine na kuiabudu, 207:20 Kum 28:37; 29:28; 1Fal 14:15; Yer 12:14; 16:13; 50:11; Za 5:5ndipo nitakapoingʼoa Israeli kutoka nchi yangu niliyowapa, nami nitalikataa Hekalu hili nililolitakasa kwa ajili ya Jina langu. Nitalifanya kitu cha kudharauliwa na kitu cha kudhihakiwa miongoni mwa watu wote. 217:21 Kum 29:24; Yer 22:8; Mao 2:15; Yer 7:14Ingawa Hekalu hili linavutia sana sasa, wote watakaolipita watashangaa na kusema, ‘Kwa nini Bwana amefanya kitu kama hiki katika nchi hii na kwa Hekalu hili?’ 227:22 Amu 2:13; Dan 9:12; 2Fal 17:18; 2Nya 36:16Watu watajibu, ‘Ni kwa sababu wamemwacha Bwana, Mungu wa baba zao, aliyewatoa Misri, nao wamekumbatia miungu mingine, wakaiabudu na kuitumikia, ndiyo sababu ameyaleta maafa haya yote juu yao.’ ”

Swedish Contemporary Bible

2 Krönikeboken 7:1-22

Herrens härlighet fyller templet

(1 Kung 8:62-66)

1När Salomo hade slutat att be, kom eld ner från himlen och förtärde brännoffret och slaktoffren. Herrens härlighet uppfyllde templet. 2Prästerna kunde inte gå in i Herrens hus, eftersom Herrens härlighet uppfyllde det. 3När alla israeliterna såg hur elden och Herrens härlighet kom ner över templet, föll de ner med ansiktet mot marken och tillbad och prisade Herren:

”Han är god

och hans nåd varar i evighet!”

4Kungen och allt folket frambar offer till Herren. 5Kung Salomo offrade 22 000 tjurar och 120 000 får och getter. Så invigde kungen och hela folket Guds hus. 6Prästerna intog sina platser, och leviterna stod med Herrens musikinstrument, som kung David gjort för tacksägelse och själv använt för att prisa Herren: ”Hans nåd varar i evighet.” Prästerna, som stod mitt emot leviterna, blåste i sina trumpeter, och alla israeliterna stod upp.

7Salomo helgade den mellersta delen av förgården framför Herrens hus, och där offrade han brännoffer och matoffer och fettstycken av gemenskapsoffer, då kopparaltaret som Salomo gjort inte kunde rymma allt brännoffer och matoffer och fettstyckena.

8Salomo firade högtiden i sju dagar tillsammans med hela Israel, en mycket stor församling, ända från Levo-Hamat till Egyptens bäck. 9Den åttonde dagen hölls en högtidssamling, för de hade firat altarets invigning i sju dagar och högtiden i sju dagar. 10Men på den tjugotredje dagen i sjunde månaden skickade han hem folket, som var glada och lyckliga över allt det goda Herren hade gjort mot David och Salomo och mot sitt folk Israel.

Gud talar till Salomo

(1 Kung 9:1-9)

11Salomo färdigställde så Herrens hus och kungapalatset. Han lyckades med allt han föresatt sig att göra i Herrens hus och i sitt eget palats. 12Då visade sig Herren en natt för Salomo och sa:

”Jag har hört din bön och valt denna plats åt mig för offer.

13Om jag stänger till himlen, så att det inte kommer något regn, eller om jag befaller gräshoppor att härja landet, eller om jag sänder epidemier över mitt folk, 14och mitt folk, som är kallat efter mitt namn, då ödmjukar sig och ber till mig, söker mig och vänder om från sina onda vägar, ska jag lyssna till dem från himlen och förlåta deras synder och bota deras land. 15Jag ska öppna mina ögon och öron till de böner som bes på den här platsen. 16Jag har nu valt och helgat det här templet för att mitt namn ska bo där för evigt. Mina ögon och mitt hjärta ska alltid vara här.

17Om du nu vandrar mina vägar, så som din far David gjorde inför mig, och i allting gör som jag befallt, följer mina bud och föreskrifter, 18ska jag låta ditt kungadöme bestå, som jag lovade din far David: Det ska aldrig saknas en ättling till dig som regerar över Israel.

19Men om ni vänder er bort och överger de bud och befallningar som jag gett er och börjar tjäna andra gudar och tillbe dem, 20då ska jag rycka upp dem ur mitt land, som jag gav dem, och förkasta detta hus som är helgat åt mitt namn. Jag ska låta det bli till ordspråk och nidvisa bland alla folk. 21Detta hus, som nu är så imponerande, ska var och en som går förbi, se på och häpet säga: Varför har Herren gjort så med detta land och detta tempel? 22Svaret ska bli: ’Därför att de har övergett Herren, sina fäders Gud, som förde dem ut ur Egypten, och i stället hållit sig till andra gudar, tillbett och tjänat dem. Det är därför han lät allt detta onda drabba dem.’ ”