2 Nyakati 7 – NEN & BDS

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Nyakati 7:1-22

Hekalu Lawekwa Wakfu

(1 Wafalme 8:62-66)

17:1 Kut 19:18; Mwa 15:17; Law 9:24; Kut 16:10; Dan 9:20; 1Fal 8:54; Isa 65:24; Mdo 4:31; Amu 6:21; 1Fal 18:38; 1Nya 21:26; 2Nya 5:13; Eze 10:3; Ufu 21:23Baada ya Solomoni kumaliza kuomba, moto ukashuka kutoka mbinguni na kuteketeza sadaka ya kuteketezwa na dhabihu, nao utukufu wa Bwana ukalijaza Hekalu. 27:2 2Nya 5:14; Kut 29:43; 1Fal 8:11Makuhani hawakuweza kuingia ndani ya Hekalu la Bwana kwa sababu utukufu wa Bwana ulilijaza. 37:3 1Nya 16:34; Ezr 3:11; 2Nya 5:13; 20:13; 20:21; Za 103:17Waisraeli wote walipoona moto ukishuka na utukufu wa Bwana ukiwa juu ya Hekalu, wakapiga magoti sakafuni wakasujudu nyuso zao mpaka chini, nao wakamwabudu na kumshukuru Bwana wakisema,

“Yeye ni mwema;

upendo wake unadumu milele.”

47:4 1Fal 8:62Ndipo mfalme na watu wote wakatoa dhabihu mbele za Bwana Mungu. 5Naye Mfalme Solomoni akatoa dhabihu ya ngʼombe 22,000 pamoja na kondoo na mbuzi 120,000. Hivyo ndivyo mfalme na watu wote walivyoweka wakfu Hekalu la Mungu. 67:6 1Nya 15:16-24; 2Nya 5:12Makuhani wakasimama kwenye nafasi zao, vivyo hivyo Walawi wakiwa na vyombo vya uimbaji vya Bwana ambavyo Mfalme Daudi alikuwa ametengeneza kwa ajili ya kumsifu Bwana, navyo vilitumika wakati aliposhukuru, akisema, “Upendo wake wadumu milele.” Mkabala na Walawi, makuhani walipiga tarumbeta zao, nao Waisraeli wote walikuwa wamesimama.

77:7 Hes 16:37; 2Nya 36:14; Ebr 13:10-12; 1Fal 8:64Solomoni akaweka wakfu sehemu ya katikati ya ua uliokuwa mbele ya Hekalu la Bwana na hapo akatoa sadaka za kuteketezwa na mafuta ya sadaka za amani, kwa sababu madhabahu ya shaba aliyokuwa ametengeneza haikutosha kuweka sadaka hizo zote za kuteketezwa, sadaka za nafaka na za mafuta.

87:8 2Nya 30:26; Mwa 15:18; Neh 8:17; Yos 13:3Hivyo Solomoni akaiadhimisha sikukuu wakati ule kwa muda wa siku saba, na Israeli wote pamoja naye. Walikuwa kusanyiko kubwa sana, watu kutoka Lebo-Hamathi hadi Kijito cha Misri. 97:9 Law 23:36Katika siku ya nane walifanya kusanyiko, kwa kuwa walikuwa wanaadhimisha kuwekwa wakfu kwa madhabahu kwa muda wa siku saba na sikukuu kwa muda wa siku nyingine saba zaidi. 10Katika siku ya ishirini na tatu ya mwezi wa saba Solomoni akawaaga watu waende nyumbani mwao, wakishangilia na kufurahi mioyoni mwao, kwa wema mwingi Bwana Mungu aliomtendea Daudi na Solomoni na kwa ajili ya watu wake Israeli.

Bwana Mungu Amtokea Solomoni

(1 Wafalme 9:1-9)

11Solomoni alipomaliza kujenga Hekalu la Bwana na jumba la kifalme, naye akiwa amefanikiwa kutenda yale yote aliyokuwa nayo moyoni mwake kufanya katika Hekalu la Bwana na katika jumba lake mwenyewe la kifalme, 127:12 Kum 12:5; Mwa 12:7; Za 78:68-69Bwana akamtokea Solomoni usiku na kumwambia:

“Nimesikia maombi yako nami nimechagua mahali hapa kwa ajili yangu mwenyewe kuwa Hekalu kwa ajili ya dhabihu.

137:13 2Nya 6:26; Kum 11:17; Amo 4:7“Wakati nitakapofunga mbingu ili isiwepo mvua, au nikiamuru nzige kula mazao ya nchi au nikituma tauni miongoni mwa watu wangu, 147:14 Yak 4:10; Eze 18:32; Kut 10:3; 1Nya 16:11; Kut 15:26; 2Nya 6:27kama watu wangu, wanaoitwa kwa Jina langu, watajinyenyekesha na kuomba na kuutafuta uso wangu na kuacha njia zao mbaya, basi nitasikia toka mbinguni na kuwasamehe dhambi yao na nitaiponya nchi yao. 157:15 1Fal 8:29; 2Nya 6:40; Neh 1:6Sasa macho yangu yatafumbuka na masikio yangu yatasikiliza kwa makini maombi yaombwayo mahali hapa. 167:16 Kum 12:5; 2Nya 6:6Kwa maana sasa nimechagua na kutakasa Hekalu hili ili kwamba Jina langu lipate kuwa huko milele. Macho yangu na moyo wangu utakuwepo huko daima.

177:17 1Fal 9:4“Kwa habari yako wewe, kama ukienenda mbele zangu kama Daudi baba yako alivyoenenda na kufanya yote nikuamuruyo, nawe ukizishika amri zangu na sheria zangu, 187:18 Mik 5:2; 2Sam 17:13; 1Nya 17:12; 2Nya 6:16Nitakiimarisha kiti chako cha enzi kama nilivyoagana na Daudi baba yako niliposema, ‘Hutakosa kamwe mtu wa kutawala juu ya Israeli.’

197:19 Kum 28:15; Law 26:14, 33“Lakini kama ukigeuka na kuyaacha maagizo na amri nilizowapa na kwenda kuitumikia miungu mingine na kuiabudu, 207:20 Kum 28:37; 29:28; 1Fal 14:15; Yer 12:14; 16:13; 50:11; Za 5:5ndipo nitakapoingʼoa Israeli kutoka nchi yangu niliyowapa, nami nitalikataa Hekalu hili nililolitakasa kwa ajili ya Jina langu. Nitalifanya kitu cha kudharauliwa na kitu cha kudhihakiwa miongoni mwa watu wote. 217:21 Kum 29:24; Yer 22:8; Mao 2:15; Yer 7:14Ingawa Hekalu hili linavutia sana sasa, wote watakaolipita watashangaa na kusema, ‘Kwa nini Bwana amefanya kitu kama hiki katika nchi hii na kwa Hekalu hili?’ 227:22 Amu 2:13; Dan 9:12; 2Fal 17:18; 2Nya 36:16Watu watajibu, ‘Ni kwa sababu wamemwacha Bwana, Mungu wa baba zao, aliyewatoa Misri, nao wamekumbatia miungu mingine, wakaiabudu na kuitumikia, ndiyo sababu ameyaleta maafa haya yote juu yao.’ ”

La Bible du Semeur

2 Chroniques 7:1-22

La gloire de l’Eternel remplit le Temple

(1 R 8.62-66)

1Lorsque Salomon eut terminé sa prière, le feu tomba du ciel et consuma l’holocauste ainsi que les sacrifices, et la gloire de l’Eternel remplit le Temple7.1 Voir Lv 9.23-24.. 2Les prêtres ne pouvaient pénétrer dans le temple de l’Eternel, car la gloire de l’Eternel avait rempli l’édifice. 3Tous les Israélites virent descendre le feu et la gloire de l’Eternel sur le Temple ; ils s’inclinèrent le visage contre terre sur le dallage du parvis, se prosternèrent et se mirent à louer l’Eternel en disant : « Oui il est bon, oui son amour est éternel ! »

4Le roi et tout le peuple offrirent des sacrifices devant l’Eternel. 5Le roi Salomon offrit en sacrifice 22 000 bœufs et 120 000 moutons. C’est de cette manière que le roi et tout le peuple inaugurèrent le temple de Dieu. 6Les prêtres se tenaient à leur poste, les lévites prirent position avec les instruments de musique de l’Eternel que le roi David avait conçus pour louer l’Eternel en chantant : « Oui, son amour dure à toujours » ; c’est David qui les avait chargés de jouer de ces instruments pour louer l’Eternel. Quant aux prêtres, ils faisaient retentir les trompettes vis-à-vis d’eux et tout Israël se tenait debout.

7Salomon consacra l’intérieur de la cour qui s’étend devant le temple de l’Eternel pour y offrir les holocaustes et les graisses des sacrifices de communion, car l’autel de bronze que Salomon avait fait fabriquer ne pouvait recevoir tous les holocaustes, les offrandes et les graisses. 8Salomon et tout Israël célébrèrent la fête7.8 Il s’agit de la fête des Cabanes (voir 5.3). pendant sept jours. Un très grand nombre de gens étaient venus depuis la région de Hamath jusqu’au torrent d’Egypte7.8 C’est-à-dire de l’extrême nord à l’extrême sud du pays. Le torrent d’Egypte est sans doute le Wadi el-Arish qui a son embouchure à quelque 80 kilomètres au sud de Gaza.. 9Le huitième jour eut lieu une réunion cultuelle. Ainsi, on avait fait la dédicace de l’autel pendant sept jours, et l’on avait célébré la fête durant sept autres jours7.9 La fête de la Dédicace avait duré du 8e au 14e jour du mois, la fête des Cabanes du 15e au 22e jour.. 10Le vingt-troisième jour du septième mois, Salomon renvoya le peuple chacun chez soi. Tous étaient joyeux et avaient le cœur content à cause des bienfaits que l’Eternel avait accordés à David, à Salomon et à Israël, son peuple.

La réponse de l’Eternel à Salomon

(1 R 9.1-9)

11Salomon acheva ainsi le temple de l’Eternel et le palais royal. Il réussit à réaliser tout ce qu’il s’était proposé de faire pour ces deux édifices. 12Alors l’Eternel apparut à Salomon pendant la nuit et lui dit : J’ai exaucé ta prière et je choisis cet endroit comme lieu de sacrifices pour moi. 13Lorsque je fermerai le ciel et qu’il n’y aura pas de pluie, lorsque j’ordonnerai aux sauterelles de ravager le pays ou que j’enverrai la peste contre mon peuple, 14si alors mon peuple qui est appelé de mon nom s’humilie, prie et recherche ma grâce, s’il se détourne de sa mauvaise conduite, moi, je l’écouterai du ciel, je lui pardonnerai ses péchés et je guérirai son pays. 15Désormais, j’écouterai attentivement et je considérerai favorablement la prière faite en ce lieu. 16A présent, je choisis cet édifice et j’en fais un lieu saint pour y être à jamais présent. Je veillerai toujours sur lui et j’y aurai mon cœur. 17Quant à toi, si tu te conduis devant moi comme ton père David, si tu fais tout ce que je t’ai ordonné et si tu obéis aux ordonnances et aux lois que je t’ai données, 18je rendrai stable pour toujours ton trône royal selon l’alliance que j’ai conclue avec ton père David lorsque je lui ai dit : « Il y aura toujours l’un de tes descendants qui gouvernera Israël7.18 Voir 1 R 2.4.. » 19Mais si vous vous détournez, si vous négligez mes ordonnances et mes lois que j’ai établies pour vous, et si vous allez rendre un culte à d’autres dieux et vous prosterner devant eux, 20alors je vous arracherai de mon pays que je vous ai donné, je rejetterai loin de ma vue ce temple que j’ai consacré pour y être présent, et je ferai en sorte que tous les peuples s’en moquent et ricanent à son sujet. 21Et ce temple qui aura été si glorieux, tous ceux qui passeront à proximité seront consternés et s’exclameront : « Pourquoi l’Eternel a-t-il traité ainsi ce pays et ce temple7.21 Voir 2 Ch 36.19. ? » 22Et l’on répondra : « C’est parce qu’ils ont abandonné l’Eternel, le Dieu de leurs ancêtres, qui les avait fait sortir d’Egypte, parce qu’ils se sont attachés à d’autres dieux, qu’ils se sont prosternés devant eux et les ont adorés. Voilà pourquoi il leur a infligé tout ce malheur. »