2 Nyakati 4 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Nyakati 4:1-22

Vifaa Vya Hekalu

(1 Wafalme 7:23-51)

14:1 Eze 43:13; Kut 27:1-2; 2Fal 16:14; 1Fal 9:25Mfalme Solomoni akatengeneza madhabahu ya shaba yenye urefu wa dhiraa ishirini,4:1 Dhiraa 20 ni sawa na mita 9. upana wa dhiraa ishirini na kimo chake dhiraa kumi.4:1 Dhiraa 10 ni sawa na mita 4.5. 24:2 Kut 30:18; Ufu 4:6; 15:2; 1Fal 7:23Akatengeneza Bahari ya kusubu, yenye umbo la mviringo, ya dhiraa kumi kutoka ukingo hadi ukingo na kimo cha dhiraa tano. Kamba ya urefu wa dhiraa thelathini4:2 Dhiraa 30 ni sawa na mita 13.5. ingeweza kuizunguka. 34:3 1Fal 7:24Chini ya huo ukingo, kulikuwa na mafahali kuizunguka, yaani mafahali kumi katika kila dhiraa moja.4:3 Dhiraa moja ni sawa na sentimita 45. Hayo mafahali waliyasubu katika safu mbili yakiwa ya kitu kimoja na hiyo Bahari.

44:4 Eze 48:30-34; Ufu 21:13Bahari hiyo ilikaa juu ya mafahali kumi na wawili, mafahali watatu walielekeza nyuso zao kaskazini, watatu magharibi, watatu kusini na watatu mashariki. Bahari hiyo ilikaa juu ya hao mafahali, nazo sehemu zao za nyuma zilielekeana. 54:5 1Fal 7:26Unene wake ulikuwa nyanda nne,4:5 Nyanda nne ni sawa na sentimita 7.5. na ukingo wake ulifanana na ukingo wa kikombe, kama ua la yungiyungi iliyochanua. Iliweza kuchukua bathi 3,000.4:5 Bathi 3,000 ni sawa na lita 60,000.

64:6 Kut 30:18; 1Fal 7:26; Ebr 9:9; 4:7Kisha akatengeneza masinia kumi kwa ajili ya kuoshea vifaa, naye akayaweka matano upande wa kusini na matano upande wa kaskazini. Ndani yake ndimo walioshea vifaa vya kutumika katika sadaka za kuteketezwa, lakini ile Bahari ilikuwa ni kwa ajili ya makuhani kunawia.

74:7 Kut 25:31, 40; 1Fal 7:49Akatengeneza vinara vya taa kumi vya dhahabu kama ilivyoainishwa kwao na kuviweka hekaluni, vinara vitano upande wa kusini na vitano upande wa kaskazini.

84:8 Kut 25:23; Hes 4:14; 1Fal 7:48-49Akatengeneza meza kumi na kuziweka hekaluni, tano upande wa kusini na tano upande wa kaskazini. Pia akatengeneza mabakuli 100 ya dhahabu ya kunyunyizia.

94:9 2Fal 21:5; 2Nya 33:5Akatengeneza ukumbi wa makuhani na ukumbi mwingine mkubwa na milango yake, naye akaifunika hiyo milango kwa shaba. 10Akaweka ile Bahari upande wa kusini, kwenye pembe ya kusini mashariki ya nyumba.

114:11 1Fal 7:14Pia akatengeneza masufuria, masepetu na mabakuli ya kunyunyizia.

Kwa hiyo Huramu akakamilisha kazi katika Hekalu la Mungu kama vile Mfalme Solomoni alikuwa amemwagiza, yaani:

12zile nguzo mbili;

yale mataji mawili yaliyokuwa juu ya hizo nguzo,

zile nyavu mbili za kupamba hayo mataji mawili yenye umbo la bakuli yaliyowekwa juu ya zile nguzo;

134:13 Yer 52:23; Wim 4:13; Kut 28:33-34; 1Fal 7:20yale makomamanga 400 kwa ajili ya hizo nyavu mbili (safu mbili za makomamanga kwa kila wavu yakipamba hayo mataji mawili yenye umbo la bakuli juu ya hizo nguzo);

144:14 1Fal 7:27-30vishikio pamoja na masinia yake;

15hiyo Bahari na hao mafahali kumi na wawili chini yake;

16pia hayo masufuria, masepetu, uma za nyama na vyombo vingine vyote vilivyohusiana.

Vitu vyote ambavyo Huramu-Abi alimtengenezea Mfalme Solomoni kwa ajili ya Hekalu la Bwana vilikuwa vya shaba iliyosuguliwa. 174:17 Mwa 33:17; 1Fal 7:46Mfalme aliagiza wavisubu vitu hivi kwenye kalibu za udongo wa mfinyanzi katika uwanda wa Yordani kati ya Sukothi na Sereda.4:17 Au Sarethani. 184:18 1Fal 7:23, 47Vitu hivi vyote Mfalme Solomoni alivyotengeneza vilikuwa vingi sana hivi kwamba uzito wa shaba haungekadirika.

194:19 Kut 25:23, 30; 2Fal 24:13; Dan 5:2-3; Yer 28:3; 1Nya 28:6Solomoni pia akatengeneza samani zote zilizokuwa ndani ya Hekalu la Mungu:

madhabahu ya dhahabu;

meza za kuweka mikate ya Wonyesho;

204:20 Kut 27:20-21vinara vya taa vya dhahabu safi pamoja na taa zake ili ziwake mbele ya sehemu takatifu ya ndani kama ilivyoelekezwa;

214:21 Kut 37:20; 1Fal 6:18-35; Kut 25:31maua ya dhahabu yaliyofanyizwa, taa na makoleo (vilikuwa vya dhahabu bora kabisa);

224:22 Hes 7:14; Law 10:1; 1Fal 6:21mikasi ya dhahabu safi, mabakuli ya kunyunyizia, masinia na vyetezo; milango ya dhahabu ya Hekalu: yaani milango ya ndani ya Patakatifu pa Patakatifu, na milango ya ukumbi mkuu.

King James Version

2 Chronicles 4:1-22

1Moreover he made an altar of brass, twenty cubits the length thereof, and twenty cubits the breadth thereof, and ten cubits the height thereof.

2¶ Also he made a molten sea of ten cubits from brim to brim, round in compass, and five cubits the height thereof; and a line of thirty cubits did compass it round about.4.2 from…: Heb. from his brim to his brim 3And under it was the similitude of oxen, which did compass it round about: ten in a cubit, compassing the sea round about. Two rows of oxen were cast, when it was cast. 4It stood upon twelve oxen, three looking toward the north, and three looking toward the west, and three looking toward the south, and three looking toward the east: and the sea was set above upon them, and all their hinder parts were inward. 5And the thickness of it was an handbreadth, and the brim of it like the work of the brim of a cup, with flowers of lilies; and it received and held three thousand baths.4.5 with flowers…: or, like a lilyflower

6¶ He made also ten lavers, and put five on the right hand, and five on the left, to wash in them: such things as they offered for the burnt offering they washed in them; but the sea was for the priests to wash in.4.6 such…: Heb. the work of burnt offering 7And he made ten candlesticks of gold according to their form, and set them in the temple, five on the right hand, and five on the left. 8He made also ten tables, and placed them in the temple, five on the right side, and five on the left. And he made an hundred basons of gold.4.8 basons: or, bowls

9¶ Furthermore he made the court of the priests, and the great court, and doors for the court, and overlaid the doors of them with brass. 10And he set the sea on the right side of the east end, over against the south.

11And Huram made the pots, and the shovels, and the basons. And Huram finished the work that he was to make for king Solomon for the house of God;4.11 basons: or, bowls4.11 finished: Heb. finished to make 12To wit, the two pillars, and the pommels, and the chapiters which were on the top of the two pillars, and the two wreaths to cover the two pommels of the chapiters which were on the top of the pillars; 13And four hundred pomegranates on the two wreaths; two rows of pomegranates on each wreath, to cover the two pommels of the chapiters which were upon the pillars.4.13 upon: Heb. upon the face of 14He made also bases, and lavers made he upon the bases;4.14 lavers: or, caldrons 15One sea, and twelve oxen under it. 16The pots also, and the shovels, and the fleshhooks, and all their instruments, did Huram his father make to king Solomon for the house of the LORD of bright brass.4.16 bright: Heb. made bright, or, scoured 17In the plain of Jordan did the king cast them, in the clay ground between Succoth and Zeredathah.4.17 clay…: Heb. thicknesses of the ground 18Thus Solomon made all these vessels in great abundance: for the weight of the brass could not be found out.

19¶ And Solomon made all the vessels that were for the house of God, the golden altar also, and the tables whereon the shewbread was set; 20Moreover the candlesticks with their lamps, that they should burn after the manner before the oracle, of pure gold; 21And the flowers, and the lamps, and the tongs, made he of gold, and that perfect gold;4.21 perfect…: Heb. perfections of gold 22And the snuffers, and the basons, and the spoons, and the censers, of pure gold: and the entry of the house, the inner doors thereof for the most holy place, and the doors of the house of the temple, were of gold.4.22 basons: or, bowls