2 Nyakati 4 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Nyakati 4:1-22

Vifaa Vya Hekalu

(1 Wafalme 7:23-51)

14:1 Eze 43:13; Kut 27:1-2; 2Fal 16:14; 1Fal 9:25Mfalme Solomoni akatengeneza madhabahu ya shaba yenye urefu wa dhiraa ishirini,4:1 Dhiraa 20 ni sawa na mita 9. upana wa dhiraa ishirini na kimo chake dhiraa kumi.4:1 Dhiraa 10 ni sawa na mita 4.5. 24:2 Kut 30:18; Ufu 4:6; 15:2; 1Fal 7:23Akatengeneza Bahari ya kusubu, yenye umbo la mviringo, ya dhiraa kumi kutoka ukingo hadi ukingo na kimo cha dhiraa tano. Kamba ya urefu wa dhiraa thelathini4:2 Dhiraa 30 ni sawa na mita 13.5. ingeweza kuizunguka. 34:3 1Fal 7:24Chini ya huo ukingo, kulikuwa na mafahali kuizunguka, yaani mafahali kumi katika kila dhiraa moja.4:3 Dhiraa moja ni sawa na sentimita 45. Hayo mafahali waliyasubu katika safu mbili yakiwa ya kitu kimoja na hiyo Bahari.

44:4 Eze 48:30-34; Ufu 21:13Bahari hiyo ilikaa juu ya mafahali kumi na wawili, mafahali watatu walielekeza nyuso zao kaskazini, watatu magharibi, watatu kusini na watatu mashariki. Bahari hiyo ilikaa juu ya hao mafahali, nazo sehemu zao za nyuma zilielekeana. 54:5 1Fal 7:26Unene wake ulikuwa nyanda nne,4:5 Nyanda nne ni sawa na sentimita 7.5. na ukingo wake ulifanana na ukingo wa kikombe, kama ua la yungiyungi iliyochanua. Iliweza kuchukua bathi 3,000.4:5 Bathi 3,000 ni sawa na lita 60,000.

64:6 Kut 30:18; 1Fal 7:26; Ebr 9:9; 4:7Kisha akatengeneza masinia kumi kwa ajili ya kuoshea vifaa, naye akayaweka matano upande wa kusini na matano upande wa kaskazini. Ndani yake ndimo walioshea vifaa vya kutumika katika sadaka za kuteketezwa, lakini ile Bahari ilikuwa ni kwa ajili ya makuhani kunawia.

74:7 Kut 25:31, 40; 1Fal 7:49Akatengeneza vinara vya taa kumi vya dhahabu kama ilivyoainishwa kwao na kuviweka hekaluni, vinara vitano upande wa kusini na vitano upande wa kaskazini.

84:8 Kut 25:23; Hes 4:14; 1Fal 7:48-49Akatengeneza meza kumi na kuziweka hekaluni, tano upande wa kusini na tano upande wa kaskazini. Pia akatengeneza mabakuli 100 ya dhahabu ya kunyunyizia.

94:9 2Fal 21:5; 2Nya 33:5Akatengeneza ukumbi wa makuhani na ukumbi mwingine mkubwa na milango yake, naye akaifunika hiyo milango kwa shaba. 10Akaweka ile Bahari upande wa kusini, kwenye pembe ya kusini mashariki ya nyumba.

114:11 1Fal 7:14Pia akatengeneza masufuria, masepetu na mabakuli ya kunyunyizia.

Kwa hiyo Huramu akakamilisha kazi katika Hekalu la Mungu kama vile Mfalme Solomoni alikuwa amemwagiza, yaani:

12zile nguzo mbili;

yale mataji mawili yaliyokuwa juu ya hizo nguzo,

zile nyavu mbili za kupamba hayo mataji mawili yenye umbo la bakuli yaliyowekwa juu ya zile nguzo;

134:13 Yer 52:23; Wim 4:13; Kut 28:33-34; 1Fal 7:20yale makomamanga 400 kwa ajili ya hizo nyavu mbili (safu mbili za makomamanga kwa kila wavu yakipamba hayo mataji mawili yenye umbo la bakuli juu ya hizo nguzo);

144:14 1Fal 7:27-30vishikio pamoja na masinia yake;

15hiyo Bahari na hao mafahali kumi na wawili chini yake;

16pia hayo masufuria, masepetu, uma za nyama na vyombo vingine vyote vilivyohusiana.

Vitu vyote ambavyo Huramu-Abi alimtengenezea Mfalme Solomoni kwa ajili ya Hekalu la Bwana vilikuwa vya shaba iliyosuguliwa. 174:17 Mwa 33:17; 1Fal 7:46Mfalme aliagiza wavisubu vitu hivi kwenye kalibu za udongo wa mfinyanzi katika uwanda wa Yordani kati ya Sukothi na Sereda.4:17 Au Sarethani. 184:18 1Fal 7:23, 47Vitu hivi vyote Mfalme Solomoni alivyotengeneza vilikuwa vingi sana hivi kwamba uzito wa shaba haungekadirika.

194:19 Kut 25:23, 30; 2Fal 24:13; Dan 5:2-3; Yer 28:3; 1Nya 28:6Solomoni pia akatengeneza samani zote zilizokuwa ndani ya Hekalu la Mungu:

madhabahu ya dhahabu;

meza za kuweka mikate ya Wonyesho;

204:20 Kut 27:20-21vinara vya taa vya dhahabu safi pamoja na taa zake ili ziwake mbele ya sehemu takatifu ya ndani kama ilivyoelekezwa;

214:21 Kut 37:20; 1Fal 6:18-35; Kut 25:31maua ya dhahabu yaliyofanyizwa, taa na makoleo (vilikuwa vya dhahabu bora kabisa);

224:22 Hes 7:14; Law 10:1; 1Fal 6:21mikasi ya dhahabu safi, mabakuli ya kunyunyizia, masinia na vyetezo; milango ya dhahabu ya Hekalu: yaani milango ya ndani ya Patakatifu pa Patakatifu, na milango ya ukumbi mkuu.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

歷代志下 4:1-22

聖殿的器具

1所羅門造了一座銅壇,長九米,寬九米,高四點五米。 2他又鑄了一個圓形銅海,高二點二五米,直徑四點五米,周長十三點五米。 3銅海邊緣下方有兩圈牛的圖案,每五十釐米有十頭牛,是鑄銅海的時候鑄上的。 4有十二頭銅牛馱著銅海,三頭向北,三頭向西,三頭向南,三頭向東,牛尾向內。 5銅海厚八釐米,邊如杯邊,又如百合花,容量為六萬六千升。 6他又造了十個盆,五個放右邊,五個放左邊,用來清洗獻燔祭所用之物。但銅海只供祭司沐浴使用。

7他照著所定的式樣,造了十個金燈臺放在殿裡,五個在右邊,五個在左邊; 8又造了十張桌子放在殿裡,五個在右邊,五個在左邊;還造了一百個金碗。 9他又建了祭司院、大院及大院的門,門都包上銅。 10銅海放在殿的右邊,就是東南方。

11戶蘭又造了盆、鏟和碗。他為所羅門王完成了上帝殿裡的工作。 12戶蘭所製造的有:兩根柱子,兩個碗狀的柱冠,兩個裝飾柱冠的網子, 13用來裝飾碗狀柱冠、安在兩個網子上的四百石榴——每個網子上兩行; 14盆座及盆座上的盆; 15銅海和銅海下面的十二頭銅牛; 16盆、鏟、肉叉及耶和華殿裡的一切器具。這些都是巧匠戶蘭用磨亮的銅為所羅門王製造的。 17這些都是照王的命令,在疏割撒利但之間的約旦平原用泥模鑄成的。 18所羅門製造的器具極多,銅的重量無法統計。

19所羅門又造了上帝殿裡的金壇和放置供餅的桌子, 20按規定放在內殿前的純金的燈臺和燈盞, 21以及純金的花飾、燈盞、火鉗、 22蠟剪、碗、碟和火鼎。殿門和至聖所的門也是金的。