2 Nyakati 35 – NEN & BDS

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Nyakati 35:1-27

Mfalme Yosia Anaadhimisha Pasaka

(2 Wafalme 23:21-23)

135:1 Kut 12:1-30; Hes 9:3; Eze 45:21; Ezr 6:17; 2Fal 23:21Yosia akaadhimisha Pasaka kwa Bwana katika Yerusalemu, mwana-kondoo wa Pasaka akachinjwa siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza. 235:2 Ezr 6:18-19; 2Nya 23:18; 29:11Akawaweka makuhani kwenye wajibu wao na kuwatia moyo katika utumishi wa Hekalu la Bwana. 335:3 Kum 33:10; 1Nya 23:26; 2Nya 34:14; 30:22; 5:7Akawaambia Walawi, waliowafundisha Waisraeli wote na waliokuwa wamejiweka wakfu kwa ajili ya kazi ya Bwana, “Liwekeni hilo Sanduku takatifu katika Hekalu lile alilojenga Solomoni mwana wa Daudi mfalme wa Israeli. Halipaswi kubebwa huku na huko mabegani mwenu. Sasa mtumikieni Bwana Mungu wenu na watu wake Israeli. 435:4 1Nya 9:10-13; Ezr 6:15; 2Nya 8:14Jiandaeni kwa kufuata jamaa zenu katika migawanyo yenu, kufuatana na maelezo yaliyoandikwa na Daudi mfalme wa Israeli na mwanawe Solomoni.

5“Simameni mahali patakatifu kwa kufuata migawanyo ya jamaa za baba zenu kulingana na koo zenu na pawepo Walawi kwa ajili ya kila mgawanyo wa nyumba ya baba zenu. 635:6 Law 11:44; 2Nya 29:5-15; Kut 19:10; Ebr 9:13-14; Kut 19:10; Ezr 6:20; Za 51:7; Yoe 2:16; 2Nya 30:3, 15Chinjeni mwana-kondoo wa Pasaka, jitakaseni, nanyi kwa niaba ya koo zenu fanyeni maandalizi, mkitenda sawasawa na neno la Bwana kwa mkono wa Mose.”

735:7 2Nya 30:24; Mik 6:7; 2Nya 31:3Ndipo Yosia akawapa watu wote wana-mbuzi waliokuwepo jumla ya kondoo wapatao 30,000 kwa ajili ya sadaka ya Pasaka, pia na ngʼombe 10,000, vyote hivi kutoka mali binafsi ya mfalme.

835:8 1Nya 29:3; 6:13; 2Kor 9:7Pia maafisa wake, wakatoa kwa hiari yao wakawapa watu, makuhani na Walawi. Hilkia, Zekaria na Yehieli, waliokuwa maafisa wakuu wa Hekalu la Mungu, wakawapa makuhani sadaka za Pasaka wana-kondoo na wana-mbuzi 2,600 na mafahali 300. 935:9 2Nya 31:12-13Konania na nduguze wawili, Shemaya na Nethaneli, pamoja na Hashabia, Yeieli na Yozabadi waliokuwa viongozi wa Walawi, nao pia wakawapa Walawi wana-kondoo na wana-mbuzi 5,000 na mafahali 500, kwa ajili ya sadaka za Pasaka.

1035:10 Ezr 6:18; 2Nya 30:16Huduma ilipomalizika kuandaliwa makuhani wakasimama mahali pao na Walawi katika migawanyo yao kama mfalme alivyokuwa ameamuru. 1135:11 2Nya 29:22; 30:17Wana-kondoo wa Pasaka wakachinjwa, nao makuhani wakanyunyiza ile damu waliyokabidhiwa, wakati Walawi wakiwa wanawachuna wale wanyama ngozi. 1235:12 Law 3:3Wakatenga sadaka za kuteketezwa ili waweze kugawia ili migawanyo kwa kufuata jamaa za baba zao ili watoe sadaka kwa Bwana kama ilivyoandikwa katika Kitabu cha Mose. Wakafanya vivyo hivyo kwa wale mafahali. 1335:13 Law 6:25; 1Sam 2:13-15; Kut 12:8; 13:6; Law 23:5-6; 2Nya 30:21; 1Kor 5:7-8Wakawaoka wale wanyama wa Pasaka kwenye moto kama ilivyoamriwa, wakachemsha zile sadaka takatifu kwenye vyungu, masufuria makubwa na vikaango na kuwagawia watu wote upesi. 1435:14 Kut 29:13Hatimaye wakafanya maandalizi kwa ajili yao wenyewe na kwa ajili ya makuhani, kwa sababu wale makuhani, yaani, wazao wa Aroni, walikuwa wanatoa sadaka za kuteketezwa pamoja na zile sehemu zilizonona mpaka usiku. Hivyo Walawi wakafanya maandalizi kwa ajili yao wenyewe na kwa ajili ya makuhani wa uzao wa Aroni.

1535:15 Neh 12:46; Za 68:25Waimbaji, wazao wa Asafu, walikuwa katika nafasi zao, kama ilivyoagizwa na Mfalme Daudi, Asafu, Hemani na Yeduthuni mwonaji wa Mfalme. Mabawabu katika kila lango hawakuhitaji kuacha nafasi zao kwa sababu Walawi wenzao walifanya maandalizi kwa ajili yao.

1635:16 2Nya 3:10; Za 35:16; Yer 5:12; 32:3Kwa hiyo wakati ule huduma yote ya Bwana ilifanyika katika kuadhimisha Pasaka, kutoa sadaka za kuteketezwa juu ya madhabahu ya Bwana kama alivyoamuru Mfalme Yosia. 1735:17 Kut 12:15; Hes 28:16-17; Kum 16:3-8Waisraeli waliokuwepo wakaadhimisha Pasaka wakati huo na Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu kwa siku saba. 1835:18 2Fal 23:22-23Kulikuwa hakujafanyika Pasaka kama hii katika Israeli tangu siku za nabii Samweli wala hakukuwa na mfalme yeyote wa Israeli ambaye kamwe alishaadhimisha Pasaka kama ile aliyofanya Mfalme Yosia, akiwa na makuhani, Walawi na watu wote wa Yuda na watu wa Israeli waliokuwepo huko, pamoja na watu wa Yerusalemu. 19Pasaka iliadhimishwa katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Mfalme Yosia.

Kifo Cha Yosia

(2 Wafalme 23:28-30)

2035:20 Isa 10:9; Yer 46:2; Mwa 2:14; 2Fal 23:29; 25:11Baada ya haya yote, Yosia alipomaliza kulitengeneza vizuri Hekalu, Neko mfalme wa Misri, akapanda ili kupigana huko Karkemishi katika Mto Frati, naye Yosia akatoka kwenda kupigana naye. 2135:21 2Fal 18:25; Dan 4:35; 1Fal 13:18; Isa 36:10; Yer 25:9Lakini Neko akamtumia wajumbe kusema, “Kuna ugomvi gani kati yangu mimi na wewe, Ee Mfalme wa Yuda? Si wewe ninayekushambulia wakati huu, bali ile nyumba ambayo nina vita nayo, Mungu ameniambia niharakishe, kwa hivyo acha kumpinga Mungu, ambaye yuko pamoja nami, la sivyo atakuangamiza.”

2235:22 Amu 5:19; 1Sam 28:8; 1Fal 22:30; 14:2; 2Nya 18:29Lakini hata hivyo, Yosia hakukubali kumwacha, bali alijibadilisha ili kupigana naye vita. Hakusikiliza yale Neko aliyokuwa amemwambia kwa agizo la Mungu bali alikwenda kupigana naye katika tambarare ya Megido.

2335:23 1Fal 22:34; Dan 2:21Wapiga upinde wakampiga Mfalme Yosia, naye akawaambia maafisa wake, “Niondoeni, nimejeruhiwa vibaya sana.” 2435:24 2Fal 23:30; Zek 12:11Kwa hiyo wakamshusha kutoka kwenye gari lake la farasi, wakamweka kwenye gari lingine alilokuwa nalo na kumleta Yerusalemu, ambako alifia. Akazikwa katika makaburi ya baba zake, nayo Yuda yote na Yerusalemu wakamwombolezea Yosia.

2535:25 Mwa 50:10; Yer 22:10-16; Mao 4:20; Mt 9:23; Amo 5:16; Mhu 12:5; Yer 9:17Nabii Yeremia akatunga maombolezo kwa ajili ya kifo chake, nao waimbaji wote, wanaume kwa wanawake, hufanya ukumbusho wa Yosia katika maombolezo hadi leo. Haya yakafanywa desturi katika Israeli, nayo yameandikwa katika Maombolezo.

2635:26 Za 112:6; Mit 10:7; 22:1Matukio mengine ya utawala wa Yosia na matendo yake mema, kulingana na yale yaliyoandikwa katika sheria ya Bwana: 27matukio yote, kuanzia mwanzo hadi mwisho, yameandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli na Yuda.

La Bible du Semeur

2 Chroniques 35:1-27

Josias célèbre la Pâque

1Josias célébra la Pâque à Jérusalem en l’honneur de l’Eternel, et l’on immola les agneaux pour cette fête le quatorzième jour du premier mois35.1 La fête est célébrée à la date réglementaire (Lv 23.5).. 2Il rétablit les prêtres dans leurs fonctions et il les encouragea dans leur service du temple de l’Eternel. 3Puis il s’adressa aux lévites chargés d’enseigner tout le peuple d’Israël et qui étaient consacrés à l’Eternel. Il leur dit : Déposez le coffre sacré dans le temple que Salomon, fils de David, roi d’Israël, a construit. Maintenant vous n’avez plus à le transporter sur vos épaules. Servez l’Eternel votre Dieu et son peuple Israël. 4Organisez-vous en vous répartissant par groupes familiaux et selon vos classes, d’après les instructions écrites de David, le roi d’Israël, et de son fils Salomon35.4 Voir 1 Ch 23 à 26 ; 2 Ch 8.14.. 5Occupez vos postes dans le sanctuaire de façon à faire correspondre une classe de groupe familial lévitique à chaque subdivision des groupes familiaux de vos compatriotes, les gens du peuple. 6Immolez les agneaux de la Pâque. Purifiez-vous rituellement et préparez la Pâque pour vos compatriotes35.6 Autre traduction : et aidez vos compatriotes à agir. selon la parole de l’Eternel, transmise par l’intermédiaire de Moïse.

7Josias préleva pour la Pâque trente mille agneaux et chevreaux ainsi que trois mille bœufs sur ses propres troupeaux pour tous les gens du peuple qui se trouvaient à Jérusalem. 8Ses grands firent aussi volontairement des dons au peuple, aux prêtres et aux lévites. Hilqiya, Zacharie et Yehiel, les responsables du Temple, donnèrent aux prêtres deux mille six cents agneaux et chevreaux pour la Pâque ainsi que trois cents bœufs. 9Konania et ses frères Shemaya et Netanéel, Hashabia, Yeïel et Yozabad, chefs des lévites, fournirent aux lévites cinq mille agneaux et chevreaux pour la Pâque et cinq cents bœufs.

10Voici comment la cérémonie fut organisée : les prêtres se tinrent à leur poste et les lévites étaient répartis selon leur classe conformément aux ordres du roi. 11Ils immolèrent les agneaux de la Pâque. Les lévites remettaient aux prêtres le sang des animaux pour qu’ils le répandent sur l’autel, puis ils ôtaient la peau des victimes. 12Ils mettaient de côté les parties des bêtes qui devaient être offertes en holocaustes pour les donner aux différentes subdivisions des groupes familiaux afin qu’ils les offrent à l’Eternel comme cela est prescrit dans le livre de Moïse. On fit de même pour le gros bétail. 13Ils firent rôtir les agneaux de la Pâque au feu, selon le rituel prescrit35.13 Voir Ex 12.8-9., tandis que les offrandes consacrées furent cuites dans des chaudières, des chaudrons et des poêles pour être ensuite rapidement distribuées à tous les gens du peuple. 14Enfin, les lévites préparèrent la Pâque pour eux-mêmes et pour les prêtres, car les prêtres descendants d’Aaron furent occupés jusqu’à la nuit à offrir les holocaustes et les graisses. C’est pourquoi les lévites préparèrent la Pâque pour eux-mêmes et pour les prêtres descendants d’Aaron.

15Les musiciens descendants d’Asaph étaient à leur poste selon les directives de David, d’Asaph, d’Hémân et de Yedoutoun, le prophète du roi. Les portiers aussi étaient à chaque porte ; ils n’eurent pas à interrompre leur service, car leurs collègues lévites firent les préparatifs pour eux. 16Ainsi furent organisées ce jour-là toutes les cérémonies en l’honneur de l’Eternel pour célébrer la Pâque et pour offrir les holocaustes sur l’autel de l’Eternel, conformément aux ordres du roi Josias.

17Les Israélites qui se trouvaient là célébrèrent la Pâque à ce moment-là et la fête des Pains sans levain pendant sept jours35.17 Voir Ex 12.1-20..

(2 R 23.22-23)

18Aucune Pâque semblable n’avait été célébrée en Israël depuis l’époque du prophète Samuel. Aucun des rois d’Israël n’avait organisé de célébration de la Pâque comparable à la Pâque célébrée par Josias avec l’aide des prêtres et des lévites, avec tout Juda et ceux d’Israël qui se trouvaient là, ainsi que les habitants de Jérusalem. 19Ce fut dans la dix-huitième année du règne de Josias que cette Pâque fut célébrée35.19 L’année même où le livre de la Loi fut découvert (voir v. 8)..

La fin de Josias

(2 R 23.28-30)

20Après tous ces événements, après que Josias eut remis le Temple en état, Néko35.20 En 609 av. J.-C., le pharaon Néko est parti combattre les Babyloniens pour secourir les Assyriens, ses alliés., roi d’Egypte, partit en guerre à Karkemish sur l’Euphrate35.20 Une grande ville sur la rive ouest de l’Euphrate, une capitale hittite, centre du commerce d’Asie occidentale.. Josias se mit en campagne pour lui barrer la route. 21Mais Néko lui envoya des messagers pour lui dire : Roi de Juda, qu’avons-nous à faire ensemble ? Ce n’est pas contre toi que je me suis mis en campagne aujourd’hui. C’est contre une autre dynastie que je suis en guerre. Dieu m’a ordonné de me dépêcher. Garde-toi de t’opposer à Dieu qui est avec moi, sinon il te détruira.

22Mais Josias ne voulut pas se retirer, et il se déguisa pour aller l’affronter sans tenir compte de l’avertissement de Néko, qui était pourtant inspiré par Dieu. Il vint livrer bataille dans la vallée de Meguiddo35.22 Antique et classique champ de bataille dans la plaine d’Esdrelon (voir Jg 5.19 ; 1 R 9.15-19 ; 2 R 9.27).. 23Au cours du combat, les archers l’atteignirent. Le roi dit à ses serviteurs : Emmenez-moi, car je suis grièvement blessé.

24Ses officiers le descendirent de son char de combat, le mirent sur son second char et le conduisirent à Jérusalem. Il mourut et fut enterré dans les tombeaux de ses ancêtres. Tout Juda et Jérusalem prirent le deuil pour Josias. 25Jérémie composa une complainte funèbre sur lui. Tous les chanteurs et toutes les chanteuses célèbrent Josias dans leurs complaintes jusqu’à ce jour, car c’est devenu une tradition en Israël. Ces chants sont consignés dans le recueil des complaintes.

26Les autres faits et gestes de Josias et ses actes de piété qu’il a accomplis conformément à ce qui est écrit dans la Loi de l’Eternel, 27ses actes, des premiers aux derniers, tout cela est cité dans le livre des rois d’Israël et de Juda.