2 Nyakati 32 – NEN & PCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Nyakati 32:1-33

Senakeribu Aitishia Yerusalemu

(2 Wafalme 18:13-37; 19:14-19, 35-37; Isaya 36:1-22; 37:8-38)

132:1 2Fal 18:13-19; Isa 37:9Baada ya yale yote aliyokuwa amefanya Hezekia kwa uaminifu mkubwa, Senakeribu mfalme wa Ashuru akaja na kuvamia Yuda. Akaizunguka miji yenye ngome kwa jeshi, akifikiri kuiteka iwe yake. 232:2 Isa 22:7; Yer 1:15Hezekia alipoona kuwa Senakeribu amekuja na kwamba alikusudia kufanya vita juu ya Yerusalemu, 3akafanya shauri na maafisa wake na mashujaa wake juu ya kuzuia maji kutoka chemchemi zilizo nje ya mji, nao wakamsaidia. 432:4 2Fal 20:20; Nah 3:14Umati mkubwa wa watu ukakusanyika na kuzuia chemchemi zote na vijito vilivyotiririka katika nchi yote, wakisema: “Kwa nini wafalme wa Ashuru waje na kukuta maji tele?” 532:5 2Nya 25:23; Isa 22:9-10; 1Fal 9:24; 2Sam 5:9; 1Nya 11:8Hezekia akafanya kazi kwa bidii kukarabati sehemu zote zilizokuwa zimebomoka za ukuta na kujenga minara juu yake. Akajenga ukuta mwingine nje ya ule uliokuwepo na kuimarisha Milo32:5 Milo maana yake Boma la Ngome. katika Mji wa Daudi. Akatengeneza pia silaha nyingi na ngao.

632:6 2Nya 30:22; Isa 40:2Akaweka maafisa wa jeshi juu ya watu, wakawakutanisha mbele yake katika uwanja kwenye lango la mji, naye akawatia moyo kwa maneno haya: 732:7 Kum 31:6; 1Nya 22:13; 28:10; 2Nya 20:15; Hes 14:9; 2Fal 6:16; Za 55:18“Kuweni hodari na wenye moyo mkuu. Msiogope, msifadhaike wala msikate tamaa kwa sababu ya mfalme wa Ashuru na hili jeshi kubwa lililo pamoja naye, kwa kuwa aliye pamoja nasi ni mkuu kuliko aliye pamoja naye. 832:8 Ay 40:9; Isa 41:10-14; 52:10; 1Sam 17:45; 2Nya 13:12; 1Nya 5:22; Rum 8:31; Yer 17:5; 1Yn 4:4; Kum 20:1-4; 31:6-8; Mit 18:10; Amo 5:14Kwake uko mkono wa mwili tu, bali kwetu yuko Bwana Mungu wetu kutusaidia na kutupigania vita vyetu.” Nao watu wakatiwa moyo kutokana na maneno aliyowaambia Hezekia mfalme wa Yuda.

932:9 2Fal 18:17; Yos 10:3Hatimaye Senakeribu mfalme wa Ashuru na majeshi yake yote walipokuwa wameuzunguka Lakishi, akawatuma maafisa wake kwenda Yerusalemu wakiwa na ujumbe huu kwa Hezekia mfalme wa Yuda, na kwa watu wote wa Yuda waliokuwako humo, kusema:

1032:10 Eze 29:16“Hili ndilo asemalo Senakeribu mfalme wa Ashuru: Je, mmeweka tumaini lenu wapi, hata mnaendelea kukaa katika Yerusalemu, hali mmezungukwa na jeshi? 1132:11 Isa 37:10Hezekia asemapo, ‘Bwana Mungu wetu atatuokoa kutokana na mkono wa mfalme wa Ashuru,’ anawapotosha ninyi, naye atawaacha mfe kwa njaa na kiu. 12Je, si Hezekia mwenyewe aliyeondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu pamoja na madhabahu zake, akiwaambia Yuda wa Yerusalemu, ‘Ni lazima mwabudu mbele ya madhabahu moja na kuteketeza dhabihu juu yake’?

1332:13 2Fal 18:33-35; Za 115:4-8“Je, hamjui yale mimi na baba zangu tuliyoyafanya kwa mataifa yote ya nchi zingine? Je, miungu ya mataifa hayo iliweza kuokoa nchi zao kutoka mkononi mwangu? 14Ni yupi miongoni mwa miungu yote ya mataifa haya ambayo baba zangu waliyaangamiza ameweza kuwaokoa watu wake mkononi mwangu? Inawezekanaje basi Mungu wenu kuwaokoa mkononi mwangu? 1532:15 Isa 37:10; Dan 3:15; Kut 5:2; Yn 19:10-11Sasa basi, msikubali Hezekia awadanganye na kuwapotosha namna hii. Msimwamini, kwa kuwa hakuna mungu wa taifa lolote wala wa ufalme wowote aliyeweza kuwaokoa watu wake kutoka mkononi mwangu au mkononi mwa baba zangu. Sembuse huyo mungu wenu atawaokoaje kutoka mkononi mwangu!”

16Maafisa wa Senakeribu wakaendelea kunena dhidi ya Bwana aliye Mungu na dhidi ya mtumishi wake Hezekia. 1732:17 Isa 37:14; Za 74:22; 2Fal 19:12Mfalme pia aliandika barua akimtukana Bwana, Mungu wa Israeli na kusema haya dhidi yake: “Kama vile miungu ya mataifa ya nchi nyingine ilivyoshindwa kuwaokoa watu wao mkononi mwangu, vivyo hivyo Mungu wa Hezekia hataweza kuwaokoa watu wake kutoka mkononi mwangu.” 1832:18 2Fal 18:28Kisha wakawaita kwa Kiebrania watu wa Yerusalemu waliokuwa juu ya ukuta ili kuwatisha na kuwatia hofu ili waweze kuuteka mji. 1932:19 Za 115:4; Yer 1:16; Za 135:15-18; Isa 10:10; Kum 4:28; 2Fal 19:18; Yer 10:3; Hos 8:5-6Wakanena juu ya Mungu wa Yerusalemu kama vile walivyonena juu ya miungu ya mataifa mengine ya dunia ambayo ni kazi ya mikono ya wanadamu.

20Mfalme Hezekia na nabii Isaya mwana wa Amozi wakalilia mbingu katika maombi kuhusu jambo hili. 2132:21 Mwa 19:13; Isa 37:38; Yer 41:2Naye Bwana akamtuma malaika ambaye aliangamiza wanajeshi wote, na viongozi na maafisa katika kambi ya mfalme wa Ashuru. Kwa hiyo, mfalme wa Ashuru akarudi nchini mwake kwa aibu. Naye alipokwenda katika hekalu la mungu wake, baadhi ya watoto wake wakamuua kwa upanga.

2232:22 Za 18:48-50; Isa 31:5Hivyo Bwana akamwokoa Hezekia na watu wa Yerusalemu kutoka mkononi mwa Senakeribu mfalme wa Ashuru na kutoka mikononi mwa wengine wote. Bwana akawastarehesha kila upande. 2332:23 1Sam 10:27; Za 76:11; 1Nya 29:25; 2Nya 17:5Watu wengi wakaleta sadaka Yerusalemu kwa ajili ya Bwana na zawadi za thamani kwa ajili ya Hezekia mfalme wa Yuda. Tangu hapo na kuendelea, Hezekia aliheshimiwa sana na mataifa yote.

Kiburi Cha Hezekia, Mafanikio Na Kifo

(2 Wafalme 20:1-3, 12-19; Isaya 38:1-3; 39:1-8)

2432:24 Isa 38:1Katika siku hizo, Hezekia akaugua, naye akawa karibu kufa. Akamwomba Bwana, ambaye alimjibu na kumpa ishara. 2532:25 2Fal 14:10; Kum 32:6; 2Nya 26:16; 19:2; 24:18; Kum 8:12; Za 116:12; Lk 17:17; 2Fal 14:10; Hab 2:4; 1Tim 3:6; 1Pet 5:5-6Lakini moyo wa Hezekia ukajaa majivuno na hakuonyesha itikio kwa wema aliotendewa, kwa hiyo ghadhabu ya Bwana ikawa juu yake na juu ya Yuda na Yerusalemu. 2632:26 Yer 26:18-19; 2Nya 34:27-28; 2Fal 19:20; Isa 39:8Ndipo Hezekia akatubu kwa ajili ya kiburi cha moyo wake, kama walivyofanya watu wa Yerusalemu, kwa hiyo ghadhabu ya Bwana haikuja juu yao katika siku za Hezekia.

2732:27 1Nya 29:12; 2Nya 9:24Hezekia alikuwa na utajiri mwingi sana na heshima, naye akajifanyia hazina kwa ajili ya fedha yake na dhahabu na kwa ajili ya vito vyake vya thamani, vikolezi, ngao na aina zote za vyombo vya thamani. 28Akajenga pia maghala ya kuhifadhi mavuno ya nafaka, divai mpya na mafuta. Akatengeneza mabanda kwa ajili ya aina mbalimbali za mifugo, na mazizi kwa ajili ya kondoo na mbuzi. 2932:29 2Nya 29:12Akajenga vijiji na kujipatia idadi kubwa ya kondoo na mbuzi, pamoja na ngʼombe kwa kuwa Mungu alikuwa amempa utajiri mwingi sana.

3032:30 2Fal 18:17; 1Fal 1:33; Isa 22:9Ilikuwa ni Hezekia aliyeziba njia za kutolea maji za chemchemi za juu za Gihoni na kuyaelekeza maji kutiririkia upande wa magharibi wa Mji wa Daudi. Akafanikiwa katika kila kitu alichofanya. 3132:31 Isa 13:1; 39:1; 38:7; Kum 8:16; Mwa 22:1; Yn 1:12Lakini wakati wajumbe walipotumwa na watawala wa Babeli kumuuliza juu ya ishara ambayo ilitokea katika nchi, Mungu alimwacha ili kumjaribu na kujua kila kitu kilichokuwa moyoni mwake.

3232:32 Isa 36:1; 2Fal 18:1Matukio mengine ya utawala wa Hezekia na matendo yake ya kujitoa kwa moyo yameandikwa katika maono ya nabii Isaya mwana wa Amozi kwenye kitabu cha wafalme wa Yuda na Israeli. 3332:33 1Sam 2:30; Mit 10:7Hezekia akalala na baba zake na akazikwa kwenye kilima mahali yalipo makaburi ya wazao wa Daudi. Yuda wote na watu wa Yerusalemu wakamheshimu alipofariki. Naye Manase mwanawe akawa mfalme baada yake.

Persian Contemporary Bible

دوم تواريخ 32:1-33

آشوری‌ها اورشليم را محاصره می‌كنند

(دوم پادشاهان 18‏:13‏-37، 19‏:14‏-19‏،35‏-37؛ اشعيا 36‏:1‏-22، 37‏:8‏-38)

1مدتی بعد از اصلاحات حزقيای پادشاه، سنحاريب، پادشاه آشور به سرزمين يهودا هجوم آورد و شهرهای حصاردار را محاصره كرد و در صدد تسخير آنها برآمد.

2وقتی حزقيا فهميد كه سنحاريب قصد حمله به اورشليم را دارد 3با مقامات مملكتی و فرماندهان سپاه به مشورت پرداخت. آنها تصميم گرفتند چشمه‌های آب بيرون شهر را ببندند. 4پس عدهٔ زيادی از مردم را جمع كردند و چشمه‌ها و نهری را كه در ميان مزرعه‌ها جاری بود، مسدود ساختند. آنها گفتند: «نبايد بگذاريم پادشاه آشور به آب دسترسی پيدا كند.»

5سپس حزقيا قسمتهای خراب شدهٔ حصار اورشليم را تعمير كرد و بر آن برجهايی ساخت. او حصار ديگری نيز در پشت حصار اصلی درست كرده به اين وسيله نيروی دفاعی خود را تقويت نمود. همچنين قلعهٔ ملو را كه در شهر داوود بود مستحكم نمود و تعداد زيادی سلاح و سپر تهيه ديد. 6حزقيا مردم شهر را فرا خواند و فرماندهان بر آنها گماشت و آنها را در دشت وسيع مقابل شهر جمع كرده، با اين كلمات آنها را تشويق نمود:

7«دلير و قوی باشيد و از پادشاه آشور و سپاه بزرگ او نترسيد، زيرا آن كه با ماست تواناتر از اوست! 8پادشاه آشور سپاه بزرگی همراه خود دارد ولی آنها انسانهايی بيش نيستند، اما ما خداوند، خدای خود را همراه خود داريم كه به ما كمک می‌كند و برای ما می‌جنگد.» اين سخنان حزقيا به ايشان قوت قلب بخشيد.

9آنگاه سنحاريب، پادشاه آشور كه با سپاه بزرگ خود شهر لاكيش را محاصره كرده بود، قاصدانی را با اين پيام نزد حزقيا و مردم يهودا كه در اورشليم جمع شده بودند فرستاد:

10«سنحاريب، امپراتور آشور چنين می‌گويد: به چه كسی اميد بسته‌ايد كه در اورشليم در محاصره باقی می‌مانيد؟ 11حزقيای پادشاه با اين وعده كه خداوند شما را از چنگ پادشاه آشور خواهد رهانيد، می‌خواهد شما را آنقدر در آنجا نگه دارد تا از گرسنگی و تشنگی بميريد. 12مگر همين حزقيا نبود كه تمام معبدهای خدا را كه بر فراز تپه‌ها بود خراب كرد و به يهودا و اورشليم دستور داد كه فقط در برابر يک قربانگاه عبادت كنند و فقط بر روی آن بخور بسوزانند؟ 13‏-14مگر نمی‌دانيد من و اجداد من چه بر سر قومهای ديگر آورده‌ايم؟ كدام يک از خدايان آن قومها توانستند برای نجات سرزمينشان كاری انجام دهند؟ پس آيا فكر می‌كنيد خدای شما می‌تواند شما را از چنگ من برهاند؟ 15نگذاريد حزقيا شما را فريب دهد. حرفهای او را باور نكنيد. باز هم می‌گويم، خدايان هيچ مملكتی تاكنون نتواسته‌اند قوم خود را از دست من و اجدادم برهانند، چه رسد به خدای شما.» 16قاصدان پادشاه آشور، سخنان اهانت‌آميز بسياری بر ضد خداوند و خدمتگزار او حزقيا گفتند. 17همچنين امپراتور آشور نامه‌ای به اين مضمون بر ضد خداوند، خدای اسرائيل نوشته، او را اهانت نمود: «خدايان ممالک ديگر نتوانستند قوم خود را از چنگ من برهانند، مسلماً خدای حزقيا هم نخواهد توانست قوم خود را از دست من برهاند.» 18قاصدان با صدای بلند به زبان عبری، مردمی را كه روی حصار شهر جمع شده بودند تهديد می‌كردند و سعی داشتند آنها را بترسانند و مضطرب كنند تا بتوانند شهر را بگيرند. 19قاصدان گمان می‌كردند خدای اورشليم هم مانند خدايان ساير كشورها ساخته و پرداختهٔ دست انسان است؛ به اين دليل بود كه چنين سخن می‌گفتند.

20سپس حزقيای پادشاه و اشعيای نبی (پسر آموص) دعا كردند و از خدا كمک طلبيدند. 21خداوند نيز فرشته‌ای فرستاد و سربازان آشور و همهٔ فرماندهان و افسرانشان را هلاک كرد. پس سنحاريب با خفت به سرزمين خود بازگشت و هنگامی كه داخل معبد خدای خود شد، پسران خودش او را در آنجا كشتند. 22به اين طريق خداوند، حزقيا و مردم اورشليم را از دست سنحاريب و ساير دشمنان نجات داد و در سراسر مملكت او صلح و امنيت برقرار نمود. 23عدهٔ زيادی به اورشليم آمده، هدايايی برای خداوند و حزقيا آوردند. از آن پس، حزقيای پادشاه در ميان تمام قومها بسيار سربلند شد.

بيماری و غرور حزقيا

(دوم پادشاهان 20‏:1‏-3‏،12‏-19؛ اشعيا 38‏:1‏-3، 39‏:1‏-8)

24در آن روزها حزقيا بيمار شد و نزديک بود بميرد. او به درگاه خداوند دعا كرد و خداوند به او نشان داد كه شفا خواهد يافت. 25اما حزقيا مغرور شد و پس از شفايش مطابق ميل خدا رفتار نكرد، به همين علت خشم خدا عليه او و يهودا و اورشليم افروخته گرديد. 26آنگاه حزقيا و ساكنان اورشليم از غرور خود توبه كردند و در نتيجه در طول حيات حزقيا، غضب خداوند بر آنها نازل نشد.

جاه و مقام حزقيا

27حزقيا بسيار ثروتمند شد و به اوج افتخار رسيد. به دستور او برای نگه داری طلا و نقره و جواهرات و عطريات و اشیا قيمتی و سپرهايش، انبارها ساختند. 28او همچنين انبارها برای ذخيره كردن غلات، شراب و روغن زيتون؛ طويله‌ها برای حيوانات و آغلها برای گله‌ها ساخت. 29خدا گله‌ها و رمه‌ها و ثروت زيادی به او بخشيد و او برای نگه داری آنها شهرها ساخت. 30حزقيا جلو نهر بالايی جيحون يک سد درست كرد و آب آن را به سمت غرب شهر داوود جاری نمود. او به هر كاری دست می‌زد موفق می‌شد.

31اما وقتی فرستادگانی از بابل آمدند تا دربارهٔ معجزهٔ شفا يافتن او اطلاعاتی كسب كنند، خدا حزقيا را به حال خود واگذاشت تا ماهيت خود را نشان دهد و معلوم شود چگونه آدمی است.

مرگ حزقيا

(دوم پادشاهان 20‏:20‏،21)

32شرح بقيهٔ رويدادهای دوران سلطنت حزقيا و كارهای خوب او در كتاب اشعيای نبی (پسر آموص) و كتاب «تاريخ پادشاهان يهودا و اسرائيل» نوشته شده است. 33وقتی حزقيا مرد او را در قسمت بالايی آرامگاه سلطنتی در كنار پادشاهان ديگر به خاک سپردند و تمام يهودا و اورشليم در زمان وفاتش نسبت به او ادای احترام كردند. پس از او پسرش منسی بر تخت سلطنت نشست.