2 Nyakati 32 – NEN & NUB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Nyakati 32:1-33

Senakeribu Aitishia Yerusalemu

(2 Wafalme 18:13-37; 19:14-19, 35-37; Isaya 36:1-22; 37:8-38)

132:1 2Fal 18:13-19; Isa 37:9Baada ya yale yote aliyokuwa amefanya Hezekia kwa uaminifu mkubwa, Senakeribu mfalme wa Ashuru akaja na kuvamia Yuda. Akaizunguka miji yenye ngome kwa jeshi, akifikiri kuiteka iwe yake. 232:2 Isa 22:7; Yer 1:15Hezekia alipoona kuwa Senakeribu amekuja na kwamba alikusudia kufanya vita juu ya Yerusalemu, 3akafanya shauri na maafisa wake na mashujaa wake juu ya kuzuia maji kutoka chemchemi zilizo nje ya mji, nao wakamsaidia. 432:4 2Fal 20:20; Nah 3:14Umati mkubwa wa watu ukakusanyika na kuzuia chemchemi zote na vijito vilivyotiririka katika nchi yote, wakisema: “Kwa nini wafalme wa Ashuru waje na kukuta maji tele?” 532:5 2Nya 25:23; Isa 22:9-10; 1Fal 9:24; 2Sam 5:9; 1Nya 11:8Hezekia akafanya kazi kwa bidii kukarabati sehemu zote zilizokuwa zimebomoka za ukuta na kujenga minara juu yake. Akajenga ukuta mwingine nje ya ule uliokuwepo na kuimarisha Milo32:5 Milo maana yake Boma la Ngome. katika Mji wa Daudi. Akatengeneza pia silaha nyingi na ngao.

632:6 2Nya 30:22; Isa 40:2Akaweka maafisa wa jeshi juu ya watu, wakawakutanisha mbele yake katika uwanja kwenye lango la mji, naye akawatia moyo kwa maneno haya: 732:7 Kum 31:6; 1Nya 22:13; 28:10; 2Nya 20:15; Hes 14:9; 2Fal 6:16; Za 55:18“Kuweni hodari na wenye moyo mkuu. Msiogope, msifadhaike wala msikate tamaa kwa sababu ya mfalme wa Ashuru na hili jeshi kubwa lililo pamoja naye, kwa kuwa aliye pamoja nasi ni mkuu kuliko aliye pamoja naye. 832:8 Ay 40:9; Isa 41:10-14; 52:10; 1Sam 17:45; 2Nya 13:12; 1Nya 5:22; Rum 8:31; Yer 17:5; 1Yn 4:4; Kum 20:1-4; 31:6-8; Mit 18:10; Amo 5:14Kwake uko mkono wa mwili tu, bali kwetu yuko Bwana Mungu wetu kutusaidia na kutupigania vita vyetu.” Nao watu wakatiwa moyo kutokana na maneno aliyowaambia Hezekia mfalme wa Yuda.

932:9 2Fal 18:17; Yos 10:3Hatimaye Senakeribu mfalme wa Ashuru na majeshi yake yote walipokuwa wameuzunguka Lakishi, akawatuma maafisa wake kwenda Yerusalemu wakiwa na ujumbe huu kwa Hezekia mfalme wa Yuda, na kwa watu wote wa Yuda waliokuwako humo, kusema:

1032:10 Eze 29:16“Hili ndilo asemalo Senakeribu mfalme wa Ashuru: Je, mmeweka tumaini lenu wapi, hata mnaendelea kukaa katika Yerusalemu, hali mmezungukwa na jeshi? 1132:11 Isa 37:10Hezekia asemapo, ‘Bwana Mungu wetu atatuokoa kutokana na mkono wa mfalme wa Ashuru,’ anawapotosha ninyi, naye atawaacha mfe kwa njaa na kiu. 12Je, si Hezekia mwenyewe aliyeondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu pamoja na madhabahu zake, akiwaambia Yuda wa Yerusalemu, ‘Ni lazima mwabudu mbele ya madhabahu moja na kuteketeza dhabihu juu yake’?

1332:13 2Fal 18:33-35; Za 115:4-8“Je, hamjui yale mimi na baba zangu tuliyoyafanya kwa mataifa yote ya nchi zingine? Je, miungu ya mataifa hayo iliweza kuokoa nchi zao kutoka mkononi mwangu? 14Ni yupi miongoni mwa miungu yote ya mataifa haya ambayo baba zangu waliyaangamiza ameweza kuwaokoa watu wake mkononi mwangu? Inawezekanaje basi Mungu wenu kuwaokoa mkononi mwangu? 1532:15 Isa 37:10; Dan 3:15; Kut 5:2; Yn 19:10-11Sasa basi, msikubali Hezekia awadanganye na kuwapotosha namna hii. Msimwamini, kwa kuwa hakuna mungu wa taifa lolote wala wa ufalme wowote aliyeweza kuwaokoa watu wake kutoka mkononi mwangu au mkononi mwa baba zangu. Sembuse huyo mungu wenu atawaokoaje kutoka mkononi mwangu!”

16Maafisa wa Senakeribu wakaendelea kunena dhidi ya Bwana aliye Mungu na dhidi ya mtumishi wake Hezekia. 1732:17 Isa 37:14; Za 74:22; 2Fal 19:12Mfalme pia aliandika barua akimtukana Bwana, Mungu wa Israeli na kusema haya dhidi yake: “Kama vile miungu ya mataifa ya nchi nyingine ilivyoshindwa kuwaokoa watu wao mkononi mwangu, vivyo hivyo Mungu wa Hezekia hataweza kuwaokoa watu wake kutoka mkononi mwangu.” 1832:18 2Fal 18:28Kisha wakawaita kwa Kiebrania watu wa Yerusalemu waliokuwa juu ya ukuta ili kuwatisha na kuwatia hofu ili waweze kuuteka mji. 1932:19 Za 115:4; Yer 1:16; Za 135:15-18; Isa 10:10; Kum 4:28; 2Fal 19:18; Yer 10:3; Hos 8:5-6Wakanena juu ya Mungu wa Yerusalemu kama vile walivyonena juu ya miungu ya mataifa mengine ya dunia ambayo ni kazi ya mikono ya wanadamu.

20Mfalme Hezekia na nabii Isaya mwana wa Amozi wakalilia mbingu katika maombi kuhusu jambo hili. 2132:21 Mwa 19:13; Isa 37:38; Yer 41:2Naye Bwana akamtuma malaika ambaye aliangamiza wanajeshi wote, na viongozi na maafisa katika kambi ya mfalme wa Ashuru. Kwa hiyo, mfalme wa Ashuru akarudi nchini mwake kwa aibu. Naye alipokwenda katika hekalu la mungu wake, baadhi ya watoto wake wakamuua kwa upanga.

2232:22 Za 18:48-50; Isa 31:5Hivyo Bwana akamwokoa Hezekia na watu wa Yerusalemu kutoka mkononi mwa Senakeribu mfalme wa Ashuru na kutoka mikononi mwa wengine wote. Bwana akawastarehesha kila upande. 2332:23 1Sam 10:27; Za 76:11; 1Nya 29:25; 2Nya 17:5Watu wengi wakaleta sadaka Yerusalemu kwa ajili ya Bwana na zawadi za thamani kwa ajili ya Hezekia mfalme wa Yuda. Tangu hapo na kuendelea, Hezekia aliheshimiwa sana na mataifa yote.

Kiburi Cha Hezekia, Mafanikio Na Kifo

(2 Wafalme 20:1-3, 12-19; Isaya 38:1-3; 39:1-8)

2432:24 Isa 38:1Katika siku hizo, Hezekia akaugua, naye akawa karibu kufa. Akamwomba Bwana, ambaye alimjibu na kumpa ishara. 2532:25 2Fal 14:10; Kum 32:6; 2Nya 26:16; 19:2; 24:18; Kum 8:12; Za 116:12; Lk 17:17; 2Fal 14:10; Hab 2:4; 1Tim 3:6; 1Pet 5:5-6Lakini moyo wa Hezekia ukajaa majivuno na hakuonyesha itikio kwa wema aliotendewa, kwa hiyo ghadhabu ya Bwana ikawa juu yake na juu ya Yuda na Yerusalemu. 2632:26 Yer 26:18-19; 2Nya 34:27-28; 2Fal 19:20; Isa 39:8Ndipo Hezekia akatubu kwa ajili ya kiburi cha moyo wake, kama walivyofanya watu wa Yerusalemu, kwa hiyo ghadhabu ya Bwana haikuja juu yao katika siku za Hezekia.

2732:27 1Nya 29:12; 2Nya 9:24Hezekia alikuwa na utajiri mwingi sana na heshima, naye akajifanyia hazina kwa ajili ya fedha yake na dhahabu na kwa ajili ya vito vyake vya thamani, vikolezi, ngao na aina zote za vyombo vya thamani. 28Akajenga pia maghala ya kuhifadhi mavuno ya nafaka, divai mpya na mafuta. Akatengeneza mabanda kwa ajili ya aina mbalimbali za mifugo, na mazizi kwa ajili ya kondoo na mbuzi. 2932:29 2Nya 29:12Akajenga vijiji na kujipatia idadi kubwa ya kondoo na mbuzi, pamoja na ngʼombe kwa kuwa Mungu alikuwa amempa utajiri mwingi sana.

3032:30 2Fal 18:17; 1Fal 1:33; Isa 22:9Ilikuwa ni Hezekia aliyeziba njia za kutolea maji za chemchemi za juu za Gihoni na kuyaelekeza maji kutiririkia upande wa magharibi wa Mji wa Daudi. Akafanikiwa katika kila kitu alichofanya. 3132:31 Isa 13:1; 39:1; 38:7; Kum 8:16; Mwa 22:1; Yn 1:12Lakini wakati wajumbe walipotumwa na watawala wa Babeli kumuuliza juu ya ishara ambayo ilitokea katika nchi, Mungu alimwacha ili kumjaribu na kujua kila kitu kilichokuwa moyoni mwake.

3232:32 Isa 36:1; 2Fal 18:1Matukio mengine ya utawala wa Hezekia na matendo yake ya kujitoa kwa moyo yameandikwa katika maono ya nabii Isaya mwana wa Amozi kwenye kitabu cha wafalme wa Yuda na Israeli. 3332:33 1Sam 2:30; Mit 10:7Hezekia akalala na baba zake na akazikwa kwenye kilima mahali yalipo makaburi ya wazao wa Daudi. Yuda wote na watu wa Yerusalemu wakamheshimu alipofariki. Naye Manase mwanawe akawa mfalme baada yake.

Swedish Contemporary Bible

2 Krönikeboken 32:1-33

Assyrien invaderar Juda

(2 Kung 18:13-37; 19:35-37; Jes 36:1-22; 37:36-38)

1Efter att Hiskia troget hade utfört detta, kom kung Sanherib av Assyrien in i Juda och belägrade de befästa städerna i tanke att erövra dem. 2När Hiskia såg att Sanherib hade kommit och tänkte anfalla Jerusalem, 3rådgjorde han med sina furstar och krigare om att täppa igen alla källor som låg utanför staden, och de hjälpte honom. 4Mycket folk samlades, och de täppte till alla källorna och dämde också upp den bäck som rann genom landet. ”Varför skulle kungen32:4 Egentligen kungar; här singularis i enlighet med bl.a. Septuaginta. av Assyrien komma hit och hitta gott om vatten?” sa de.

5Hiskia arbetade hårt med att reparera alla de raserade murarna och byggde upp tornen vid dem. Han byggde en andra mur utanför den första, befäste Millo i Davids stad och lät tillverka en mängd vapen och sköldar. 6Han utsåg officerare över armén och sammankallade dem till sig på den öppna platsen vid stadsporten. Han talade till dem och försökte stärka deras mod:

7”Var starka och modiga, och var inte rädda för kungen i Assyrien och hans väldiga armé, för den som är med oss är större än den som är med honom! 8Med honom finns bara en mänsklig armé, men vi har Herren, vår Gud, som hjälper oss och strider för oss.”

Folket fick nytt mod av Hiskias, Juda kungs, ord.

9Kung Sanherib av Assyrien, som med hela sin armé låg vid Lakish, skickade efter en tid bud till Jerusalem till kung Hiskia av Juda och alla judéer som var där och lät säga:

10Så säger Sanherib, kungen av Assyrien: ”Vad är det ni förtröstar på när ni nu stannar kvar i det belägrade Jerusalem? 11Hiskia lurar ju er till att ni ska dö av hunger och törst, när han säger: ’Herren, vår Gud, ska rädda oss undan kungen av Assyrien’ 12Var det inte samme Hiskia som förstörde alla hans offerhöjder och altaren och befallde Juda och Jerusalem: ’Ni ska tillbe vid ett enda altare och tända rökelse på det.’

13Vet ni inte vad jag och mina fäder har gjort med folken i andra länder? Kunde dessa folks gudar rädda sina länder ur mitt våld? 14Vilken av alla gudar hos dessa folk som mina fäder har förintat har kunnat rädda sitt folk från min makt? Hur skulle då er Gud kunna rädda er ur min makt? 15Låt inte Hiskia lura och bedra er så här! Tro inte på honom, för ingen gud i något land har någonsin kunnat rädda sitt folk från mig eller mina fäder. Varför skulle då er Gud kunna göra det?”

16Hans män talade ännu mer mot Herren Gud och hånade hans tjänare Hiskia. 17Sanherib skrev också brev, där han hädade Herren, Israels Gud, och sa om honom: ”Lika lite som andra folks gudar lyckades rädda sina folk ur mitt våld, lika lite ska Hiskias Gud kunna rädda sitt folk ur mitt våld.”

18De ropade högt på hebreiska till folket från Jerusalem som samlats på stadsmurarna, för att skrämma dem och göra dem rädda, så att de skulle kunna inta staden. 19De talade om Jerusalems Gud på samma sätt som om gudarna hos andra folk på jorden, som är gjorda av människor.

20Kung Hiskia och profeten Jesaja, Amos son, ropade då i bön till Gud i himlen, 21och Herren skickade en ängel som förintade alla tappra krigare, furstar och officerare i den assyriske kungens läger, så att han med skam fick vända tillbaka till sitt land. Och när han kom till sin guds hus, blev han dödad med svärd av några av sina söner. 22Så räddade Herren Hiskia och folket i Jerusalem ur den assyriske kungen Sanheribs våld, och ur alla andras. Han beskyddade dem på alla sidor32:22 Eller lät dem få fred på alla sidor; något olika i olika handskrifter..

23Många kom till Jerusalem med gåvor till Herren och dyrbara gåvor till Juda kung Hiskia. Han blev härefter högt ansedd bland folken.

Hiskia prövas

(2 Kung 20:1-21; Jes 38:1-8; 39:1-8)

24Vid denna tid blev Hiskia dödssjuk och bad till Herren, och Herren svarade honom med ett under. 25Men Hiskia återgäldade inte det goda han fått utan var högmodig; därför kom vreden över honom och över Juda och Jerusalem. 26Då ödmjukade sig den högmodige Hiskia och Jerusalems invånare och drabbades därför inte av Herrens vrede under Hiskias livstid.

27Hiskia blev mycket rik och högt aktad. Han byggde skattkamrar för allt sitt silver och guld, för dyrbara stenar, kryddor, sköldar och andra värdefulla föremål. 28Han byggde också förrådshus för säd, vin och olja och stallar för alla slags boskap och fållor för hjordarna. 29Han byggde städer och köpte får och nötboskap i mängd. Gud gav honom oerhörda rikedomar.

30Det var också Hiskia som dämde upp övre källan i Gichon och förde dess vatten ner till västra sidan av Davids stad. Hiskia lyckades med allt han företog sig. 31Men när sändebud kom från Babylons furstar för att få veta mer om det under som inträffat i landet, lämnade Gud honom för att pröva honom och se vad som fanns i hans innersta.

32Hiskias historia i övrigt och hans fromma gärningar finns nedtecknade i profeten Jesajas, Amos sons, syner i boken om Judas och Israels kungar.

33När Hiskia dog begravdes han bland de övriga kungarna högst upp bland Davids ättlingars gravar, och hela Juda och Jerusalem ärade honom vid hans död.

Hans son Manasse blev kung efter honom.