2 Nyakati 32 – NEN & BDS

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Nyakati 32:1-33

Senakeribu Aitishia Yerusalemu

(2 Wafalme 18:13-37; 19:14-19, 35-37; Isaya 36:1-22; 37:8-38)

132:1 2Fal 18:13-19; Isa 37:9Baada ya yale yote aliyokuwa amefanya Hezekia kwa uaminifu mkubwa, Senakeribu mfalme wa Ashuru akaja na kuvamia Yuda. Akaizunguka miji yenye ngome kwa jeshi, akifikiri kuiteka iwe yake. 232:2 Isa 22:7; Yer 1:15Hezekia alipoona kuwa Senakeribu amekuja na kwamba alikusudia kufanya vita juu ya Yerusalemu, 3akafanya shauri na maafisa wake na mashujaa wake juu ya kuzuia maji kutoka chemchemi zilizo nje ya mji, nao wakamsaidia. 432:4 2Fal 20:20; Nah 3:14Umati mkubwa wa watu ukakusanyika na kuzuia chemchemi zote na vijito vilivyotiririka katika nchi yote, wakisema: “Kwa nini wafalme wa Ashuru waje na kukuta maji tele?” 532:5 2Nya 25:23; Isa 22:9-10; 1Fal 9:24; 2Sam 5:9; 1Nya 11:8Hezekia akafanya kazi kwa bidii kukarabati sehemu zote zilizokuwa zimebomoka za ukuta na kujenga minara juu yake. Akajenga ukuta mwingine nje ya ule uliokuwepo na kuimarisha Milo32:5 Milo maana yake Boma la Ngome. katika Mji wa Daudi. Akatengeneza pia silaha nyingi na ngao.

632:6 2Nya 30:22; Isa 40:2Akaweka maafisa wa jeshi juu ya watu, wakawakutanisha mbele yake katika uwanja kwenye lango la mji, naye akawatia moyo kwa maneno haya: 732:7 Kum 31:6; 1Nya 22:13; 28:10; 2Nya 20:15; Hes 14:9; 2Fal 6:16; Za 55:18“Kuweni hodari na wenye moyo mkuu. Msiogope, msifadhaike wala msikate tamaa kwa sababu ya mfalme wa Ashuru na hili jeshi kubwa lililo pamoja naye, kwa kuwa aliye pamoja nasi ni mkuu kuliko aliye pamoja naye. 832:8 Ay 40:9; Isa 41:10-14; 52:10; 1Sam 17:45; 2Nya 13:12; 1Nya 5:22; Rum 8:31; Yer 17:5; 1Yn 4:4; Kum 20:1-4; 31:6-8; Mit 18:10; Amo 5:14Kwake uko mkono wa mwili tu, bali kwetu yuko Bwana Mungu wetu kutusaidia na kutupigania vita vyetu.” Nao watu wakatiwa moyo kutokana na maneno aliyowaambia Hezekia mfalme wa Yuda.

932:9 2Fal 18:17; Yos 10:3Hatimaye Senakeribu mfalme wa Ashuru na majeshi yake yote walipokuwa wameuzunguka Lakishi, akawatuma maafisa wake kwenda Yerusalemu wakiwa na ujumbe huu kwa Hezekia mfalme wa Yuda, na kwa watu wote wa Yuda waliokuwako humo, kusema:

1032:10 Eze 29:16“Hili ndilo asemalo Senakeribu mfalme wa Ashuru: Je, mmeweka tumaini lenu wapi, hata mnaendelea kukaa katika Yerusalemu, hali mmezungukwa na jeshi? 1132:11 Isa 37:10Hezekia asemapo, ‘Bwana Mungu wetu atatuokoa kutokana na mkono wa mfalme wa Ashuru,’ anawapotosha ninyi, naye atawaacha mfe kwa njaa na kiu. 12Je, si Hezekia mwenyewe aliyeondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu pamoja na madhabahu zake, akiwaambia Yuda wa Yerusalemu, ‘Ni lazima mwabudu mbele ya madhabahu moja na kuteketeza dhabihu juu yake’?

1332:13 2Fal 18:33-35; Za 115:4-8“Je, hamjui yale mimi na baba zangu tuliyoyafanya kwa mataifa yote ya nchi zingine? Je, miungu ya mataifa hayo iliweza kuokoa nchi zao kutoka mkononi mwangu? 14Ni yupi miongoni mwa miungu yote ya mataifa haya ambayo baba zangu waliyaangamiza ameweza kuwaokoa watu wake mkononi mwangu? Inawezekanaje basi Mungu wenu kuwaokoa mkononi mwangu? 1532:15 Isa 37:10; Dan 3:15; Kut 5:2; Yn 19:10-11Sasa basi, msikubali Hezekia awadanganye na kuwapotosha namna hii. Msimwamini, kwa kuwa hakuna mungu wa taifa lolote wala wa ufalme wowote aliyeweza kuwaokoa watu wake kutoka mkononi mwangu au mkononi mwa baba zangu. Sembuse huyo mungu wenu atawaokoaje kutoka mkononi mwangu!”

16Maafisa wa Senakeribu wakaendelea kunena dhidi ya Bwana aliye Mungu na dhidi ya mtumishi wake Hezekia. 1732:17 Isa 37:14; Za 74:22; 2Fal 19:12Mfalme pia aliandika barua akimtukana Bwana, Mungu wa Israeli na kusema haya dhidi yake: “Kama vile miungu ya mataifa ya nchi nyingine ilivyoshindwa kuwaokoa watu wao mkononi mwangu, vivyo hivyo Mungu wa Hezekia hataweza kuwaokoa watu wake kutoka mkononi mwangu.” 1832:18 2Fal 18:28Kisha wakawaita kwa Kiebrania watu wa Yerusalemu waliokuwa juu ya ukuta ili kuwatisha na kuwatia hofu ili waweze kuuteka mji. 1932:19 Za 115:4; Yer 1:16; Za 135:15-18; Isa 10:10; Kum 4:28; 2Fal 19:18; Yer 10:3; Hos 8:5-6Wakanena juu ya Mungu wa Yerusalemu kama vile walivyonena juu ya miungu ya mataifa mengine ya dunia ambayo ni kazi ya mikono ya wanadamu.

20Mfalme Hezekia na nabii Isaya mwana wa Amozi wakalilia mbingu katika maombi kuhusu jambo hili. 2132:21 Mwa 19:13; Isa 37:38; Yer 41:2Naye Bwana akamtuma malaika ambaye aliangamiza wanajeshi wote, na viongozi na maafisa katika kambi ya mfalme wa Ashuru. Kwa hiyo, mfalme wa Ashuru akarudi nchini mwake kwa aibu. Naye alipokwenda katika hekalu la mungu wake, baadhi ya watoto wake wakamuua kwa upanga.

2232:22 Za 18:48-50; Isa 31:5Hivyo Bwana akamwokoa Hezekia na watu wa Yerusalemu kutoka mkononi mwa Senakeribu mfalme wa Ashuru na kutoka mikononi mwa wengine wote. Bwana akawastarehesha kila upande. 2332:23 1Sam 10:27; Za 76:11; 1Nya 29:25; 2Nya 17:5Watu wengi wakaleta sadaka Yerusalemu kwa ajili ya Bwana na zawadi za thamani kwa ajili ya Hezekia mfalme wa Yuda. Tangu hapo na kuendelea, Hezekia aliheshimiwa sana na mataifa yote.

Kiburi Cha Hezekia, Mafanikio Na Kifo

(2 Wafalme 20:1-3, 12-19; Isaya 38:1-3; 39:1-8)

2432:24 Isa 38:1Katika siku hizo, Hezekia akaugua, naye akawa karibu kufa. Akamwomba Bwana, ambaye alimjibu na kumpa ishara. 2532:25 2Fal 14:10; Kum 32:6; 2Nya 26:16; 19:2; 24:18; Kum 8:12; Za 116:12; Lk 17:17; 2Fal 14:10; Hab 2:4; 1Tim 3:6; 1Pet 5:5-6Lakini moyo wa Hezekia ukajaa majivuno na hakuonyesha itikio kwa wema aliotendewa, kwa hiyo ghadhabu ya Bwana ikawa juu yake na juu ya Yuda na Yerusalemu. 2632:26 Yer 26:18-19; 2Nya 34:27-28; 2Fal 19:20; Isa 39:8Ndipo Hezekia akatubu kwa ajili ya kiburi cha moyo wake, kama walivyofanya watu wa Yerusalemu, kwa hiyo ghadhabu ya Bwana haikuja juu yao katika siku za Hezekia.

2732:27 1Nya 29:12; 2Nya 9:24Hezekia alikuwa na utajiri mwingi sana na heshima, naye akajifanyia hazina kwa ajili ya fedha yake na dhahabu na kwa ajili ya vito vyake vya thamani, vikolezi, ngao na aina zote za vyombo vya thamani. 28Akajenga pia maghala ya kuhifadhi mavuno ya nafaka, divai mpya na mafuta. Akatengeneza mabanda kwa ajili ya aina mbalimbali za mifugo, na mazizi kwa ajili ya kondoo na mbuzi. 2932:29 2Nya 29:12Akajenga vijiji na kujipatia idadi kubwa ya kondoo na mbuzi, pamoja na ngʼombe kwa kuwa Mungu alikuwa amempa utajiri mwingi sana.

3032:30 2Fal 18:17; 1Fal 1:33; Isa 22:9Ilikuwa ni Hezekia aliyeziba njia za kutolea maji za chemchemi za juu za Gihoni na kuyaelekeza maji kutiririkia upande wa magharibi wa Mji wa Daudi. Akafanikiwa katika kila kitu alichofanya. 3132:31 Isa 13:1; 39:1; 38:7; Kum 8:16; Mwa 22:1; Yn 1:12Lakini wakati wajumbe walipotumwa na watawala wa Babeli kumuuliza juu ya ishara ambayo ilitokea katika nchi, Mungu alimwacha ili kumjaribu na kujua kila kitu kilichokuwa moyoni mwake.

3232:32 Isa 36:1; 2Fal 18:1Matukio mengine ya utawala wa Hezekia na matendo yake ya kujitoa kwa moyo yameandikwa katika maono ya nabii Isaya mwana wa Amozi kwenye kitabu cha wafalme wa Yuda na Israeli. 3332:33 1Sam 2:30; Mit 10:7Hezekia akalala na baba zake na akazikwa kwenye kilima mahali yalipo makaburi ya wazao wa Daudi. Yuda wote na watu wa Yerusalemu wakamheshimu alipofariki. Naye Manase mwanawe akawa mfalme baada yake.

La Bible du Semeur

2 Chroniques 32:1-33

La menace assyrienne

1Après ces événements qui démontrèrent la fidélité d’Ezéchias envers Dieu, Sennachérib, roi d’Assyrie, vint envahir le territoire de Juda. Il assiégea les villes fortifiées et ordonna d’en forcer les remparts32.1 Autre traduction : avec l’intention de s’en emparer.. 2Ezéchias, voyant que Sennachérib était venu avec l’intention d’attaquer Jérusalem, 3tint conseil avec ses ministres et ses officiers pour faire obturer les sources d’eau situées en dehors de la ville. Tous l’aidèrent 4et beaucoup de gens se rassemblèrent. Ils bouchèrent toutes les sources, y compris celle dont l’eau s’écoulait par un canal souterrain32.4 Primitivement, les eaux de la source de Guihôn s’écoulaient vers le Cédron. Pour empêcher les assiégeants de trouver de l’eau pour leurs besoins, Ezéchias fit obstruer l’écoulement extérieur et capta les eaux pour les amener par un canal souterrain à l’intérieur de la ville où elles ravitaillaient les assiégés en eau potable (voir 2 R 20.20).. « Pourquoi, disaient-ils, les rois d’Assyrie trouveraient-ils à leur arrivée de l’eau en abondance ? » 5Ensuite, Ezéchias se mit courageusement à reconstruire toute la muraille de la ville là où elle avait des brèches et il suréleva les tours. Il la doubla d’une seconde muraille à l’extérieur, renforça les terrasses aménagées pour les cultures dans la Cité de David. Il fit aussi fabriquer une grande quantité d’armes et de boucliers. 6Enfin, il établit des chefs militaires sur l’armée, puis il les rassembla autour de lui sur la place près de la porte de la ville pour les encourager. Il leur dit : 7Soyez forts et prenez courage ! Soyez sans crainte, ne vous laissez pas effrayer par le roi d’Assyrie et les troupes nombreuses qui l’accompagnent ; car nous avons avec nous quelqu’un de plus puissant que lui. 8Ce roi n’a avec lui qu’une force humaine, mais nous, nous avons avec nous l’Eternel notre Dieu. Il viendra à notre secours et il combattra pour nous.

Alors toute la population fit confiance aux paroles d’Ezéchias, roi de Juda.

Le défi

(2 R 18.17-35)

9Après cela, Sennachérib, roi d’Assyrie, envoya une délégation à Jérusalem vers Ezéchias, roi de Juda, et vers tous ceux de Juda qui étaient dans Jérusalem pendant qu’il était lui-même devant Lakish avec toutes ses forces. Il leur fit dire32.9 Voir v. 9-19 : parallèles à Es 36.2-20. : 10Voici ce que déclare Sennachérib, roi d’Assyrie : En quoi placez-vous votre confiance, pour que vous restiez ainsi enfermés dans la forteresse de Jérusalem ? 11Ne voyez-vous pas qu’Ezéchias vous trompe pour vous faire mourir de faim et de soif quand il dit : « L’Eternel, notre Dieu, nous délivrera du roi d’Assyrie ? » 12N’est-ce pas précisément ce Dieu dont Ezéchias a fait disparaître les hauts lieux et les autels, en disant aux habitants de Juda et de Jérusalem de rendre leur culte uniquement devant un seul autel et d’y brûler des parfums ? 13Ne savez-vous pas ce que nous avons fait, moi et mes ancêtres, à tous les peuples des autres pays ? Leurs dieux ont-ils pu délivrer leur pays de mon emprise ? 14De tous les dieux de ces peuples exterminés par mes ancêtres, quels sont ceux qui ont délivré leur peuple pour que votre Dieu soit capable de vous délivrer ? 15Maintenant, ne vous laissez donc pas tromper par Ezéchias et qu’il ne vous abuse pas de cette manière ! Ne vous fiez pas à lui ! Car aucun dieu d’aucun peuple ni d’aucun royaume n’a pu délivrer son peuple de moi-même, ou de mes ancêtres. Et vos dieux ne vous délivreront pas davantage de mon emprise !

16Les envoyés de Sennachérib continuèrent à parler contre l’Eternel Dieu et contre Ezéchias son serviteur. 17Sennachérib avait aussi écrit des lettres outrageantes pour l’Eternel, le Dieu d’Israël, dans lesquelles il le prenait à partie disant : Pas plus que les dieux des autres pays n’ont délivré leur peuple de mon emprise, le Dieu d’Ezéchias ne délivrera son peuple de mon emprise.

18Les envoyés crièrent d’une voix forte en hébreu, à l’adresse des habitants de Jérusalem qui étaient sur la muraille, afin de les effrayer et de les terroriser pour pouvoir s’emparer de la ville. 19Ils parlèrent du Dieu de Jérusalem comme s’il s’agissait d’un dieu des peuples païens, simple ouvrage fabriqué par des hommes.

Dieu répond aux prières

(2 R 19.35-37)

20Le roi Ezéchias et le prophète Esaïe, fils d’Amots, se mirent à prier à ce sujet, et ils crièrent vers le ciel pour implorer du secours32.20 Voir v. 20-21 : parallèles à Es 37.36-38.. 21Alors l’Eternel envoya un ange qui extermina dans le camp du roi d’Assyrie tous les guerriers valeureux, y compris les généraux et les officiers, si bien que le roi retourna dans son pays tout confus. Un jour, il pénétra dans le temple de son dieu, et ses propres fils l’y assassinèrent d’un coup d’épée.

22C’est ainsi que l’Eternel délivra Ezéchias et les habitants de Jérusalem de Sennachérib, roi d’Assyrie, et de tout autre ennemi. Il leur accorda la paix sur toutes leurs frontières32.22 D’après l’ancienne version grecque et la Vulgate ; le texte hébreu traditionnel a : il les conduisit ou il prit soin d’eux.. 23Nombreux furent ceux qui apportèrent alors à Jérusalem une offrande à l’Eternel et de riches présents pour Ezéchias, roi de Juda. A la suite de ces événements, il acquit un grand prestige aux yeux de tous les autres peuples.

La fin du règne d’Ezéchias

(2 R 20.1-21)

24A cette époque Ezéchias tomba très gravement malade. Il pria l’Eternel qui lui donna un signe prodigieux32.24 Miracle raconté en 2 R 20.1-11 que le Chroniste suppose connu de ses lecteurs. Voir v. 24-33 : parallèles à Es 38.1-8 ; 39.1-8.. 25Mais Ezéchias ne se conduisit pas ensuite d’une manière qui marque sa reconnaissance pour cela ; au contraire, il devint orgueilleux et attira la colère de l’Eternel sur lui, sur Juda et sur Jérusalem. 26Alors Ezéchias s’humilia de son orgueil et les habitants de Jérusalem firent de même, de sorte que l’Eternel ne fit pas éclater sa colère contre eux du vivant d’Ezéchias.

27Ezéchias fut grandement comblé de richesses et de gloire. Il se constitua des réserves d’argent, d’or, de pierres précieuses, de parfums et d’aromates, de boucliers32.27 Sans doute des boucliers décoratifs, peut-être en or (voir 1 R 10.16-17). et de toutes sortes d’objets précieux. 28Il fit bâtir des entrepôts pour engranger les récoltes de blé, de vin nouveau et d’huile. Il construisit des étables pour toutes sortes d’animaux domestiques et aménagea des enclos pour ses troupeaux. 29Il édifia des villes et eut des troupeaux nombreux de petit et de gros bétail, car Dieu lui avait donné d’immenses richesses. 30Ce fut aussi lui, Ezéchias, qui fit obturer l’issue supérieure des eaux de la source de Guihôn et les canalisa plus bas vers l’ouest de la Cité de David. Ainsi, Ezéchias réussit dans toutes ses entreprises.

31Cependant, lors de la visite des ambassadeurs des dirigeants babyloniens envoyés pour s’informer sur le prodige qui avait eu lieu dans le pays, Dieu l’abandonna à lui-même pour le mettre à l’épreuve et savoir ce qui était réellement au fond de son cœur.

32Les autres faits et gestes d’Ezéchias, et ses actes de piété sont cités dans la révélation du prophète Esaïe32.32 Voir Es 36 à 39., fils d’Amots, et dans le livre des rois de Juda et d’Israël32.32 Voir 16.11 et note..

33Ezéchias rejoignit ses ancêtres décédés, et on l’enterra dans la partie supérieure des tombeaux des descendants de David. Tout Juda et les habitants de Jérusalem lui rendirent les derniers honneurs. Son fils Manassé lui succéda sur le trône.