2 Nyakati 31 – NEN & BDS

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Nyakati 31:1-21

Sehemu Za Ibada Za Kipagani Zaondolewa

131:1 2Fal 18:4; Isa 36:7; 2Nya 13:14Baada ya mambo haya yote kumalizika, Waisraeli ambao walikuwako huko wakaenda kwenye miji ya Yuda, wakayavunja yale mawe ya kuabudia na kuzikatakata zile nguzo za Ashera. Wakabomoa mahali pa juu pa kuabudia miungu pamoja na madhabahu zake kila mahali katika Yuda na Benyamini na katika Efraimu na Manase. Baada ya kuviharibu hivi vyote, Waisraeli wakarudi katika miji yao wenyewe na kwenye milki zao.

231:2 2Nya 29:9; Za 71:22; 1Nya 23:28-32; 15:2Hezekia akawapanga makuhani na Walawi katika migawanyo, kila mgawanyo kulingana na wajibu wao, kama ni makuhani au Walawi, ili kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani, kuhudumu, kushukuru na kuimba sifa katika malango ya makao ya Bwana. 331:3 1Nya 29:3; Eze 45:17; Hes 28:1; 29:40Mfalme akatoa matoleo kutoka mali zake mwenyewe kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa za asubuhi na za jioni na sadaka za kuteketezwa kwa siku za Sabato, kwa Sikukuu za Mwezi Mwandamo na kwa ajili ya sikukuu zilizoamriwa kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Bwana. 431:4 Neh 13:10-12; Mal 2:7; 1Kor 9:13; Hes 18:8Akawaagiza watu wanaoishi Yerusalemu watoe sehemu iliyo haki ya makuhani na Walawi ili waweze kujitoa kikamilifu kutimiza wajibu wao katika Sheria ya Bwana. 531:5 Neh 13:12; Eze 44:30; Kum 12:17; 1Kor 15:20; Kut 22:29; 23:19; Hes 18:12; Eze 20:40; Yak 1:18; Mit 3:9Mara tu baada ya kutolewa tangazo hilo, Waisraeli wakatoa kwa ukarimu malimbuko ya nafaka zao, divai mpya, mafuta na asali pamoja na vyote vilivyotoka mashambani. Wakaleta kiasi kikubwa cha fungu la kumi la kila kitu. 631:6 Law 27:30; Neh 13:10-12; Kum 14:28; Rut 3:7Watu wa Israeli na Yuda walioishi katika miji ya Yuda wakaleta pia fungu la kumi la makundi yao ya ngʼombe na makundi ya kondoo na mbuzi pia na fungu la kumi la vitu vitakatifu vilivyowekwa wakfu kwa ajili ya Bwana Mungu wao na kuvikusanya katika malundo. 731:7 Kut 23:16Wakaanza kufanya haya katika mwezi wa tatu na kumaliza katika mwezi wa saba. 831:8 Za 144:13-15; Mwa 14:19; 2Sam 6:18; Kum 33:29; 1Fal 8:55-56; 2Nya 6:3; Za 33:12; 144:15Wakati Hezekia na maafisa wake walipokuja na kuona yale malundo, wakamsifu Bwana na kuwabariki watu wake Israeli.

9Hezekia akawauliza makuhani na Walawi kuhusu yale malundo, 1031:10 2Sam 8:17; Kut 36:5; Hag 2:19; Mal 3:10-12naye Azaria aliyekuwa kuhani mkuu, kutoka jamaa ya Sadoki, akajibu, “Tangu watu walipoanza kuleta sadaka zao katika Hekalu la Bwana tumekuwa na chakula cha kutosha na vingi vya kuweka akiba kwa sababu Bwana amewabariki watu wake, hivyo tumekuwa na kiasi kingi kilichobaki.”

Kutambuliwa Kwa Makuhani Na Walawi

11Hezekia akatoa agizo la kutengeneza vyumba vya ghala katika Hekalu la Bwana nalo hili likafanyika. 1231:12 2Nya 35:9; Neh 13:13Kisha kwa uaminifu wakaleta sadaka zao, mafungu yao ya kumi na vitu vilivyowekwa wakfu. Konania Mlawi, ndiye alikuwa msimamizi wa vitu hivi na Shimei ndugu yake ndiye alikuwa msaidizi wake. 13Yehieli, Azazia, Nahathi, Asaheli, Yeremothi, Yozabadi, Elieli, Ismakia, Mahathi na Benaya walikuwa waangalizi chini ya Konania na Shimei ndugu yake, waliokuwa wamewekwa na Mfalme Hezekia na Azaria, afisa msimamizi wa Hekalu la Mungu.

14Kore mwana wa Imna, Mlawi, bawabu wa Lango la Mashariki, alikuwa msimamizi wa sadaka za hiari zilizotolewa kwa Mungu, akiyagawanya hayo matoleo yaliyotolewa kwa Bwana na pia zile sadaka zilizowekwa wakfu. 1531:15 2Nya 29:12; Yos 21:9-19Edeni, Miniamini, Yeshua, Shemaya, Amaria na Shekania walimsaidia kwa uaminifu katika miji ya makuhani, wakiwagawia makuhani wenzao kufuatana na migawanyo yao, wazee kwa vijana sawasawa.

1631:16 1Nya 23:3; Ezr 3:4Zaidi ya hao wakawagawia wanaume wenye umri wa miaka mitatu au zaidi ambao majina yao yalikuwa kwenye orodha ya vizazi, wale wote ambao wangeingia katika Hekalu la Bwana ili kufanya kazi zao mbalimbali za kila siku kulingana na wajibu katika mgawanyo wao. 1731:17 1Nya 23:24, 27Kuandikishwa kwa makuhani kulikuwa kwa kufuata chimbuko la nyumba za baba zao na Walawi kuanzia umri wa miaka ishirini au zaidi ilikuwa kufuatana na huduma zao, kwa migawanyo yao. 18Makuhani waliandikishwa pamoja na watoto wao wadogo, wake zao, watoto wao wa kiume na wa kike, jamii yote iliandikishwa kwa kufuata orodha ya vizazi vyao. Kwa kuwa walikuwa waaminifu katika kujitakasa.

1931:19 Law 25:34; 2Nya 31:12-15; Hes 35:2Kuhusu makuhani, wazao wa Aroni walioishi kwenye mashamba yaliyozunguka miji yao au katika miji mingine yoyote, watu walitajwa majina ili kumgawia kila mwanaume miongoni mwao na kwa wote waliokuwa katika orodha ya vizazi vya Walawi.

2031:20 2Fal 20:3; 22:2; 1The 2:10; 1Fal 15:5; Yn 1:47Hivi ndivyo Hezekia alivyofanya katika Yuda yote, akifanya lile lililo jema, sawa na la uaminifu mbele za Bwana Mungu wake. 2131:21 Kum 29:9; Mit 3:9; Yos 4:7; Mal 3:10; 1Tim 4:8Naye katika kila kitu alichofanya katika huduma kwenye Hekalu la Mungu na katika utii kwa sheria na amri, alimtafuta Mungu wake na kufanya kazi kwa moyo wake wote. Naye hivyo akafanikiwa.

La Bible du Semeur

2 Chroniques 31:1-21

Ezéchias réorganise le service du Temple

1Lorsque toute la fête fut terminée, tous les Israélites qui se trouvaient là partirent pour les villes de Juda et brisèrent les stèles des idoles, abattirent les pieux sacrés d’Ashéra et démolirent les hauts lieux et les autels dans tout Juda et Benjamin, ainsi que dans les territoires d’Ephraïm et de Manassé, jusqu’à ce qu’il n’en reste plus. Puis tous les Israélites retournèrent dans leurs villes, chacun dans sa propriété.

2Ezéchias rétablit l’organisation des prêtres et des lévites d’après leurs classes. Dans ces classes, il assigna à chacun sa fonction propre ; les prêtres et les lévites devaient s’occuper des holocaustes et des sacrifices de communion, du service, du chant des cantiques de louange et de remerciement aux portes de la demeure de l’Eternel. 3Le roi réserva une part de ses biens pour les holocaustes du matin et du soir et pour ceux des sabbats, des nouvelles lunes et des autres fêtes, selon ce qui est écrit dans la Loi de l’Eternel31.3 Sur les sacrifices, voir Nb 28 et 29.. 4D’autre part, il ordonna à la population de Jérusalem de donner la part des prêtres et des lévites, afin qu’ils puissent se consacrer aux tâches que leur prescrit la Loi de l’Eternel31.4 Pour les v. 4-5, voir Nb 18.12-13, 21.. 5Dès que cet ordre eut été publié, les Israélites apportèrent en grandes quantités les premières récoltes de blé, de vin nouveau, d’huile, de miel et de tous les produits agricoles. Ils apportèrent aussi la dîme de tout en abondance. 6Les Israélites et les Judéens qui habitaient dans les villes de Juda apportèrent eux aussi la dîme du gros bétail, des moutons et des chèvres, ainsi que celle des offrandes saintes qui étaient consacrées à l’Eternel leur Dieu. On fit des tas considérables des divers produits. 7Cette accumulation, commencée en mai-juin, ne prit fin qu’en septembre-octobre. 8Ezéchias et les ministres vinrent voir tout ce qui avait été apporté, et ils bénirent l’Eternel et son peuple d’Israël. 9Ezéchias s’enquit au sujet de ces dons auprès des prêtres et des lévites. 10Alors le grand-prêtre Azaria, un descendant de Tsadoq, lui répondit : Depuis que le peuple a commencé d’apporter sa contribution au temple de l’Eternel, nous avons eu de quoi manger à satiété, et il en reste énormément, car l’Eternel a béni le peuple. Ce qui est entassé ici, c’est le surplus.

11Ezéchias donna l’ordre d’aménager des entrepôts dans le temple de l’Eternel. Quand ils furent prêts, 12on y déposa fidèlement les contributions du peuple, les dîmes et les autres offrandes saintes. Le lévite Konania s’en vit confier la responsabilité. Il était secondé par son frère Shimeï.

13Sous leur direction, Yehiel, Azazia, Nahath, Asaël, Yerimoth, Yozabad, Eliel, Yismakia, Mahath et Benaya assuraient la supervision des opérations par décision du roi Ezéchias et d’Azaria, le surintendant du temple de Dieu. 14Le lévite Qoré, fils de Yimna, qui était gardien de la porte orientale, fut chargé de recevoir les dons volontaires faits à Dieu et de répartir les contributions apportées pour l’Eternel et les offrandes très saintes. 15Il avait sous ses ordres des lévites dans les villes sacerdotales31.15 Voir Nb 35.1-8 ; Jos 21.1-42.. C’étaient Eden, Minyamîn, Josué, Shemaya, Amaria et Shekania. Ils étaient chargés de distribuer consciencieusement les vivres à leurs collègues selon leurs classes, sans faire de différences entre ceux de rang important et ceux de rang moins important. 16Ils accordaient des parts, non seulement à tous les hommes enregistrés depuis l’âge de trois ans sur les listes du recensement sacerdotal, mais encore à tous ceux qui accomplissaient jour par jour les tâches relatives à leur service, selon leur classe, dans le temple de l’Eternel. 17Les prêtres furent enregistrés d’après leurs groupes familiaux, tandis que les lévites de vingt ans et plus étaient inscrits d’après leur service et leur classe. 18Ils étaient enregistrés avec leurs enfants, leurs femmes, leurs fils et leurs filles et cela était le cas pour toute la communauté des prêtres et des lévites, parce qu’ils s’acquittaient fidèlement des rites de purification pour être saints. 19Quant aux prêtres descendants d’Aaron, qui demeuraient à la campagne dans les alentours des villes sacerdotales, certains d’entre eux furent désignés nommément dans chaque localité pour assurer la distribution des vivres à tous les hommes parmi les prêtres et à tous les lévites enregistrés.

(2 R 18.5-7)

20C’est ainsi qu’Ezéchias agit dans tout le pays de Juda. Il fit ce qui est bien, juste et fidèle devant l’Eternel son Dieu. 21Pour tout ce qu’il entreprit, qu’il s’agisse du service du temple de Dieu ou de l’obéissance à la Loi et aux commandements, il chercha à plaire à son Dieu de tout son cœur, et tout lui réussit.