2 Nyakati 30 – NEN & PCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Nyakati 30:1-27

Hezekia Aadhimisha Pasaka

130:1 Mwa 41:52; Kut 12:11; Hes 28:16Hezekia akatuma ujumbe kuwaita Israeli wote na Yuda, pia akaandika barua kwa Efraimu na Manase, kuwakaribisha ili waje hekaluni mwa Bwana huko Yerusalemu kuadhimisha Pasaka kwa Bwana, Mungu wa Israeli. 230:2 Hes 9:10Mfalme na maafisa wake pamoja na kusanyiko lote katika Yerusalemu waliamua kuadhimisha Pasaka katika mwezi wa pili. 330:3 Hes 9:6-13; Kut 12:6; 2Nya 29:34Kwa sababu makuhani hawakuwa wamejitakasa idadi ya kutosha na watu wakawa hawajakusanyika huko Yerusalemu, hawakuwa wameweza kuadhimisha Pasaka kwa wakati wake wa kawaida. 4Mpango huu ukaonekana wafaa kwa mfalme na kusanyiko lote. 530:5 Amu 20:1Wakaamua kupeleka tangazo Israeli kote, kuanzia Beer-Sheba hadi Dani, wakiwaita watu waje Yerusalemu kuadhimisha Pasaka ya Bwana, Mungu wa Israeli. Ilikuwa haijaadhimishwa na idadi kubwa ya watu kama hiyo kufuatana na yale yaliyokuwa yameandikwa.

630:6 1Sam 7:3-4; Yoe 2:13; Mal 3:7; Isa 55:6-7; Hos 6:1; 2Fal 15:19-20Kwa amri ya mfalme, matarishi wakapita katika Israeli na Yuda kote wakiwa na barua kutoka kwa mfalme na kutoka kwa maafisa wake zikisema:

“Watu wa Israeli, mrudieni Bwana, Mungu wa Abrahamu, Isaki na Israeli, ili naye awarudie ninyi mliosalia, mlionusurika kutoka mikononi mwa wafalme wa Ashuru. 730:7 Yer 11:10; Eze 20:18; Kum 28:25; 2Nya 29:8-10Msiwe kama baba zenu na ndugu zenu, ambao hawakuwa waaminifu kwa Bwana, Mungu wa baba zao, hivyo akawafanya kitu cha kushangaza kama mnavyoona. 830:8 Kut 32:9; Hes 25:4; 2Nya 29:10; Kum 10:16Msiwe na shingo ngumu, kama baba zenu walivyokuwa, bali nyenyekeeni kwa Bwana. Njooni mahali patakatifu, alipopatakasa milele. Mtumikieni Bwana Mungu wenu, ili hasira yake kali igeuziwe mbali nanyi. 930:9 Yer 25:5; Kut 3:21; 34:6-7; Mik 7:18; Law 26:40; Isa 55:7Kama mkimrudia Bwana ndipo wale ndugu zenu waliotekwa pamoja na watoto wenu watakapoonewa huruma na wale waliowateka na kuwaachia warudi katika nchi hii, kwa kuwa Bwana Mungu wenu ni mwenye neema na huruma, hatageuzia uso wake mbali nanyi kama ninyi mkimrudia yeye.”

1030:10 Neh 2:19; 2Nya 36:16; Lk 8:53; Mt 21:35; Mdo 17:32; Yer 5:12; Ebr 11:36Matarishi wakaenda mji hadi mji katika Efraimu na Manase, wakafika mpaka Zabuloni, lakini watu wakawadharau na kuwadhihaki. 1130:11 2Nya 11:16Lakini, baadhi ya watu wa Asheri, Manase na Zabuloni, wakajinyenyekeza wakaja Yerusalemu. 1230:12 Ebr 13:21; Yer 32:39; 2Nya 20:33Pia katika Yuda mkono wa Mungu ulikuwa juu ya watu kuwapa umoja katika kutenda yale ambayo mfalme na maafisa wake waliwaamuru, kulingana na neno la Bwana.

1330:13 Hes 28:16Basi umati mkubwa wa watu ukakusanyika huko Yerusalemu kuadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu katika mwezi wa pili. 1430:14 2Nya 28:24; 2Sam 15:23; Isa 2:17-21Wakajitia kazini kuyaondoa yale madhabahu yaliyokuwa huko Yerusalemu, wakayaondoa pia yale madhabahu ya kufukizia uvumba kwa miungu na kuyatupa Bonde la Kidroni.

1530:15 2Nya 29:34Kisha wakamchinja mwana-kondoo wa Pasaka katika siku ya kumi na nne ya mwezi wa pili. Makuhani na Walawi waliona aibu, wakajitakasa na kuleta sadaka za kuteketezwa katika Hekalu la Bwana. 1630:16 2Nya 35:10Kisha wakachukua nafasi zao za kawaida kama ilivyoelezwa katika Sheria ya Mose mtu wa Mungu. Makuhani wakanyunyiza ile damu waliyokabidhiwa na Walawi. 1730:17 2Nya 29:34Kwa kuwa wengi waliokuwa katika lile kusanyiko walikuwa hawajajitakasa, iliwapasa Walawi wachinje wana-kondoo wengine wa Pasaka kwa ajili ya wale watu ambao hawakuwa safi, kwa kufuata taratibu za ibada ili kuwatakasa kwa Bwana. 1830:18 Kut 12:43-49; Hes 9:6-16Ingawa watu wengi miongoni mwa wale waliotoka Efraimu, Manase, Isakari na Zabuloni walikuwa hawajajitakasa, hata hivyo walikula Pasaka kinyume na ilivyoandikwa. Lakini Hezekia akawaombea, akisema, “Bwana, ambaye ni mwema na amsamehe kila mmoja 1930:19 Ezr 7:10; 2Nya 19:3; 1Nya 29:18; Ay 11:13; 2Nya 20:33ambaye anauelekeza moyo wake kumtafuta Mungu, Bwana, Mungu wa baba zake, hata kama yeye si safi kulingana na sheria za mahali patakatifu.” 2030:20 2Nya 6:20; 7:14; Kut 15:26; Yak 5:16; Za 103:3Naye Bwana akamsikia Hezekia akawaponya watu.

2130:21 Kut 12:15-17; Lk 22:1-7; Kut 13:6; 1Kor 5:7-8; Law 23:6Waisraeli waliokuwa Yerusalemu wakaadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu kwa muda wa siku saba, nao Walawi na makuhani walikuwa wakiimba kila siku, wakiwa na ala za uimbaji za kumsifu Bwana.

2230:22 Isa 40:2; Kum 33:10; 2Nya 17:9; 35:3; 2Tim 4:2; Ezr 10:11Hezekia akazungumza akiwatia moyo Walawi wote, ambao walionyesha ustadi katika kumtumikia Bwana. Hivyo watu wakala chakula cha sikukuu kwa siku saba, wakitoa sadaka za amani na kumshukuru Bwana, Mungu wa baba zao.

2330:23 1Fal 8:65; 2Nya 17:9; Isa 40:2Kisha kusanyiko lote likakubali kuendelea na sikukuu kwa siku saba zaidi, kwa hiyo kwa siku saba nyingine wakaendelea kuiadhimisha kwa furaha. 2430:24 1Fal 8:5; Ezr 6:17; 2Nya 35:7-8; 29:34Hezekia, mfalme wa Yuda akatoa mafahali 1,000, kondoo na mbuzi 7,000 kwa ajili ya kusanyiko, nao maafisa wakatoa mafahali 1,000 pamoja na kondoo na mbuzi 10,000. Idadi kubwa ya makuhani wakajiweka wakfu. 2530:25 2Nya 30:11, 18Kusanyiko lote la Yuda, pamoja na makuhani na Walawi na lile kusanyiko lote lililotoka Israeli, pamoja na wale wageni waliotoka Israeli na wale walioishi katika Yuda wakafurahi. 26Kulikuwa na furaha kubwa katika Yerusalemu, kwa sababu tangu siku za Mfalme Solomoni mwana wa Daudi mfalme wa Israeli halijakuwepo jambo kama hili katika Yerusalemu. 2730:27 Hes 6:23; Za 68:5; Isa 57:15; 66:1Ndipo makuhani na Walawi wakasimama wakawabariki watu, naye Mungu akawasikia, kwa sababu maombi yao yalifika mbinguni, makao yake matakatifu.

Persian Contemporary Bible

دوم تواريخ 30:1-27

حزقيا عيد پسح را جشن می‌گيرد

1حزقيای پادشاه، نامه‌هايی به سراسر اسرائيل و يهودا و مخصوصاً قبايل افرايم و منسی فرستاد و همه را دعوت نمود تا به اورشليم بيايند و در خانهٔ خداوند عيد پسح را برای خداوند، خدای اسرائيل جشن بگيرند. 2‏-3پادشاه و مقامات مملكتی و تمام جماعت اورشليم پس از مشورت با هم تصميم گرفتند مراسم عيد پسح را به جای وقت معمول آن در ماه اول، اين بار در ماه دوم برگزار نمايند. علت اين بود كه كاهنان كافی در اين زمان تقديس نشده بودند و قوم نيز در اورشليم جمع نشده بودند. 4اين تصميم با توافق پادشاه و تمام جماعت اخذ شد. 5پس به سراسر اسرائيل، از دان تا بئرشبع پيغام فرستادند و همه را دعوت كردند تا به اورشليم بيايند و عيد پسح را برای خداوند، خدای اسرائيل جشن بگيرند. زيرا مدت زيادی بود كه آن را بر اساس شريعت، به طور دسته جمعی جشن نگرفته بودند.

6قاصدان از طرف پادشاه و مقامات مملكت با نامه‌ها به سراسر اسرائيل و يهودا اعزام شدند. متن نامه‌ها چنين بود: «ای بنی‌اسرائيل، به سوی خداوند، خدای ابراهيم و اسحاق و يعقوب بازگشت كنيد، تا او نيز به سوی شما بازماندگان قوم كه از چنگ پادشاهان آشور جان به در برده‌ايد، بازگشت نمايد. 7مانند پدران و برادران خود نباشيد كه نسبت به خداوند، خدای اجدادشان گناه كردند و به طوری كه می‌دانيد به شدت مجازات شدند. 8مثل آنها ياغی نباشيد، بلكه از خداوند اطاعت نماييد و به خانهٔ او بياييد كه آن را تا به ابد تقديس فرموده است و خداوند، خدای خود را عبادت كنيد تا خشم او از شما برگردد. 9اگر شما به سوی خداوند بازگشت نماييد، برادران و فرزندان شما مورد لطف كسانی قرار می‌گيرند كه ايشان را اسير كرده‌اند و به اين سرزمين باز خواهند گشت. زيرا خداوند، خدای شما رحيم و مهربان است و اگر شما به سوی او بازگشت نماييد او شما را خواهد پذيرفت.»

10پس قاصدان، شهر به شهر از افرايم و منسی تا زبولون رفتند. ولی در اكثر جاها با ريشخند و اهانت مردم مواجه شدند. 11اما از قبيله‌های اشير، منسی و زبولون عده‌ای اطاعت نمودند و به اورشليم آمدند. 12در سرزمين يهودا نيز خدا تمام قوم را متحد ساخت تا فرمان پادشاه و مقامات را كه از جانب خداوند بود اطاعت كنند.

13گروه عظيمی در ماه دوم در شهر اورشليم جمع شدند تا عيد پسح را جشن بگيرند. 14ايشان برخاسته، تمام قربانگاه‌های اورشليم را كه روی آنها قربانی و بخور به بتها تقديم می‌شد در هم كوبيده به درهٔ قدرون ريختند.

15در روز چهاردهم ماه دوم، بره‌های عيد پسح را سر بريدند. كاهنان و لاويانی كه برای انجام مراسم آماده نشده بودند، خجالت كشيده، فوری خود را تقديس كردند و به تقديم قربانی مشغول شدند. 16آنها با ترتيبی كه در تورات موسی، مرد خدا آمده است سر خدمت خود ايستادند و كاهنان، خونی را كه لاويان به دست ايشان دادند، بر قربانگاه پاشيدند.

17‏-19عدهٔ زيادی از قوم كه از سرزمینهای افرايم، منسی، يساكار و زبولون آمده بودند مراسم طهارت و تقديس را بجا نياورده بودند و نمی‌توانستند بره‌های خود را ذبح كنند، پس لاويان مأمور شدند اين كار را برای ايشان انجام دهند. حزقيای پادشاه نيز برای ايشان دعا كرد تا بتوانند خوراک عيد پسح را بخورند، هر چند اين برخلاف شريعت بود. حزقيا چنين دعا كرد: «ای خداوند مهربان، خدای اجداد ما، هر كسی را كه قصد دارد تو را پيروی نمايد ولی شرعاً خود را برای شركت در اين مراسم تقديس نكرده است، بيامرز.» 20خداوند دعای حزقيا را شنيد و آنها را مجازات نكرد. 21پس بنی‌اسرائيل هفت روز عيد پسح را با شادی فراوان در شهر اورشليم جشن گرفتند.

ضمناً لاويان و كاهنان هر روز با آلات موسيقی خداوند را ستايش می‌كردند. 22(حزقيای پادشاه از تمام لاويانی كه مراسم عبادتی را خوب انجام داده بودند قدردانی كرد.) هفت روز مراسم عيد برقرار بود. قوم قربانیهای سلامتی تقديم كردند و خداوند، خدای اجدادشان را ستايش نمودند.

23تمام جماعت پس از مشورت، تصميم گرفتند عيد پسح هفت روز ديگر ادامه يابد؛ پس با شادی هفت روز ديگر اين عيد را جشن گرفتند. 24حزقيا هزار گاو و هفت هزار گوسفند برای قربانی به جماعت بخشيد. مقامات مملكتی نيز هزار گاو و ده هزار گوسفند هديه كردند. در اين هنگام عدهٔ زيادی از كاهنان نيز خود را تقديس نمودند.

25تمام مردم يهودا، همراه با كاهنان و لاويان و آنانی كه از مملكت اسرائيل آمده بودند، و نيز غريبان ساكن اسرائيل و يهودا، شادی می‌كردند. 26اورشليم از زمان سليمان پسر داوود پادشاه تا آن روز، چنين روز شادی به خود نديده بود. 27در خاتمه، كاهنان و لاويان ايستاده، قوم را بركت دادند و خدا دعای آنها را از قدس خود در آسمان شنيد و اجابت فرمود.