2 Nyakati 3 – NEN & NUB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Nyakati 3:1-17

Solomoni Ajenga Hekalu

(1 Wafalme 6:1-38; 7:15-22)

13:1 Mdo 7:47; Mwa 28:17; 2Sam 24:18; Yn 2:19-21; 1Fal 6:1; 1Nya 29:19; 1Kor 6:19; Mwa 22:2Ndipo Solomoni akaanza kujenga Hekalu la Bwana katika Yerusalemu juu ya Mlima Moria, pale ambapo Bwana alikuwa amemtokea Daudi baba yake. Ilikuwa katika kiwanja cha kupuria cha Arauna,3:1 Pia anaitwa Ornani kwa Kiebrania. Myebusi, mahali palipotolewa na Daudi. 23:2 Ezr 5:11Alianza kujenga siku ya pili ya mwezi wa pili katika mwaka wa nne wa utawala wake.

33:3 Eze 41:2; 1Fal 6:2-3Msingi aliouweka Solomoni kwa ajili ya kulijenga Hekalu la Mungu ulikuwa urefu wa dhiraa sitini3:3 Dhiraa 60 ni sawa na mita 27. na upana dhiraa ishirini.3:3 Dhiraa 20 ni sawa na mita 9. 43:4 1Fal 6:3Ukumbi wa mbele wa Hekalu ulikuwa na urefu wa dhiraa ishirini, yaani, kuanzia upande mmoja hadi upande mwingine wa upana wa nyumba hiyo na kimo chake dhiraa thelathini.3:4 Dhiraa 30 ni sawa na mita 13.5.

Akaufunika ndani kwa dhahabu safi. 53:5 Eze 40:16; 1Fal 6:17Akaufunika ukumbi mkuu kwa mbao za miberoshi na kufunikwa kwa dhahabu safi na kuupamba kwa miti ya mitende na kuifanyizia kwa minyororo. 6Alilipamba Hekalu kwa vito vya thamani. Hiyo dhahabu aliyotumia ilikuwa dhahabu ya Parvaimu. 73:7 1Fal 6:29-35; Eze 41:18Akazifunika boriti za dari, miimo na vizingiti vya milango, kuta na milango ya Hekalu kwa dhahabu, naye akatia nakshi ya makerubi kwenye kuta.

83:8 Kut 26:32-33Akajenga Patakatifu pa Patakatifu, urefu na upana wake ulikuwa dhiraa ishirini, sawasawa na upana wa Hekalu. Alifunika ndani kwa talanta 1203:8 Talanta 120 za dhahabu ni sawa na tani 23. za dhahabu safi. 9Misumari ya dhahabu ilikuwa na uzito wa shekeli hamsini.3:9 Shekeli 50 za dhahabu ni sawa na gramu 600. Alivifunika pia vyumba vya juu kwa dhahabu.

103:10 Kut 25:18; 1Fal 6:23Katika sehemu ya Patakatifu pa Patakatifu akafanyiza jozi moja ya makerubi ya kuchongwa na kuyafunika kwa dhahabu. 11Urefu wa mabawa ya hao makerubi ulikuwa jumla ya dhiraa ishirini. Bawa moja la kerubi wa kwanza lilikuwa na urefu wa dhiraa tano,3:11 Dhiraa 5 ni sawa na mita 2.25. nalo liligusa ukuta wa Hekalu, bawa lake lingine, lilikuwa pia na urefu wa dhiraa tano, ambalo liligusa bawa la kerubi lingine. 12Vivyo hivyo bawa moja la kerubi wa pili lilikuwa na urefu wa dhiraa tano na liligusa ukuta mwingine wa pili wa Hekalu na bawa lake lingine, lilikuwa pia na urefu wa dhiraa tano nalo liligusa bawa la kerubi wa kwanza. 13Mabawa ya makerubi hawa yalitanda dhiraa ishirini. Walisimama kwa miguu yao, nyuso zao zikielekea ukumbi mkubwa.

143:14 Kut 26:31-33; Ebr 9:3; Mwa 3:24; Mt 27:51Akatengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, zambarau na nyekundu, na za kitani safi, na kutarizi makerubi juu yake.

153:15 1Fal 7:15; Ufu 3:12; Yer 52:21Mbele ya Hekalu Solomoni akatengeneza nguzo mbili, ambazo kwa pamoja zilikuwa na dhiraa thelathini na tano kwenda juu kwake, na urefu wa kila moja ilikuwa na taji juu yake yenye dhiraa tano. 163:16 1Fal 7:17-22Akatengeneza minyororo iliyosokotwa, na kuiweka juu ya zile nguzo. Pia akatengeneza makomamanga 100, na kuyashikamanisha kwenye minyororo. 17Akazisimamisha hizo nguzo mbele ya Hekalu, moja upande wa kusini na nyingine upande wa kaskazini. Ile moja ya upande wa kusini akaiita Yakini,3:17 Yakini maana yake Atathibitisha. na ya upande wa kaskazini akaiita Boazi.3:17 Boazi maana yake Imo nguvu.

Swedish Contemporary Bible

2 Krönikeboken 3:1-17

Templet börjar byggas

(1 Kung 6:1-38)

1Så började Salomo bygga Herrens hus på Moria berg i Jerusalem, där Herren visat sig för hans far, kung David, på den plats som David gjort i ordning på jevusén Ornans tröskplats. 2Han började bygga på den andra dagen3:2 Dagen finns inte i grundtexten men kan antas. i andra månaden av sitt fjärde regeringsår.

3När Salomo byggde Guds hus, lade han grunden så att den blev 30 meter lång och 10 meter bred. 4Portalen, som låg framför templet, var 10 meter bred, liksom själva templet, och höjden var 10 meter3:4 Uppgiften om höjden är olika i olika handskrifter; enligt den masoretiska texten var den 120 alnar, alltså ca 60 meter. 20 alnar, här 10 meter, vilket är mer sannolikt, kommer från vissa Septuaginta- och syriska handskrifter.. Han belade insidan med rent guld.

5Det stora rummet klädde han med panel av cypressträ, som han klädde med rent guld och prydde med palmer och kedjor. 6Han smyckade huset ytterligare med dyrbara stenar. Guldet som han använde kom från Parvajim. 7Han belade templets väggar, bjälkar, dörrar och trösklar med guld och graverade keruber på väggarna.

8Han gjorde också det allra heligaste. Dess bredd motsvarade templets, och det var 10 meter långt och 10 meter brett. Han belade det med 21 ton3:8 Ordagrant: 600 talenter. En talent motsvarade ca 34 kilo (vikten har varierat genom tiderna). finaste guld. 9Guldet till spikarna vägde 600 gram. De övre rummen belade han också med guld. 10Inne i det allra heligaste gjorde Salomo två skulpturer, två keruber, belagda med guld. 11Den sammanlagda längden på kerubernas vingar var 10 meter. Den ena kerubens ena vinge, som var 2,5 meter lång, rörde vid tempelväggen, och dess andra vinge, också 2,5 meter, rörde vid den andra kerubens vinge. 12Den andra kerubens ena vinge, som också var 2,5 meter lång, rörde vid tempelväggen, och dess andra vinge, även den 2,5 meter, rörde vid den första kerubens vinge. 13Dessa kerubers vingar bredde alltså ut sig 10 meter. De stod på sina fötter med ansiktena mot det yttre rummet. 14Framför ingången till det allra heligaste gjorde han ett förhänge av blått, purpurrött, karminrött och vitt lingarn, som han smyckade med keruber.

15Därefter gjorde Salomo två pelare, sjutton och en halv meter höga, och varje kapitäl upptill var 2,5 meter högt. 16Han gjorde också kedjor till koret3:16 Det hebreiska uttryckets betydelse är osäker. och satte dem högst upp på pelarna med 100 granatäpplen fästa vid kedjorna. 17Han placerade pelarna framför templet, en till höger och en till vänster. Den till höger kallade han Jakin, och den till vänster Boas.