2 Nyakati 3 – NEN & KLB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Nyakati 3:1-17

Solomoni Ajenga Hekalu

(1 Wafalme 6:1-38; 7:15-22)

13:1 Mdo 7:47; Mwa 28:17; 2Sam 24:18; Yn 2:19-21; 1Fal 6:1; 1Nya 29:19; 1Kor 6:19; Mwa 22:2Ndipo Solomoni akaanza kujenga Hekalu la Bwana katika Yerusalemu juu ya Mlima Moria, pale ambapo Bwana alikuwa amemtokea Daudi baba yake. Ilikuwa katika kiwanja cha kupuria cha Arauna,3:1 Pia anaitwa Ornani kwa Kiebrania. Myebusi, mahali palipotolewa na Daudi. 23:2 Ezr 5:11Alianza kujenga siku ya pili ya mwezi wa pili katika mwaka wa nne wa utawala wake.

33:3 Eze 41:2; 1Fal 6:2-3Msingi aliouweka Solomoni kwa ajili ya kulijenga Hekalu la Mungu ulikuwa urefu wa dhiraa sitini3:3 Dhiraa 60 ni sawa na mita 27. na upana dhiraa ishirini.3:3 Dhiraa 20 ni sawa na mita 9. 43:4 1Fal 6:3Ukumbi wa mbele wa Hekalu ulikuwa na urefu wa dhiraa ishirini, yaani, kuanzia upande mmoja hadi upande mwingine wa upana wa nyumba hiyo na kimo chake dhiraa thelathini.3:4 Dhiraa 30 ni sawa na mita 13.5.

Akaufunika ndani kwa dhahabu safi. 53:5 Eze 40:16; 1Fal 6:17Akaufunika ukumbi mkuu kwa mbao za miberoshi na kufunikwa kwa dhahabu safi na kuupamba kwa miti ya mitende na kuifanyizia kwa minyororo. 6Alilipamba Hekalu kwa vito vya thamani. Hiyo dhahabu aliyotumia ilikuwa dhahabu ya Parvaimu. 73:7 1Fal 6:29-35; Eze 41:18Akazifunika boriti za dari, miimo na vizingiti vya milango, kuta na milango ya Hekalu kwa dhahabu, naye akatia nakshi ya makerubi kwenye kuta.

83:8 Kut 26:32-33Akajenga Patakatifu pa Patakatifu, urefu na upana wake ulikuwa dhiraa ishirini, sawasawa na upana wa Hekalu. Alifunika ndani kwa talanta 1203:8 Talanta 120 za dhahabu ni sawa na tani 23. za dhahabu safi. 9Misumari ya dhahabu ilikuwa na uzito wa shekeli hamsini.3:9 Shekeli 50 za dhahabu ni sawa na gramu 600. Alivifunika pia vyumba vya juu kwa dhahabu.

103:10 Kut 25:18; 1Fal 6:23Katika sehemu ya Patakatifu pa Patakatifu akafanyiza jozi moja ya makerubi ya kuchongwa na kuyafunika kwa dhahabu. 11Urefu wa mabawa ya hao makerubi ulikuwa jumla ya dhiraa ishirini. Bawa moja la kerubi wa kwanza lilikuwa na urefu wa dhiraa tano,3:11 Dhiraa 5 ni sawa na mita 2.25. nalo liligusa ukuta wa Hekalu, bawa lake lingine, lilikuwa pia na urefu wa dhiraa tano, ambalo liligusa bawa la kerubi lingine. 12Vivyo hivyo bawa moja la kerubi wa pili lilikuwa na urefu wa dhiraa tano na liligusa ukuta mwingine wa pili wa Hekalu na bawa lake lingine, lilikuwa pia na urefu wa dhiraa tano nalo liligusa bawa la kerubi wa kwanza. 13Mabawa ya makerubi hawa yalitanda dhiraa ishirini. Walisimama kwa miguu yao, nyuso zao zikielekea ukumbi mkubwa.

143:14 Kut 26:31-33; Ebr 9:3; Mwa 3:24; Mt 27:51Akatengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, zambarau na nyekundu, na za kitani safi, na kutarizi makerubi juu yake.

153:15 1Fal 7:15; Ufu 3:12; Yer 52:21Mbele ya Hekalu Solomoni akatengeneza nguzo mbili, ambazo kwa pamoja zilikuwa na dhiraa thelathini na tano kwenda juu kwake, na urefu wa kila moja ilikuwa na taji juu yake yenye dhiraa tano. 163:16 1Fal 7:17-22Akatengeneza minyororo iliyosokotwa, na kuiweka juu ya zile nguzo. Pia akatengeneza makomamanga 100, na kuyashikamanisha kwenye minyororo. 17Akazisimamisha hizo nguzo mbele ya Hekalu, moja upande wa kusini na nyingine upande wa kaskazini. Ile moja ya upande wa kusini akaiita Yakini,3:17 Yakini maana yake Atathibitisha. na ya upande wa kaskazini akaiita Boazi.3:17 Boazi maana yake Imo nguvu.

Korean Living Bible

역대하 3:1-17

솔로몬의 성전 건축

1마침내 성전 건축 공사가 시작되었다. 그 위치는 예루살렘의 모리아산이었다. 이 곳은 여호와께서 솔로몬의 아버지 다윗에게 나타났던 곳으로 여부스 사람 오르난의 타작 마당이었으나 다윗이 성전 부지로 선정한 곳이었다.

2성전 건축 공사가 시작된 날은 솔로몬왕 4년 2월 2일이었다.

3성전 지대는 3:3 히 ‘길 60규빗, 폭 20규빗’길이가 27미터, 폭이 9미터이며

4현관의 폭과 높이는 성전의 폭과 같이 각각 3:4 원문에는 ‘현관의높이 120규빗’ 54미터로되어있다.9미터였고 현관 내부는 순금으로 입혔다.

5성전 본당은 백향목으로 만들고 그 위에 순금을 입혔으며 거기에 종려나무와 사슬 모양의 형상을 새겼다.

6또 아름다운 보석을 벽에 박아 한층 돋보이게 하고 바르와임에서 수입해 온 금으로 성전을 화려하게 장식했는데

7성전 벽 전체와 들보와 문과 문지방을 금으로 입히고, 벽에는 그룹 천사를 아로새겼다.

8그리고 성전 안에 길이와 폭이 다 같이 9미터 되는 지성소를 만들고 순금 3:8 히 ‘600달란트’약 20톤으로 그 벽을 입혔고

9또 금 3:9 히 ‘50세겔’570그램으로 지성소에 쓸 못을 만들었으며 다락도 역시 금으로 입혔다.

10지성소 안에는 조각하여 만든 두 그룹 천사를 금으로 입혀 놓았으며

11-13그 두 그룹 천사는 정면을 향해 서로 나란히 서 있게 하였다. 이 그룹 천사들의 날개는 각각 두 개씩이며 각 날개의 길이는 약 2.3미터였다. 이 날개들은 지성소 중앙에서 한쪽 끝을 서로 맞대고 다른 한쪽 끝은 각각 성전 벽에 닿았는데 두 그룹 천사의 날개가 뻗어 있는 전체 길이는 9미터였다.

14그리고 지성소의 휘장은 청색, 자색, 홍색 실과 고운 베로 만들었으며 그 위에 그룹 천사를 수놓았다.

15성전 정면에는 높이 3:15 원문에는 ‘35규빗’ 곧 16미터로되어있다.8.1미터 되는 두 기둥을 세웠으며 이 기둥에는 약 2.3미터 되는 기둥머리를 씌웠고,

16또 그 기둥머리를 사슬로 장식하여 그 사슬에 놋으로 만든 석류 100개를 달았다.

17이 기둥은 성전 입구 양쪽에 세웠으며 오른쪽에 세운 것을 3:17 ‘하나님이세우신다’ 는뜻.‘야긴’ 이라 부르고 왼쪽에 세운 것을 3:17 ‘그의힘으로’ 라는뜻.‘보아스’ 라고 불렀다.