2 Nyakati 3 – NEN & JCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Nyakati 3:1-17

Solomoni Ajenga Hekalu

(1 Wafalme 6:1-38; 7:15-22)

13:1 Mdo 7:47; Mwa 28:17; 2Sam 24:18; Yn 2:19-21; 1Fal 6:1; 1Nya 29:19; 1Kor 6:19; Mwa 22:2Ndipo Solomoni akaanza kujenga Hekalu la Bwana katika Yerusalemu juu ya Mlima Moria, pale ambapo Bwana alikuwa amemtokea Daudi baba yake. Ilikuwa katika kiwanja cha kupuria cha Arauna,3:1 Pia anaitwa Ornani kwa Kiebrania. Myebusi, mahali palipotolewa na Daudi. 23:2 Ezr 5:11Alianza kujenga siku ya pili ya mwezi wa pili katika mwaka wa nne wa utawala wake.

33:3 Eze 41:2; 1Fal 6:2-3Msingi aliouweka Solomoni kwa ajili ya kulijenga Hekalu la Mungu ulikuwa urefu wa dhiraa sitini3:3 Dhiraa 60 ni sawa na mita 27. na upana dhiraa ishirini.3:3 Dhiraa 20 ni sawa na mita 9. 43:4 1Fal 6:3Ukumbi wa mbele wa Hekalu ulikuwa na urefu wa dhiraa ishirini, yaani, kuanzia upande mmoja hadi upande mwingine wa upana wa nyumba hiyo na kimo chake dhiraa thelathini.3:4 Dhiraa 30 ni sawa na mita 13.5.

Akaufunika ndani kwa dhahabu safi. 53:5 Eze 40:16; 1Fal 6:17Akaufunika ukumbi mkuu kwa mbao za miberoshi na kufunikwa kwa dhahabu safi na kuupamba kwa miti ya mitende na kuifanyizia kwa minyororo. 6Alilipamba Hekalu kwa vito vya thamani. Hiyo dhahabu aliyotumia ilikuwa dhahabu ya Parvaimu. 73:7 1Fal 6:29-35; Eze 41:18Akazifunika boriti za dari, miimo na vizingiti vya milango, kuta na milango ya Hekalu kwa dhahabu, naye akatia nakshi ya makerubi kwenye kuta.

83:8 Kut 26:32-33Akajenga Patakatifu pa Patakatifu, urefu na upana wake ulikuwa dhiraa ishirini, sawasawa na upana wa Hekalu. Alifunika ndani kwa talanta 1203:8 Talanta 120 za dhahabu ni sawa na tani 23. za dhahabu safi. 9Misumari ya dhahabu ilikuwa na uzito wa shekeli hamsini.3:9 Shekeli 50 za dhahabu ni sawa na gramu 600. Alivifunika pia vyumba vya juu kwa dhahabu.

103:10 Kut 25:18; 1Fal 6:23Katika sehemu ya Patakatifu pa Patakatifu akafanyiza jozi moja ya makerubi ya kuchongwa na kuyafunika kwa dhahabu. 11Urefu wa mabawa ya hao makerubi ulikuwa jumla ya dhiraa ishirini. Bawa moja la kerubi wa kwanza lilikuwa na urefu wa dhiraa tano,3:11 Dhiraa 5 ni sawa na mita 2.25. nalo liligusa ukuta wa Hekalu, bawa lake lingine, lilikuwa pia na urefu wa dhiraa tano, ambalo liligusa bawa la kerubi lingine. 12Vivyo hivyo bawa moja la kerubi wa pili lilikuwa na urefu wa dhiraa tano na liligusa ukuta mwingine wa pili wa Hekalu na bawa lake lingine, lilikuwa pia na urefu wa dhiraa tano nalo liligusa bawa la kerubi wa kwanza. 13Mabawa ya makerubi hawa yalitanda dhiraa ishirini. Walisimama kwa miguu yao, nyuso zao zikielekea ukumbi mkubwa.

143:14 Kut 26:31-33; Ebr 9:3; Mwa 3:24; Mt 27:51Akatengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, zambarau na nyekundu, na za kitani safi, na kutarizi makerubi juu yake.

153:15 1Fal 7:15; Ufu 3:12; Yer 52:21Mbele ya Hekalu Solomoni akatengeneza nguzo mbili, ambazo kwa pamoja zilikuwa na dhiraa thelathini na tano kwenda juu kwake, na urefu wa kila moja ilikuwa na taji juu yake yenye dhiraa tano. 163:16 1Fal 7:17-22Akatengeneza minyororo iliyosokotwa, na kuiweka juu ya zile nguzo. Pia akatengeneza makomamanga 100, na kuyashikamanisha kwenye minyororo. 17Akazisimamisha hizo nguzo mbele ya Hekalu, moja upande wa kusini na nyingine upande wa kaskazini. Ile moja ya upande wa kusini akaiita Yakini,3:17 Yakini maana yake Atathibitisha. na ya upande wa kaskazini akaiita Boazi.3:17 Boazi maana yake Imo nguvu.

Japanese Contemporary Bible

歴代誌Ⅱ 3:1-17

3

神殿の建設

1ついに神殿の建設が始まりました。敷地はエルサレムのモリヤ山上で、ここは、かつて主がソロモンの父ダビデに姿を現したエブス人オルナンの打ち場があった所です。ダビデはかねて、そこを神殿の建設予定地にしていました。 2工事が始まったのは、ソロモン王の治世第四年、第二の月の二日でした。

3まず神殿の土台は、長さ六十キュビト(約二・六メートル)、幅二十キュビト(八・八メートル)。 4屋根つきの玄関は、神殿の幅と同じ二十キュビトの長さで、内側の壁と天井には純金を張りつめました。屋根の高さは百二十キュビト(約五・三メートル)。 5神殿の主要部は糸杉で覆い、純金を張りつめ、なつめやしの木と鎖を彫刻しました。 6壁の内側はより美しさを増すために、宝石で飾りました。ここで用いた金はパルワイム産の最上のものです。 7神殿内は、壁も、梁も、扉も、敷居も金を張りつめ、壁にはケルビム(天使を象徴する像)を刻みました。

8神殿の奥に、二十キュビト四方の至聖所(神の箱を安置する部屋)がありました。ここにも、六百タラント(二十・四トン)の金を張りつめました。 9五十シェケル(五百七十五グラム)の金の釘を使い、階上の部屋も金を張りました。

10一番奥の至聖所に、王はケルビムを二つすえ、それにも金をかぶせました。 11-13この像は床の上に立ち、顔を部屋の外に向け、一方の壁からもう一方の壁まで翼をいっぱいに広げていました。 14王はまた、至聖所の入口に、ケルビムの縫い取り模様のある青と紅の亜麻布製の幕をかけました。

15神殿の前には、二本の柱を立てました。それぞれ高さは三十五キュビト(十五・四メートル)で、さらにその上に、高さ五キュビト(二・二メートル)の柱頭がありました。 16その頂に百個のざくろがついた鎖を取りつけました。 17それから、この柱を神殿正面の右と左に立て、右側の柱をヤキン、左側の柱をボアズと名づけました。