2 Nyakati 3 – NEN & BDS

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Nyakati 3:1-17

Solomoni Ajenga Hekalu

(1 Wafalme 6:1-38; 7:15-22)

13:1 Mdo 7:47; Mwa 28:17; 2Sam 24:18; Yn 2:19-21; 1Fal 6:1; 1Nya 29:19; 1Kor 6:19; Mwa 22:2Ndipo Solomoni akaanza kujenga Hekalu la Bwana katika Yerusalemu juu ya Mlima Moria, pale ambapo Bwana alikuwa amemtokea Daudi baba yake. Ilikuwa katika kiwanja cha kupuria cha Arauna,3:1 Pia anaitwa Ornani kwa Kiebrania. Myebusi, mahali palipotolewa na Daudi. 23:2 Ezr 5:11Alianza kujenga siku ya pili ya mwezi wa pili katika mwaka wa nne wa utawala wake.

33:3 Eze 41:2; 1Fal 6:2-3Msingi aliouweka Solomoni kwa ajili ya kulijenga Hekalu la Mungu ulikuwa urefu wa dhiraa sitini3:3 Dhiraa 60 ni sawa na mita 27. na upana dhiraa ishirini.3:3 Dhiraa 20 ni sawa na mita 9. 43:4 1Fal 6:3Ukumbi wa mbele wa Hekalu ulikuwa na urefu wa dhiraa ishirini, yaani, kuanzia upande mmoja hadi upande mwingine wa upana wa nyumba hiyo na kimo chake dhiraa thelathini.3:4 Dhiraa 30 ni sawa na mita 13.5.

Akaufunika ndani kwa dhahabu safi. 53:5 Eze 40:16; 1Fal 6:17Akaufunika ukumbi mkuu kwa mbao za miberoshi na kufunikwa kwa dhahabu safi na kuupamba kwa miti ya mitende na kuifanyizia kwa minyororo. 6Alilipamba Hekalu kwa vito vya thamani. Hiyo dhahabu aliyotumia ilikuwa dhahabu ya Parvaimu. 73:7 1Fal 6:29-35; Eze 41:18Akazifunika boriti za dari, miimo na vizingiti vya milango, kuta na milango ya Hekalu kwa dhahabu, naye akatia nakshi ya makerubi kwenye kuta.

83:8 Kut 26:32-33Akajenga Patakatifu pa Patakatifu, urefu na upana wake ulikuwa dhiraa ishirini, sawasawa na upana wa Hekalu. Alifunika ndani kwa talanta 1203:8 Talanta 120 za dhahabu ni sawa na tani 23. za dhahabu safi. 9Misumari ya dhahabu ilikuwa na uzito wa shekeli hamsini.3:9 Shekeli 50 za dhahabu ni sawa na gramu 600. Alivifunika pia vyumba vya juu kwa dhahabu.

103:10 Kut 25:18; 1Fal 6:23Katika sehemu ya Patakatifu pa Patakatifu akafanyiza jozi moja ya makerubi ya kuchongwa na kuyafunika kwa dhahabu. 11Urefu wa mabawa ya hao makerubi ulikuwa jumla ya dhiraa ishirini. Bawa moja la kerubi wa kwanza lilikuwa na urefu wa dhiraa tano,3:11 Dhiraa 5 ni sawa na mita 2.25. nalo liligusa ukuta wa Hekalu, bawa lake lingine, lilikuwa pia na urefu wa dhiraa tano, ambalo liligusa bawa la kerubi lingine. 12Vivyo hivyo bawa moja la kerubi wa pili lilikuwa na urefu wa dhiraa tano na liligusa ukuta mwingine wa pili wa Hekalu na bawa lake lingine, lilikuwa pia na urefu wa dhiraa tano nalo liligusa bawa la kerubi wa kwanza. 13Mabawa ya makerubi hawa yalitanda dhiraa ishirini. Walisimama kwa miguu yao, nyuso zao zikielekea ukumbi mkubwa.

143:14 Kut 26:31-33; Ebr 9:3; Mwa 3:24; Mt 27:51Akatengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, zambarau na nyekundu, na za kitani safi, na kutarizi makerubi juu yake.

153:15 1Fal 7:15; Ufu 3:12; Yer 52:21Mbele ya Hekalu Solomoni akatengeneza nguzo mbili, ambazo kwa pamoja zilikuwa na dhiraa thelathini na tano kwenda juu kwake, na urefu wa kila moja ilikuwa na taji juu yake yenye dhiraa tano. 163:16 1Fal 7:17-22Akatengeneza minyororo iliyosokotwa, na kuiweka juu ya zile nguzo. Pia akatengeneza makomamanga 100, na kuyashikamanisha kwenye minyororo. 17Akazisimamisha hizo nguzo mbele ya Hekalu, moja upande wa kusini na nyingine upande wa kaskazini. Ile moja ya upande wa kusini akaiita Yakini,3:17 Yakini maana yake Atathibitisha. na ya upande wa kaskazini akaiita Boazi.3:17 Boazi maana yake Imo nguvu.

La Bible du Semeur

2 Chroniques 3:1-17

La construction du bâtiment à l’emplacement prévu par David

(1 R 6.1-29)

1Salomon commença à bâtir le temple de l’Eternel à Jérusalem, sur la colline de Moriya3.1 Seul passage de l’Ancien Testament qui identifie la colline de Sion avec le mont Morija où Abraham s’est rendu pour sacrifier Isaac (Gn 22.2). Pour l’apparition de l’Eternel à David, voir 2 S 24.16-17 ; 1 Ch 21.15-16. où l’Eternel était apparu à son père David, et à l’emplacement que celui-ci avait prévu sur l’aire d’Ornân, le Yebousien3.1 Voir 1 Ch 21.15 à 22.1.. 2Salomon commença à bâtir le deuxième jour du deuxième mois3.2 L’année israélite commence en mars-avril. Le deuxième mois tombe donc en avril-mai. de la quatrième année de son règne. 3Les fondations du Temple avaient, selon l’ancienne unité de mesure, trente mètres de long et dix mètres de large. 4Le portique d’entrée avait dix mètres de large, comme le Temple, et dix mètres de haut3.4 Le texte hébreu indique 120 coudées (60 mètres de haut). Certains manuscrits des anciennes versions grecque et syriaque ont 20 coudées (10 mètres), rétablissant sans doute le chiffre primitif.. Salomon le fit recouvrir intérieurement d’or pur. 5La grande salle3.5 C’est-à-dire le lieu saint. fut lambrissée de bois de cyprès et plaquée d’or pur, et on y cisela des feuilles de palmier et des guirlandes. 6Pour décorer le Temple, on incrusta des pierres précieuses ; l’or était de l’or de Parvaïm. 7Tout le Temple fut plaqué d’or : la salle, les poutres, les seuils, les parois, et les battants des portes, puis Salomon fit sculpter des chérubins sur les parois.

Le lieu très saint

8A l’intérieur, il fit construire la salle du lieu très saint3.8 Voir Ex 26.33-34. ; elle avait dix mètres de long, sur la largeur du Temple, et dix mètres de large. Il utilisa vingt tonnes du meilleur or pour la recouvrir. 9Les clous, en or, pesaient six cents grammes. Il fit aussi couvrir d’or les plafonds.

10Pour la salle du lieu très saint, on sculpta deux chérubins et on les recouvrit d’or3.10 Pour les v. 10-13, voir Ex 25.18-20.. 11L’envergure totale de leurs ailes était de dix mètres. L’aile de l’un, longue de deux mètres cinquante, touchait le mur de la salle, l’autre aile de deux mètres cinquante touchait celle du second chérubin. 12Celui-ci étendait une aile de deux mètres cinquante jusqu’à l’autre paroi de la salle, et son autre aile de deux mètres cinquante touchait l’aile du premier chérubin. 13Ainsi, les ailes déployées de ces chérubins avaient bien une envergure totale de dix mètres. Les deux chérubins étaient debout sur leurs pieds et regardaient vers la salle.

14Salomon fit tisser le voile de fils violets, pourpres et carmins, et de lin, et il y fit broder des chérubins3.14 Voir Ex 26.31. Le voile, dans le Temple, était doublé d’une porte (4.22 ; 1 R 6.31)..

Les colonnes de bronze

(1 R 7.15-22)

15Devant le Temple, il fit édifier deux colonnes hautes de dix-sept mètres surmontées d’un chapiteau de deux mètres cinquante de haut. 16Le sommet de ces colonnes était décoré de guirlandes comme celles du sanctuaire. Cent grenades étaient suspendues à ces guirlandes. 17Il fit ériger les colonnes sur la façade du Temple de part et d’autre de l’entrée. Salomon appela celle de droite Yakîn (Il affermit) et celle de gauche Boaz (La force est en Lui).