2 Nyakati 29 – NEN & NTLR

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Nyakati 29:1-36

Hezekia Mfalme Wa Yuda

(2 Wafalme 18:1-12)

129:1 1Nya 3:13; 2Nya 26:5; 2Fal 18:1Hezekia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka ishirini na tisa. Mama yake aliitwa Abiya binti Zekaria. 229:2 2Nya 28:1; 34:2Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana kama Daudi baba yake alivyofanya.

329:3 2Fal 18:16; 2Nya 28:24; Mit 8:17Katika mwezi wa kwanza wa mwaka wa kwanza wa utawala wa alifungua milango ya Hekalu la Bwana, na kuikarabati. 4Akawaingiza makuhani na Walawi ndani na kuwakutanisha katika uwanja upande wa mashariki 529:5 Law 11:44; Neh 13:9; Efe 5:26-27; 1Nya 15:12; 2Nya 35:6; Eze 36:25; Mt 21:12-13; 1Kor 3:16-17; 2Kor 6:16na kusema: “Nisikilizeni mimi, enyi Walawi! Jitakaseni nafsi zenu sasa, mkaitakase na nyumba ya Bwana, Mungu wa baba zenu. Ondoeni uchafu wote kutoka mahali patakatifu. 629:6 Eze 23:35; Dan 9:5-6; 1Nya 5:25; Eze 8:16; Yer 2:27Baba zetu hawakuwa waaminifu, walifanya maovu machoni pa Bwana Mungu wetu na wakamwacha yeye. Wakageuza nyuso zao mbali na Maskani ya Bwana wakamgeuzia visogo vyao. 729:7 2Fal 16:17-18; 2Nya 28:24Pia walifunga milango ya ukumbi wa Hekalu na kuzima taa zake. Hawakufukiza uvumba wala kutoa sadaka yoyote ya kuteketezwa katika mahali patakatifu kwa Mungu wa Israeli. 829:8 Kum 28:25; 2Nya 24:18; Law 26:32; Eze 8:16; Yer 18:16; 1Fal 9:8; Yer 19:8; 29:18Kwa hiyo, hasira ya Bwana ikashuka juu ya Yuda na Yerusalemu, naye akawa amewafanya kitu cha kutisha, cha kushangaza na kitu cha kufanyia mzaha kama mnavyoona kwa macho yenu wenyewe. 929:9 2Nya 28:5-8, 17; Law 26:17Hii ndiyo sababu baba zetu wameanguka kwa upanga na ndiyo sababu wana wetu na binti zetu, pia wake zetu wamekuwa mateka. 1029:10 2Fal 11:17; 2Nya 15:12; Neh 9:38; Ezr 10:3; 2Nya 23:16Sasa ninadhamiria moyoni mwangu kuweka Agano na Bwana, Mungu wa Israeli, ili hasira yake kali igeuziwe mbali nasi. 1129:11 Hes 3:6; 8:6-14; 1Nya 15:2; 1Kor 6:9Wanangu, basi msipuuze jambo hili sasa, kwa kuwa Bwana amewachagua ninyi msimame mbele zake na kumtumikia, mkawe watumishi wake na mkamfukizie uvumba.”

1229:12 Hes 3:17-20; 2Nya 31:15Ndipo Walawi wafuatao wakaanza kazi:

Kutoka kwa Wakohathi,

Mahathi mwana wa Amasai na Yoeli mwana wa Azaria;

kutoka kwa Wamerari,

Kishi mwana wa Abdi na Azaria mwana wa Yahaleleli;

kutoka kwa Wagershoni,

Yoa mwana wa Zima na Edeni mwana wa Yoa;

1329:13 1Nya 6:36kutoka kwa wana wa Elisafani,

Shimri na Yeieli;

kutoka kwa wana wa Asafu,

Zekaria na Matania;

14kutoka kwa wana wa Hemani,

Yehieli na Shimei;

kutoka kwa wana wa Yeduthuni,

Shemaya na Uzieli.

1529:15 1Nya 23:28; Isa 1:25; 2Nya 30:12Walipomaliza kuwakusanya ndugu zao na kujiweka wakfu, wakaingia ndani ili kutakasa Hekalu la Bwana, kama vile mfalme alivyokuwa ameagiza, kwa kufuata neno la Bwana. 1629:16 2Sam 15:23Makuhani wakaingia patakatifu pa Hekalu la Bwana ili kupatakasa. Wakatoa nje penye ua wa Hekalu la Mungu kila kitu kichafu walichokikuta kwenye Hekalu la Bwana. Walawi wakavichukua na kuvipeleka nje katika Bonde la Kidroni. 1729:17 1Fal 6:3Walianza kazi ya utakaso siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza na kufikia siku ya nane ya mwezi huo wakawa wamefikia kwenye ukumbi wa Bwana. Kwa siku zingine nane wakalitakasa Hekalu lenyewe la Bwana wakakamilisha katika siku ya kumi na sita ya mwezi huo wa kwanza.

18Kisha wakaingia ndani kwa Mfalme Hezekia kutoa habari na kusema: “Tumelitakasa Hekalu lote la Bwana, madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa pamoja na vyombo vyake vyote, meza ya kupanga mikate iliyowekwa wakfu, pamoja na vyombo vyake vyote. 1929:19 2Nya 28:24Tumeviandaa na kuvitakasa vyombo vyote vile ambavyo Mfalme Ahazi, kwa kukosa uaminifu kwake, aliviondoa wakati alipokuwa mfalme. Sasa viko mbele ya madhabahu ya Bwana.”

Ibada Hekaluni Yarejeshwa

20Ndipo Mfalme Hezekia akainuka asubuhi na mapema, akakusanya pamoja maafisa wa mji wakakwea hekaluni mwa Bwana. 2129:21 Law 4:13-14Wakaleta mafahali saba, kondoo dume saba, wana-kondoo dume saba na mabeberu saba kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili ya ufalme, kwa ajili ya mahali patakatifu na kwa ajili ya Yuda. Mfalme akawaamuru makuhani, wazao wa Aroni, kuvitoa vitu hivyo sadaka katika madhabahu ya Bwana. 2229:22 Law 4:18; Hes 18:17; Ebr 9:21; Law 8:14-24Hivyo wakachinja wale mafahali, nao makuhani wakachukua ile damu na kuinyunyiza kwenye madhabahu, halafu wakawachinja wale kondoo dume saba na kunyunyiza hiyo damu yao kwenye madhabahu, kisha wakawachinja wale wana-kondoo dume na kunyunyiza damu yao kwenye madhabahu. 2329:23 Law 4:15, 24Wale mabeberu waliokuwa kwa ajili ya sadaka ya dhambi wakaletwa mbele ya mfalme na kusanyiko nao wakaweka mikono yao juu hao mabeberu. 2429:24 Kut 29:36; Law 4:20-26; Kol 1:20Ndipo makuhani wakawachinja hao mabeberu na kuweka damu yao kwenye madhabahu kwa ajili ya sadaka ya dhambi ili kufanya upatanisho kwa ajili ya Israeli yote, kwa sababu mfalme alikuwa ameamuru hiyo sadaka ya kuteketezwa na hiyo sadaka ya dhambi kwa ajili ya Israeli yote.

2529:25 1Nya 28:19; 2Nya 8:14; 1Sam 22:5; 2Sam 24:11; 1Nya 16:4; 23:6; 25:6; 2Nya 30:12Akawaweka Walawi kwenye Hekalu la Bwana wakiwa na matoazi, vinubi na zeze kama ilivyoagizwa na Daudi na Gadi mwonaji wa mfalme pamoja na nabii Nathani kwani hili lilikuwa limeamriwa na Bwana kupitia manabii wake. 2629:26 1Nya 15:16-24; 23:5; Hes 10:10; 2Nya 12:13; Amo 6:5; 1Nya 16:6Hivyo Walawi wakasimama tayari wakiwa na ala za uimbaji za Daudi na makuhani walikuwa na tarumbeta zao.

2729:27 1Sam 16:16; 2Nya 23:18; 20:21Hezekia akatoa amri ya kutoa sadaka ya kuteketezwa madhabahuni. Walipoanza kutoa sadaka, wakaanza pia kumwimbia Bwana pamoja na tarumbeta na zile ala za uimbaji za Daudi mfalme wa Israeli. 28Kusanyiko lote wakaabudu kwa kusujudu, wakati waimbaji wakiwa wanaimba na wenye tarumbeta wakipiga tarumbeta zao. Yote haya yaliendelea mpaka walipomaliza kutoa ile dhabihu ya sadaka ya kuteketezwa.

2929:29 2Nya 20:18; Rum 14:11Kutoa sadaka kulipomalizika, mfalme na kila mtu aliyekuwepo pamoja naye wakapiga magoti na kuabudu. 3029:30 Za 32:11; Flp 4:4Mfalme Hezekia na maafisa wake wakawaamuru Walawi kumsifu Bwana kwa maneno ya Daudi na ya Asafu mwonaji. Hivyo wakaimba sifa kwa furaha nao wakainamisha vichwa vyao na kuabudu.

3129:31 Ebr 13:15-16; Kut 35:22; 25:2; Law 7:12; 2Nya 13:9Kisha Hezekia akasema, “Sasa mmejiweka wakfu kwa Bwana. Njooni mlete dhabihu na sadaka za shukrani Hekaluni mwa Bwana.” Hivyo kusanyiko likaleta dhabihu na sadaka za shukrani, nao wote waliokuwa na mioyo ya hiari wakaleta sadaka za kuteketezwa.

32Idadi ya sadaka za kuteketezwa zilizoletwa na kusanyiko zilikuwa mafahali sabini, kondoo dume 100 na wana-kondoo dume 200. Wote hawa walikuwa kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa kwa Bwana. 33Wanyama waliowekwa wakfu kwa sadaka ya kuteketezwa walikuwa mafahali 600, pamoja na kondoo na mbuzi 3,000. 3429:34 2Nya 35:11; Hes 8:15; 2Nya 30:3; Eze 44:11; 1Nya 29:17; Za 7:10Lakini makuhani walikuwa wachache sana kuweza kuchuna wale wanyama wote wa sadaka za kuteketezwa, kwa hiyo ndugu zao Walawi wakawasaidia mpaka kazi ile ikakamilika na mpaka makuhani wengine walipowekwa wakfu, kwa kuwa Walawi walikuwa makini kujiweka wakfu kuliko walivyokuwa makuhani. 3529:35 Mwa 4:4; 35:14; Hes 15:5-10; Law 3:16; 7:11-21; Kut 29:13Kulikuwa na sadaka nyingi za kuteketezwa, pamoja na mafuta ya wanyama ya sadaka za amani na sadaka za kinywaji ambazo ziliambatana na sadaka za kuteketezwa.

Kwa hiyo huduma ya Hekalu la Bwana ikarudishwa kwa upya. 3629:36 Za 118:23; Mdo 2:41Hezekia pamoja na watu wote wakafurahi kwa sababu ya lile Mungu alilolifanya kwa ajili ya watu wake, kwa kuwa lilitendeka papo hapo.

Nouă Traducere În Limba Română

2 Cronici 29:1-36

Domnia lui Ezechia peste Iuda – purificarea Casei Domnului

(2 Regi 18:1-3)

1Ezechia a devenit rege la vârsta de douăzeci și cinci de ani și a domnit la Ierusalim timp de douăzeci și nouă de ani. Mama lui se numea Abia și era fiica lui Zaharia. 2El a făcut ce este drept în ochii Domnului, tot așa cum făcuse David, tatăl său.

3În cel dintâi an al domniei sale, în prima lună, el a deschis ușile Casei Domnului și le‑a reparat. 4I‑a adus pe preoți și pe leviți, i‑a strâns în Piața de Răsărit 5și le‑a zis:

„Leviților, ascultați‑mă! Sfințiți‑vă5 Vezi nota de la 7:7., sfințiți Casa Domnului, Dumnezeul părinților voștri, și scoateți necurăția din Lăcaș. 6Căci strămoșii noștri au fost necredincioși, au făcut ce este rău în ochii Domnului, Dumnezeul nostru, și L‑au părăsit. Ei și‑au întors fața de la Lăcașul Domnului, și‑au arătat ceafa. 7Mai mult, au închis porțile porticului, au stins candelele, nu au mai adus tămâie și nu au mai adus în Lăcaș arderi‑de‑tot Dumnezeului lui Israel. 8De aceea mânia Domnului este peste Iuda și peste Ierusalim și i‑a făcut o pricină de groază, de spaimă și de fluierat, așa cum vedeți cu ochii voștri. 9Iată, din cauza aceasta, părinții noștri au căzut loviți de sabie, iar fiii noștri, fiicele noastre și soțiile noastre sunt în captivitate. 10Acum, am pe inimă să încheiem un legământ cu Domnul, Dumnezeul lui Israel, pentru ca mânia Lui cea aprigă să se abată de la noi. 11Fiii mei, nu fiți nepăsători, căci pe voi v‑a ales Domnul ca să‑I stați înainte pentru slujire, să‑I slujiți și să‑I aduceți tămâie.“ 12Atunci s‑au ridicat următorii leviți:

dintre chehatiți –

Mahat, fiul lui Amasai, și Ioel, fiul lui Azaria;

dintre merariți –

Chiș, fiul lui Abdi, și Azaria, fiul lui Iehalel‑El;

dintre gherșoniți –

Ioah, fiul lui Zima, și Eden, fiul Ioah;

13dintre urmașii lui Elițafan –

Șimri și Ieiel;

dintre urmașii lui Asaf –

Zaharia și Matania;

14dintre urmașii lui Heman –

Iehiel și Șimei,

iar dintre urmașii lui Iedutun –

Șemaia și Uziel.

15Aceștia și‑au adunat frații, s‑au sfințit și au venit pentru a curăți Casa Domnului, după porunca regelui, potrivit cuvintelor Domnului. 16Preoții au intrat înăuntrul Casei Domnului ca s‑o curățească și au scos afară, în curtea Templului16 Vezi nota de la 3:17. Domnului, toate necurățiile pe care le‑au găsit în Casa Domnului. Leviții le‑au luat și le‑au dus afară, lângă uedul16 Vezi nota de la 15:16. Chidron. 17Au început să‑l sfințească în prima zi a lunii întâi. În a opta zi a lunii au intrat în porticul Domnului. Au sfințit apoi Casa Domnului timp de opt zile, și au încheiat în a șaisprezecea zi a lunii întâi.

18Ei s‑au dus înăuntru la regele Ezechia și au zis: „Am curățit Casa Domnului în întregime, altarul arderilor‑de‑tot și toate uneltele lui, masa pentru pâinea prezentării și toate obiectele ei, 19precum și toate obiectele care au fost spurcate de regele Ahaz în timpul domniei lui, din cauza necredincioșiei lui. Le‑am pregătit, le‑am sfințit și iată că acum sunt în fața altarului Domnului.“

20Regele Ezechia s‑a sculat dis‑de‑dimineață, a adunat conducătorii cetății și s‑au suit la Casa Domnului. 21Au luat cu ei șapte tauri, șapte berbeci, șapte miei și șapte țapi ca să‑i aducă drept jertfă pentru păcat, pentru regat, pentru Sfântul Lăcaș și pentru Iuda. Regele le‑a zis urmașilor lui Aaron, preoții, să aducă arderile‑de‑tot pe altarul Domnului. 22Au înjunghiat vitele, iar preoții au luat sângele și au stropit altarul; apoi au înjunghiat berbecii și au stropit cu sânge altarul, după care au înjunghiat mieii și au stropit cu sânge altarul. 23Apoi au luat țapii pentru jertfa pentru păcat și i‑au adus înaintea regelui și a adunării. Aceștia și‑au pus mâinile peste ei, 24iar preoții au înjunghiat țapii și au făcut ispășire cu sângele acestora pentru tot Israelul, căci regele poruncise ca arderea‑de‑tot și jertfa pentru păcat să fie aduse pentru tot Israelul.

25El îi pusese pe leviți să stea în Casa Domnului cu chimvale, cu harfe și cu lire, așa cum porunciseră David, Gad, văzătorul regelui, și profetul Natan, căci porunca fusese dată de Domnul prin profeții Săi. 26Deci leviții stăteau acolo cu instrumentele lui David, iar preoții cu trâmbițele.

27Când Ezechia a poruncit să aducă arderea‑de‑tot pe altar, chiar în clipa în care a început arderea‑de‑tot, a început și cântarea Domnului în sunetul trâmbițelor și al instrumentelor lui David, regele lui Israel. 28Toată adunarea s‑a închinat; cântăreții au cântat cântarea și au sunat trâmbițele până s‑a terminat arderea‑de‑tot.

29Când s‑a terminat arderea‑de‑tot, regele împreună cu toți cei prezenți au îngenuncheat și s‑au închinat. 30Regele Ezechia și conducătorii i‑au îndemnat pe leviți să‑L laude pe Domnul prin cuvintele lui David și ale văzătorului Asaf. Ei L‑au lăudat cu bucurie, s‑au plecat și s‑au închinat. 31Văzând acestea, Ezechia a zis: „Acum că v‑ați dedicat Domnului, apropiați‑vă și aduceți jertfe și daruri de mulțumire la Casa Domnului!“

Astfel, adunarea a adus jertfe și daruri de mulțumire, iar toți aceia care aveau o inimă generoasă au adus arderi‑de‑tot. 32Numărul arderilor‑de‑tot aduse de către adunare a fost de șaptezeci de viței, o sută de berbeci și două sute de miei. Toate aceste vite au fost aduse Domnului ca ardere‑de‑tot. 33Au închinat33 Lit.: au sfințit. Verbul poate avea sensul de a pune pe cineva/ceva într‑o stare specială (fizic sau spiritual), a consacra, a pune deoparte pentru Dumnezeu (uneori printr‑un ritual de ungere cu ulei sau sânge, spălare și/sau rugăciune ori declarație publică). Domnului șase sute de boi și trei mii de oi. 34Preoții au fost însă prea puțini, astfel încât nu au putut să jupuiască toate arderile‑de‑tot. Prin urmare, frații lor, leviții, i‑au ajutat până au terminat slujba și până ce s‑au sfințit și ceilalți preoți, căci leviții se sfințiseră cu mai multă râvnă. 35Au fost multe arderi‑de‑tot, în afară de grăsimea jertfelor de pace35 Vezi nota de la 7:7. și de jertfele de băutură care însoțeau arderea‑de‑tot.

Și astfel a fost restabilită slujba la Casa Domnului. 36Ezechia și tot poporul s‑au bucurat pentru că Dumnezeu a purtat de grijă poporului, căci aceasta s‑a întâmplat pe neașteptate.