2 Nyakati 29 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Nyakati 29:1-36

Hezekia Mfalme Wa Yuda

(2 Wafalme 18:1-12)

129:1 1Nya 3:13; 2Nya 26:5; 2Fal 18:1Hezekia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka ishirini na tisa. Mama yake aliitwa Abiya binti Zekaria. 229:2 2Nya 28:1; 34:2Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana kama Daudi baba yake alivyofanya.

329:3 2Fal 18:16; 2Nya 28:24; Mit 8:17Katika mwezi wa kwanza wa mwaka wa kwanza wa utawala wa alifungua milango ya Hekalu la Bwana, na kuikarabati. 4Akawaingiza makuhani na Walawi ndani na kuwakutanisha katika uwanja upande wa mashariki 529:5 Law 11:44; Neh 13:9; Efe 5:26-27; 1Nya 15:12; 2Nya 35:6; Eze 36:25; Mt 21:12-13; 1Kor 3:16-17; 2Kor 6:16na kusema: “Nisikilizeni mimi, enyi Walawi! Jitakaseni nafsi zenu sasa, mkaitakase na nyumba ya Bwana, Mungu wa baba zenu. Ondoeni uchafu wote kutoka mahali patakatifu. 629:6 Eze 23:35; Dan 9:5-6; 1Nya 5:25; Eze 8:16; Yer 2:27Baba zetu hawakuwa waaminifu, walifanya maovu machoni pa Bwana Mungu wetu na wakamwacha yeye. Wakageuza nyuso zao mbali na Maskani ya Bwana wakamgeuzia visogo vyao. 729:7 2Fal 16:17-18; 2Nya 28:24Pia walifunga milango ya ukumbi wa Hekalu na kuzima taa zake. Hawakufukiza uvumba wala kutoa sadaka yoyote ya kuteketezwa katika mahali patakatifu kwa Mungu wa Israeli. 829:8 Kum 28:25; 2Nya 24:18; Law 26:32; Eze 8:16; Yer 18:16; 1Fal 9:8; Yer 19:8; 29:18Kwa hiyo, hasira ya Bwana ikashuka juu ya Yuda na Yerusalemu, naye akawa amewafanya kitu cha kutisha, cha kushangaza na kitu cha kufanyia mzaha kama mnavyoona kwa macho yenu wenyewe. 929:9 2Nya 28:5-8, 17; Law 26:17Hii ndiyo sababu baba zetu wameanguka kwa upanga na ndiyo sababu wana wetu na binti zetu, pia wake zetu wamekuwa mateka. 1029:10 2Fal 11:17; 2Nya 15:12; Neh 9:38; Ezr 10:3; 2Nya 23:16Sasa ninadhamiria moyoni mwangu kuweka Agano na Bwana, Mungu wa Israeli, ili hasira yake kali igeuziwe mbali nasi. 1129:11 Hes 3:6; 8:6-14; 1Nya 15:2; 1Kor 6:9Wanangu, basi msipuuze jambo hili sasa, kwa kuwa Bwana amewachagua ninyi msimame mbele zake na kumtumikia, mkawe watumishi wake na mkamfukizie uvumba.”

1229:12 Hes 3:17-20; 2Nya 31:15Ndipo Walawi wafuatao wakaanza kazi:

Kutoka kwa Wakohathi,

Mahathi mwana wa Amasai na Yoeli mwana wa Azaria;

kutoka kwa Wamerari,

Kishi mwana wa Abdi na Azaria mwana wa Yahaleleli;

kutoka kwa Wagershoni,

Yoa mwana wa Zima na Edeni mwana wa Yoa;

1329:13 1Nya 6:36kutoka kwa wana wa Elisafani,

Shimri na Yeieli;

kutoka kwa wana wa Asafu,

Zekaria na Matania;

14kutoka kwa wana wa Hemani,

Yehieli na Shimei;

kutoka kwa wana wa Yeduthuni,

Shemaya na Uzieli.

1529:15 1Nya 23:28; Isa 1:25; 2Nya 30:12Walipomaliza kuwakusanya ndugu zao na kujiweka wakfu, wakaingia ndani ili kutakasa Hekalu la Bwana, kama vile mfalme alivyokuwa ameagiza, kwa kufuata neno la Bwana. 1629:16 2Sam 15:23Makuhani wakaingia patakatifu pa Hekalu la Bwana ili kupatakasa. Wakatoa nje penye ua wa Hekalu la Mungu kila kitu kichafu walichokikuta kwenye Hekalu la Bwana. Walawi wakavichukua na kuvipeleka nje katika Bonde la Kidroni. 1729:17 1Fal 6:3Walianza kazi ya utakaso siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza na kufikia siku ya nane ya mwezi huo wakawa wamefikia kwenye ukumbi wa Bwana. Kwa siku zingine nane wakalitakasa Hekalu lenyewe la Bwana wakakamilisha katika siku ya kumi na sita ya mwezi huo wa kwanza.

18Kisha wakaingia ndani kwa Mfalme Hezekia kutoa habari na kusema: “Tumelitakasa Hekalu lote la Bwana, madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa pamoja na vyombo vyake vyote, meza ya kupanga mikate iliyowekwa wakfu, pamoja na vyombo vyake vyote. 1929:19 2Nya 28:24Tumeviandaa na kuvitakasa vyombo vyote vile ambavyo Mfalme Ahazi, kwa kukosa uaminifu kwake, aliviondoa wakati alipokuwa mfalme. Sasa viko mbele ya madhabahu ya Bwana.”

Ibada Hekaluni Yarejeshwa

20Ndipo Mfalme Hezekia akainuka asubuhi na mapema, akakusanya pamoja maafisa wa mji wakakwea hekaluni mwa Bwana. 2129:21 Law 4:13-14Wakaleta mafahali saba, kondoo dume saba, wana-kondoo dume saba na mabeberu saba kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili ya ufalme, kwa ajili ya mahali patakatifu na kwa ajili ya Yuda. Mfalme akawaamuru makuhani, wazao wa Aroni, kuvitoa vitu hivyo sadaka katika madhabahu ya Bwana. 2229:22 Law 4:18; Hes 18:17; Ebr 9:21; Law 8:14-24Hivyo wakachinja wale mafahali, nao makuhani wakachukua ile damu na kuinyunyiza kwenye madhabahu, halafu wakawachinja wale kondoo dume saba na kunyunyiza hiyo damu yao kwenye madhabahu, kisha wakawachinja wale wana-kondoo dume na kunyunyiza damu yao kwenye madhabahu. 2329:23 Law 4:15, 24Wale mabeberu waliokuwa kwa ajili ya sadaka ya dhambi wakaletwa mbele ya mfalme na kusanyiko nao wakaweka mikono yao juu hao mabeberu. 2429:24 Kut 29:36; Law 4:20-26; Kol 1:20Ndipo makuhani wakawachinja hao mabeberu na kuweka damu yao kwenye madhabahu kwa ajili ya sadaka ya dhambi ili kufanya upatanisho kwa ajili ya Israeli yote, kwa sababu mfalme alikuwa ameamuru hiyo sadaka ya kuteketezwa na hiyo sadaka ya dhambi kwa ajili ya Israeli yote.

2529:25 1Nya 28:19; 2Nya 8:14; 1Sam 22:5; 2Sam 24:11; 1Nya 16:4; 23:6; 25:6; 2Nya 30:12Akawaweka Walawi kwenye Hekalu la Bwana wakiwa na matoazi, vinubi na zeze kama ilivyoagizwa na Daudi na Gadi mwonaji wa mfalme pamoja na nabii Nathani kwani hili lilikuwa limeamriwa na Bwana kupitia manabii wake. 2629:26 1Nya 15:16-24; 23:5; Hes 10:10; 2Nya 12:13; Amo 6:5; 1Nya 16:6Hivyo Walawi wakasimama tayari wakiwa na ala za uimbaji za Daudi na makuhani walikuwa na tarumbeta zao.

2729:27 1Sam 16:16; 2Nya 23:18; 20:21Hezekia akatoa amri ya kutoa sadaka ya kuteketezwa madhabahuni. Walipoanza kutoa sadaka, wakaanza pia kumwimbia Bwana pamoja na tarumbeta na zile ala za uimbaji za Daudi mfalme wa Israeli. 28Kusanyiko lote wakaabudu kwa kusujudu, wakati waimbaji wakiwa wanaimba na wenye tarumbeta wakipiga tarumbeta zao. Yote haya yaliendelea mpaka walipomaliza kutoa ile dhabihu ya sadaka ya kuteketezwa.

2929:29 2Nya 20:18; Rum 14:11Kutoa sadaka kulipomalizika, mfalme na kila mtu aliyekuwepo pamoja naye wakapiga magoti na kuabudu. 3029:30 Za 32:11; Flp 4:4Mfalme Hezekia na maafisa wake wakawaamuru Walawi kumsifu Bwana kwa maneno ya Daudi na ya Asafu mwonaji. Hivyo wakaimba sifa kwa furaha nao wakainamisha vichwa vyao na kuabudu.

3129:31 Ebr 13:15-16; Kut 35:22; 25:2; Law 7:12; 2Nya 13:9Kisha Hezekia akasema, “Sasa mmejiweka wakfu kwa Bwana. Njooni mlete dhabihu na sadaka za shukrani Hekaluni mwa Bwana.” Hivyo kusanyiko likaleta dhabihu na sadaka za shukrani, nao wote waliokuwa na mioyo ya hiari wakaleta sadaka za kuteketezwa.

32Idadi ya sadaka za kuteketezwa zilizoletwa na kusanyiko zilikuwa mafahali sabini, kondoo dume 100 na wana-kondoo dume 200. Wote hawa walikuwa kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa kwa Bwana. 33Wanyama waliowekwa wakfu kwa sadaka ya kuteketezwa walikuwa mafahali 600, pamoja na kondoo na mbuzi 3,000. 3429:34 2Nya 35:11; Hes 8:15; 2Nya 30:3; Eze 44:11; 1Nya 29:17; Za 7:10Lakini makuhani walikuwa wachache sana kuweza kuchuna wale wanyama wote wa sadaka za kuteketezwa, kwa hiyo ndugu zao Walawi wakawasaidia mpaka kazi ile ikakamilika na mpaka makuhani wengine walipowekwa wakfu, kwa kuwa Walawi walikuwa makini kujiweka wakfu kuliko walivyokuwa makuhani. 3529:35 Mwa 4:4; 35:14; Hes 15:5-10; Law 3:16; 7:11-21; Kut 29:13Kulikuwa na sadaka nyingi za kuteketezwa, pamoja na mafuta ya wanyama ya sadaka za amani na sadaka za kinywaji ambazo ziliambatana na sadaka za kuteketezwa.

Kwa hiyo huduma ya Hekalu la Bwana ikarudishwa kwa upya. 3629:36 Za 118:23; Mdo 2:41Hezekia pamoja na watu wote wakafurahi kwa sababu ya lile Mungu alilolifanya kwa ajili ya watu wake, kwa kuwa lilitendeka papo hapo.

New International Reader’s Version

2 Chronicles 29:1-36

Hezekiah Purifies the Temple

1Hezekiah was 25 years old when he became king. He ruled in Jerusalem for 29 years. His mother’s name was Abijah. She was the daughter of Zechariah. 2Hezekiah did what was right in the eyes of the Lord, just as King David had done.

3In the first month of Hezekiah’s first year as king, he opened the doors of the Lord’s temple. He repaired them. 4He brought the priests and Levites in. He gathered them together in the open area on the east side of the temple. 5He said, “Levites, listen to me! Set yourselves apart to the Lord. Set apart the temple of the Lord. He’s the God of your people who lived long ago. Remove anything ‘unclean’ from the temple. 6Our people weren’t faithful. They did what was evil in the eyes of the Lord our God. They deserted him. They turned their faces away from the place where he lives. They turned their backs on him. 7They also shut the doors of the temple porch. They put the lamps out. They didn’t burn incense at the temple. They didn’t sacrifice burnt offerings there to the God of Israel. 8So the Lord has become angry with Judah and Jerusalem. He has made them look so bad that everyone is shocked when they see them. They laugh at them. You can see it with your own eyes. 9That’s why our fathers have been killed by swords. That’s why our sons and daughters and wives have become prisoners. 10So I’m planning to make a covenant with the Lord, the God of Israel. Then he’ll stop being angry with us. 11My sons, don’t fail to obey the Lord. He has chosen you to stand in front of him and work for him. He wants you to serve him and burn incense to him.”

12Here are the Levites who went to work.

Mahath and Joel were from the family line of Kohath.

Mahath was the son of Amasai. Joel was the son of Azariah.

Kish and Azariah were from the family line of Merari.

Kish was the son of Abdi. Azariah was the son of Jehallelel.

Joah and Eden were from the family line of Gershon.

Joah was the son of Zimmah. Eden was the son of Joah.

13Shimri and Jeiel were from the family line of Elizaphan.

Zechariah and Mattaniah were from the family line of Asaph.

14Jehiel and Shimei were from the family line of Heman.

Shemaiah and Uzziel were from the family line of Jeduthun.

15All these Levites gathered the other Levites together. They set themselves apart to the Lord. Then they went in to purify the Lord’s temple. That’s what the king had ordered them to do. They did what the Lord told them to. 16The priests went into the Lord’s temple to make it pure. They brought out to the temple courtyard everything that was “unclean.” They had found “unclean” things in the Lord’s temple. The Levites took them and carried them out to the Kidron Valley. 17On the first day of the first month they began to set everything in the temple apart to the Lord. By the eighth day of the month they reached the Lord’s porch. For eight more days they set the Lord’s temple itself apart to him. They finished on the 16th day of the first month.

18Then they went to King Hezekiah. They reported, “We’ve purified the whole temple of the Lord. That includes the altar for burnt offerings and all its tools. It also includes the table for the holy bread and all its objects. 19We’ve prepared all the things King Ahaz had removed. We’ve set them apart to the Lord. Ahaz had removed them while he was king. He wasn’t faithful to the Lord. Those things are now in front of the Lord’s altar.”

20Early the next morning King Hezekiah gathered together the city officials. They all went up to the Lord’s temple. 21They brought seven bulls, seven rams, seven male lambs and seven male goats with them. They sacrificed the animals as a sin offering for the kingdom, for the temple and for Judah. The king commanded the priests to offer them on the Lord’s altar. The priests were from the family line of Aaron. 22They killed the bulls. Then they splashed the blood against the altar. Next they killed the rams and splashed the blood against the altar. Then they killed the lambs and splashed the blood against the altar. 23The goats for the sin offering were brought to the king and the whole community. They placed their hands on them. 24Then the priests killed the goats. They put the blood on the altar as a sin offering. It paid for the sin of the whole nation of Israel. The king had ordered the burnt offering and the sin offering for the whole nation.

25Hezekiah stationed the Levites in the Lord’s temple. They had cymbals, harps and lyres. They did everything in the way King David, his prophet Gad, and Nathan the prophet had required. The Lord had given commands about all these things through his prophets. 26So the Levites stood ready with David’s musical instruments. And the priests had their trumpets ready.

27Hezekiah gave the order to sacrifice the burnt offering on the altar. The offering began. Singing to the Lord also began. The singing was accompanied by the trumpets and by the instruments of David. He had been king of Israel. 28The whole community bowed down. They worshiped the Lord. At the same time the musicians played their musical instruments. The priests blew their trumpets. All of that continued until the burnt offering had been sacrificed.

29So the offerings were finished. King Hezekiah got down on his knees. He worshiped the Lord. So did everyone who was with him. 30The king and his officials ordered the Levites to praise the Lord. They used the words of David and Asaph the prophet. They sang praises with joy. They bowed down and worshiped the Lord.

31Then Hezekiah said, “You have set yourselves apart to the Lord. Come and bring sacrifices and thank offerings to his temple.” So the whole community brought sacrifices and thank offerings. Everyone who wanted to brought burnt offerings.

32The whole community brought 70 bulls, 100 rams and 200 male lambs. They brought all of them as burnt offerings to the Lord. 33The total number of animals set apart as sacrifices to the Lord was 600 bulls and 3,000 sheep and goats. 34But there weren’t enough priests to skin all the burnt offerings. So their relatives, the Levites, helped them. They worked until the task was finished. By that time other priests had been set apart to the Lord. The Levites had been more careful than the priests when they set themselves apart. 35There were large numbers of burnt offerings, along with the drink offerings and the fat from the friendship offerings. They were offered along with the burnt offerings.

So the service of the Lord’s temple was started up again. 36Hezekiah and all the people were filled with joy. That’s because everything had been done so quickly. God had provided for his people in a wonderful way.