2 Nyakati 22 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Nyakati 22:1-12

Ahazia Mfalme Wa Yuda

(2 Wafalme 8:25-29; 9:21-28)

122:1 2Nya 33:25; 23:20-21; 21:16-17; 26:1; 1Fal 8:24Watu wa Yerusalemu wakamfanya Ahazia, mdogo wa wote wa wana wa Yerohamu, kuwa mfalme mahali pa baba yake, kwa sababu washambuliaji wa ghafula waliokuwa wameingia kambini pamoja na Waarabu, walikuwa wamewaua wana wakubwa wote wa Yehoramu. Kwa hiyo Ahazia mwana wa Yehoramu mfalme wa Yuda akaanza kutawala.

222:2 1Fal 16:28; 2Fal 8:26; 2Nya 21:6Ahazia alikuwa na umri wa miaka ishirini na miwili alipoanza kutawala, naye akatawala katika Yerusalemu kwa mwaka mmoja. Mama yake aliitwa Athalia, mjukuu wa Omri.

322:3 2Nya 18:1; 21:6Ahazia naye akaenenda katika njia za nyumba ya Ahabu, kwa sababu mama yake alimshawishi katika kutenda maovu. 422:4 2Nya 24:17; Mit 1:10; 19:27Akafanya yaliyo maovu machoni pa Bwana kama walivyokuwa wamefanya nyumba ya Ahabu, kwa kuwa baada ya kufa kwa baba yake nyumba ya Ahabu ndio waliokuwa washauri wake, kwa uangamivu wake. 522:5 2Nya 18:11, 34; 2Fal 8:28Pia akafuata shauri lao alipokwenda pamoja na Yoramu mwana wa Ahabu mfalme wa Israeli kupigana na Hazaeli mfalme wa Aramu huko Ramoth-Gileadi. Waaramu wakamjeruhi Yoramu. 622:6 1Fal 19:15; 2Fal 9:15Hivyo akarudi Yezreeli ili apate kuuguza majeraha aliyojeruhiwa huko Ramothi22:6 Yaani Rama kwa Kiebrania. alipopigana na Hazaeli mfalme wa Aramu.

Ndipo Ahazia mwana wa Yehoramu, mfalme wa Yuda, akashuka kwenda Yezreeli kumtazama Yoramu mwana wa Ahabu, kwa sababu alikuwa amejeruhiwa.

722:7 Amu 14:4; 2Nya 10:15; Amo 3:6; Mdo 2:23; 2Fal 9:16; 1Fal 12:15; Za 5:10; 9:16; 1Fal 19:16Mungu alikuwa ameamuru kwamba kuanguka kwa Ahazia kungetokea atakapokwenda kumwona Yoramu. Ahazia alipowasili, wakatoka pamoja na Yoramu ili kwenda kukutana na Yehu mwana wa Nimshi, ambaye Bwana alikuwa amemtia mafuta kuangamiza nyumba ya Ahabu. 822:8 2Fal 10:13Yehu alipokuwa anatekeleza hukumu juu ya nyumba ya Ahabu, akawakuta wakuu wa Yuda na wana wa jamaa ya Ahazia waliokuwa wanamhudumia Ahazia, naye akawaua. 922:9 Amu 9:5; 2Nya 17:4; 2Fal 9:27Ndipo akaenda kumsaka Ahazia, nao watu wake wakamkamata alipokuwa amejificha huko Samaria. Akaletwa kwa Yehu, naye Yehu akamuua. Wakamzika kwani walisema, “Alikuwa mwana wa Yehoshafati, ambaye alimtafuta Bwana kwa moyo wake wote.” Hivyo hapakuwa na mtu mwenye uwezo katika nyumba ya Ahazia aliyeweza kushika ufalme.

Athalia Na Yoashi

(2 Wafalme 11:1-3)

10Wakati Athalia mamaye Ahazia alipoona kuwa mwanawe amekufa, akainuka na kuiangamiza jamaa yote ya mfalme ya nyumba ya Yuda. 1122:11 2Fal 11:2Lakini Yehosheba, binti wa Mfalme Yehoramu, akamtwaa Yoashi mwana wa Ahazia kwa siri kutoka miongoni mwa wana wa mfalme waliokuwa karibu kuuawa. Akamweka Yoashi pamoja na yaya wake ndani ya chumba cha kulala. Kwa kuwa Yehosheba, aliyekuwa binti wa Mfalme Yehoramu, na pia alikuwa mke wa kuhani Yehoyada, alikuwa dada yake Ahazia, akamficha huyo mtoto ili Athalia asimuue. 12Alibaki amefichwa pamoja nao katika Hekalu la Mungu kwa muda wa miaka sita wakati Athalia alikuwa akitawala nchi.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

歷代志下 22:1-12

猶大王亞哈謝

1耶路撒冷的居民擁立約蘭的小兒子亞哈謝22·1 亞哈謝」即21·17提到的「亞哈斯」。為王。因為約蘭的其他兒子都被那些與阿拉伯人同來攻營的匪徒殺了,於是猶大約蘭的兒子亞哈謝做了王。 2亞哈謝二十二歲22·2 參考七十士譯本、敘利亞譯本和列王紀下8·26。希伯來文是「四十二歲」。登基,在耶路撒冷執政一年。他母親叫亞她利雅,是暗利的孫女。 3他重蹈亞哈家的覆轍,因為他的母親唆使他作惡。 4他像亞哈家一樣做耶和華視為惡的事,因為他父親死後,亞哈家便唆使他作惡,使他走向滅亡。 5他照亞哈家的主意,與以色列亞哈的兒子約蘭一起去基列拉末征討亞蘭哈薛亞蘭人擊傷約蘭6約蘭便回到耶斯列療傷。猶大亞哈謝22·6 亞哈謝」希伯來文是「亞撒利雅」。前去探望他。

7亞哈謝去見約蘭,遇害身亡,這事出於上帝。原來他到那裡後便與約蘭去攻擊寧示的孫子耶戶耶戶是耶和華膏立去毀滅亞哈家的人。 8耶戶討伐亞哈家的時候,遇見猶大眾首領和亞哈謝的眾侄兒,他們都是服侍亞哈謝的,耶戶就把他們全部殺掉。 9然後耶戶搜捕亞哈謝,民眾找到躲在撒瑪利亞亞哈謝,把他押到耶戶那裡殺了。他們念他是全心尋求耶和華的約沙法的孫子,就把他埋葬了。這樣,亞哈謝家無人能保住王位。

亞她利雅篡權

10亞哈謝的母親亞她利雅見她兒子死了,便決定除掉猶大王室的後裔。 11約蘭王的女兒、亞哈謝的妹妹約示芭亞哈謝的兒子約阿施從將要被殺的王子中偷出來,將他和他的乳母藏在一間臥室裡躲避亞她利雅的殺害。約示芭耶何耶大祭司的妻子。 12約阿施和他們在上帝的殿裡藏了六年。那時亞她利雅篡位當政。