2 Nyakati 15 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Nyakati 15:1-19

Asa Afanya Matengenezo

115:1 Hes 24:4; Amu 3:10; 2Nya 24:20; 2Sam 23:2; 2Nya 20:14; 2Pet 1:21Roho wa Bwana akamjia Azaria mwana wa Odedi. 215:2 Yak 4:8; 2Nya 20:17; Kum 31:17; 1Nya 28:9; Ebr 12:25; 2Nya 33:12-13; Yer 29:13; Mt 7:7; 2Nya 12:1-3; Rum 11:1-2Akatoka ili kumlaki Asa na kumwambia, “Nisikilizeni, Asa na Yuda wote na Benyamini. Bwana yu pamoja nanyi mkiwa pamoja naye. Kama mkimtafuta, ataonekana kwenu, lakini kama mkimwacha yeye, naye atawaacha ninyi. 315:3 Law 10:11; Mao 2:9; Amo 8:11; Hos 3:4Kwa muda mrefu Israeli walikuwa hawana Mungu wa kweli, walikuwa hawana kuhani wa kuwafundisha na wala hawakuwa na sheria. 415:4 Kum 4:29Lakini katika taabu yao walimrudia Bwana, Mungu wa Israeli na kumtafuta, naye akaonekana kwao. 515:5 Amu 19:20; Zek 8:10; Amu 5:6Katika siku hizo hapakuwa na amani kwa yeyote aliyesafiri, kutoka wala kuingia, kwa kuwa wakazi wote wa nchi walikuwa katika machafuko makubwa. 615:6 Mt 24:7; Isa 19:2; Mk 13:8Taifa moja lilipigana na taifa lingine na mji mmoja ukapigana na mji mwingine, kwa sababu Mungu alikuwa anawahangaisha kwa taabu za kila aina. 715:7 1Sam 24:19; Mit 14:14; Rut 2:12; Za 58:11; Mt 5:12-46; Lk 6:35; Kol 3:24Lakini kwa habari yenu ninyi, kuweni hodari wala msikate tamaa, kwa kuwa mtapata thawabu kwa kazi yenu.”

815:8 2Nya 13:19; 8:12; 1Fal 8:64Asa aliposikia maneno haya na unabii wa Azaria mwana wa Odedi nabii, akajipa moyo. Akaziondoa sanamu zote zilizokuwa machukizo katika nchi yote ya Yuda na Benyamini na kutoka miji aliyoiteka ya vilima vya Efraimu. Akakarabati madhabahu ya Bwana iliyokuwa mbele ya ukumbi wa Hekalu la Bwana.

915:9 2Nya 11:16-17Kisha akakutanisha Yuda wote, Benyamini na watu kutoka Efraimu, watu wa Manase na Simeoni waliokuwa wanaishi miongoni mwao, kwa maana idadi kubwa walikuwa wamemjia kutoka Israeli walipoona kwamba Bwana Mungu wake alikuwa pamoja naye.

10Basi wakakusanyika huko Yerusalemu mwezi wa tatu katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Asa. 1115:11 2Nya 14:13-15Wakati huo wakamtolea Bwana dhabihu za ngʼombe 700, kondoo na mbuzi 7,000 kutoka zile nyara walizoteka. 1215:12 2Fal 11:17; 2Nya 23:16; Neh 10:29; 1Nya 16:11; 2Fal 23:3; 2Nya 34:31Wakafanya agano kumtafuta Bwana, Mungu wa baba zao kwa moyo wao wote na kwa roho yao yote. 1315:13 Kut 22:20; Kum 13:9-16Wale wote ambao hawangemtafuta Bwana, Mungu wa Israeli wangelazimika kuuawa, akiwa mdogo au mkubwa, mwanaume au mwanamke. 14Wakamwapia Bwana kwa sauti kuu, kwa kupiga kelele, tarumbeta na kwa mabaragumu. 1515:15 Kum 4:29; 1Nya 22:9; 2Nya 14:7Yuda wote wakafurahia kile kiapo kwa sababu walikuwa wameapa kwa moyo wao wote. Wakamtafuta Mungu kwa bidii, naye akaonekana kwao. Kwa hiyo Bwana akawastarehesha pande zote.

1615:16 Kut 34:13; 2Nya 14:2-5; 1Fal 15:2, 10Mfalme Asa akamwondolea Maaka mama yake wadhifa wake kama mama malkia kwa sababu alikuwa ametengeneza nguzo ya Ashera ya kuchukiza. Asa akaikata hiyo nguzo, akaivunjavunja na kuiteketeza kwa moto katika Bonde la Kidroni. 1715:17 2Fal 12:3; 1Fal 3:2-4; Kum 12:7; 1Fal 15:14; 2Nya 14:3-5Ijapokuwa hakuondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu katika Israeli, moyo wa Asa ulikuwa umejiweka kwa Bwana kikamilifu maisha yake yote. 18Akaleta ndani ya Hekalu la Mungu fedha na dhahabu na vile vyombo ambavyo yeye na baba yake walikuwa wameviweka wakfu.

19Hapakuwepo vita tena mpaka mwaka wa thelathini na tano wa utawala wake Asa.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

歷代志下 15:1-19

亞撒的改革

1上帝的靈降在俄德的兒子亞撒利雅身上, 2他便出來迎接亞撒,對他說:「亞撒啊,所有的猶大人和便雅憫人啊,請聽我說!你們若順從耶和華,祂必與你們同在。你們若尋求祂,祂必讓你們尋見。你們若背棄祂,祂必離棄你們。 3以色列人已經許久沒有真神,沒有祭司教導,也沒有律法。 4然而,他們在患難時歸向以色列的上帝耶和華,尋求祂,祂就讓他們尋見。 5那時,人們出入不得平安,因為各地都有動亂。 6邦國與邦國、城邑與城邑互相攻擊破壞,因為上帝用各樣的災難擾亂他們。 7但你們要剛強,不要雙手發軟,因為你們必因所行的而得獎賞。」

8亞撒聽了俄德的兒子亞撒利雅先知的預言,就鼓起勇氣在猶大便雅憫全境以及他在以法蓮山區奪取的各城邑剷除可憎的神像,並在耶和華殿的走廊前重修耶和華的祭壇。

9當時,有許多以法蓮人、瑪拿西人和西緬人看見亞撒的上帝耶和華與他同在,就從以色列來投奔他,寄居在猶大亞撒把他們和所有的猶大人與便雅憫人都招聚在一起。 10亞撒執政第十五年三月,他們聚集在耶路撒冷11當天,他們從擄物中取出七百頭牛和七千隻羊獻給耶和華。 12他們又與他們祖先的上帝耶和華立約,要全心全意地尋求祂。 13凡不尋求以色列的上帝耶和華的,無論男女老幼,一律處死。 14他們高聲向耶和華起誓,並吹響號角。 15猶大人都為所起的誓而歡喜快樂,因他們誠心起誓、誠意尋求耶和華,耶和華就讓他們尋見,並賜他們四境平安。

16亞撒王廢除了他祖母瑪迦的太后之位,因為她造了可憎的亞舍拉神像。亞撒將她的神像砍倒、打碎,燒毀在汲淪溪旁。 17儘管他還沒有把邱壇從以色列除去,但他一生對耶和華忠心。 18他將他父親和自己奉獻給上帝的金銀及器皿都帶到上帝的殿裡。

19從那時直到亞撒執政第三十五年,國中都沒有戰爭。