2 Nyakati 13 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Nyakati 13:1-22

Abiya Mfalme Wa Yuda

(1 Wafalme 15:1-8)

1Katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Yeroboamu, Abiya akawa mfalme wa Yuda, 213:2 2Nya 11:20; 1Fal 15:6naye akatawala huko Yerusalemu miaka mitatu. Mama yake aliitwa Maaka, binti Urieli wa Gibea.

Basi kulikuwa na vita kati ya Abiya na Yeroboamu. 3Abiya aliingia vitani na jeshi la watu 400,000 wenye uwezo wa kupigana, naye Yeroboamu akapanga jeshi dhidi ya Abiya akiwa na jeshi la watu 800,000 wenye uwezo.

413:4 Yos 18:22; 1Nya 11:1Abiya akasimama juu ya Mlima Semaraimu, katika nchi ya vilima ya Efraimu, naye akasema, “Yeroboamu na Israeli yote, nisikilizeni mimi! 513:5 2Sam 7:13; 1Nya 17:12; Law 2:13; Hes 18:19; Amu 11:21-24; Eze 43:24; 1Sam 16:13; Za 89:20; Lk 1:31-33Hamfahamu kwamba Bwana, Mungu wa Israeli, alimpa Daudi na wazao wake ufalme juu ya Israeli milele kwa Agano la chumvi? 613:6 1Fal 11:26; 12:20; 2Nya 10:19Hata hivyo Yeroboamu mwana wa Nebati afisa wa Solomoni mwana wa Daudi, aliasi dhidi ya bwana wake. 713:7 Amu 9:4; Za 26:4; Mdo 17:5; Mit 12:11Baadhi ya watu wasiofaa kitu, wabaya kabisa walimkusanyikia na kumpinga Rehoboamu mwana wa Solomoni alipokuwa kijana mdogo asiyekuwa na uamuzi, asiye na nguvu za kuweza kupingana nao.

813:8 Za 68:25; 1Nya 25:10-24; 2Nya 29:2513:8 Kut 32:4; 1Fal 12:28; Hos 8:6“Hata sasa unapanga kupingana na ufalme wa Bwana ambao uko mikononi mwa wazao wa Daudi. Kweli ninyi ni jeshi kubwa nanyi mnazo ndama za dhahabu Yeroboamu alizozitengeneza kuwa miungu yenu. 913:9 2Nya 11:14-15; Kut 29:35-36; Gal 4:8; Yer 2:11Lakini je, hamkuwafukuza makuhani wa Bwana, wana wa Aroni na Walawi na kujifanyia makuhani wenu wenyewe kama yafanyavyo mataifa ya nchi nyingine? Yeyote anayekuja kujiweka wakfu akiwa na ndama dume na kondoo dume saba aweza kuwa kuhani wa kile ambacho ni miungu kwenu.

10“Lakini kwetu sisi, Bwana ndiye Mungu wetu, wala hatujamwacha. Makuhani wanaomtumikia Bwana ni wana wa Aroni, nao Walawi wakiwasaidia. 1113:11 Kut 29:39; 2Nya 2:4; Law 24:2-6; 1Nya 9:24; Kut 27:20-21Kila asubuhi na jioni wao hutoa sadaka za kuteketezwa na kufukiza uvumba wa harufu nzuri kwa Bwana. Wao huweka mikate juu ya meza safi kwa taratibu za kiibada na kuwasha taa kwenye kinara cha dhahabu kila jioni. Sisi tunazishika kanuni za Bwana Mungu wetu. Lakini ninyi mmemwacha Mungu. 1213:12 Hes 10:8-9; Amu 2:15; Mdo 5:39; Kum 20:4; Yos 5:4; Za 20:7; Ay 15:25-26; Mdo 9:4-5Mungu yu pamoja nasi, yeye ndiye kiongozi wetu. Makuhani wake wakiwa na tarumbeta zao watapiga baragumu ya vita dhidi yenu. Watu wa Israeli, msipigane dhidi ya Bwana, Mungu wa baba zenu, kwa maana hamtashinda.”

1313:13 2Nya 20:22; Yos 8:9Basi Yeroboamu alikuwa ametuma jeshi kuzunguka nyuma ya Yuda ili kwamba akiwa mbele ya Yuda, jeshi liwavizie kwa nyuma. 1413:14 1Nya 5:20; 2Nya 18:31Basi Yuda wakageuka na kuona kwamba wanashambuliwa mbele na nyuma. Ndipo wakamlilia Bwana. Makuhani wakapiga tarumbeta zao, 1513:15 2Nya 14:12; Hes 32:4nao watu wa Yuda wakapaza sauti ya kilio cha vita. Katika kupiga kelele za vita, Mungu akawafukuza Yeroboamu na Israeli wote mbele ya Mfalme Abiya na Yuda. 1613:16 2Nya 16:8Waisraeli wakakimbia mbele ya Yuda, naye Mungu akawatia Israeli mikononi mwao. 17Abiya na watu wake wakawachinja kwa machinjo makuu, hata wakawepo majeruhi 500,000 miongoni mwa watu wenye uwezo wa Israeli. 1813:18 1Nya 5:20; Za 22:5; Amu 8:28; 2Fal 18:5; 2Nya 16:8-9; 20:20Watu wa Israeli walitiishwa katika tukio lile, nao watu wa Yuda wakawa washindi kwa sababu walimtegemea Bwana, Mungu wa baba zao.

1913:19 Yos 15:9; Yn 11:54Abiya akamfuatia Yeroboamu na kuteka miji ya Betheli, Yeshana na Efroni kutoka kwake, pamoja na vijiji vinavyoizunguka miji hiyo. 2013:20 1Sam 25:38; Eze 24:16; Mdo 12:23; 1Sam 26:10; 1Fal 14:20Yeroboamu hakupata nguvu tena wakati wa utawala wa Abiya. Naye Bwana akampiga Yeroboamu akafa.

21Lakini Abiya akapata nguvu. Alioa wanawake kumi na wanne na alikuwa na wana ishirini na wawili na binti kumi na sita.

2213:22 2Nya 9:29; 12:15Matukio mengine ya utawala wa Abiya, pamoja na mambo aliyofanya na aliyosema, yameandikwa katika kitabu cha maelezo cha nabii Ido.

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

历代志下 13:1-22

亚比雅与耶罗波安争战

1耶罗波安王执政第十八年,亚比雅登基做犹大王, 2耶路撒冷执政三年。他母亲叫米该亚13:2 米该亚”在代下11:20是“押沙龙的女儿玛迦”。,是基比亚乌列的女儿。亚比雅耶罗波安之间常有争战。 3有一次,亚比雅率领四十万精兵出战,耶罗波安率领八十万精兵列阵迎战。

4亚比雅站在以法莲山区的西玛莲山上说:“耶罗波安和全体以色列人啊,你们听我说, 5你们不知道以色列的上帝耶和华曾经立下永世之约13:5 永世之约”希伯来文是“盐约”。,要把以色列国永远赐给大卫和他的子孙吗? 6尼八的儿子耶罗波安本是大卫的儿子所罗门的仆人,他却背叛他的主人, 7召集一群无赖恶棍,与所罗门的儿子罗波安作对。那时,罗波安年轻怯懦,无力抵抗。

8“现在你们仗着人多势众,又有耶罗波安制造的金牛犊作为你们的神明,便企图反抗大卫子孙所治理的耶和华的国度。 9你们赶走了做耶和华祭司的亚伦之后裔和利未人,效法外族人的恶俗为自己设立祭司。任何人牵来一头公牛犊和七只公绵羊,就可以自封为假神的祭司。

10“至于我们,耶和华是我们的上帝,我们没有背弃祂,我们有亚伦的后裔做祭司事奉耶和华,也有利未人各尽其职。 11他们每天早晚向耶和华献燔祭,烧芬芳的香,把供饼摆在洁净13:11 洁净”指宗教礼仪上的洁净。的桌子上,每晚点上金灯台的灯。我们遵守我们上帝耶和华的吩咐,你们却背弃祂。 12上帝与我们同在,祂率领我们。祂的祭司就要吹响向你们进攻的号角。以色列人啊,不要与你们祖先的上帝耶和华作对,因为你们绝不会得胜。”

13耶罗波安却在犹大人后面设伏兵,企图前后夹攻他们。 14犹大人转身,发现自己前后受敌,就呼求耶和华。祭司吹响号角, 15犹大人便吶喊,上帝使耶罗波安以色列人败在亚比雅犹大人面前。 16以色列人从犹大人面前逃跑,上帝把他们交在犹大人手中。 17亚比雅和他的军队大败以色列人,歼灭了他们五十万精兵。 18这样,以色列人被击败,犹大人因为倚靠他们祖先的上帝耶和华而大获全胜。

19亚比雅追赶耶罗波安,攻取了伯特利耶沙拿以法拉音各城以及它们周围的村庄。 20亚比雅在世之日,耶罗波安再也没有恢复势力。后来,耶和华攻击他,他就死了。 21亚比雅却日渐强大,他有十四个妻妾、二十二个儿子、十六个女儿。 22亚比雅其余的事及其言行都记在易多先知的史记上。