2 Nyakati 12 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Nyakati 12:1-16

Shishaki Ashambulia Yerusalemu

(1 Wafalme 14:25-28)

112:1 2Nya 11:17; Kum 8:14; 1Fal 14:22-24Baada ya nafasi ya Rehoboamu kuimarika na kuwa na nguvu, yeye na Israeli yote waliiacha sheria ya Bwana Mungu. 212:2 1Nya 5:25; 1Fal 11:40; 14:24-25Kwa sababu hawakuwa waaminifu kwa Bwana, Shishaki mfalme wa Misri akashambulia Yerusalemu katika mwaka wa tano wa utawala wa Mfalme Rehoboamu. 312:3 Mwa 10:6; Amo 9:7; 2Nya 16:8Akiwa na magari ya vita 1,200 na wapanda farasi 60,000 na idadi isiyohesabika ya majeshi ya Walibia, Wasukii na Wakushi12:3 Yaani watu kutoka sehemu ya Naili ya juu. yaliyokuja pamoja naye kutoka Misri. 412:4 2Nya 11:10Akateka miji ya Yuda yenye ngome akaendelea mpaka Yerusalemu.

512:5 2Nya 11:1; Kum 28:15; 2Nya 15:1-2Ndipo nabii Shemaya akaja kwa Rehoboamu na kwa viongozi wa Yuda waliokuwa wamekusanyika huko Yerusalemu kwa ajili ya hofu ya Shishaki naye akawaambia, “Hivi ndivyo asemavyo Bwana, ‘Ninyi mmeniacha mimi, kwa hiyo, mimi nami sasa ninawaacha ninyi mkononi mwa Shishaki.’ ”

612:6 Law 26:40-42; Ezr 9:15; Yak 4:10; Kut 9:27; 10:3; 2Nya 33:12; 34:27; Za 78:34Viongozi wa Israeli na mfalme wakajinyenyekeza na kusema, “Bwana Mungu ni mwenye haki.”

712:7 1Fal 21:29; Za 78:38Bwana Mungu alipoona kwamba wamejinyenyekeza, neno hili la Bwana likamjia Shemaya: “Maadamu wamejinyenyekeza, sitawaangamiza bali hivi karibuni nitawapatia wokovu. Ghadhabu yangu haitamwagwa juu ya Yerusalemu kwa kupitia Shishaki. 812:8 Kum 28:48; Isa 26:13Hata hivyo, watamtumikia Shishaki ili wapate kujifunza tofauti kati ya kunitumikia mimi na kuwatumikia wafalme wa nchi nyingine.”

912:9 2Nya 9:16; 1Fal 14:25Shishaki mfalme wa Misri alipoishambulia Yerusalemu, alichukua hazina za Hekalu la Bwana na hazina za jumba la kifalme. Akachukua kila kitu, pamoja na zile ngao za dhahabu ambazo Solomoni alikuwa amezitengeneza. 1012:10 2Sam 8:18; 23:23; 1Nya 11:25Kwa hiyo Mfalme Rehoboamu akatengeneza ngao za shaba badala ya zile za dhahabu na kuzikabidhi kwa majemadari wa ulinzi wa zamu kwenye ingilio la jumba la mfalme. 11Kila wakati mfalme alipokwenda katika Hekalu la Bwana walinzi walikwenda pamoja naye wakiwa wamebeba hizo ngao na baadaye walizirudisha kwenye chumba cha ulinzi.

1212:12 1Fal 14:13; 2Nya 19:3; Mwa 18:24Kwa sababu Rehoboamu alijinyenyekeza, hasira ya Bwana ikageukia mbali naye, hakuangamizwa kabisa. Kukawa na hali nzuri katika Yuda.

1312:13 2Nya 6:6; 13:7; Kum 12:5; 1Fal 14:21; Za 48:1-3Mfalme Rehoboamu akajiweka imara katika Yerusalemu na akaendelea kuwa mfalme. Alikuwa na umri wa miaka arobaini na mmoja alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na saba, mji ambao Bwana alikuwa ameuchagua miongoni mwa makabila yote ya Israeli ili aliweke Jina lake humo. Mama yake aliitwa Naama, alikuwa Mwamoni. 1412:14 Mt 7:7; Mdo 9:11Rehoboamu akatenda maovu kwa sababu hakuuelekeza moyo wake katika kumtafuta Bwana Mungu.

1512:15 2Nya 9:29; 13:22Kwa habari ya matukio katika utawala wa Rehoboamu, tangu mwanzo mpaka mwisho, je, hayakuandikwa katika kumbukumbu za nabii Shemaya na mwonaji Ido zinazohusiana na vizazi? Kulikuwako na vita mara kwa mara kati ya Rehoboamu na Yeroboamu. 1612:16 2Nya 11:20Rehoboamu akalala na baba zake, akazikwa katika Mji wa Daudi. Naye Abiya mwanawe akawa mfalme baada yake.

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

历代志下 12:1-16

埃及侵犯犹大

1罗波安王位稳定、国势强盛后,就离弃耶和华的律法,以色列人也都随从他。 2罗波安王执政第五年,埃及示撒上来攻打耶路撒冷,因为犹大君民对耶和华不忠。 3示撒率领一千二百辆战车、六万骑兵及无数的路比人、苏基人和古实人。 4他攻陷了犹大的坚城,直逼耶路撒冷

5那时,犹大各首领因为战事都聚集在耶路撒冷示玛雅先知去见罗波安和众首领,对他们说:“耶和华说,‘你们背弃了我,所以我也要离弃你们,把你们交在示撒手中。’” 6王与以色列的众首领听了,就谦卑下来说:“耶和华是公义的。” 7耶和华见他们谦卑下来,就对示玛雅说:“既然他们谦卑下来,我就不灭绝他们,给他们留一条生路。我也不会借示撒耶路撒冷倾倒我的愤怒。 8然而,他们必做示撒的仆人,好让他们体验事奉我和服侍世上的君王的不同。”

9埃及示撒带兵攻陷了耶路撒冷,把耶和华殿里和王宫里的财宝及所罗门造的金盾牌掳掠一空。 10罗波安王就造了铜盾牌代替金盾牌,交给看守宫门的护卫长看管。 11每次王进耶和华的殿,护卫兵就带上盾牌,用完后放回护卫房。 12王谦卑下来后,耶和华便不再向他发怒,没有将他完全毁灭。况且,在犹大还有一些善事。

罗波安逝世

13罗波安王在耶路撒冷巩固了自己的势力,继续做王。他四十一岁登基,在耶路撒冷执政十七年。耶和华从以色列众支派中选择耶路撒冷作为立祂名的城。罗波安的母亲叫拿玛,是亚扪人。 14罗波安行为邪恶,因为他不专心寻求耶和华。

15他执政期间的事件自始至终都记在示玛雅先知和易多先见的史记上。罗波安耶罗波安之间常有争战。 16罗波安与祖先同眠后,葬在大卫城。他儿子亚比雅继位。