2 Nyakati 1 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Nyakati 1:1-17

Solomoni Aomba Hekima

(1 Wafalme 3:1-15)

11:1 1Fal 2:26; 2Nya 12:1; Mwa 39:2; Hes 14:43; 1Nya 29:25; Mwa 21:22; 1Nya 17:8; Mt 28:20Solomoni mwana wa Daudi alijiimarisha kwenye milango yote! Katika ufalme wake, kwa kuwa Bwana Mungu wake alikuwa pamoja naye, naye akamfanya mkuu mno.

21:2 1Nya 28:1; 2Nya 29:20; 30:2Ndipo Solomoni akasema na Israeli wote, majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia, waamuzi na viongozi wote katika Israeli, pamoja na wakuu wa jamaa. 31:3 Law 17:4; Kut 36:8; 40:18; 1Fal 3:4Naye Solomoni na kusanyiko lote wakakwea mpaka mahali pa juu pa kuabudia huko Gibeoni, kwa kuwa huko ndiko Hema la Kukutania la Mungu lilipokuwa, ambalo Mose mtumishi wa Bwana alikuwa amelitengeneza huko jangwani. 41:4 2Sam 6:2, 17; 1Nya 15:25Basi Daudi alikuwa amelipandisha Sanduku la Mungu kutoka Kiriath-Yearimu mpaka mahali alipokuwa amepatengeneza kwa ajili yake, kwa sababu alikuwa amesimamisha hema kwa ajili ya hilo Sanduku huko Yerusalemu. 51:5 Kut 38:2; 31:2; 1Nya 13:3Lakini yale madhabahu ya shaba ambayo Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, alikuwa ametengeneza yalikuwa huko Gibeoni mbele ya Maskani ya Bwana Mungu, hivyo Solomoni na kusanyiko lote walimtafuta Mungu huko. 61:6 1Fal 3:4Solomoni akapanda huko yalikokuwa madhabahu ya shaba mbele za Bwana katika Hema la Kukutania, na kutoa dhabihu 1,000 za sadaka za kuteketezwa juu yake.

71:7 2Nya 7:12; Isa 58:9; 1Fal 3:5; Mit 3:5Usiku ule Mungu akamtokea Solomoni na kumwambia, “Omba lolote utakalo nikupe.”

81:8 1Nya 23:1; 28:5Solomoni akamjibu Mungu, “Umemwonyesha baba yangu Daudi fadhili nyingi, nawe umeniweka niwe mfalme mahali pake. 91:9 2Sam 7:25; 1Fal 8:25; Mwa 12:2Sasa, Bwana Mungu, ahadi yako kwa baba yangu Daudi na ithibitike, kwa kuwa umenifanya mimi mfalme juu ya watu ambao ni wengi kama mavumbi ya nchi. 101:10 Hes 27:17; Mit 8:15-16; Kum 31:2; 1Fal 3:9; Za 119:34; Mit 3:13; Yak 1:5Nakuomba unipe mimi hekima na maarifa, ili niweze kuongoza watu hawa, kwa kuwa ni nani awezaye kutawala hawa watu wako walio wengi hivi?”

111:11 Kum 17:17; 1Sam 16:7; 1Fal 3:11; 8:18Mungu akamwambia Solomoni, “Kwa kuwa jambo hili ndilo shauku ya moyo wako na hukuomba mali, utajiri au heshima, wala kifo kwa ajili ya adui zako, nawe kwa kuwa hukuomba maisha marefu, bali umeomba hekima na maarifa ili kuongoza watu wangu ambao nimekufanya uwe mfalme juu yao, 121:12 1Nya 29:12-25; Neh 13:26; Efe 3:20; 2Nya 9:22; Za 34:9-10; Mt 6:33; Mhu 2:9kwa hiyo utapewa hekima na maarifa. Tena nitakupa pia mali, utajiri na heshima, ambavyo hakuna mfalme yeyote aliyekuwepo kabla yako amewahi kuwa navyo, na hakuna yeyote baada yako atakayekuwa navyo.”

Fahari Ya Solomoni

(1 Wafalme 10:26-29)

13Ndipo Solomoni akaenda mpaka Yerusalemu kutoka mahali pa juu pa kuabudia huko Gibeoni, kutoka mbele ya Hema la Kukutania. Naye akatawala Israeli.

141:14 1Sam 8:11; 1Fal 9:19; 4:26Solomoni akakusanya magari ya vita na farasi. Alikuwa na magari 1,400 na farasi 12,000, ambayo aliyaweka katika miji ya magari na mengine akawa nayo huko Yerusalemu. 151:15 1Fal 9:28; Isa 60:5; Ay 22:24; 1Fal 10:27Mfalme akafanya fedha na dhahabu kuwa vitu vya kawaida kama mawe huko Yerusalemu, mierezi akaifanya kuwa mingi kama mikuyu vilimani. 16Farasi wa Solomoni waliletwa kutoka Misri na kutoka Kue.1:16 Yaani Kilikia. Wafanyabiashara wa mfalme waliwanunua kutoka Kue. 171:17 Wim 1:9Waliagiza magari kutoka Misri kwa bei ya shekeli 6001:17 Shekeli 600 za fedha ni sawa na kilo 7. za fedha, na farasi kwa shekeli 150.1:17 Shekeli 150 ni sawa na kilo 1.7. Pia waliwauza nje kwa wafalme wote wa Wahiti na wa Waaramu.

New International Reader’s Version

2 Chronicles 1:1-17

Solomon Asks God for Wisdom

1Solomon was the son of David. Solomon made his position secure over his kingdom. The Lord his God was with him. He made Solomon very great.

2Solomon spoke to the whole community of Israel. He spoke to the commanders of thousands of men and commanders of hundreds. He spoke to the judges and all the leaders in Israel. He spoke to the leaders of Israel’s families. 3Solomon and the whole community went to the high place at Gibeon. That’s because God’s tent of meeting was there. The Lord’s servant Moses had made the tent in the desert. 4David had carried up the ark of God from Kiriath Jearim. He had it brought to the place he had prepared for it. He had set up a tent for it in Jerusalem. 5But the bronze altar that Bezalel had made was in Gibeon. Bezalel was the son of Uri. Uri was the son of Hur. The altar was in front of the Lord’s holy tent. So Solomon and the whole community asked the Lord for advice in Gibeon. 6Solomon went up to the bronze altar in front of the Lord at the tent of meeting. Solomon sacrificed 1,000 burnt offerings on the altar.

7That night God appeared to Solomon. He said to him, “Ask for anything you want me to give you.”

8Solomon answered God, “You were very kind to my father David. Now you have made me king in his place. 9Lord God, let the promise you gave to my father David come true. You have made me king. My people are as many as the dust of the earth. They can’t be counted. 10Give me wisdom and knowledge. Then I’ll be able to lead these people. Without your help, who would be able to rule this great nation of yours?”

11God said to Solomon, “I am glad that those are the things you really want. You have not asked for wealth, possessions or honor. You have not even asked to have your enemies killed. You have not asked to live for a long time. Instead, you have asked for wisdom and knowledge. You want to be able to rule my people wisely. I have made you king over them. 12So wisdom and knowledge will be given to you. I will also give you wealth, possessions and honor. You will have more than any king before you ever had. And no king after you will have as much.”

13Then Solomon left the high place at Gibeon. He went from the tent of meeting there to Jerusalem. And he ruled over Israel.

14Solomon had 1,400 chariots and 12,000 horses. He kept some of them in the chariot cities. He kept others with him in Jerusalem. 15The king made silver and gold as common in Jerusalem as stones. He made cedar wood as common there as sycamore-fig trees in the western hills. 16Solomon got horses from Egypt and Kue. The king’s buyers purchased them from Kue at the current price. 17They could get a chariot from Egypt for 15 pounds of silver. They could get a horse for less than four pounds of silver. They sold horses and chariots to all the Hittite and Aramean kings.