2 Nyakati 1 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Nyakati 1:1-17

Solomoni Aomba Hekima

(1 Wafalme 3:1-15)

11:1 1Fal 2:26; 2Nya 12:1; Mwa 39:2; Hes 14:43; 1Nya 29:25; Mwa 21:22; 1Nya 17:8; Mt 28:20Solomoni mwana wa Daudi alijiimarisha kwenye milango yote! Katika ufalme wake, kwa kuwa Bwana Mungu wake alikuwa pamoja naye, naye akamfanya mkuu mno.

21:2 1Nya 28:1; 2Nya 29:20; 30:2Ndipo Solomoni akasema na Israeli wote, majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia, waamuzi na viongozi wote katika Israeli, pamoja na wakuu wa jamaa. 31:3 Law 17:4; Kut 36:8; 40:18; 1Fal 3:4Naye Solomoni na kusanyiko lote wakakwea mpaka mahali pa juu pa kuabudia huko Gibeoni, kwa kuwa huko ndiko Hema la Kukutania la Mungu lilipokuwa, ambalo Mose mtumishi wa Bwana alikuwa amelitengeneza huko jangwani. 41:4 2Sam 6:2, 17; 1Nya 15:25Basi Daudi alikuwa amelipandisha Sanduku la Mungu kutoka Kiriath-Yearimu mpaka mahali alipokuwa amepatengeneza kwa ajili yake, kwa sababu alikuwa amesimamisha hema kwa ajili ya hilo Sanduku huko Yerusalemu. 51:5 Kut 38:2; 31:2; 1Nya 13:3Lakini yale madhabahu ya shaba ambayo Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, alikuwa ametengeneza yalikuwa huko Gibeoni mbele ya Maskani ya Bwana Mungu, hivyo Solomoni na kusanyiko lote walimtafuta Mungu huko. 61:6 1Fal 3:4Solomoni akapanda huko yalikokuwa madhabahu ya shaba mbele za Bwana katika Hema la Kukutania, na kutoa dhabihu 1,000 za sadaka za kuteketezwa juu yake.

71:7 2Nya 7:12; Isa 58:9; 1Fal 3:5; Mit 3:5Usiku ule Mungu akamtokea Solomoni na kumwambia, “Omba lolote utakalo nikupe.”

81:8 1Nya 23:1; 28:5Solomoni akamjibu Mungu, “Umemwonyesha baba yangu Daudi fadhili nyingi, nawe umeniweka niwe mfalme mahali pake. 91:9 2Sam 7:25; 1Fal 8:25; Mwa 12:2Sasa, Bwana Mungu, ahadi yako kwa baba yangu Daudi na ithibitike, kwa kuwa umenifanya mimi mfalme juu ya watu ambao ni wengi kama mavumbi ya nchi. 101:10 Hes 27:17; Mit 8:15-16; Kum 31:2; 1Fal 3:9; Za 119:34; Mit 3:13; Yak 1:5Nakuomba unipe mimi hekima na maarifa, ili niweze kuongoza watu hawa, kwa kuwa ni nani awezaye kutawala hawa watu wako walio wengi hivi?”

111:11 Kum 17:17; 1Sam 16:7; 1Fal 3:11; 8:18Mungu akamwambia Solomoni, “Kwa kuwa jambo hili ndilo shauku ya moyo wako na hukuomba mali, utajiri au heshima, wala kifo kwa ajili ya adui zako, nawe kwa kuwa hukuomba maisha marefu, bali umeomba hekima na maarifa ili kuongoza watu wangu ambao nimekufanya uwe mfalme juu yao, 121:12 1Nya 29:12-25; Neh 13:26; Efe 3:20; 2Nya 9:22; Za 34:9-10; Mt 6:33; Mhu 2:9kwa hiyo utapewa hekima na maarifa. Tena nitakupa pia mali, utajiri na heshima, ambavyo hakuna mfalme yeyote aliyekuwepo kabla yako amewahi kuwa navyo, na hakuna yeyote baada yako atakayekuwa navyo.”

Fahari Ya Solomoni

(1 Wafalme 10:26-29)

13Ndipo Solomoni akaenda mpaka Yerusalemu kutoka mahali pa juu pa kuabudia huko Gibeoni, kutoka mbele ya Hema la Kukutania. Naye akatawala Israeli.

141:14 1Sam 8:11; 1Fal 9:19; 4:26Solomoni akakusanya magari ya vita na farasi. Alikuwa na magari 1,400 na farasi 12,000, ambayo aliyaweka katika miji ya magari na mengine akawa nayo huko Yerusalemu. 151:15 1Fal 9:28; Isa 60:5; Ay 22:24; 1Fal 10:27Mfalme akafanya fedha na dhahabu kuwa vitu vya kawaida kama mawe huko Yerusalemu, mierezi akaifanya kuwa mingi kama mikuyu vilimani. 16Farasi wa Solomoni waliletwa kutoka Misri na kutoka Kue.1:16 Yaani Kilikia. Wafanyabiashara wa mfalme waliwanunua kutoka Kue. 171:17 Wim 1:9Waliagiza magari kutoka Misri kwa bei ya shekeli 6001:17 Shekeli 600 za fedha ni sawa na kilo 7. za fedha, na farasi kwa shekeli 150.1:17 Shekeli 150 ni sawa na kilo 1.7. Pia waliwauza nje kwa wafalme wote wa Wahiti na wa Waaramu.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

歷代志下 1:1-17

所羅門王求智慧

1大衛的兒子所羅門鞏固了自己的王位。因為他的上帝耶和華與他同在,使他極其偉大。

2所羅門召集所有以色列人,包括千夫長、百夫長、審判官、首領和族長, 3與他們一起去基遍的邱壇,因為那裡有上帝的會幕,是耶和華的僕人摩西在曠野製造的。 4大衛已經把上帝的約櫃從基列·耶琳搬到耶路撒冷,因為他在那裡為約櫃搭了一個帳篷。 5戶珥的孫子、烏利的兒子比撒列造的銅壇在基遍耶和華的會幕前,所羅門和會眾就在那裡求問耶和華。 6所羅門上到耶和華會幕前的銅壇那裡,獻上一千頭祭牲作為燔祭。

7當天晚上,上帝向所羅門顯現,問他:「你要我給你什麼?只管求吧。」 8所羅門回答說:「你厚待我父大衛,並讓我繼位。 9耶和華上帝啊,求你成就你給我父大衛的應許。你立我為王,使我統治這多如地上塵土的百姓。 10現在,求你賜我智慧和知識以帶領他們。不然,誰能治理這麼多的百姓呢?」 11上帝對所羅門說:「你既然有此心願,不為自己求富貴、資財、尊榮、長壽,也沒有求滅絕你的敵人,只求智慧和知識以治理我的子民——我交在你王權之下的百姓, 12我必賜你智慧和知識,並且我還要賜你空前絕後的富貴、資財和尊榮。」

13於是,所羅門基遍邱壇的會幕前回到耶路撒冷治理以色列

所羅門王的兵力和財富

14所羅門組建了戰車和騎兵,有一千四百輛戰車、一萬二千名騎兵,駐紮在屯車城和他所在的耶路撒冷15王使耶路撒冷的金銀多如石頭,使香柏木多如丘陵的無花果樹。 16所羅門的馬匹都是由王室商隊從埃及古厄按定價買來的。 17他們從埃及買來的車馬,每輛車六百塊銀子,每匹馬一百五十塊銀子,他們也把車馬賣給人諸王和亞蘭諸王。