1 Yohana 5 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Yohana 5:1-21

Imani Katika Mwana Wa Mungu Huushinda Ulimwengu

15:1 Yn 3:15; 1Yn 2:22; 2:23; Yn 8:42Kila mtu anayeamini kwamba Yesu ndiye Kristo amezaliwa na Mungu, na yeyote ampendaye Baba humpenda pia mtoto aliyezaliwa naye. 25:2 1Yn 2:3; 3:14Hivi ndivyo tunavyojua kwamba tunawapenda watoto wa Mungu, kwa kumpenda Mungu na kuzitii amri zake. 35:3 Yn 14:15; Mt 11:30; 23:4Huku ndiko kumpenda Mungu, yaani, kuzitii amri zake. Nazo amri zake si nzito. 45:4 Yn 1:13; 16:33Kwa maana kila aliyezaliwa na Mungu huushinda ulimwengu. Huku ndiko kushinda kuushindako ulimwengu, yaani, hiyo imani yetu. 55:5 1Yn 2:23Ni nani yule aushindaye ulimwengu? Ni yule tu aaminiye kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu.

Ushuhuda Kuhusu Mwana Wa Mungu

65:6 Yn 19:34; 14:17Huyu ndiye alikuja kwa maji na damu, yaani, Yesu Kristo. Hakuja kwa maji peke yake, bali kwa maji na damu. Naye Roho ndiye ashuhudiaye, kwa sababu Roho ndiye kweli. 75:7 Mt 18:16Kwa maana wako watatu washuhudiao[ mbinguni: hao ni Baba, Neno na Roho Mtakatifu. Hawa watatu ni umoja. 8Pia wako mashahidi watatu duniani]: Roho, Maji na Damu; hawa watatu wanakubaliana katika umoja. 95:9 Yn 5:34; Mt 3:16, 17; Yn 5:32, 37; 8:15, 18Kama tunaukubali ushuhuda wa wanadamu, basi ushuhuda wa Mungu ni mkuu zaidi, kwa kuwa huu ndio ushuhuda wa Mungu kwamba amemshuhudia Mwanawe. 105:10 Rum 8:16; Gal 4:6; Yn 3:33; 1Yn 1:10Kila mtu amwaminiye Mwana wa Mungu anao huu ushuhuda moyoni mwake. Kila mtu asiyemwamini Mungu amemfanya yeye kuwa mwongo, kwa sababu hakuamini ushuhuda Mungu alioutoa kuhusu Mwanawe. 115:11 Mt 25:46; Yn 1:4Huu ndio ushuhuda: kwamba Mungu ametupa uzima wa milele, nao huo uzima umo katika Mwanawe. 125:12 Yn 3:15, 16, 36Aliye naye Mwana wa Mungu anao uzima, yeye asiye na Mwana wa Mungu hana uzima.

Maneno Ya Mwisho

135:13 Yn 3:23; 1Yn 5:11; Mt 25:46Nawaandikia mambo haya ninyi mnaoliamini Jina la Mwana wa Mungu ili mpate kujua ya kuwa mnao uzima wa milele. 145:14 Efe 3:12; 1Yn 3:21; Mt 7:7Huu ndio ujasiri tulio nao tunapomkaribia Mungu, kwamba kama tukiomba kitu sawasawa na mapenzi yake, atusikia. 155:15 1Yn 5:18, 20; 1Fal 3:12Nasi kama tunajua atusikia, lolote tuombalo, tunajua ya kwamba tumekwisha kupata zile haja tulizomwomba.

165:16 Yak 5:15; Kut 23:21; Ebr 6:4-6; 10:26; Yer 7:16; 14:11Kama mtu akimwona ndugu yake akitenda dhambi isiyo ya mauti, inampasa aombe, naye Mungu atampa uzima mtu huyo. Ninamaanisha wale ambao dhambi yao si ya mauti. Iko dhambi ya mauti, sisemi kwamba utaomba kwa ajili ya hiyo. 175:17 1Yn 3:4; 5:16; 2:1Jambo lolote lisilo la haki ni dhambi, lakini iko dhambi isiyo ya mauti.

185:18 Yn 1:13; Mt 5:37; 14:30Tunajua ya kuwa yeye aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi, bali aliyezaliwa na Mungu hujilinda, wala yule mwovu hawezi kumdhuru. 195:19 1Yn 4:6; Yn 12:31; 14:30; 17:15Sisi twajua kuwa tu watoto wa Mungu na ya kwamba ulimwengu wote uko chini ya utawala wa yule mwovu. 205:20 1Yn 5:5; Lk 24:45; Yn 17:3; 1Yn 5:11; Mt 25:46Nasi pia twajua ya kwamba Mwana wa Mungu amekuja, naye ametupa sisi ufahamu ili tupate kumjua yeye aliye Kweli. Nasi tumo ndani yake yeye aliye Kweli, yaani, ndani ya Yesu Kristo Mwanawe. Yeye ndiye Mungu wa kweli na uzima wa milele.

215:21 1Yn 2:1; 1Kor 10:14; 1The 1:9Watoto wapendwa, jilindeni nafsi zenu kutokana na sanamu. Amen.

New International Reader’s Version

1 John 5:1-21

Faith in God’s Son Who Became a Human Being

1Everyone who believes that Jesus is the Christ is a child of God. And everyone who loves the Father loves his children as well. 2Here is how we know that we love God’s children. We know it when we love God and obey his commands. 3In fact, here is what it means to love God. We love him by obeying his commands. And his commands are not hard to obey. 4That’s because everyone who is a child of God has won the battle over the world. Our faith has won the battle for us. 5Who is it that has won the battle over the world? Only the person who believes that Jesus is the Son of God.

6Jesus Christ was born as we are, and he died on the cross. He wasn’t just born as we are. He also died on the cross. The Holy Spirit is a truthful witness about him. That’s because the Spirit is the truth. 7There are three that are witnesses about Jesus. 8They are the Holy Spirit, the birth of Jesus, and the death of Jesus. And the three of them agree. 9We accept what people say when they are witnesses. But it’s more important when God is a witness. That’s because it is what God says about his Son. 10Whoever believes in the Son of God accepts what God says about him. Whoever does not believe God is calling him a liar. That’s because they have not believed what God said about his Son. 11Here is what God says about the Son. God has given us eternal life. And this life is found in his Son. 12Whoever belongs to the Son has life. Whoever doesn’t belong to the Son of God doesn’t have life.

Final Words

13I’m writing these things to you who believe in the name of the Son of God. I’m writing so you will know that you have eternal life. 14Here is what we can be sure of when we come to God in prayer. If we ask anything in keeping with what he wants, he hears us. 15If we know that God hears what we ask for, we know that we have it.

16Suppose you see any brother or sister commit a sin. But this sin is not the kind that leads to death. Then you should pray, and God will give them life. I’m talking about someone whose sin does not lead to death. But there is a sin that does lead to death. I’m not saying you should pray about that sin. 17Every wrong thing we do is sin. But there are sins that do not lead to death.

18We know that those who are children of God do not keep on sinning. The Son of God keeps them safe. The evil one can’t harm them. 19We know that we are children of God. We know that the whole world is under the control of the evil one. 20We also know that the Son of God has come. He has given us understanding. So we can know the God who is true. And we belong to the true God by belonging to his Son, Jesus Christ. He is the true God and eternal life.

21Dear children, keep away from statues of gods.