1 Yohana 4 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Yohana 4:1-21

Zijaribuni Hizo Roho

14:1 Mt 7:15; 1Kor 10:14; Yer 29:9; 1Kor 12:10; 2The 2:2; 1Yn 2:18Wapendwa, msiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho mwone kama zimetoka kwa Mungu, kwa sababu manabii wengi wa uongo wametokea ulimwenguni. 24:2 Yn 1:4; 1Yn 2:23; 1Kor 12:3Hivi ndivyo mnavyoweza kutambua Roho wa Mungu: Kila roho inayokubali kwamba Yesu Kristo amekuja katika mwili yatoka kwa Mungu. 34:3 1Yn 2:22; 2Yn 7; 1Yn 2:18Lakini kila roho ambayo haimkubali Yesu haitoki kwa Mungu. Hii ndiyo roho ya mpinga Kristo, ambayo mmesikia kwamba inakuja na sasa tayari iko ulimwenguni.

44:4 Rum 8:31; 2Fal 6:16Watoto wapendwa, ninyi mmetokana na Mungu, nanyi mmewashinda kwa sababu yeye aliye ndani yenu ni mkuu kuliko yeye aliye katika ulimwengu. 54:5 Yn 17:14, 16Wao wanatokana na ulimwengu na kwa hiyo hunena yaliyo ya ulimwengu, hivyo ulimwengu huwasikiliza. 64:6 Yn 8:47; 14:17Sisi twatokana na Mungu na yeyote anayemjua Mungu hutusikiliza, lakini asiyetokana na Mungu hatusikilizi. Hivi ndivyo tunavyoweza kutambua Roho wa Kweli na roho ya upotovu.

Mungu Ni Pendo

74:7 1Yn 3:11; 2:4Wapendwa, tupendane, kwa kuwa pendo latoka kwa Mungu. Kila apendaye amezaliwa na Mungu, naye anamjua Mungu. 84:8 1Yn 4:7, 16; 2:4; 3:6Yeye asiyependa hamjui Mungu, kwa sababu Mungu ni pendo. 94:9 Yn 3:16; 17; 1Yn 5:11Hivi ndivyo Mungu alivyoonyesha pendo lake kwetu: Mungu alimtuma Mwanawe wa pekee ulimwenguni, ili tupate uzima kupitia kwake. 104:10 Rum 5:8, 10; 1Yn 2:2Hili ndilo pendo: si kwamba tulimpenda Mungu, bali yeye alitupenda, akamtuma Mwanawe, ili yeye awe dhabihu ya upatanisho kwa ajili ya dhambi zetu. 114:11 Yak 3:16; 1Yn 2:25; Yn 1:4; 1Yn 4:9Marafiki wapendwa, kama Mungu alivyotupenda sisi, imetupasa na sisi kupendana. 124:12 Yn 1:18; 1Tim 6:16Hakuna mtu yeyote aliyemwona Mungu wakati wowote. Lakini tukipendana, Mungu anakaa ndani yetu, na pendo lake limekamilika ndani yetu.

134:13 1Yn 3:24; 2:3Tunajua kwamba twakaa ndani yake na yeye ndani yetu, kwa sababu ametupa sisi sehemu ya Roho wake. 144:14 Yn 15:27; Lk 2:10Nasi tumeona na kushuhudia kwamba Baba amemtuma Mwanawe ili awe Mwokozi wa ulimwengu. 154:15 1Yn 5:5; Rum 10:9Kila akiriye kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu, basi Mungu hukaa ndani yake, naye ndani ya Mungu. 164:16 1Yn 4:8, 12, 13; 3:24Hivyo nasi twajua na kulitumainia pendo la Mungu alilo nalo kwa ajili yetu.

Mungu ni Upendo. Kila akaaye katika upendo hukaa ndani ya Mungu na Mungu hukaa ndani yake. 174:17 1Yn 4:12; 2:5; Efe 3:12; Mt 10:15Kwa njia hii, pendo hukamilishwa miongoni mwetu ili tupate kuwa na ujasiri katika siku ya hukumu, kwa sababu kama alivyo ndivyo tulivyo sisi katika ulimwengu huu. 184:18 Rum 8:15; 1Yn 4:12Katika pendo hakuna hofu. Lakini pendo lililo kamili huitupa nje hofu, kwa sababu hofu inahusika na adhabu. Kila mwenye hofu hakukamilika katika pendo.

194:19 1Yn 4:10Twampenda yeye kwa sababu yeye alitupenda kwanza. 204:20 1Yn 2:9; 3:17; Yn 1:18Ikiwa mtu atasema, “Nampenda Mungu,” lakini anamchukia ndugu yake, yeye ni mwongo. Kwa maana kila mtu asiyempenda ndugu yake ambaye anamwona, atampendaje Mungu asiyemuona? 21Naye ametupa amri hii: Yeyote anayempenda Mungu lazima pia ampende ndugu yake.

King James Version

1 John 4:1-21

1Beloved, believe not every spirit, but try the spirits whether they are of God: because many false prophets are gone out into the world. 2Hereby know ye the Spirit of God: Every spirit that confesseth that Jesus Christ is come in the flesh is of God: 3And every spirit that confesseth not that Jesus Christ is come in the flesh is not of God: and this is that spirit of antichrist, whereof ye have heard that it should come; and even now already is it in the world. 4Ye are of God, little children, and have overcome them: because greater is he that is in you, than he that is in the world. 5They are of the world: therefore speak they of the world, and the world heareth them. 6We are of God: he that knoweth God heareth us; he that is not of God heareth not us. Hereby know we the spirit of truth, and the spirit of error.

7Beloved, let us love one another: for love is of God; and every one that loveth is born of God, and knoweth God. 8He that loveth not knoweth not God; for God is love. 9In this was manifested the love of God toward us, because that God sent his only begotten Son into the world, that we might live through him. 10Herein is love, not that we loved God, but that he loved us, and sent his Son to be the propitiation for our sins. 11Beloved, if God so loved us, we ought also to love one another. 12No man hath seen God at any time. If we love one another, God dwelleth in us, and his love is perfected in us. 13Hereby know we that we dwell in him, and he in us, because he hath given us of his Spirit. 14And we have seen and do testify that the Father sent the Son to be the Saviour of the world. 15Whosoever shall confess that Jesus is the Son of God, God dwelleth in him, and he in God. 16And we have known and believed the love that God hath to us. God is love; and he that dwelleth in love dwelleth in God, and God in him. 17Herein is our love made perfect, that we may have boldness in the day of judgment: because as he is, so are we in this world. 18There is no fear in love; but perfect love casteth out fear: because fear hath torment. He that feareth is not made perfect in love. 19We love him, because he first loved us. 20If a man say, I love God, and hateth his brother, he is a liar: for he that loveth not his brother whom he hath seen, how can he love God whom he hath not seen? 21And this commandment have we from him, That he who loveth God love his brother also.