13:1 Yn 3:16; 15:21Tazameni ni pendo kuu namna gani alilotupa Baba, kwamba sisi tuitwe wana wa Mungu! Na ndivyo tulivyo. Kwa sababu hii ulimwengu haututambui, kwa kuwa haukumtambua yeye. 23:2 Rum 8:29; 2Pet 1:4; Za 17:15Wapendwa, sasa tu wana wa Mungu, lakini bado haijadhihirika tutakavyokuwa, lakini twajua ya kwamba yeye atakapodhihirishwa, tutafanana naye, kwa maana tutamwona kama alivyo. 33:3 2Kor 7:1; 2Pet 3:13, 14Kila mmoja mwenye matumaini haya ndani yake hujitakasa, kama vile yeye alivyo mtakatifu.
43:4 1Yn 5:17; Mt 7:23; Rum 4:15Kila mtu atendaye dhambi afanya uasi, kwa kuwa dhambi ni uasi. 53:5 2Kor 5:21; 1Yn 1:2; Isa 53:5, 6, 11; 1Tim 1:15; Ebr 1:3; 9:26; 1Pet 2:24Lakini mwajua ya kuwa yeye alidhihirishwa ili aziondoe dhambi, wala ndani yake hamna dhambi. 63:6 1Yn 5:18; 3Yn 1; 1Yn 2:4Kila mtu akaaye ndani yake hatendi dhambi. Kila mtu atendaye dhambi hakumwona yeye wala hakumtambua.
73:7 1Yn 2:1; 2:26; 2:29Watoto wapendwa, mtu yeyote asiwadanganye. Kila mtu atendaye haki ana haki, kama yeye alivyo na haki. 83:8 Yn 1:13; Za 119:3; 1Pet 1:23Yeye atendaye dhambi ni wa ibilisi, kwa sababu ibilisi amekuwa akitenda dhambi tangu mwanzo. Kwa kusudi hili Mwana wa Mungu alidhihirishwa, ili aziangamize kazi za ibilisi. 93:9 Yn 1:13; 1Yn 3:6; Za 119:3; 1Yn 5:18; 1Pet 1:23Yeyote aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi, kwa sababu uzao wa Mungu wakaa ndani yake, wala hawezi kutenda dhambi kwa sababu amezaliwa na Mungu. 103:10 1Yn 3:1, 2; Yn 1:12; 1Yn 3:8; 4:8; 2:9Kwa jinsi hii tunaweza kujua dhahiri watoto wa Mungu na pia watoto wa ibilisi. Yeyote asiyetenda haki hatokani na Mungu, wala yeye asiyempenda ndugu yake.
Mpendane Ninyi Kwa Ninyi
113:11 1Yn 1:5; Yn 15:12Hili ndilo neno mlilolisikia tangu mwanzo: Kwamba imetupasa tupendane sisi kwa sisi. 123:12 Mwa 4:8; Mt 5:37; Za 38:20; Mit 29:10Msiwe kama Kaini aliyekuwa wa yule mwovu akamuua ndugu yake. Basi kwa nini alimuua? Ni kwa sababu matendo yake Kaini yalikuwa mabaya na ya ndugu yake yalikuwa ya haki. 133:13 Yn 15:18, 19; 17:14Ndugu zangu, ninyi msistaajabu kama ulimwengu ukiwachukia. 143:14 Yn 5:24; 1Yn 2:9Sisi tunajua ya kwamba tumepita mautini kuingia uzimani, kwa sababu tunawapenda ndugu. Kila asiyempenda ndugu yake akaa mautini. 153:15 Mt 5:21, 22; Gal 5:20, 21; Yn 3:16Yeyote amchukiaye ndugu yake ni muuaji, nanyi mwajua ya kwamba muuaji hana uzima wa milele ndani yake.
163:16 Yn 10:11; 15:13; Flp 2:17; 1The 2:8Kwa namna hii twaweza kulijua pendo la Mungu: Kwa sababu Yesu Kristo aliutoa uhai wake kwa ajili yetu. Nasi imetupasa kuutoa uhai kwa ajili ya hao ndugu. 173:17 Yak 2:15, 16; 1Yn 4:20Ikiwa mtu anavyo vitu vya ulimwengu huu na akamwona ndugu yake ni mhitaji lakini asimhurumie, upendo wa Mungu wakaaje ndani ya mtu huyo? 183:18 1Yn 2:1; Eze 33:1; Rum 12:9Watoto wapendwa, tusipende kwa maneno au kwa ulimi bali kwa tendo na kweli. 193:19 Yn 18:37; 1Yn 1:8Basi hivi ndivyo tutakavyoweza kujua ya kuwa sisi tu wa kweli na hivyo twaithibitisha mioyo yetu mbele za Mungu 203:20 1Kor 4:4kila mara mioyo yetu inapotuhukumu. Kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mioyo yetu, naye anajua kila kitu.
213:21 Efe 3:12; 1Kor 10:14; 1Yn 5:14Wapendwa, kama mioyo yetu haituhukumu, tunao ujasiri mbele za Mungu, 223:22 Mt 7:7; Ebr 13:21lolote tuombalo, twalipokea kutoka kwake, kwa sababu tumezitii amri zake na kutenda yale yanayompendeza. 233:23 Yn 6:23; 13:34Hii ndiyo amri yake: kwamba tuliamini Jina la Mwanawe, Yesu Kristo, na kupendana sisi kwa sisi kama yeye alivyotuamuru. 243:24 1Yn 4:15; 1The 4:8Wale wote wanaozishika amri zake hukaa ndani yake na yeye ndani yao. Hivi ndivyo tunavyojua kwamba anakaa ndani yetu. Nasi twajua hili kwa njia ya Roho yule aliyetupa.
上帝的兒女
1你們看,父上帝何等愛我們,稱我們為祂的兒女!我們也實在是祂的兒女,世人之所以不認識我們,是因為他們不認識父上帝。 2親愛的弟兄姊妹,我們現在是上帝的兒女,將來如何還未顯明。但我們知道,當主顯現的時候,我們必會像祂,因為我們必見到祂的本體。 3凡心存這種盼望的人都會自潔,因為主是聖潔的。
4犯罪的人都違背上帝的律法,違背上帝的律法就是罪。 5你們知道,耶穌降世是為了除掉人的罪,祂自己並沒有罪。 6住在祂裡面的人不會一直犯罪;一直犯罪的人既沒見過祂也不認識祂。
7孩子們,不要受人迷惑,要知道行義的才是義人,正如主是公義的。 8一直犯罪的人是屬魔鬼的,因為魔鬼從起初便犯罪,但上帝兒子的顯現是為了摧毀魔鬼的工作。 9從上帝生的人不會繼續犯罪,因為他裡面有上帝的生命3·9 「上帝的生命」希臘文是「上帝的種子」。。他不能犯罪,因為他是從上帝生的。 10這樣,就可以看出誰是上帝的兒女,誰是魔鬼的兒女。凡不按公義行事、不愛弟兄姊妹的,都不是上帝的兒女。
彼此相愛
11我們應當彼此相愛,這是你們起初聽見的信息。 12不要步該隱的後塵。他屬於那惡者,殺害了自己的弟弟。他為什麼要殺害自己的弟弟呢?因為他的行為邪惡,而他弟弟秉行公義。
13弟兄姊妹,世人若恨你們,不要驚奇。 14我們因愛弟兄姊妹,便知道自己已經出死入生了。不愛弟兄姊妹的,仍然陷在死亡中。 15恨弟兄姊妹的就是殺人的,你們知道殺人的沒有永生。 16主耶穌為我們捨命,我們由此便知道什麼是愛,我們也應當為弟兄姊妹捨命。 17如果一個豐衣足食的人看見貧窮的弟兄姊妹,卻毫無憐憫之心,怎能說他愛上帝呢? 18所以,孩子們啊,不要單在口頭上說愛人,總要以真誠的行動表現出來。
19-20這樣,我們必知道自己屬於真理,即使我們心中自責,也可以在上帝面前心安,因為上帝比我們的心大,祂知道一切。
21親愛的弟兄姊妹,我們若能凡事問心無愧,就可以在上帝面前坦然無懼。 22這樣,我們無論向上帝祈求什麼,都必得到,因為我們遵守祂的命令,做祂喜悅的事。 23其實上帝的命令是:我們要信祂兒子耶穌基督的名,遵照祂的命令彼此相愛。 24遵行上帝命令的人就住在上帝裡面,上帝也住在他裡面。我們藉著上帝賜給我們的聖靈知道:祂住在我們裡面。