1 Yohana 1 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Yohana 1:1-10

Neno La Uzima

11:1 Yn 1:2; 2Pet 1:16; Yn 20:27Tunawajulisha lile lililokuwepo tangu mwanzo, lile tulilosikia, ambalo tumeliona kwa macho yetu, ambalo tumelitazama na kuligusa kwa mikono yetu, kuhusu Neno la uzima. 21:2 Yn 14:6; 1Pet 1:20Uzima huo ulidhihirishwa; nasi tumeuona na kuushuhudia, nasi twawatangazia uzima wa milele, ambao ulikuwa pamoja na Baba, nao ukadhihirishwa kwetu. 31:3 1Kor 1:9; 1Yn 1:1; Mdo 4:20; Yn 17:21; 1Yn 2:24Twawatangazia lile tuliloliona na kulisikia, ili nanyi mwe na ushirika nasi. Na ushirika wetu hasa ni pamoja na Baba na Mwanawe, Yesu Kristo. 4Tunaandika mambo haya ili furaha yetu ipate kuwa timilifu.

Kutembea Nuruni

51:5 1Yn 3:11; 2Yn 12Huu ndio ujumbe tuliosikia kutoka kwake na kuwatangazia ninyi: kwamba Mungu ni nuru na ndani yake hamna giza lolote. 61:6 Efe 5:8; 1Yn 4:20Kama tukisema kwamba twashirikiana naye huku tukienenda gizani, twasema uongo, wala hatutendi lililo kweli. 71:7 Ufu 7:14; Ebr 9:14; Ufu 1:5Lakini tukienenda nuruni, kama yeye alivyo nuruni, twashirikiana sisi kwa sisi na damu yake Yesu, Mwana wake, yatusafisha dhambi yote.

81:8 Yer 2:35; Yn 8:44Kama tukisema kwamba hatuna dhambi, twajidanganya wenyewe wala kweli haimo ndani yetu. 91:9 Mit 28; 13; Za 32:5; 51:2; Mit 28:13; 1Yn 1:7; Mik 7:18-20; Ebr 10:22Kama tukiziungama dhambi zetu, yeye ni mwaminifu na wa haki, atatusamehe dhambi zetu na kutusafisha kutoka kwenye udhalimu wote. 101:10 1Yn 5:10; Yn 5:38; 1Yn 1:8; 5:10; Yn 5:38; 2:15Kama tukisema hatukutenda dhambi, twamfanya yeye kuwa mwongo na neno lake halimo ndani yetu.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

約翰一書 1:1-10

生命之道

1論到從太初就已經存在的生命之道,我們曾經耳聞目睹,親眼看過,親手摸過。 2這生命曾顯現過,我們看見了,現在做見證,向你們傳揚這原本與父同在、曾向我們顯現的永恆生命。 3我們把所見所聞傳給你們,使你們可以與我們相交。誠然,我們是與父和祂兒子耶穌基督相交。 4我們將這些話寫給你們,是要讓大家都充滿喜樂。

要活在光中

5我們從耶穌那裡聽見、現在傳給你們的信息就是:上帝是光,在祂裡面毫無黑暗。 6如果我們說與祂相交,卻仍過著黑暗的生活,就是撒謊,沒有遵行真理。 7如果我們生活在光明之中,像上帝在光明中一樣,就能夠彼此相交,上帝兒子耶穌的血能洗淨我們一切的罪。

8如果我們說自己沒有罪,便是自欺,真理就不在我們心中。 9如果我們承認自己的罪,上帝是信實公義的,必赦免我們的罪,洗淨我們一切的不義。 10我們如果說自己沒有犯過罪,就是把上帝看作說謊的,祂的道也不在我們心中。