1 Wathesalonike 5 – NEN & NIVUK

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Wathesalonike 5:1-28

Kuweni Tayari Kwa Siku Ya Bwana

15:1 Mdo 1:7; 1The 4:9Basi, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira hatuna haja ya kuwaandikia, 25:2 1Kor 1:8; 2Pet 3:10kwa kuwa mnajua vyema kwamba siku ya Bwana itakuja kama mwizi ajapo usiku. 35:3 Yer 6:14; Yn 16:21, 22; Mt 24:39; Lk 21:34, 35Wakati watu wanaposema, “Kuna amani na salama,” maangamizi huwajia ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwanamke mwenye mimba; nao hakika hawatatoroka.

45:4 Mdo 26:18; 1Yn 2:8Bali ninyi, ndugu, hampo gizani hata siku ile iwakute ghafula kama mwizi. 55:5 Rum 13:12; Efe 5:9Ninyi nyote ni wana wa nuru na wana wa mchana. Sisi si wana wa giza wala wa usiku. 65:6 Rum 13:11Kwa hiyo basi, tusilale kama watu wengine walalavyo, bali tukeshe na kuwa na kiasi. 75:7 Lk 21:34, 36; Rum 13:13; 1Kor 15:34Kwa kuwa wote walalao hulala usiku na wale walewao hulewa usiku. 85:8 Isa 59:17; Efe 6:14, 16, 17Lakini kwa kuwa sisi ni wana wa mchana, basi tuwe na kiasi, tukijivika imani na upendo kama dirii kifuani na tumaini letu la wokovu kama chapeo. 95:9 2The 2:13-14Kwa maana Mungu hakutuita ili tupate ghadhabu bali tupate wokovu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo. 105:10 2Kor 5:15Yeye alikufa kwa ajili yetu ili hata kama tuko macho au tumelala, tupate kuishi pamoja naye. 115:11 1The 4:18Kwa hiyo farijianeni na kujengana, kama vile mnavyofanya sasa.

Maagizo Ya Mwisho, Salamu Na Kuwatakia Heri

125:12 1Tim 5:17; Ebr 13:17Sasa tunawaomba, ndugu, waheshimuni wale wanaofanya kazi kwa bidii miongoni mwenu, wale ambao wana mamlaka juu yenu katika Bwana na ambao wanawaonya. 135:13 Mk 9:50; 2The 3:6-11; Rum 14:1Waheshimuni sana katika upendo kwa ajili ya kazi zao. Ishini kwa amani ninyi kwa ninyi. 145:14 2The 3:11, 12; Ebr 12:12; Rum 4:1; 15:1Nasi twawasihi, ndugu, waonyeni walio wavivu, watieni moyo waoga, wasaidieni wanyonge na kuwavumilia watu wote. 155:15 1Pet 3:9; Gal 6:10; Efe 4:32Angalieni kuwa mtu asimlipe mwenzake maovu kwa maovu, bali siku zote tafuteni kutendeana mema ninyi kwa ninyi na kwa watu wote.

165:16 2Kor 6:10; Flp 4:4Furahini siku zote; 175:17 Lk 18:1; 21:36; Rum 12:12; Efe 6:18; Kol 4:12ombeni bila kukoma; 185:18 Efe 5:20; Kol 3:17shukuruni kwa kila jambo, kwa maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu kwa ajili yenu katika Kristo Yesu.

195:19 Efe 4:30Msiuzime moto wa Roho Mtakatifu; 205:20 1Kor 14:1-40msiyadharau maneno ya unabii. 215:21 1Kor 14:29; 1Yn 4:1Jaribuni kila kitu. Yashikeni yaliyo mema. 225:22 1The 4:12Jiepusheni na uovu wa kila namna.

235:23 Rum 15:33; Ebr 4:12; 1The 3:13; 2:19Mungu mwenyewe, Mungu wa amani, awatakase ninyi kabisa. Nanyi mhifadhiwe roho zenu, nafsi zenu na miili yenu, bila kuwa na lawama katika Bwana wetu Yesu Kristo. 245:24 Rum 8:28; 1Kor 1:9; Hes 23:19; Flp 1:6Yeye aliyewaita ni mwaminifu naye atafanya hayo.

255:25 Kol 4:3; 2The 3:1; Ebr 13:18; Efe 6:9Ndugu, tuombeeni. 26Wasalimuni ndugu wote kwa busu takatifu. 27Nawaagizeni mbele za Bwana mhakikishe kuwa ndugu wote wanasomewa barua hii.

28Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi. Amen.

New International Version – UK

1 Thessalonians 5:1-28

The day of the Lord

1Now, brothers and sisters, about times and dates we do not need to write to you, 2for you know very well that the day of the Lord will come like a thief in the night. 3While people are saying, ‘Peace and safety’, destruction will come on them suddenly, as labour pains on a pregnant woman, and they will not escape.

4But you, brothers and sisters, are not in darkness so that this day should surprise you like a thief. 5You are all children of the light and children of the day. We do not belong to the night or to the darkness. 6So then, let us not be like others, who are asleep, but let us be awake and sober. 7For those who sleep, sleep at night, and those who get drunk, get drunk at night. 8But since we belong to the day, let us be sober, putting on faith and love as a breastplate, and the hope of salvation as a helmet. 9For God did not appoint us to suffer wrath but to receive salvation through our Lord Jesus Christ. 10He died for us so that, whether we are awake or asleep, we may live together with him. 11Therefore encourage one another and build each other up, just as in fact you are doing.

Final instructions

12Now we ask you, brothers and sisters, to acknowledge those who work hard among you, who care for you in the Lord and who admonish you. 13Hold them in the highest regard in love because of their work. Live in peace with each other. 14And we urge you, brothers and sisters, warn those who are idle and disruptive, encourage the disheartened, help the weak, be patient with everyone. 15Make sure that nobody pays back wrong for wrong, but always strive to do what is good for each other and for everyone else.

16Rejoice always, 17pray continually, 18give thanks in all circumstances; for this is God’s will for you in Christ Jesus.

19Do not quench the Spirit. 20Do not treat prophecies with contempt 21but test them all; hold on to what is good, 22reject every kind of evil.

23May God himself, the God of peace, sanctify you through and through. May your whole spirit, soul and body be kept blameless at the coming of our Lord Jesus Christ. 24The one who calls you is faithful, and he will do it.

25Brothers and sisters, pray for us.

26Greet all God’s people with a holy kiss.

27I charge you before the Lord to have this letter read to all the brothers and sisters.

28The grace of our Lord Jesus Christ be with you.