1 Wathesalonike 5 – NEN & BDS

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Wathesalonike 5:1-28

Kuweni Tayari Kwa Siku Ya Bwana

15:1 Mdo 1:7; 1The 4:9Basi, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira hatuna haja ya kuwaandikia, 25:2 1Kor 1:8; 2Pet 3:10kwa kuwa mnajua vyema kwamba siku ya Bwana itakuja kama mwizi ajapo usiku. 35:3 Yer 6:14; Yn 16:21, 22; Mt 24:39; Lk 21:34, 35Wakati watu wanaposema, “Kuna amani na salama,” maangamizi huwajia ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwanamke mwenye mimba; nao hakika hawatatoroka.

45:4 Mdo 26:18; 1Yn 2:8Bali ninyi, ndugu, hampo gizani hata siku ile iwakute ghafula kama mwizi. 55:5 Rum 13:12; Efe 5:9Ninyi nyote ni wana wa nuru na wana wa mchana. Sisi si wana wa giza wala wa usiku. 65:6 Rum 13:11Kwa hiyo basi, tusilale kama watu wengine walalavyo, bali tukeshe na kuwa na kiasi. 75:7 Lk 21:34, 36; Rum 13:13; 1Kor 15:34Kwa kuwa wote walalao hulala usiku na wale walewao hulewa usiku. 85:8 Isa 59:17; Efe 6:14, 16, 17Lakini kwa kuwa sisi ni wana wa mchana, basi tuwe na kiasi, tukijivika imani na upendo kama dirii kifuani na tumaini letu la wokovu kama chapeo. 95:9 2The 2:13-14Kwa maana Mungu hakutuita ili tupate ghadhabu bali tupate wokovu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo. 105:10 2Kor 5:15Yeye alikufa kwa ajili yetu ili hata kama tuko macho au tumelala, tupate kuishi pamoja naye. 115:11 1The 4:18Kwa hiyo farijianeni na kujengana, kama vile mnavyofanya sasa.

Maagizo Ya Mwisho, Salamu Na Kuwatakia Heri

125:12 1Tim 5:17; Ebr 13:17Sasa tunawaomba, ndugu, waheshimuni wale wanaofanya kazi kwa bidii miongoni mwenu, wale ambao wana mamlaka juu yenu katika Bwana na ambao wanawaonya. 135:13 Mk 9:50; 2The 3:6-11; Rum 14:1Waheshimuni sana katika upendo kwa ajili ya kazi zao. Ishini kwa amani ninyi kwa ninyi. 145:14 2The 3:11, 12; Ebr 12:12; Rum 4:1; 15:1Nasi twawasihi, ndugu, waonyeni walio wavivu, watieni moyo waoga, wasaidieni wanyonge na kuwavumilia watu wote. 155:15 1Pet 3:9; Gal 6:10; Efe 4:32Angalieni kuwa mtu asimlipe mwenzake maovu kwa maovu, bali siku zote tafuteni kutendeana mema ninyi kwa ninyi na kwa watu wote.

165:16 2Kor 6:10; Flp 4:4Furahini siku zote; 175:17 Lk 18:1; 21:36; Rum 12:12; Efe 6:18; Kol 4:12ombeni bila kukoma; 185:18 Efe 5:20; Kol 3:17shukuruni kwa kila jambo, kwa maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu kwa ajili yenu katika Kristo Yesu.

195:19 Efe 4:30Msiuzime moto wa Roho Mtakatifu; 205:20 1Kor 14:1-40msiyadharau maneno ya unabii. 215:21 1Kor 14:29; 1Yn 4:1Jaribuni kila kitu. Yashikeni yaliyo mema. 225:22 1The 4:12Jiepusheni na uovu wa kila namna.

235:23 Rum 15:33; Ebr 4:12; 1The 3:13; 2:19Mungu mwenyewe, Mungu wa amani, awatakase ninyi kabisa. Nanyi mhifadhiwe roho zenu, nafsi zenu na miili yenu, bila kuwa na lawama katika Bwana wetu Yesu Kristo. 245:24 Rum 8:28; 1Kor 1:9; Hes 23:19; Flp 1:6Yeye aliyewaita ni mwaminifu naye atafanya hayo.

255:25 Kol 4:3; 2The 3:1; Ebr 13:18; Efe 6:9Ndugu, tuombeeni. 26Wasalimuni ndugu wote kwa busu takatifu. 27Nawaagizeni mbele za Bwana mhakikishe kuwa ndugu wote wanasomewa barua hii.

28Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi. Amen.

La Bible du Semeur

1 Thessaloniciens 5:1-28

1Quant à l’époque et au moment de ces événements, vous n’avez pas besoin, frères et sœurs, qu’on vous écrive à ce sujet : 2vous savez fort bien vous-mêmes que le jour du Seigneur viendra de façon aussi inattendue qu’un voleur en pleine nuit5.2 Voir Mt 24.43 et Lc 12.39..

3Lorsque les gens diront : « Paix et sécurité ! », alors la ruine fondra subitement sur eux, comme les douleurs saisissent la femme enceinte, et aucun n’échappera.

4Mais vous, frères et sœurs, vous n’êtes pas dans les ténèbres pour que le jour du Seigneur vous surprenne comme un voleur. 5Car vous êtes tous enfants de la lumière, enfants du jour. Nous n’appartenons ni à la nuit ni aux ténèbres. 6Ne dormons donc pas comme le reste des hommes, mais restons vigilants et faisons preuve de modération.

7Ceux qui dorment, dorment la nuit, et ceux qui s’enivrent, s’enivrent la nuit. 8Mais nous qui sommes enfants du jour, faisons preuve de modération : revêtons-nous de la cuirasse de la foi et de l’amour, et mettons le casque de l’espérance du salut5.8 Es 59.17.. 9Car Dieu ne nous a pas destinés à connaître sa colère, mais à posséder le salut par notre Seigneur Jésus-Christ : 10il est mort pour nous afin que, vivants ou morts, nous entrions ensemble, avec lui, dans la vie. 11C’est pourquoi encouragez-vous les uns les autres et aidez-vous mutuellement à grandir dans la foi, comme vous le faites déjà.

Recommandations

12Nous vous demandons, frères et sœurs, d’apprécier ceux qui travaillent parmi vous, qui vous dirigent au nom du Seigneur et qui vous avertissent. 13Témoignez-leur une grande estime et de l’affection à cause de leur travail. Vivez en paix entre vous.

14Nous vous le recommandons, frères et sœurs : avertissez ceux qui mènent une vie déréglée, réconfortez ceux qui sont découragés, soutenez les faibles, soyez patients envers tous. 15Veillez à ce que personne ne rende le mal pour le mal mais, en toute occasion, recherchez le bien, dans vos rapports mutuels comme envers tous les hommes.

16Soyez toujours dans la joie. 17Priez sans cesse. 18Remerciez Dieu en toute circonstance : telle est pour vous la volonté que Dieu a exprimée en Jésus-Christ.

19N’éteignez pas l’action de l’Esprit : 20ne méprisez pas les prophéties ; 21au contraire, examinez toutes choses, retenez ce qui est bon, 22et gardez-vous de ce qui est mauvais, sous quelque forme que ce soit.

Prière et salutation

23Que le Dieu de paix vous rende lui-même entièrement saints et qu’il vous garde parfaitement esprit, âme et corps5.23 D’autres comprennent : et qu’il garde votre être entier, c’est-à-dire l’esprit, l’âme et le corps… pour que vous soyez irréprochables lors de la venue de notre Seigneur Jésus-Christ.

24Celui qui vous appelle est fidèle et c’est lui qui accomplira tout cela.

25Frères et sœurs, priez aussi pour nous.

26Saluez-vous entre vous par un baiser fraternel.

27Je vous en conjure par le Seigneur : que cette lettre soit lue à tous les frères et sœurs.

28Que la grâce de notre Seigneur Jésus-Christ soit avec vous.