1 Wathesalonike 1 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Wathesalonike 1:1-10

Salamu

11:1 Mdo 16:1; 17:1; Rum 1:7Paulo, Silvano1:1 Yaani Sila. na Timotheo:

Kwa kanisa la Wathesalonike, ninyi mlio ndani ya Mungu Baba yetu na ndani ya Bwana Yesu Kristo:

Neema iwe kwenu na amani.

Shukrani Kwa Ajili Ya Imani Ya Wathesalonike

21:2 Rum 1:8; 2The 1:11; Efe 1:16; Flm 4Siku zote tunamshukuru Mungu kwa ajili yenu ninyi nyote, tukiwataja kwenye maombi yetu daima. 31:3 2The 1:11; 1The 2:13; Yn 6:29; Gal 5:6; 1The 3:6; Yak 2:17; Rum 16:6Tunaikumbuka daima kazi yenu ya imani mbele za Mungu aliye Baba yetu, taabu yenu katika upendo na saburi yenu ya tumaini katika Bwana wetu Yesu Kristo.

41:4 Kol 3:12; 2The 2:13Ndugu zetu mpendwao na Mungu, kwa kuwa tunajua kwamba Mungu amewachagua, 51:5 2The 2:14; Mk 16:20; 1Kor 6:6; Kol 2:2kwa sababu ujumbe wetu wa Injili haukuja kwenu kwa maneno matupu bali pia ulidhihirishwa katika nguvu na katika Roho Mtakatifu, tena ukiwa na uthibitisho kamili, kama vile ninyi wenyewe mnavyojua jinsi tulivyoenenda katikati yenu kwa ajili yenu. 61:6 1Kor 4:16; Mdo 17:5-10; 13:52Nanyi mkawa wafuasi wetu na wa Bwana, ingawa mlipata mateso mengi, mlilipokea lile Neno kwa furaha katika Roho Mtakatifu. 71:7 1The 4:10; Flp 3:7; 1Pet 5:3; 1Tim 4:12Hivyo ninyi mkawa kielelezo kwa waumini wote katika Makedonia na Akaya. 81:8 Rum 1:8; 10:18Kwa maana kutoka kwenu neno la Bwana limesikika, si katika Makedonia na Akaya tu, bali pia imani yenu katika Mungu imejulikana kila mahali kiasi kwamba hatuna haja ya kusema lolote kwa habari yake. 91:9 1Kor 12:2; Gal 4:8Kwa maana watu wa maeneo hayo wenyewe wanaeleza jinsi mlivyotupokea na jinsi mlivyomgeukia Mungu mkaacha sanamu, ili kumtumikia Mungu aliye hai na wa kweli 101:10 Mdo 2:24; Rum 5:9na ili kumngojea Mwanawe kutoka mbinguni, ambaye Mungu alimfufua kutoka kwa wafu: yaani, Yesu, yeye aliyetuokoa kutoka ghadhabu inayokuja.

New International Version

1 Thessalonians 1:1-10

1Paul, Silas1:1 Greek Silvanus, a variant of Silas and Timothy,

To the church of the Thessalonians in God the Father and the Lord Jesus Christ:

Grace and peace to you.

Thanksgiving for the Thessalonians’ Faith

2We always thank God for all of you and continually mention you in our prayers. 3We remember before our God and Father your work produced by faith, your labor prompted by love, and your endurance inspired by hope in our Lord Jesus Christ.

4For we know, brothers and sisters1:4 The Greek word for brothers and sisters (adelphoi) refers here to believers, both men and women, as part of God’s family; also in 2:1, 9, 14, 17; 3:7; 4:1, 10, 13; 5:1, 4, 12, 14, 25, 27. loved by God, that he has chosen you, 5because our gospel came to you not simply with words but also with power, with the Holy Spirit and deep conviction. You know how we lived among you for your sake. 6You became imitators of us and of the Lord, for you welcomed the message in the midst of severe suffering with the joy given by the Holy Spirit. 7And so you became a model to all the believers in Macedonia and Achaia. 8The Lord’s message rang out from you not only in Macedonia and Achaia—your faith in God has become known everywhere. Therefore we do not need to say anything about it, 9for they themselves report what kind of reception you gave us. They tell how you turned to God from idols to serve the living and true God, 10and to wait for his Son from heaven, whom he raised from the dead—Jesus, who rescues us from the coming wrath.