1 Wakorintho 16 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Wakorintho 16:1-24

Changizo Kwa Ajili Ya Watakatifu

116:1 Mdo 24:17; 9:13; 16:6Basi kuhusu changizo kwa ajili ya watakatifu: Kama nilivyoyaagiza makanisa ya Galatia, fanyeni vivyo hivyo. 216:2 Mdo 20:7; 2Kor 9:4-5Siku ya kwanza ya kila juma, kila mmoja wenu atenge kiasi cha fedha, kulingana na mapato yake na fedha hizo aziweke akiba, ili nitakapokuja pasiwe na lazima ya kufanya mchango. 316:3 2Kor 3:1; 8:18-19Kwa hiyo nitakapowasili, nitawapa wale mtakaowachagua barua za kuwatambulisha, ili kuwatuma wapeleke zawadi zenu huko Yerusalemu. 416:4 2Kor 8:4, 19Kama ikionekana ni vyema na mimi niende, basi hao watu watafuatana nami.

Mahitaji Binafsi

516:5 1Kor 4:19; Mdo 16:9Baada ya kupitia Makedonia nitakuja kwenu, maana ninakusudia kupitia Makedonia. 616:6 Rum 15:24; Tit 3:13Huenda nitakaa nanyi kwa muda, au hata kukaa nanyi kipindi chote cha baridi, ili mweze kunisaidia katika safari yangu, popote niendapo. 716:7 Mdo 18:21Kwa maana sitaki niwaone sasa na kupita tu; natarajia kuwa nanyi kwa muda wa kutosha, kama Bwana akipenda. 816:8 Mdo 18:19; 2:1Lakini nitakaa Efeso mpaka wakati wa Pentekoste, 916:9 Mdo 14:27; 2Kor 2:12; Kol 4:3; Ufu 3:8; Mdo 19:9kwa maana mlango mkubwa umefunguliwa kwangu kufanya kazi yenye matunda, nako huko kuna adui wengi wanaonipinga.

1016:10 Mdo 16:1; 19:22; Rum 16:21; Flp 2:20, 22; 1The 3:2Ikiwa Timotheo atakuja kwenu, hakikisheni kwamba hana hofu yoyote akiwa nanyi, kwa sababu anafanya kazi ya Bwana, kama mimi nifanyavyo. 1116:11 1Tim 4:12; 2Kor 1:16; 3Yn 6; Mdo 19:9Basi asiwepo mtu atakayekataa kumpokea. Msafirisheni kwa amani ili aweze kunijia tena. Namtarajia pamoja na ndugu.

1216:12 Mdo 18:24; 1Kor 1:12Basi kwa habari za ndugu yetu Apolo, nimemsihi kwa bidii aje kwenu pamoja na hao ndugu. Ingawa alikuwa hapendi kabisa kuja sasa, lakini atakuja apatapo nafasi.

Maneno Ya Mwisho

1316:13 1Kor 1:8; 2Kor 1:21; Gal 5:1; Flp 1:27; 1The 3:8; Tit 1:9; Efe 6:10Kesheni, simameni imara katika imani, fanyeni kiume, kuweni mashujaa kuweni hodari. 1416:14 1Kor 14:1Fanyeni kila kitu katika upendo.

1516:15 1Kor 1:6; Rum 16:5; Mdo 18; 12; 24; 17; 9:13Ninyi mnajua kwamba watu wa nyumbani mwa Stefana ndio waliokuwa wa kwanza kuamini katika Akaya, nao wamejitoa kwa ajili ya kuwahudumia watakatifu. Ndugu nawasihi, 1616:16 1The 5:12; Ebr 13:17mjitie katika kuwahudumia watu kama hawa na kila mmoja aingiaye kwenye kazi na kuifanya kwa bidii. 1716:17 2Kor 11:9; Flp 2:30Nilifurahi wakati Stefana, Fortunato na Akaiko walipofika, kwa sababu wamenipatia yale niliyopungukiwa kutoka kwenu. 1816:18 Rum 15:32; Flp 1:7; 2:29Kwa kuwa waliiburudisha roho yangu na zenu pia. Watu kama hawa wanastahili kutambuliwa.

Salamu Za Mwisho

1916:19 Mdo 2:9; 18:2; Rum 16:5Makanisa ya Asia yanawasalimu. Akila na Prisila,16:19 Prisila kwa Kiyunani ni Priska, hivyo tafsiri nyingine zimemuita Priska. pamoja na kanisa lililoko nyumbani kwao wanawasalimu sana katika Bwana. 2016:20 Rum 16:16; 2Kor 13:12; 1Pet 5:14Ndugu wote walioko hapa wanawasalimu. Salimianeni kwa busu takatifu.

2116:21 Gal 6:11; Kol 4:18; 2The 3:17Mimi, Paulo, naandika salamu hizi kwa mkono wangu mwenyewe.

2216:22 Efe 6:24; Rum 9:3; Ufu 22:20Kama mtu yeyote hampendi Bwana Yesu Kristo, na alaaniwe. Bwana wetu, njoo.16:22 Kwa Kiaramu ni Marana tha.

2316:23 Rum 16:20Neema ya Bwana Yesu iwe nanyi.

24Upendo wangu uwe nanyi nyote katika Kristo Yesu. Amen.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

哥林多前書 16:1-24

捐助聖徒

1至於捐款幫助聖徒這件事,你們可以照我吩咐加拉太各教會的方法辦理。 2每逢週日,各人應按照自己的收入抽出一部分留起來,免得我到的時候才現湊。 3我到了以後,會差遣你們委託的人帶著推薦信把你們的捐款送到耶路撒冷4如果我也需要去的話,他們可以跟我一起去。

保羅的計劃

5我正打算從馬其頓經過,過了馬其頓,我就去探望你們。 6我也許會和你們住一段時期,甚至在你們那裡過冬。之後,我無論去什麼地方,你們都可以給我送行。 7我不想只是現在順道探望你們,主若許可,我盼望能夠和你們同住一段時期。 8我會在以弗所停留到五旬節, 9因為大門為我敞開了,工作很有成效,不過反對我的人也很多。

10提摩太到了以後,你們要好好接待他,讓他在你們那裡安心,因為他和我一樣,都是在為主做工。 11所以誰也不許輕視他。你們要幫助他平安地回到我這裡,我正在等候他和弟兄們同來。 12至於亞波羅弟兄,我雖然再三勸他和弟兄們去你們那裡,但他目前還不願啟行。不過他有機會就會去。

勸勉與問候

13你們要警醒,在信仰上堅定不移,做勇敢剛強的人。 14無論做什麼事,都要有愛心。

15弟兄姊妹,你們都知道司提法納一家在亞該亞是最早信主的16·15 最早信主的」希臘文是「最早的果子」。,也知道他們怎樣盡心竭力地服侍聖徒。 16你們要順服這樣的人,也要順服所有同心努力服侍的人。 17我很高興司提法納福徒拿都亞該古來我這裡,因為你們幫不到我的地方,他們都補足了。 18他們使我和你們心裡都感到十分欣慰,你們要敬重這樣的人。

19亞細亞的各教會問候你們。亞居拉百基拉夫婦和常在他們家裡聚會的信徒,奉主的名衷心地向你們問安。 20全體弟兄姊妹都問候你們。你們要以聖潔的吻彼此問候。

21保羅親筆問候你們。

22如果有人不愛主,這人可咒可詛!主啊,我願你來!

23願主耶穌基督的恩典與你們同在! 24我在基督耶穌裡愛你們所有的人。阿們!