1 Wakorintho 11 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Wakorintho 11:1-34

111:1 1Kor 4:16; Rum 15:13; 1Pet 2:12Igeni mfano wangu, kama ninavyouiga mfano wa Kristo.

Utaratibu Katika Kuabudu

211:2 1Kor 4:17; 15:2-3; 2The 2:15; 3:6Ninawasifu kwa kuwa mnanikumbuka katika kila jambo na kwa kushika mafundisho niliyowapa.

311:3 Efe 1:22; 5:23; Mwa 3:16Napenda mfahamu kwamba kichwa cha kila mwanaume ni Kristo, na kichwa cha mwanamke ni mwanaume, nacho kichwa cha Kristo ni Mungu. 411:4 Mdo 11:27; 1Kor 12:10, 28; 14:1Kila mwanaume anayeomba au kutoa unabii akiwa amefunika kichwa chake, anakiaibisha kichwa chake. 511:5 Mdo 21:9; Kum 21:12Naye kila mwanamke anayeomba au kutoa unabii pasipo kufunika kichwa chake, anakiaibisha kichwa chake, kwani ni sawa na yeye aliyenyoa nywele. 611:6 Hes 5:18; Kum 22:5Kama mwanamke hatajifunika kichwa chake, basi inampasa kunyoa nywele zake. Lakini kama ni aibu kwa mwanamke kukata au kunyoa nywele zake, basi afunike kichwa chake. 711:7 Mwa 1:29; 9:6; Yak 3:9Haimpasi mwanaume kufunika kichwa chake kwa kuwa yeye ni mfano wa Mungu na utukufu wa Mungu, lakini mwanamke ni utukufu wa mwanaume. 811:8 Mwa 2:21-23; 1Tim 2:13Kwa maana mwanaume hakutoka kwa mwanamke, bali mwanamke alitoka kwa mwanaume. 911:9 Mwa 2:18Wala mwanaume hakuumbwa kwa ajili ya mwanamke, bali mwanamke kwa ajili ya mwanaume. 1011:10 Mwa 24:65; Mhu 5:6Kwa sababu hii na kwa sababu ya malaika, inampasa mwanamke awe na ishara ya mamlaka juu yake.

11Lakini katika Bwana, mwanamke hajitegemei pasipo mwanaume na mwanaume hajitegemei pasipo mwanamke. 1211:12 Rum 11:36Kama vile mwanamke alivyoumbwa kutoka kwa mwanaume, vivyo hivyo mwanaume huzaliwa na mwanamke. Lakini vitu vyote vyatoka kwa Mungu. 13Hukumuni ninyi wenyewe: Je, inafaa kwa mwanamke kumwomba Mungu bila kufunika kichwa chake? 14Je, maumbile ya asili hayatufundishi kuwa ni aibu kwa mwanaume kuwa na nywele ndefu? 15Lakini mwanamke akiwa na nywele ndefu ni utukufu kwake? Kwa maana mwanamke amepewa nywele ndefu ili kumfunika. 1611:16 1Kor 7:17; 10:32Kama mtu anataka kubishana juu ya jambo hili, sisi wala makanisa ya Mungu hatutambui desturi nyingine.

Matumizi Mabaya Ya Meza Ya Bwana

1711:17 1Kor 11:2, 22Basi katika maagizo yafuatayo, siwezi kuwasifu, kwa sababu mkutanikapo si kwa ajili ya faida bali kwa hasara. 1811:18 1Kor 1:10-12; 3:3Kwanza, mnapokutana kama kanisa, nasikia kwamba kuna mgawanyiko miongoni mwenu, nami kwa kiasi fulani nasadiki kuwa ndivyo ilivyo. 1911:19 1Yn 2:19Bila shaka lazima pawe na tofauti miongoni mwenu ili kuonyesha ni nani anayekubaliwa na Mungu. 20Mkutanikapo pamoja si chakula cha Bwana mnachokula, 2111:21 2Pet 2:13; Yud 23kwa kuwa mnapokula, kila mmoja wenu anakula bila kuwangoja wengine. Mmoja hukaa njaa na mwingine analewa. 2211:22 Yak 2:6Je, hamna nyumbani kwenu ambako mnaweza kula na kunywa? Au mnalidharau kanisa la Mungu na kuwadhalilisha wale wasio na kitu? Niwaambie nini? Je, niwasifu juu ya jambo hili? La, hasha!

Kuanzishwa Kwa Meza Ya Bwana

(Mathayo 26:26-29; Marko 14:22-25; Luka 22:14-20)

2311:23 Gal 1:12; 1Kor 15:3Kwa maana mimi nilipokea kutoka kwa Bwana yale niliyowapa ninyi, kwamba Bwana Yesu, usiku ule aliposalitiwa, alitwaa mkate, 2411:24 1Kor 10:16naye akiisha kushukuru, akaumega, akasema, “Huu ndio mwili wangu, uliotolewa kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu.” 2511:25 Lk 22:20; 1Kor 10:16Vivyo hivyo baada ya kula, akakitwaa kikombe, akisema, “Kikombe hiki ni agano jipya katika damu yangu. Fanyeni hivi kila mnywapo, kwa ukumbusho wangu.” 2611:26 1Kor 1:17; 1:7; Mt 26:29Maana kila mlapo mkate huu na kunywea kikombe hiki, mnatangaza mauti ya Bwana mpaka ajapo.

Kushiriki Meza Ya Bwana Isivyostahili

2711:27 Ebr 10:29Kwa hiyo, mtu yeyote alaye mkate huo au kukinywea kikombe hicho cha Bwana isivyostahili, atakuwa na hatia ya dhambi juu ya mwili na damu ya Bwana. 2811:28 2Kor 13:5; Mt 26:22Inampasa mtu ajichunguze mwenyewe, kabla ya kula mkate na kukinywea kikombe. 29Kwa maana mtu yeyote alaye na kunywa pasipo kuutambua mwili wa Bwana, hula na kunywa hukumu juu yake mwenyewe. 3011:30 Mt 9:24; 1Kor 15:20; Efe 5:14; 1The 5:6Hii ndiyo sababu wengi miongoni mwenu ni wagonjwa na dhaifu na wengine wenu hata wamekufa. 3111:31 Za 32:5; 1Yn 1:9Lakini kama tungejichunguza wenyewe tusingehukumiwa. 3211:32 Za 94:12; 118:18; Mit 3:11-12; Ebr 12:7-10; Ufu 3:19Tunapohukumiwa na Bwana, tunaadibishwa ili tusije tukahukumiwa pamoja na ulimwengu.

33Kwa hiyo, ndugu zangu, mkutanikapo pamoja ili kula, mngojane. 3411:34 1Kor 4:19; Tit 1:5; 1Kor 7:17; 11:22Kama mtu akiwa na njaa, ale nyumbani kwake ili mkutanapo pamoja msije mkahukumiwa.

Nami nitakapokuja nitawapa maelekezo zaidi.

New International Version

1 Corinthians 11:1-34

1Follow my example, as I follow the example of Christ.

On Covering the Head in Worship

2I praise you for remembering me in everything and for holding to the traditions just as I passed them on to you. 3But I want you to realize that the head of every man is Christ, and the head of the woman is man,11:3 Or of the wife is her husband and the head of Christ is God. 4Every man who prays or prophesies with his head covered dishonors his head. 5But every woman who prays or prophesies with her head uncovered dishonors her head—it is the same as having her head shaved. 6For if a woman does not cover her head, she might as well have her hair cut off; but if it is a disgrace for a woman to have her hair cut off or her head shaved, then she should cover her head.

7A man ought not to cover his head,11:4-7 Or 4 Every man who prays or prophesies with long hair dishonors his head. 5 But every woman who prays or prophesies with no covering of hair dishonors her head—she is just like one of the “shorn women.” 6 If a woman has no covering, let her be for now with short hair; but since it is a disgrace for a woman to have her hair shorn or shaved, she should grow it again. 7 A man ought not to have long hair since he is the image and glory of God; but woman is the glory of man. 8For man did not come from woman, but woman from man; 9neither was man created for woman, but woman for man. 10It is for this reason that a woman ought to have authority over her own11:10 Or have a sign of authority on her head, because of the angels. 11Nevertheless, in the Lord woman is not independent of man, nor is man independent of woman. 12For as woman came from man, so also man is born of woman. But everything comes from God.

13Judge for yourselves: Is it proper for a woman to pray to God with her head uncovered? 14Does not the very nature of things teach you that if a man has long hair, it is a disgrace to him, 15but that if a woman has long hair, it is her glory? For long hair is given to her as a covering. 16If anyone wants to be contentious about this, we have no other practice—nor do the churches of God.

Correcting an Abuse of the Lord’s Supper

17In the following directives I have no praise for you, for your meetings do more harm than good. 18In the first place, I hear that when you come together as a church, there are divisions among you, and to some extent I believe it. 19No doubt there have to be differences among you to show which of you have God’s approval. 20So then, when you come together, it is not the Lord’s Supper you eat, 21for when you are eating, some of you go ahead with your own private suppers. As a result, one person remains hungry and another gets drunk. 22Don’t you have homes to eat and drink in? Or do you despise the church of God by humiliating those who have nothing? What shall I say to you? Shall I praise you? Certainly not in this matter!

23For I received from the Lord what I also passed on to you: The Lord Jesus, on the night he was betrayed, took bread, 24and when he had given thanks, he broke it and said, “This is my body, which is for you; do this in remembrance of me.” 25In the same way, after supper he took the cup, saying, “This cup is the new covenant in my blood; do this, whenever you drink it, in remembrance of me.” 26For whenever you eat this bread and drink this cup, you proclaim the Lord’s death until he comes.

27So then, whoever eats the bread or drinks the cup of the Lord in an unworthy manner will be guilty of sinning against the body and blood of the Lord. 28Everyone ought to examine themselves before they eat of the bread and drink from the cup. 29For those who eat and drink without discerning the body of Christ eat and drink judgment on themselves. 30That is why many among you are weak and sick, and a number of you have fallen asleep. 31But if we were more discerning with regard to ourselves, we would not come under such judgment. 32Nevertheless, when we are judged in this way by the Lord, we are being disciplined so that we will not be finally condemned with the world.

33So then, my brothers and sisters, when you gather to eat, you should all eat together. 34Anyone who is hungry should eat something at home, so that when you meet together it may not result in judgment.

And when I come I will give further directions.