1 Wafalme 8 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

1 Wafalme 8:1-66

Sanduku La Agano Laletwa Hekaluni

(2 Nyakati 5)

18:1 Ezr 7:7Kisha Mfalme Solomoni akawaita mbele zake huko Yerusalemu wazee wa Israeli, viongozi wote wa makabila na wakuu wa jamaa za Waisraeli, ili walilete Sanduku la Agano la Bwana kutoka Sayuni, Mji wa Daudi. 28:2 1Nya 3:22Wanaume wote wa Israeli wakakusanyika kwa Mfalme Solomoni wakati wa sikukuu ya mwezi wa Ethanimu, ndio mwezi wa saba.

38:3 1Nya 3:22; Ezr 2:3Wazee wote wa Israeli walipofika, makuhani wakajitwika Sanduku la Agano, 48:4 Ezr 2:6nao wakalipandisha Sanduku la Bwana, na Hema la Kukutania pamoja na vyombo vyote vitakatifu vilivyokuwa ndani yake. Makuhani na Walawi wakavibeba, 5naye Mfalme Solomoni na kusanyiko lote la Israeli waliokusanyika kumzunguka walikuwa mbele ya hilo Sanduku, nao wakatoa dhabihu nyingi za kondoo na ngʼombe ambao idadi yao haikuwezekana kuandikwa au kuhesabiwa.

68:6 Ezr 2:15; Neh 7:20Makuhani wakalileta Sanduku la Agano la Bwana hadi mahali pake ndani ya sehemu takatifu ndani ya Hekalu, yaani Patakatifu pa Patakatifu, na kuliweka chini ya mabawa ya makerubi. 7Makerubi yalitandaza mabawa yao juu ya mahali pa Sanduku la Agano na kutia kivuli Sanduku pamoja na mipiko yake ya kubebea. 8Mipiko hiyo ilikuwa mirefu sana kiasi kwamba ncha zake zilionekana kutoka Mahali Patakatifu mbele ya Patakatifu pa Patakatifu, lakini sio nje ya Mahali Patakatifu. Hiyo mipiko ipo hata leo. 9Ndani ya Sanduku hapakuwepo kitu kingine chochote isipokuwa zile mbao mbili za mawe ambazo Mose alikuwa ameziweka ndani yake huko Horebu, mahali ambapo Bwana alifanya Agano na Waisraeli baada ya kutoka Misri.

10Makuhani walipoondoka katika Mahali Patakatifu, wingu likajaza Hekalu la Bwana. 11Nao makuhani hawakuweza kufanya huduma yao kwa sababu ya lile wingu, kwa kuwa utukufu wa Bwana ulijaza Hekalu lake.

12Ndipo Solomoni akasema, “Bwana alisema kwamba ataishi katika giza nene; 138:13 Ezr 2:13naam, hakika nimekujengea Hekalu zuri sana, mahali pako pa kuishi milele.”

Hotuba Ya Solomoni

(2 Nyakati 6:3-11)

14Kusanyiko lote la Israeli lilipokuwa limesimama hapo, mfalme akageuka na kuwabariki. 158:15 Ezr 2:40; 7:7; Mdo 16:13; 20:28; Za 137:1; Mit 27:23; Ebr 13:17; Ezr 7:7; Hes 8:1Kisha akasema:

“Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye kwa mkono wake mwenyewe ametimiza lile alilomwahidi Daudi baba yangu kwa kinywa chake mwenyewe. Kwa kuwa alisema, 16‘Tangu siku niliyowatoa watu wangu Israeli kutoka Misri, sikuchagua mji katika kabila lolote la Israeli ili Hekalu lijengwe humo ili Jina langu lipate kuwamo humo, bali nimemchagua Daudi kuwatawala watu wangu Israeli.’

178:17 Ezr 2:43“Ilikuwa moyoni mwa Daudi baba yangu kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana, Mungu wa Israeli. 188:18 Ezr 5:5; 7:28; Neh 8:7; Rum 8:28; Mit 3:6; Law 10:10-11; 2Nya 30:22Lakini Bwana akamwambia Daudi baba yangu, ‘Kwa sababu ilikuwa moyoni mwako kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina langu, ulifanya vyema kuwa na jambo hili moyoni mwako. 19Hata hivyo, sio wewe utakayenijengea hekalu, bali mwanao, ambaye ni nyama yako na damu yako mwenyewe, yeye ndiye atakayejenga Hekalu kwa ajili ya Jina langu.’

208:20 1Nya 9:2; Ezr 2:43Bwana ametimiza ahadi aliyoiweka: Nimeingia mahali pa Daudi baba yangu na sasa ninakikalia kiti cha ufalme cha Israeli, kama vile Bwana alivyoahidi, nami nimejenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana, Mungu wa Israeli. 218:21 2Nya 9:2; Ezr 2:438:21 2Nya 20:3; Za 27:11; Law 16:29; Za 5:8; 2Nya 20:3; Law 16:29; Isa 58:3-5Nimetenga nafasi humo kwa ajili ya Sanduku la Agano, ambamo ndani yake kuna lile Agano la Bwana alilofanya na baba zetu wakati alipowatoa Misri.”

Maombi Ya Solomoni Ya Kuweka Hekalu Wakfu

(2 Nyakati 6:12-42)

228:22 Neh 2:9; Yer 41:16; 2Nya 15:2; 1Kor 9:15; 1Nya 28:9; Ezr 7:6-9; Za 33:18-19; Isa 3:10; Rum 8:28; 1Pet 3:12; Za 34:16; 2Nya 15:2Kisha Solomoni akasimama mbele ya madhabahu ya Bwana machoni pa kusanyiko lote la Israeli, akakunjua mikono yake kuelekea mbinguni 238:23 2Nya 33:13; Kum 4:29; Mdo 14:23; 1Nya 5:20; Isa 19:22; Yer 29:12-13na kusema:

“Ee Bwana, Mungu wa Israeli, hakuna Mungu kama wewe juu mbinguni wala chini duniani, wewe unayetunza Agano lako la upendo na watumishi wanaodumu katika njia yako kwa moyo wote. 24Umetimiza ahadi yako kwa mtumishi wako Daudi baba yangu, kwa kinywa chako uliahidi na kwa mkono wako umetimiza, kama ilivyo leo.

258:25 Ezr 7:15-16“Sasa Bwana, Mungu wa Israeli, mtimizie mtumishi wako Daudi baba yangu ahadi zako ulizomwahidi uliposema, ‘Kamwe hutakosa kuwa na mtu atakayeketi mbele zangu kwenye kiti cha ufalme cha Israeli, kama wanao wakiangalia yote wayafanyayo kuenenda mbele zangu kama vile ulivyofanya.’ 26Sasa, Ee Mungu wa Israeli, acha neno lako lile ulilomwahidi mtumishi wako Daudi baba yangu litimie.

27“Lakini kweli, je, Mungu atafanya makao duniani? Mbingu, hata mbingu zilizo juu sana, haziwezi kukutosha wewe. Sembuse Hekalu hili nililojenga! 288:28 Kum 33:8; Law 21:6; 22:2-3; 2Nya 24:14; Hes 4:4; Isa 52:11; 1Nya 23:28Hata hivyo sikiliza dua ya mtumishi wako na maombi yake kwa huruma, Ee Bwana Mungu wangu. Sikia kilio na dua ambayo mtumishi wako anaomba mbele zako siku hii ya leo. 298:29 1Nya 26:20-26; Lk 12:38-39Macho yako na yafumbuke kuelekea Hekalu hili usiku na mchana, mahali hapa ambapo ulisema, ‘Jina langu litakuwako humo,’ ili kwamba upate kusikia maombi ambayo mtumishi wako ataomba kuelekea mahali hapa. 30Usikie maombi ya mtumishi wako na ya watu wako Israeli wakati wanapoomba kuelekea mahali hapa. Sikia kutoka mbinguni, mahali pa makao yako na usikiapo, samehe.

318:31 Ay 5:19-24; Isa 41:10-14; Ezr 7:6-7, 28“Mtu anapomkosea jirani yake na akatakiwa kuapa, akija na kuapa mbele ya madhabahu yako ndani ya Hekalu hili, 328:32 Mwa 40:13; Neh 2:11; Isa 56:6; 14:1basi, sikia kutoka mbinguni na ukatende. Hukumu kati ya watumishi wako, ukimhukumu yule mwenye hatia na kuleta juu ya kichwa chake yale aliyoyatenda. Umtangazie mwenye haki kwamba hana hatia, hivyo ukathibitishe kuwa haki kwake.

338:33 Neh 3:3, 21-24“Wakati watu wako Israeli watakapokuwa wameshindwa na adui kwa sababu ya dhambi walizofanya dhidi yako, watakapokugeukia na kulikiri jina lako, wakiomba na kufanya dua kwako katika Hekalu hili, 34basi usikie kutoka mbinguni, ukasamehe dhambi ya watu wako Israeli na kuwarudisha katika nchi uliyowapa baba zao.

358:35 Ezr 6:17“Wakati mbingu zitakapokuwa zimefungwa kusiwe na mvua kwa sababu watu wako wametenda dhambi dhidi yako, watakapoomba kuelekea mahali hapa na kulikiri jina lako nao wakageuka kutoka dhambi zao kwa sababu umewaadhibu, 368:36 Ezr 7:21-24; Zek 8:1-23; Es 9:3basi usikie kutoka mbinguni na usamehe dhambi ya watumishi wako, watu wako Israeli. Wafundishe njia sahihi ya kuishi na ukanyeshe mvua juu ya nchi uliyowapa watu wako kuwa urithi.

37“Wakati njaa au tauni vikija juu ya nchi, au koga au kawa, nzige au panzi, au wakati adui atakapowazingira katika mji wao wowote, maafa ya namna yoyote au ugonjwa wowote unaoweza kuwajia, 38wakati dua au maombi yatakapofanywa na mmojawapo wa watu wako Israeli, kila mmoja akitambua taabu za moyo wake mwenyewe, naye akainyoosha mikono yake kuelekea Hekalu hili: 39basi usikie kutoka mbinguni, katika makao yako. Usamehe na utende, umpe kila mtu kulingana na matendo yake, kwa kuwa unaujua moyo wake (kwa kuwa ni wewe peke yako ujuaye mioyo ya watu wote), 40ili wakuogope kwa wakati wote watakaoishi katika nchi uliyowapa baba zetu.

41“Kwa habari ya mgeni ambaye si miongoni mwa watu wako Israeli, lakini amekuja kutoka nchi ya mbali kwa sababu ya jina lako, 42kwa maana watu watasikia juu ya Jina lako kuu na juu ya mkono wako wenye nguvu na mkono wako ulionyooshwa, atakapokuja na kuomba kuelekea Hekalu hili, 43basi na usikie kutoka mbinguni, mahali pa makao yako, ukafanye lolote ambalo mgeni huyo anakuomba, ili mataifa yote ya dunia wapate kujua jina lako na wakuogope kama wafanyavyo watu wako Israeli nao wapate pia kujua kwamba nyumba hii niliyoijenga imeitwa kwa Jina lako.

44“Wakati watu wako watakapokwenda vitani dhidi ya adui zao, popote utakapowapeleka, wakati watakapoomba kwa Bwana kuelekea mji ambao umeuchagua, na Hekalu nililolijenga kwa ajili ya Jina lako, 45basi usikie dua na maombi yao kutoka mbinguni, ukawatetee haki yao.

46“Watakapotenda dhambi dhidi yako, kwa kuwa hakuna mtu yeyote ambaye hatendi dhambi, nawe ukachukizwa nao na kuwakabidhi kwa adui, ambaye atawachukua utumwani katika nchi yake mwenyewe, mbali au karibu; 47na kama watabadilika mioyo yao katika nchi wanakoshikiliwa mateka, nao wakatubu na kukulilia katika nchi ya wale waliowashinda na kusema, ‘Tumetenda dhambi, tumefanya makosa, tumetenda uovu’; 48kama wakikugeukia kwa moyo wao wote na nafsi zao katika nchi ya adui zao ambao waliwachukua mateka, wakakuomba kuelekea nchi uliyowapa baba zao, kuelekea mji uliouchagua na Hekalu nililolijenga kwa ajili ya Jina lako; 49basi kutoka mbinguni, mahali pa makao yako, usikie dua yao na maombi yao na kuitetea haki yao. 50Uwasamehe watu wako, waliotenda dhambi dhidi yako; uwasamehe makosa yote waliyoyatenda dhidi yako, ukawafanye wale waliowashinda kuwaonea huruma; 51kwa maana ni watu wako na urithi wako, uliowatoa Misri, kutoka kwenye lile tanuru la kuyeyushia chuma.

52“Macho yako na yafumbuke juu ya ombi la mtumishi wako na ombi la watu wako Israeli, nawe uwasikilize wakati wowote wanapokulilia. 53Kwa maana uliwachagua wao kutoka mataifa yote ya ulimwengu kuwa urithi wako mwenyewe, kama ulivyotangaza kupitia mtumishi wako Mose wakati wewe, Ee Bwana Mwenyezi, ulipowatoa baba zetu kutoka Misri.”

54Wakati Solomoni alipomaliza dua hizi zote na maombi kwa Bwana, akainuka kutoka mbele ya madhabahu ya Bwana, mahali alipokuwa amepiga magoti, mikono yake ikawa imekunjuliwa kuelekea juu mbinguni. 55Akasimama na kubariki kusanyiko lote la Israeli kwa sauti kubwa akisema:

56“Ahimidiwe Bwana, aliyewapa pumziko watu wake Israeli kama vile alivyokuwa ameahidi. Hakuna hata neno moja lililopunguka kati ya ahadi zote nzuri alizozitoa kupitia mtumishi wake Mose. 57Bwana Mungu wetu na awe pamoja nasi kama alivyokuwa na baba zetu, kamwe asituache wala kutukataa. 58Yeye na aielekeze mioyo yetu kwake, ili tutembee katika njia zake zote na kuzishika amri na maagizo na masharti aliyowapa baba zetu. 59Nami maneno yangu haya, ambayo nimeyaomba mbele za Bwana, yawe karibu na Bwana Mungu wetu usiku na mchana, ili kwamba atetee shauri la mtumishi wake na la watu wake Israeli kulingana na hitaji lao la kila siku, 60ili kwamba mataifa yote ya dunia wajue kwamba Bwana ndiye Mungu na kwamba hakuna mwingine. 61Lakini ni lazima mwiweke mioyo yenu kikamilifu kwa Bwana Mungu wetu, kuishi kwa maagizo yake na kutii amri zake, kama ilivyo wakati huu.”

Kuwekwa Wakfu Hekalu

(2 Nyakati 7:4-10)

62Kisha mfalme na Israeli wote pamoja naye wakatoa dhabihu mbele za Bwana. 63Solomoni akatoa dhabihu sadaka za amani kwa Bwana: ngʼombe 22,000, pamoja na kondoo na mbuzi 120,000. Hivyo ndivyo mfalme na Waisraeli wote walivyoweka wakfu Hekalu la Bwana.

64Siku iyo hiyo mfalme akaweka wakfu sehemu ya katikati ya ua uliokuwa mbele ya Hekalu la Bwana na hapo akatoa sadaka za kuteketezwa, sadaka za nafaka na mafuta ya sadaka za amani, kwa sababu madhabahu ya shaba iliyokuwa mbele za Bwana ilikuwa ndogo sana kuweza kubeba sadaka hizo za kuteketezwa, sadaka za nafaka na mafuta ya sadaka ya amani.

65Hivyo Solomoni akaiadhimisha sikukuu kwa wakati ule, na Israeli wote pamoja naye. Walikuwa kusanyiko kubwa sana, watu kutoka Lebo-Hamathi hadi Kijito cha Misri. Wakaiadhimisha mbele za Bwana Mungu wetu kwa siku saba na siku saba zaidi, yaani, jumla siku kumi na nne. 66Siku iliyofuata, aliwaruhusu watu waondoke. Wakambariki mfalme, kisha wakaenda nyumbani, wakiwa na mashangilio na furaha rohoni kwa ajili ya mambo yote mema ambayo Bwana ametenda kwa ajili ya Daudi mtumishi wake na watu wake Israeli.

New International Reader’s Version

1 Kings 8:1-66

The Ark Is Brought to the Temple

1Then King Solomon sent for the elders of Israel. He told them to come to him in Jerusalem. They included all the leaders of the tribes. They also included the chiefs of the families of Israel. Solomon wanted them to bring up the ark of the Lord’s covenant from Zion. Zion was the City of David. 2All the Israelites came together to where King Solomon was. It was at the time of the Feast of Booths. The feast was held in the month of Ethanim. That’s the seventh month.

3All the elders of Israel arrived. Then the priests picked up the ark and carried it. 4They brought up the ark of the Lord. They also brought up the tent of meeting and all the sacred things in the tent. The priests and Levites carried everything up. 5The entire community of Israel had gathered around King Solomon. All of them were in front of the ark. They sacrificed huge numbers of sheep and cattle. There were so many animals that they couldn’t be recorded. In fact, they couldn’t even be counted.

6The priests brought the ark of the Lord’s covenant law to its place in the Most Holy Room of the temple. They put it under the wings of the cherubim. 7Their wings were spread out over the place where the ark was. They covered the ark. They also covered the poles used to carry it. 8The poles were very long. Their ends could be seen from the Holy Room in front of the Most Holy Room. But they couldn’t be seen from outside the Holy Room. They are still there to this day. 9There wasn’t anything in the ark except the two stone tablets. Moses had placed them in it at Mount Horeb. That’s where the Lord had made a covenant with the Israelites. He made it after they came out of Egypt.

10The priests left the Holy Room. Then the cloud filled the temple of the Lord. 11The priests couldn’t do their work because of it. That’s because the glory of the Lord filled his temple.

12Then Solomon said, “Lord, you have said you would live in a dark cloud. 13As you can see, I’ve built a beautiful temple for you. You can live in it forever.”

14The whole community of Israel was standing there. The king turned around and gave them his blessing. 15Then he said,

“I praise the Lord. He is the God of Israel. With his own mouth he made a promise to my father David. With his own powerful hand he made it come true. He said, 16‘I brought my people Israel out of Egypt. Ever since, I haven’t chosen a city in any tribe of Israel where a temple could be built for my Name. But I have chosen David to rule over my people Israel.’

17“With all his heart my father David wanted to build a temple. He wanted to do it so the Lord could put his Name there. The Lord is the God of Israel. 18But the Lord spoke to my father David. He said, ‘With all your heart you wanted to build a temple for my Name. It is good that you wanted to do that. 19But you will not build the temple. Instead, your son will build the temple for my Name. He is your own flesh and blood.’

20“The Lord has kept the promise he made. I’ve become the next king after my father David. Now I’m sitting on the throne of Israel. That’s exactly what the Lord promised would happen. I’ve built the temple where the Lord will put his Name. He is the God of Israel. 21I’ve provided a place for the ark there. The tablets of the Lord’s covenant law are inside it. He made that covenant with our people of long ago. He made it when he brought them out of Egypt.”

Solomon Prays to Set the Temple Apart to the Lord

22Then Solomon stood in front of the Lord’s altar. He stood in front of the whole community of Israel. He spread out his hands toward heaven. 23He said,

Lord, you are the God of Israel. There is no God like you in heaven above or on earth below. You keep the covenant you made with us. You show us your love. You do that when we follow you with all our hearts. 24You have kept your promise to my father David. He was your servant. With your mouth you made a promise. With your powerful hand you have made it come true. And today we can see it.

25Lord, you are the God of Israel. Keep the promises you made to my father David. Do it for him. He was your servant. Here is what you said to him. ‘A son from your family line will sit before me on the throne of Israel. This will always be true if your children after you are careful in everything they do. They must live in my sight faithfully the way you have lived.’ 26God of Israel, let your promise to my father David come true.

27“But will you really live on earth? After all, the heavens can’t hold you. In fact, even the highest heavens can’t hold you. So this temple I’ve built certainly can’t hold you! 28But please pay attention to my prayer. Lord my God, be ready to help me as I make my appeal to you. Listen to my cry for help. Hear the prayer I’m praying to you today. 29Let your eyes look toward this temple night and day. You said, ‘I will put my Name there.’ So please listen to the prayer I’m praying toward this place. 30Hear me when I ask you to help us. Listen to your people Israel when they pray toward this place. Listen to us from heaven. It’s the place where you live. When you hear us, forgive us.

31“Suppose someone does something wrong to their neighbor. And the person who has done something wrong is required to give their word. They must tell the truth about what they have done. They must come and do it in front of your altar in this temple. 32When they do, listen to them from heaven. Take action. Judge between the person and their neighbor. Punish the guilty one. Do to that person what they have done to their neighbor. Deal with the one who isn’t guilty in a way that shows they are free from blame. That will prove they aren’t guilty.

33“Suppose your people Israel have lost the battle against their enemies. And suppose they’ve sinned against you. But they turn back to you and praise your name. They pray to you in this temple. And they ask you to help them. 34Then listen to them from heaven. Forgive the sin of your people Israel. Bring them back to the land you gave to their people who lived long ago.

35“Suppose your people have sinned against you. And because of that, the sky is closed up and there isn’t any rain. But your people pray toward this place. They praise you by admitting they’ve sinned. And they turn away from their sin because you have made them suffer. 36Then listen to them from heaven. Forgive the sin of your people Israel. Teach them the right way to live. Send rain on the land you gave them as their share.

37“Suppose there isn’t enough food in the land. And a plague strikes the land. The hot winds completely dry up our crops. Or locusts or grasshoppers come and eat them up. Or an enemy surrounds one of our cities and gets ready to attack it. Or trouble or sickness comes. 38But suppose one of your people prays to you. They ask you to help them. They are aware of how much their own heart is suffering. And they spread out their hands toward this temple to pray. 39Then listen to them from heaven. It’s the place where you live. Forgive them. Take action. Deal with everyone in keeping with everything they do. You know their hearts. In fact, you are the only one who knows every human heart. 40Your people will have respect for you. They will respect you as long as they are in the land you gave our people long ago.

41“Suppose there are outsiders who don’t belong to your people Israel. And they have come from a land far away. They’ve come because they’ve heard about your name. 42When they get here, they will find out even more about your great name. They’ll hear about how you reached out your mighty hand and powerful arm. So they’ll come and pray toward this temple. 43Then listen to them from heaven. It’s the place where you live. Do what those outsiders ask you to do. Then all the nations on earth will know you. They will have respect for you. They’ll respect you just as your own people Israel do. They’ll know that your Name is in this house I’ve built.

44“Suppose your people go to war against their enemies. It doesn’t matter where you send them. And suppose they pray to you toward the city you have chosen. They pray toward the temple I’ve built for your Name. 45Then listen to them from heaven. Listen to their prayer for your help. Stand up for them.

46“Suppose your people sin against you. After all, there isn’t anyone who doesn’t sin. And suppose you get angry with them. You hand them over to their enemies. They take them as prisoners to their own lands. It doesn’t matter whether those lands are near or far away. 47But suppose your people change their ways in the land where they are held as prisoners. They turn away from their sins. They beg you to help them in the land of those who won the battle over them. They say, ‘We have sinned. We’ve done what is wrong. We’ve done what is evil.’ 48And they turn back to you with all their heart and soul. Suppose it happens in the land of their enemies who took them away as prisoners. There they pray to you toward the land you gave their people long ago. They pray toward the city you have chosen. And they pray toward the temple I’ve built for your Name. 49Then listen to them from heaven. It’s the place where you live. Listen to their prayer. Listen to them when they ask you to help them. Stand up for them. 50Your people have sinned against you. Please forgive them. Forgive them for all the wrong things they’ve done against you. And make those who won the battle over them show mercy to them. 51After all, they are your people. They belong to you. You brought them out of Egypt. You brought them out of that furnace that melts iron down and makes it pure.

52“Let your eyes be open to me when I ask you to help us. Let them be open to your people Israel when they ask you to help them. Pay attention to them every time they cry out to you. 53After all, you chose them out of all the nations in the world. You made them your very own people. You did it just as you had announced through your servant Moses. That’s when you brought out of Egypt our people of long ago. You are our Lord and King.”

54Solomon finished praying. He finished asking the Lord to help his people. Then he got up from in front of the Lord’s altar. He had been down on his knees with his hands spread out toward heaven. 55He stood in front of the whole community of Israel. He blessed them with a loud voice. He said,

56“I praise the Lord. He has given peace and rest to his people Israel. That’s exactly what he promised to do. He gave his people good promises through his servant Moses. Every single word of those promises has come true. 57May the Lord our God be with us, just as he was with our people who lived long ago. May he never leave us. May he never desert us. 58May he turn our hearts to him. Then we will live the way he wants us to. We’ll obey the commands, rules and directions he gave our people of long ago. 59I’ve prayed these words to the Lord our God. May he keep them close to him day and night. May he stand up for me. May he also stand up for his people Israel. May he give us what we need every day. 60Then all the nations on earth will know that the Lord is God. They’ll know that there isn’t any other god. 61And may you commit your lives completely to the Lord our God. May you live by his rules. May you obey his commands. May you always do as you are doing now.”

The Temple Is Set Apart to the Lord

62Then the king and the whole community of Israel offered sacrifices to the Lord. 63Solomon sacrificed friendship offerings to the Lord. He sacrificed 22,000 oxen. He also sacrificed 120,000 sheep and goats. So the king and the whole community set the temple of the Lord apart to him.

64On that same day the king set the middle area of the courtyard apart to the Lord. It was in front of the Lord’s temple. There Solomon sacrificed burnt offerings and grain offerings. He also sacrificed the fat of the friendship offerings there. He did it there because the bronze altar that stood in front of the Lord was too small. It wasn’t big enough to hold all the burnt offerings, the grain offerings and the fat of the friendship offerings.

65At that time Solomon celebrated the Feast of Booths. The whole community of Israel was with him. It was a huge crowd. People came from as far away as Lebo Hamath and the Wadi of Egypt. For seven days they celebrated in front of the Lord our God. The feast continued for seven more days. That made a total of 14 days. 66On the following day Solomon sent the people away. They asked the Lord to bless the king. Then they went home. The people were glad. Their hearts were full of joy. That’s because the Lord had done so many good things for his servant David and his people Israel.